Home Afya Shule ICT Burudani Dini Maktaba Maswali Madrasa Apps Blog Legacy Login

KUZIKA-NAMNA YA KUZIKA HATUA KWA HATUA


image


Mambo ya faradh kwa maiti ya muislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)


Kuzika.

 

  • Kusindikiza jeneza.

-    Waislamu (watu) wataongozana nayo mpaka kaburini kimya kimya.

-    Jeneza lisitanguliwe na watu (msafara).

-    Haitakiwi watu kukaa kabla ya jeneza kukalishwa chini.

 

  • Kaburi.

-    Kaburi liwe pana na kina cha kutosha, mtu kuweza kusimama na kunyoosha mkono kama kuna uwezekano.

-    Kisha lichimbwe shimo dogo (mwana ndani) upande wa Qibla ndani ya kaburi.

-    Urefu na ukubwa wa kaburi unategemea na ukubwa wa maiti.

 

  • Namna ya Kuzika hatua kwa hatua.
  1. Waingie watu kaburini kwa idadi ya witiri; 3, 5, 7, n.k.
  2. Jeneza liwekwe upande wa kaburi itakapokuwa miguu ya maiti.
  3. Maiti itolewe na kutanguliza kichwa kuelekea kaburini.
  4. Wapokeaji kaburini watamuweka magotini mwao ili kufungua kamba kichwani, tumboni na miguuni. Pia watafunua shavu la kulia ili liguse ardhini (mchanga) atakapolazwa ndani ya mwana-ndani.

 

  1. Maiti italazwa katika mwana-ndani kwa ubavu wa kulia na kuelekezwa Qibla. Wakati wa kuilaza ni sunnah kusema, 

Kama ilivyosimuliwa na Ibn Umar (r.a) kuwa, Mtume (s.a.w) alipokuwa akizika alikuwa akisema: 

        “Bismillaah wabilahi wa’alaa millati Rasuulullaahi”         

        Tafsiri:

“Kwa jina la Allah na kwa uwezo wa Allah na kwa mujibu wa mwenendo wa Mtume wa Allah.” (Ahmad, Tirmidh, Ibn Majah).

 

  1. Maiti ipindishwe miguuni na kichwani ili uso na miguu iweze kugusa kuta za mwana-ndani. Kifua, tumbo na sehemu za katikati zibinuliwe nyuma kidogo.

 

  1. Maiti iwekewe mawe au udongo nyuma ya kichwa na miguu isibinuke. Pia ni sunnah kusoma aya za Qur’an (2:1-5) au (2:285-286).

 

  1. Baada ya maiti kulazwa na kusomewa aya hizi, ifunikwe kwa ubao na kama kuna matundu ya kupitisha udongo pazibwe kwa majani.

 

  1. Kabla kaburi halijafunikwa, vitupiwe viganja vitatu vya udongo, na kila tupo unasoma aya ya Qur’an (20:55).
    • Tupo la 1: “Min-haa khalaq-naakum” – Kutokana na hii (ardhi) tumekuumbeni.
    • Tupo la 2: “Wa fiyhaa nughiydukum” – Na humo (katika ardhi)                          tutakurudisheni.
    • Tupo la 3: “Wa min-haa nukhrjukum taaratan-ukhraa” – Na humo 

                      (katika ardhi) tutakutoweni mara nyingine.

 

  1. Kaburi lijazwe udongo mpaka lijae na kuinuliwa kiasi cha shiburi moja na kuwekewa alama miguuni na kichwani au kupanda miti mibichi.

-  Ni vizuri kumiminia maji juu yake ili kuepusha vumbi kupeperushwa na upepo.  

- Ni haramu kujengea kaburi kwa namna yeyote ile, kukaa juu   yake, kuwasha taa

   juu yake na kuielekea wakati wa kuswali.

‘Jabir (r.a) amesimulia kuwa Mtume wa Allah amekataza kuyajengea makaburi   au kuyajengea nyumba juu yake au kukaa juu yake’. (Muslim)

 

Abu Marsad Al-ghafariyyi ameeleza kuwa Mtume wa Allah amesema: 

     “Msikae juu ya makaburi na wala msiswali kwa kuyaelekea.” 

                    (Muslim)

 

        -  Baada ya kuzika Mtume (s.a.w) alikuwa akisimama na kusema: 

            “Muombeeni msamaha ndugu yenu na muombeeni awe

                na kauli thabiti kwani sasa anaulizwa”

 

        -  Ni sunnah baada ya mazishi kuwapa mikono wafiwa na kuwausia subira

            Rejea Qur’an (2:155-156).

        -  Pia haifai kusema (kusengenya) mabaya ya marehemu.



Sponsored Posts


  ðŸ‘‰    1 Magonjwa na afya       ðŸ‘‰    2 Jifunze fiqh       ðŸ‘‰    3 Maktaba ya vitabu       ðŸ‘‰    4 Madrasa kiganjani       ðŸ‘‰    5 Mafunzo ya html kwa kiswahili       ðŸ‘‰    6 ICT    


Je! una maswali, mapendekezo ama maoni? tuma ujumbe wa meseji SMS hapo chini ili kuunganishwa na muhusika au bofya hapa

SMS SMS

Imeandikwa na Tags Dini , DARSA , ALL , Tarehe 2022/01/02/Sunday - 03:05:23 pm     Share On facebook or WhatsApp Topic school Zaidi Dini AFYA ICT Burudani Tags Uzazi maswali Afya mengineyo dini HIV Sira vyakula Matunda HTML php Alif Lela 1 Alif Lela 2 FANGASI Dawa SQL Tips Quran Sunnah fiqh DARSA Magonjwa Tajwid tawhid simulizi Dua Academy Wahenga chemshabongo WAJUWA Michezo ICT Imesomwa mara 972



Post Nyingine


image Maadui wakubwa wa dola ya uislamu madinah
Dola ya uislamu madinah (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

image Mtazamo wa uislamu juu ya dini
Kwenye kipengele hichi tutajifunza mitazamo ya kikafiri juu ya dini. Soma Zaidi...

image Kumuamini mwenyezi Mungu (S.W)
Nguzo za imani (EDK form 2: elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

image Sanda ya mwanaume na namna ya kumkafini
Mambo ya faradh kwa maiti ya muislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

image Zoezi la 5
Maswali mbalimbali kuhusu fiqih Soma Zaidi...

image Faida (matunda) ya kusimamisha swala katika jamii
Nguzo za uislamu (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

image Haki za maadui katika vita (mateka wa kivita)
Haki na uadilifu katika uislamu (EDK form 3: Dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

image Maana ya zakat
Nguzo za uislamu,kutoa zakat na sadaqat (EDK form 2; dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

image Kukusanywa na kuhifadhiwa kwa quran
Quran (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

image Aina za hijjah
Nguzo za uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...