image

Historia na asili ya kuzibiti uzazi na uzazi wa mpango

Historia na asili ya kuzibiti uzazi na uzazi wa mpango

Historia ya Kampeni ya Kudhibiti Uzazi



Upo ushahidi wa kutosha kuwa watu binafsi katika zama zote wamekuwa wakijitahidi kuzaa watoto wanaopishana miaka iii kuhifadhi afya ya mama na mtoto. Juhudi za serikali huko nyuma (yaani kabla ya kame ya 20) zilikuwa ni kuwashawishi raia kuoana na kuzaana. Lakini kuanzia karne ya 20 serikali zimejiingiza katika kampeni za kuwataka raia wadhibiti kizazi.



Neno kudhibiti uzazi (birth control) ambalo lilibuniwa na Margaret Sanger, mpiganiaji haki za wanawake wa huko Marekani, mwaka 1913 - 1915 lina maana ya njia za kuzuia mimba kwa kumtumia mwanamume au mwanamke, na hivi sasa zinajumuisha njia zote za kuzuia kizazi, ikiwa ni pamoja na kutoa mimba (abortion) au kuviza kizazi (sterilization). Hata hivyo jina Ia kampeni hii limekuwa likibadilika badilika. Katika miaka ya 1930 jina lilikuwa mpango wa familia (family planning) na katika miaka ya 1940 jina likawa mpango wa uzazi (planned parenthood). Baadaye yakazuka majina mengine mengi kama vile kuzuia mimba (controceptive), uzazi wa hiari (voluntary parenthood), kupunguza familia (family limitation), vita dhidi ya mimba (anti conception) na kadhalika.



Kampeni hizo zilipokuja Afrika Mashariki zilipewa majina mbali mbali kama vile uzazi wa majira, mpango wa familia, uzazi na malezi bora, na sasa kampeni hii imepewa jina Ia Elimu ya ngono (sex education) na Tanzania Elimu ya ngono hufundishwa mashuleni kwa jina Ia Elimu ya Afya na Uzazi.



Kwa vile tumemtaja Margaret Sanger kama mwanzilishi wa harakati za "bith control", ni vyema tumzungumzie kwa ufupi ili tupate kuelewa vyema uzito wa neno alilolizua.
Margret Sanger alizaliwa 1879 na kuolewa na William Sanger akiwa na umri kati ya miaka 20 na 25. Alijenga na kuitekeleza kwa vitendo dhana ya "mtu kuwa huru" kutembea na mwanamume yeyote anayemtaka. Alizikuza tamaa zake juu ya ngono na hivyo akawa kahaba mkubwa wa zama zake japo alikuwa kaolewa.



Yaonesha kuwa bwana William, kinyume na tabia ya mkewe, alikuwa ni mtu na heshima zake. Katika hatma ya mambo hakuwa na Ia kufanya ila kumwacha Margaret. Kwani kila alipojaribu kumsema juu ya uzinifu wake, Margret alimshauri mumewe naye azini.



Ndoa yake ya pili iliangukia kwa mume ambaye naye aliikubali dhana angamizi ya mtu kufanya zinaa apendavyo hata akiwa ndani ya ndoa. Na bwana huyu ndiye aliyezipa nguvu harakati za Margret za kampeni za kudhibiti uzazi.



Kiu ya Margret isiyokatika, na ulafi uliopindukia wa ngono, ulimfanya azini na wanaume wanne tofauti wakati yupo katika fungate ya ndoa yake ya pili. Huyo ndiye mwanzilishi wa sera ya kudhibiti uzazi:



Kwa mujibu wa Encyclopedia Britannica (1985) mojawapo ya sababu zilizopelekea kuenea kwa kampeni hii ni manufaa ya faida ya kibiashara iliyotokana na kuuza madawa au vifaa vya kuzuia mimba. Makampuni yanayotengeneza madawa hayo yalijikuta yanaingiza mamilioni ya dola. Hivyo, yakazidi kuitangaza biashara yao. Katika kuzivutia nchi changa, madawa hayo yamekuwa yakitolewa bure. Lakini sasa, baada ya kunogewa na sera hii, inabidi wasake madawa ya kuzuia mimba na magonjwa ya zinaa kwa bei mbaya.




                   






           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 406


Sponsored links
👉1 Kitau cha Fiqh     👉2 kitabu cha Simulizi     👉3 Madrasa kiganjani     👉4 Kitabu cha Afya    

Post zifazofanana:-

Maandalizi kwa ajili ya kifo
Mwanadamu anatakiwa aishi huku akikumbuka kuwa ipo siki atakufa. Hivyo basi inatupata lujiandaa mapema kwa ajili ya kifo. Soma Zaidi...

Kusimamisha Swala na kuamrisha mema
Swala iliyosimamishwa vilivyo ndiyo nyenzo kuu ya kumtakasa Muislamu na kumpa sifa zinazomuwezesha kustahiki kufanya kazi takatifu ya kusimamisha Uislamu katika jamii. Soma Zaidi...

Yajuwe mandalizi ya Ibada ya hija
Soma Zaidi...

Yaliyo haramu kwa mtu asiyekuwa na udhu
Post hii inakwenda kukufundisha kuhusu mambo ambauo ni haramu kwa mtu asiye na udhu. Soma Zaidi...

Hukumu ya Talaka kabla ya kufanya jimai
Talaka Kabla ya Jimai:Mwanamume au mwanamke anaweza kughairi na kuamua kuvunja ndoa mapema kabla ya kufanya tendo Ia ndoa. Soma Zaidi...

SHARTI ZA KUWAJIBIKA KWA ZAKA
Soma Zaidi...

kanunu na sheria za biashara katika islamu
Soma Zaidi...

Namna ya kujitwaharisha Najisi ndogo
Soma Zaidi...

Namna ya kutambuwa kibla na umuhimu wa kuelekea kibla wakati wa kuswali
4. Soma Zaidi...

Zijuwe funga za kafara na jinsi ya kuzigunga
Post hii itakufundisha kuhusu funga za kafara, zinavyotokea na na jinsi ya kuzifunga. Soma Zaidi...

Aina za swala..
Nguzo za uislamu,aina za swala (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Uzuri wa Benki za kiislamu
Kwa nini benki za kiislamu ni bora kuliko benki nyingine? Soma Zaidi...