picha

Nini maana ya Kushahadia nguzo ya kwanza ya uislamu

Nini maana ya Kushahadia nguzo ya kwanza ya uislamu

Kutoa Shahada Mbili

Kwa mujibu wa Hadith, tuliyoirejea katika utangulizi, nguzo ya kwanza ya Uislamu ni kutoa shahada mbili kwa kusema:



Ash hadu an laailaha illa llaahu wa ash hadu anna Muhammadar Rasuulu llahi

Tafsiri:

Nashuhudia kuwa hapana mungu ila Allah na ninashuhudia kuwa Muhammad ni Mtume wa Allah.

Shahada ndio kiingilio cha Uislamu. Yaani wasiokuwa Waislamu, wakiamua kuingia katika Uislamu, hukaribishwa na Waislamu kwa kutamkishwa hizi shahada mbili. Ukweli ni kwamba mtu hatakuwa Muislamu kwa kutamka tu haya maneno ya shahada bila ya kufahamu maana ya ndani.



Maana ya Shahada ya Kwanza:

“Nashuhudia kuwa hapana mola apasaye kuabudiwa kwa haki ila Allah”

Maana yake ni kwamba, huyu mja baada ya uchunguzi wa kina kwa kuzingatia dalili mbali mbali zinazodhihiri katika umbile la mbingu na ardhi na vyote vilivyomo, katika nafsi ya mwanaadamu, katika historia ya mwanaadamu, katika maisha ya Mitume na mafundisho yao, anayakinisha moyoni mwake kuwa yuko Mungu Muumba, Mpweke, Mwenye Uwezo juu ya kila kitu na Mmiliki wa kila kitu. Baada ya kuwa na yakini hii, huyu mja sasa anatoa ahadi kwa Allah(s.w) na kwa walimwengu wote kuwa, hatakuwa na mwingine yeyote atakaye muabudu au atakayemtii katika kukiendea kila kipengele cha maisha yake kinyume na Allah (s.w).Kwa maana nyingine mja anayetoa shahada hii, anaahidi kuwa ataendesha maisha yake yote ndani ya mipaka aliyowekewa na Allah (s.w) katika kukiendea kila kipengele cha maisha yake ya kibinafsi na kijamii. Yaani wenye kumshuhudia Allah kikweli ni wale wanaofuata Uislamu katika kila kipengele cha maisha yao kama Allah (s.w) anavyowaamrisha katika aya zifuatazo:



“Enyi Mlioamini! Ingieni katika Uislamu wote (katika hukumu zote za Uislamu) wala msifuate nyayo za Shetani, kwa hakika yeye kwenu ni adui aliye dhahiri”. (2:208).



“Enyi m lioam ini! Mcheni Mw enyezi Mungu kam a ipasavyo kum cha; w ala msife isipokuwa mmekwishakuwa Waislamu kamili”. (3:102).



 

Maana ya Shahada ya Pili

“Na ninashuhudia kuwa Muhammad ni Mtume wa Allah”

Hii ndio sehemu ya pili ya shahada ambayo huikamilisha shahada ya kwanza. Labda swali litaulizwa: “Kumshuhudia Mtume Muhammad (s.a.w) kunakamilishaje shahada ya kwanza?” Tumeona kuwa maana halisi ya kumshuhudia Allah (s.w) ni kumuabudu Allah pekee katika kila kipengele cha maisha yetu.Tutamuabudu vipi Allah (s.w) katika kila kipengele cha maisha yetu? Tutajuaje ni yepi aliyoyaharamisha Allah na yepi aliyoyahalalisha? Ni njia ipi tuifuate ili tupate radhi zake na ipi tuiepuke ili tuepukane na ghadhabu zake? Tutajuaje ipi njia sahihi na ipi potofu? Yote haya hatuwezi kuyajua mpaka tupate muongozo kutoka kwa Allah (s.w) mwenyewe.



Utaratibu aliouweka Allah (s.w) katika kuwaongoza wanaadamu ni kuwaleta Mitume miongoni mwa wanaadamu wanaume ambao huwaletea mwongozo na kuwafanya Waalimu wajuzi wenye hekima ili wawafundishe wanaadamu wenzao kinadharia na kimatendo juu ya Allah (s.w) na namna ya kumuabudu. Hivyo ili mja aweze kumjua Allah (s.w) na kumuamini ipasavyo na kisha aweze kumuabudu inavyostahiki katika kila kipengele cha maisha yake, hanabudi kwanza kumuamini Mtume na kufuata mafundisho yake. Kwahiyo, sisi watu wa Umma huu wa Mtume wa mwisho, hatuwezi kuwa Waumini wa kweli wa Allah (s.w) bila ya kumshuhudia Mtume Muhammad (s.a.w) kuwa ni Mtume wa Allah (s.w).



