Menu



Ni nini maana ya Talaka katika uislamu

Post hii inakwenda kukufundisha maana ya neno talaka katika uislamu kisheria na kilugha.

Maana ya Talaka
Talaka ni utaratibu wa kuvunja mkataba wa ndoa waliofunga mume na mke wakati wa kufunga ndoa mbele ya mashahidi wawili. Baada ya kuvunja mkataba huu kwa kufuata sharia ya Kiislamu, mwanamke aliyetalakiwa huwa huru kuolewa na mume mwingine.

 


Talaka katika Uislamu
Talaka katika Uislamu si jambo Ia kupendeza. Kwa hiyo mume na mke wanatakiwa wajitahidi kusuluhishana na kuvumiliana iii hatua ya kupeana talaka isifikiwe.


Talaka ni jambo Ia halali hub ruhusiwa inapokuwa hapana budi na wala Si jambo Ia kuhifanyia mas-khara kama tunavyojifunza katika Hadith zifuatazo:

 


Ibn Umar amesimulia kuwa Mtume wa Mwenyezi Mungu amesema: "Katika halali inayochukiza mbele ya Mwenyezi Mungu (s.w) ni talaka ". (Abu Daud).

 


Kwa upande mwingine, kama Mwenyezi Mungu (s.w) angahiharamisha talaka, hali ya maisha ingahikuwaje katika famihia zile ambazo mume na mke wamekosana kiasi cha kila mmoja kutotaka kumuona mwenziwe! Kwa hiyo, mume au mke atakapofanya kosa au makosa makubwa yasiyovumihika kwa mwenziwe, Mwenyezi Mungu (s.w) ametoa ruhusa wapeane talaka na kuachana kwa wema na mapenzi kama inavyosisitizwa katika Qur-an:

 

Talaka (za kuweza kurejeana) ni mara mbili. Kisha ni kumuweka kwa wema au kumwacha kwa ihsani ... ". (2:229). Na mtakapowapa wanawake talaka nao wakafikia kumaliza eda yao, basi warejeeni kwa wema au tokaneni nao kwa wema... (2:231). Basi wanapofikia muda wao, ima warejeeni kwa wema, au farikianeni nao kwa wema... (65:2).

 


Kwakuwa ndoa ni mkataba waliowekeana mume na mke wa kuishi kwa wema na kuachana kwa wema ikibidi kuachana, hapana sababu kabisa ya kujenga chuki na uhasama kati ya wawili hawa kwa sababu tu eti wanashindwa kuuendeleza mkataba wao. Katika aya hizi tunaamrishwa kuvunja mkataba huu kwa wema kwa kufuata utaratibu aliouweka Mwenyezi Mungu (s.w) na baada ya hapo kila mmoja kuwa huru.

 

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass

Nyuma Endelea

Ndio     Hapana     Save post
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Fiqh Main: Post File: Download PDF Views 1565

Share On:

Facebook WhatsApp

Post zinazofanana:

Dhana ya haki na uadilifu katika uislamu

Haki na uadilifu katika uislamu (EDK form 3:dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Wanaostahiki kupewa zakat

Nguzo za uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Maana ya hadathi na aina zake

Post hii inakwenda kukugundisha maana ya hadathi pamoja na kutaja aina za hadathi

Soma Zaidi...
Jinsi ya kujitwaharisha kutokana na najisi

Post hii inakwenda kukufundisha jinsi ya kujitwaharisha kutokana na najisi.

Soma Zaidi...
Kwanini wengi wanaoswali hawafikii lengo la swala zao

Nguzo za uislamu (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...