Mambo ya faradh kwa maiti ya muislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)
Kuzika.
- Waislamu (watu) wataongozana nayo mpaka kaburini kimya kimya.
- Jeneza lisitanguliwe na watu (msafara).
- Haitakiwi watu kukaa kabla ya jeneza kukalishwa chini.
- Kaburi liwe pana na kina cha kutosha, mtu kuweza kusimama na kunyoosha mkono kama kuna uwezekano.
- Kisha lichimbwe shimo dogo (mwana ndani) upande wa Qibla ndani ya kaburi.
- Urefu na ukubwa wa kaburi unategemea na ukubwa wa maiti.
Kama ilivyosimuliwa na Ibn Umar (r.a) kuwa, Mtume (s.a.w) alipokuwa akizika alikuwa akisema:
“Bismillaah wabilahi wa’alaa millati Rasuulullaahi”
Tafsiri:
“Kwa jina la Allah na kwa uwezo wa Allah na kwa mujibu wa mwenendo wa Mtume wa Allah.” (Ahmad, Tirmidh, Ibn Majah).
(katika ardhi) tutakutoweni mara nyingine.
- Ni vizuri kumiminia maji juu yake ili kuepusha vumbi kupeperushwa na upepo.
- Ni haramu kujengea kaburi kwa namna yeyote ile, kukaa juu yake, kuwasha taa
juu yake na kuielekea wakati wa kuswali.
‘Jabir (r.a) amesimulia kuwa Mtume wa Allah amekataza kuyajengea makaburi au kuyajengea nyumba juu yake au kukaa juu yake’. (Muslim)
Abu Marsad Al-ghafariyyi ameeleza kuwa Mtume wa Allah amesema:
“Msikae juu ya makaburi na wala msiswali kwa kuyaelekea.”
(Muslim)
- Baada ya kuzika Mtume (s.a.w) alikuwa akisimama na kusema:
“Muombeeni msamaha ndugu yenu na muombeeni awe
na kauli thabiti kwani sasa anaulizwa”
- Ni sunnah baada ya mazishi kuwapa mikono wafiwa na kuwausia subira
Rejea Qur’an (2:155-156).
- Pia haifai kusema (kusengenya) mabaya ya marehemu.
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.
Download NowJe umeipenda post hii ?
Post hiibinakwenda kukufundisha mambo ambayo yanaharibu udhu.
Soma Zaidi...Kwenye kipengele hichi tutajifinza vyanzo mbalimbali vya sheria ua kiislamu.
Soma Zaidi...Msimamo wa Uislamu juu ya kudhibiti uzaziKama tulivyoona, msukumo wa kampeni ya kudhibiti kizazi, umetokana na mfumo mbaya wa kijamii na kiuchumi ulioundwa na wanadamu kutokana na matashi yao ya ubinafsi.
Soma Zaidi...