Kumshuhudia Muhammad (s.a.w) kuwa ni Mtume wa Allah (s.w), ni kutoa ahadi kuwa utafuata mafundisho ya Mtume (s.a.w) vilivyo kwa kutekeleza yale yote aliyoyaamrisha na kuacha yale yote aliyoyakataza na kumuigiza mwenendo na tabia yake kama inavyosisitizwa katika Qur’an:

“Sema ( Muhammad kuwaambia watu): ‘Ikiwa nyinyi mnampenda Mw enyezi Mungu, basi nifuateni; (hapo)Mwenyezi Mungu atakupendeni na atakughufirieni madhambi yenu.Na Mwenyezi Mungu ni mwenye Maghufira na Mwenye Rehema ”. (3:31)



“...Na anachokupeni Mtum e basi pokeeni na anachokukatazeni jiepusheni nacho. Na muogopeni Mw enyezi Mungu; kwa yakini Mwenyezi Mungu ni mkali wa kuadhibu”. (59:7)



“Bila shaka mnao mfano mw ema kw a Mtume wa Mw enyezi Mungu kw a mwenye kumuogopa Mwenyezi Mungu na siku ya Mwisho, na kumtaja Mwenyezi Mungu sana ”. (33:21)

Kwahiyo, Muumini anapotoa shahada mbili anaahidi kwa dhati ya moyo wake kuwa atamtii Allah(s.w) na Mtume Muhammad (s.a.w) kwa unyenyekevu kwa kukiendea kila kipengele cha maisha ya kibinafsi na ya kijamii kwa mujibu wa mwongozo wa Qur-an na Sunnah ya Mtume (s.a.w). Mtu hatakuwa Muumini pale atakapoendesha maisha yake ya kibinafsi au ya kijamii kinyume na shahada kama tunavyokumbushwa katika aya ifuatayo:



“Haiwi kwa mwanamume aliyeamini wala kwa mwanamke aliyeamini, Mwenyezi Mungu na Mtume wake w anapokata shauri,

w awe na hiari katika shauri lao. Na Mw enye kumuasi Mwenyezi Mungu na Mtume wake, hakika amepotea upotofu uliowazi.” (33:36).



                   

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 2018-08-01 Topic: Fiqh Main: Dini File: Download PDF Views 4782

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Bongolite - Game zone - Play free game    👉2 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    👉3 Dua za Mitume na Manabii    👉4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉5 web hosting    👉6 Kitabu cha Afya   

Post zinazofanana:

Jukumu la serikali katika kuzuia dhuluma

Serikali ina nafasi kubwa katika kuzuia dhulma na kufanya uchumibuwe huru kuyokana na dhulma.

Soma Zaidi...
Maana ya uadilifu na usawa na tofauti zao

Posti hii itakwenda kukufunza utofauti kati ya uadilifu na usawa

Soma Zaidi...
Jinsi ya kuswali swala ya kuoatwa kwa juwa ama swala ya kuoatwa kwa mwezi.

Post hii itakufundisha kuhusu swala ya kupatwa yaani kupatwa kwa juwa na kupatwa kwa mwezi swalat kusuf na swalat khusuf

Soma Zaidi...
Kutoa zakat

Nguzo za uislamu (EDK form 3:dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Jinsi ya kutwaharisha aina mbalimbali za najisi

Kila najisi ina namna yake ya kutwaharisha, hata hivyo namna hizo hufanana. Katika post hii utakwenda kujifunza jinsi ya kutwaharisha najisi mbalimbali.

Soma Zaidi...
Sifa za kuwa maamuma kwenye swala na namna ya kumfuata imamu

Post hii inakwenda kukuelezea sifa za kuwa maamuma na taratibu za kumfuata imamu.

Soma Zaidi...
Mgawanyo wa mirathi kutoka kwenye Quran

Quran imegawanya mirathi katika haki. Mgawanyo huu ndio unaotakiwa utumike na si vinhinevyo.

Soma Zaidi...
haki ya kutaliki: kuacha na kuachwa katika ndoa ya kiislamu

Haki ya KutalikiKatika jamii nyingi za kjahili haki ya kutoa talaka iko kwa mwanamume tu na mwanamke hana haki yoyote ya kumtaliki mumee.

Soma Zaidi...
Hukumu na sherei zinazohusu ajira na kazi katika uislamu

Wajibu wa KufanyakaziUislamu siyo tu unawahimiza watu kufanya kazi na kutokuwa wavivu bali kufanya kazi ni Ibada.

Soma Zaidi...
Je kama maiti imekatika baadhi ya viungo je viungo vyake tunafata utaratibu gani katika kumuosha na kumkafini?

Assalamu Alaykum Warahmatu-llah Wabarakaatuh Naomba kuuliza: Je kama maiti imekatika baadhi ya viungo je viungo vyake tunafata utaratibu gani katika kumuosha na kumkafini?

Soma Zaidi...