picha

Kuzika-namna ya kuzika hatua kwa hatua

Mambo ya faradh kwa maiti ya muislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Kuzika.

 

-    Waislamu (watu) wataongozana nayo mpaka kaburini kimya kimya.

-    Jeneza lisitanguliwe na watu (msafara).

-    Haitakiwi watu kukaa kabla ya jeneza kukalishwa chini.

 

-    Kaburi liwe pana na kina cha kutosha, mtu kuweza kusimama na kunyoosha mkono kama kuna uwezekano.

-    Kisha lichimbwe shimo dogo (mwana ndani) upande wa Qibla ndani ya kaburi.

-    Urefu na ukubwa wa kaburi unategemea na ukubwa wa maiti.

 

  1. Waingie watu kaburini kwa idadi ya witiri; 3, 5, 7, n.k.
  2. Jeneza liwekwe upande wa kaburi itakapokuwa miguu ya maiti.
  3. Maiti itolewe na kutanguliza kichwa kuelekea kaburini.
  4. Wapokeaji kaburini watamuweka magotini mwao ili kufungua kamba kichwani, tumboni na miguuni. Pia watafunua shavu la kulia ili liguse ardhini (mchanga) atakapolazwa ndani ya mwana-ndani.

 

  1. Maiti italazwa katika mwana-ndani kwa ubavu wa kulia na kuelekezwa Qibla. Wakati wa kuilaza ni sunnah kusema, 

Kama ilivyosimuliwa na Ibn Umar (r.a) kuwa, Mtume (s.a.w) alipokuwa akizika alikuwa akisema: 

        “Bismillaah wabilahi wa’alaa millati Rasuulullaahi”         

        Tafsiri:

“Kwa jina la Allah na kwa uwezo wa Allah na kwa mujibu wa mwenendo wa Mtume wa Allah.” (Ahmad, Tirmidh, Ibn Majah).

 

  1. Maiti ipindishwe miguuni na kichwani ili uso na miguu iweze kugusa kuta za mwana-ndani. Kifua, tumbo na sehemu za katikati zibinuliwe nyuma kidogo.

 

  1. Maiti iwekewe mawe au udongo nyuma ya kichwa na miguu isibinuke. Pia ni sunnah kusoma aya za Qur’an (2:1-5) au (2:285-286).

 

  1. Baada ya maiti kulazwa na kusomewa aya hizi, ifunikwe kwa ubao na kama kuna matundu ya kupitisha udongo pazibwe kwa majani.

 

  1. Kabla kaburi halijafunikwa, vitupiwe viganja vitatu vya udongo, na kila tupo unasoma aya ya Qur’an (20:55).
    • Tupo la 1: “Min-haa khalaq-naakum” – Kutokana na hii (ardhi) tumekuumbeni.
    • Tupo la 2: “Wa fiyhaa nughiydukum” – Na humo (katika ardhi)                          tutakurudisheni.
    • Tupo la 3: “Wa min-haa nukhrjukum taaratan-ukhraa” – Na humo 

                      (katika ardhi) tutakutoweni mara nyingine.

 

  1. Kaburi lijazwe udongo mpaka lijae na kuinuliwa kiasi cha shiburi moja na kuwekewa alama miguuni na kichwani au kupanda miti mibichi.

-  Ni vizuri kumiminia maji juu yake ili kuepusha vumbi kupeperushwa na upepo.  

- Ni haramu kujengea kaburi kwa namna yeyote ile, kukaa juu   yake, kuwasha taa

   juu yake na kuielekea wakati wa kuswali.

‘Jabir (r.a) amesimulia kuwa Mtume wa Allah amekataza kuyajengea makaburi   au kuyajengea nyumba juu yake au kukaa juu yake’. (Muslim)

 

Abu Marsad Al-ghafariyyi ameeleza kuwa Mtume wa Allah amesema: 

     “Msikae juu ya makaburi na wala msiswali kwa kuyaelekea.” 

                    (Muslim)

 

        -  Baada ya kuzika Mtume (s.a.w) alikuwa akisimama na kusema: 

            “Muombeeni msamaha ndugu yenu na muombeeni awe

                na kauli thabiti kwani sasa anaulizwa”

 

        -  Ni sunnah baada ya mazishi kuwapa mikono wafiwa na kuwausia subira

            Rejea Qur’an (2:155-156).

        -  Pia haifai kusema (kusengenya) mabaya ya marehemu.

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 2022/01/02/Sunday - 03:05:23 pm Topic: Fiqh Main: Dini File: Download PDF Views 2288

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 ai web app    👉2 Kitau cha Fiqh    👉3 Dua za Mitume na Manabii    👉4 web hosting    👉5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉6 Tafasiri ya Riyadh Swalihina   

Post zinazofanana:

Ni upibutaratibu wa kuingia eda na kutoka eda

Katika uislamu hakuna sheria ya mwanamke kuingizwa eda na kutolewa eda kama ilivyozoeleka. Endelea na post hii ujifunze zaidi

Soma Zaidi...
Lengo la kusimamisha swala

Nguzo za uislamu (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Nguzo za uislamu

Katika kipengele hiki tutajifunza nguzo za uislamu.aina tano za nguzo za uislamu,dhana ya nguzo za uislamu,lengo na umuhimu wa nguzo za uislamu

Soma Zaidi...
Kutoa zakat

Nguzo za uislamu (EDK form 3:dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Sanda ya mwanamke na namna ya kumkafini

Mambo ya faradh kwa maiti ya muislamu (EDK form 2: Dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Haki za nafsi

Haki na uadilifu katika uislamu (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Jinsi ya kiswali swala ya tahajud na swala za usiku yaani qiyamu layl

Post hii itakujuza jinsi ya kiswali swala ya tahajudi. Pia utajifunza jinsi ya kuswali swala za usikubyaanibqiyamublayl

Soma Zaidi...
Sifa za imamu wa swala ya jamaa

Post hii inakwenda kukupa sifa za imamu wa msikitini anayepasa kuswalisha swala ya jamii.

Soma Zaidi...