picha

Kujitwaharisha najisi kubwa najisi ya mbwa na Nguriwe

Kujitwaharisha najisi kubwa najisi ya mbwa na Nguriwe

(b)Najisi Kubwa:



Najisi hii imeitwa kubwa kutokana na uzito unaochukuliwa katika kujitwah aris ha.
Namna ya kujitwaharisha kutokana na najisi ya mbwa na nguruwe ni kuikosha sehemu hiyo mara saba na mojawapo katika hayo makosho saba iwe kwa kusugua kwa udongo safi. Hivi ndivyo Mtume (s.a.w) alivyotufundisha kama inavyobainika katika Hadithi zifu atazo:



Abu Hurairah amesimulia kuwa Mtume (s.a.w) amesema: Kutw aharisha chombo cha yeyote kati yenu, baada ya kulambwa na mbwa ni kukikosha mara saba, ukitumia udongo katika safari ya kwanza. (Muslim)



Ibn Mughafal amesimulia kuwa Mtume (s.a.w) aliamuru kuuawa mbwa (wenye ugonjwa au wasio na waangalizi) kisha akaulizwa: β€œVipi juu ya mbwa wengine?” Kisha akaruhusu kufuga mbwa kwa ajili ya kuwindia, kuchungia (na ulinzi kwa ujumla) na akasema: Mbwa atakapolambachombo, kioshe mara saba na kisugue na udongo kwa mara ya nane”. (Muslim)



Hadithi hizi zinatupa msimamo wa Uislamu juu ya mbwa, ufugaji wake na namna ya kujitwaharisha kutokana na naye. Tumejifunza kuwa japo mbwa ni mnyama najisi tunaruhusiwa kumfuga kwa ajili ya kuwindia, na ulinzi wa nyumbani. Kama itabidi tufuge mbwa kwa ajili ya madhumuni haya, tutalazimika kuwafunza na kuwatayarishia makao yao yasiyohusiana na watu kwa malazi, chakula au ukaribu wowote.



Katika utafiti uliofanywa na Daktari mmoja huko Marekani (1978) iligundulika kuwa mbwa (na nguruwe) ni wachukuzi wa vijidudu vya magonjwa mbali mbali. Baadhi ya vijidudu hivyo havifi kwa dawa yoyote isipokuwa udongo




                   


Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 2018-08-01 Topic: Fiqh Main: Dini File: Download PDF Views 2799

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
πŸ‘‰1 Dua za Mitume na Manabii    πŸ‘‰2 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    πŸ‘‰3 kitabu cha Simulizi    πŸ‘‰4 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    πŸ‘‰5 web hosting    πŸ‘‰6 Bongolite - Game zone - Play free game   

Post zinazofanana:

Aina za twahara na aina za najisi

Katika post hii utakwenda kuzijuwa aina za twahara katika uislamu. Utaviona vigawanyo vya twahara kulingana na maulamaa wa Fiqh

Soma Zaidi...
Jinsi ya kumuosha maiti wa kiislami mwanaume au mwanamke

Post hii inakwenda kukufundisha hatuwa kwa hatuwa jinsi ya kumuosha maiti wa kiislamu

Soma Zaidi...
Kuwapa wanaostahiki

Nguzo za uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Maana ya sadaqat

Nguzo za imani, maana ya sadaqat (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Zaka ni nini? Nini maana ya zaka katika uislamu

Zaka, kilugha ni kukua; kubariki na kuzidi kheri.

Soma Zaidi...
Umuhimu wa funga ya ramadhan

Nguzo za uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Je ni kwa nini lengo la finga halifikiwi kwa wafungaji

Lengo la funga ni kuwa mchamungu sasa ni kwa nini wafungaji hawalifikii lengo hili na kuwa wachamungu.

Soma Zaidi...