Muislamu aliyetoa shahada ya kweli hanabudi kumfanya Mtume (s.
Muislamu aliyetoa shahada ya kweli hanabudi kumfanya Mtume (s.a.w) kuwa kiigizo chake kimwenendo na kitabia. Mtume (s.a.w) alikuwa na tabia njema kabisa kama tunavyofahamishwa katika Qur’an:
“Na bila shaka (Wewe Muhammad) una tabia njema kabisa.” (68:4) |
Mtume (s.a.w) mwenyewe amewahimiza waumini kujipamba na tabia njema kama tunavyojifunza katika Hadithi zifuatazo:
Abdullah bin Amr (r.a) ameeleza kuwa Mtume wa Allah amesema: “Aliye kipenzi changu kuliko wote katika nyinyi (Wa is lam u) ni yule aliyew azidi kwa tabia njema”. (Bukhari)
Harithat bin Wahab (r.a) ameeleza kuwa Mtume w a Allah amesema: “Yule ambaye tabia yake ni mbaya na katili, hataingia Peponi”. (Abu Daud)
Abu Hurairah (r.a) ameeleza kuw a Mtume w a Allah amesema: “Mw enye imani iliyopea katika Waislamu ni yule mwenye tabia njema, na aliye mbora katika nyinyi ni yule anayemtendea wema mkewe”. (Tirmidh)
Abu Darda (r.a) amesimulia kuwa Mtume (s.a.w) amesema: “Hapana kitu kitakachotia uzito katika m izani ya Muum ini katika siku ya hukum u kuliko tabia njema...” (Tirmidh)
Abu Hurairah (r.a) amesimulia kuwa Mtume (s.a.w) aliulizwa juu ya mambo yatakayopelekea watu wengi kuingia Peponi. Alijibu Mtume: “Uchaji - Mungu na tabia njema”. Kisha akaulizwa tena: “Ni mambo yepi yatakayompelekea m tu kuingizw a Motoni? ” Alijibu Mtum e, “Mdom o n a tup u (viungo vy a s iri)”. (Tirm idh)
Hivyo, muumini wa kweli hanabudi kujipamba na vipengele vya tabia njema vilivyoainishwa katika Qur-an na Sunnah. Katika juzuu hii
tumerejea vipengele vya tabia njema vifuatavyo:
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.
Download NowUmeionaje Makala hii.. ?
Post hii itakufundisha taratibu za kuajiri, kufanya kazi na malipo.
Soma Zaidi...Nguzo za uislamu, masharti ya utoaji wa zakat na sadaqat (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)
Soma Zaidi...Post hii inakwenda kukuelezea sifa za kuwa maamuma na taratibu za kumfuata imamu.
Soma Zaidi...Uchumi wa kiislamu unatofautiana sana na uchumi wa kikafiri. Hapa utajifunza tofauti hizo.
Soma Zaidi...Kabla ya kuhubiriwa uislamu watu wa Maka walikuwa na tarayibu zenye dhuluma ndani yake katika ugawaji wa mirathi.
Soma Zaidi...