Lengo la Funga
Lengo la funga limebainishwa katika Qur-an pale ilipotolewa amri ya kufunga:
โEnyi mlioamini! Mmeamrishwa kufunga kama walivyoamrishwa waliokuwa kabla yenu ili mpate kumcha Mungu โ. (2:183)
Hapa tunabainishwiwa kuwa lengo la kufunga ni kuwafanya Waumini kuwa wacha-Mungu. Neno โTaqwa โ ambalo linatafsiriwa kuwa ni โUchamunguโ lina maana pana zaidi. โTaqwaโ ni hali ya kuhofu ghadhabu za Mwenyezi Mungu (s.w) ambayo humfanya mja ajiepushe mbali na yale yote yanayomghadhibisha Mwenyezi Mungu (s.w) na ayaendee mbio kwa unyenyekevu na kwa jitihada kubwa yale yote aliyoamrisha Mwenyezi Mungu (s.w) na yale yote anayoyaridhia. Maana ya โTaqwaโ inabainishwa vyema na Hadith ifuatayo:
Siku moja Umar (r.a) alimuuliza Ubbay bin Ka โb (r.a) amueleweshe maana hasa ya Taqwa. Ubbay (r.a) alijibu: โAmir Muuminin, umewahi kupita njia ya kichaka chenye miba?โ Umar (r.a) akajibu: โNaam, nimepita mara nyingiโ Kisha Ubbay (r.a) akamuuliza ni hadhari gani uliyoichukua wakati ukipita huko? โNilishikilia na kukusanya pamoja nguo zangu na kutembea kwa uangalifu katika kupita njia hiyoโ, alisema Umar (r.a) ili sehemu yoyote ya nguo zangu isije shikwa na miba hiyoโ. Kutokana na jibu hili, Ubbay (r.a) alisema: โHii hasa ndio maana ya โTaqwaโ.
Kutokana na mfano huu mtu mwenye โTaqwaโ au Muttaq ni yule mwenye shauku na jitihada kubwa kuepukana na kila aina ya mwiba (uovu) katika kila hatua na kila kipengele cha maisha yake yote na wakati huo huo huwa na shauku na jitihada kubwa ya kuyakimbilia mema katika kila hatua ya maisha yake ili kupata radhi za Mwenyezi Mungu (s.w). Muttaq ni mtu mwenye cheo na hadhi kubwa sana mbele ya Mwenyezi Mungu (s.w) kama tunavyofahamishwa katika Qur-an:
โ... Hakika aheshimiwaye sana miongoni mwenu mbele ya Mwenyezi Mungu ni yule aliye Muttaq (am chaye Mw enyezi Mungu zaidi) katika nyinyi. Kw a yakini Mwenyezi Mungu ni Mjuzi Mw enye khabari ya mambo yote. (49:13).
Hiki ni cheo kikubwa sana ambacho hakina mfano wake katika vyeo vya hapa ulimwenguni. Cheo hiki hakipatikani kwa kuomba kura au kwa hongo, bali kinapatikana kwa kujizatiti kujiepusha na makatazo yote ya Mwenyezi Mungu (s.w) na kujitahidi kutenda mema na kutekeleza maamrisho yote ya Mwenyezi Mungu (s.w) kwa matarajio ya kupata Radhi ya Mwenyezi Mungu (s.w).
Umeionaje Makala hii.. ?
Kwa nini ni muhimu kuswali? Post hii itakwenda kukufundisha kuhusu umuhimu wa kusimamisha swala.
Soma Zaidi...Post hii inakwenda kukufundisha sunnah 9 za swala. Sunnah hizi ni zile ambazo ukiziwacha swala yako haibatiliki.
Soma Zaidi...Ugawaji wa mirathi-Mume ana nusu (1/2) = 1/2 -Mama ana sudusi.
Soma Zaidi...ุนููู ุฃูุจูู ุนูุจูุฏู ุงูููููู ุงููููุนูู ูุงูู ุจููู ุจูุดููุฑู ุฑูุถููู ุงูููููู ุนูููููู ูุงุ ููุงูู: ุณูู ูุนูุช ุฑูุณูููู ุงูููููู ุตูู ุงููู ุนููู ู ุณูู ูููู?...
Soma Zaidi...