UISLAMU UNAVYOKEMEA TABIA YA OMBAOMBA


image


Uislamu umekataza tabia ya kuombaomba kama ndio njia ya kuendesha maisha. Pia ukaweka suluhisho la kukomesha tabia hiyo


5

Suala la omba-omba
Tukiliangalia suala la omba-omba kwa upana kidogo, ambalo hivi sasa linaongelewa katika vikao mbalimbali vya kitaifa na kimataifa, tutaona kuwa ni Uislamu pekee unaotoa namna bora ya kulishughulikia suala hili. Omba omba ni kitendo kibaya sana kikiwa kimefanywa na mtu binafsi au taifa na kinashusha hadhi ya mtu binafsi na hadhi ya taifa kwa ujumla. Hivyo Uislamu ambao ndio njia sahihi pekee ya maisha, hauwezi kamwe ukapalilia omba omba na wala Zaka na sadaka kazi yake si kupalilia omba-omba, bali kinyume chake zaka na sadaka ni miongoni mwa silaha zinazotumiwa kutokomeza omba omba. Uislamu unawashutumu vikali omba omba kama tunavyojifunza katika Hadithi ifuatayo:

 


Hubshi bin Junadah ameeleza kuwa Mtume wa Al-lah amesema: Kuomba-omba si halali kwa mwenye uwezo wala kwa mwenye uzima wa afya na mwenye nguvu (za kufanya kazi) ila kwa mwenye kupigwa ufakiri na mw enye deni kubw a (asilow eza kulilipa). Na yule anayeomba watu ili ajiongezee mali yake atakuwa na mkwaruzo usoni mwake katika siku ya Kiyama na atayala kwa ulafi mkubwa mawe ya moto kutoka motoni. Kwa hiyo anayetaka, mwache aombe kidogo, n a m w ache a om be k ingi. (Tirm idh)

 


Wanaoruhusiwa kuomba kwa mujibu wa Hadith ni:
(i)Mtu aliyesimama kumdhamini mtu mwingine ili kuleta suluhu kati ya wagomvi wawili. huyu anaruhusiwa kuomba hata akiwa tajiri. Kwa mnasaba huu, waumini wa misikitini, madarasa, na shughuli mbali mbali za Kiislamu wanaruhusiwa kuomba michango ya Waislamu ili kufanikisha shughuli hizo.

 


(ii)Mtu aliyepata ajali na kuharibikiwa kabisa na vitu vyake vyote kama vile ajali ya moto, mafuriko, nakadhalika.

 


(iii)Mtu ambaye amepigwa na ufakiri na amekosa kabisa mahitaji muhimu ya maisha kama vile chakula, malazi na makazi, lakini mtu akiwa na angalau chakula cha siku moja na malazi mkononi mwake haruhusiwi kuomba kama tunavyofahamishwa katika Hadithi zifu atazo:

 


Abdullah bin Mas ’ud ameeleza kuwa Mtume wa Al-lah amesema: Anayeomba omba watu na ilhali ana mahitaji muhimu ya maisha atakuja siku ya Kiyama na mikwaruzo, vidonda au majeraha usoni mwake. Iliulizwa: Ee Mtume wa Allah! Ni kiasi gani kinachomtosha mtu? Akajibu: Dirham 50 au thamani yake. (Abu Daud, Tirmidh, Nisai, Ibn Majah).

 


Sahl bin Haohaliyya ameeleza kuwa Mtume wa Al-lah amesema:Yeyote yule anayeomba na ilihali anajitosheleza kwa mahitaji muhimu, anaomba moto (Jahannam). Nufaili ambaye ni miongoni mwa wasimulizi wa Hadithi hii katika sehemu nyingine aliuliza: Ni yupi mwenye uwezo ambaye kuomba ni haramu? Alijibu (Mtume s.a.w.): Yule mwenye uwezo wa kupata chakula cha asubuhi na usiku. Mahali pengine amesema: Yule mwenye chakula cha siku moja (usiku na mchana) (Abu Daud).
Hivyo ikibidi mtu aombe, basi aombe kwa sababu hizo tatu zilizotajwa katika Hadithi hii. Kuomba omba bila ya sababu za msingi kumeharamishwa kwa sababu kuu tatu zifu atazo:

 


(i)Kuomba omba kunamfanya mtu apoteze moyoni mwake ile hali ya kumtegemea Allah (s.w.) na atajenga moyoni mwake hali ya kulalamika juu ya neema za Allah zilizomzunguka kila mahali. Kwa msingi huu hatima ya kuomba omba ni kumfanya mja awategemee wengine kwa mahitajio yake badala ya kumtegemea Allah (s.w.) na kumfanya ashindwe kushukuru neema za Allah (s.w.).

 


(ii)Kuomba omba humfanya mtu awe mnyonge na ajidhalilishe kwa wengine ambapo Muislamu anatakiwa ajidhalilishe kwa Allah (s.w.) peke yake.

 


(iii)Vile vile kuomba omba kumekatazwa kwa sababu kunamuweka yule anayeombwa katika hali ngumu. Wakati mwingine anayeombwa hali yake si nzuri vile vile lakini kwa kuombwa hulazimika kutoa jambo ambalo linaweza kumuathiri yeye na wale anaowaangalia. Uislamu haukuishia kwenye kukemea tu tabia ya omba omba bali umetoa njia za kutatua tatizo hili kama ifu atavyo:

 


(i)Kuwasaidia wale wote wenye matatizo na dhiki mbali mbali kwa kuwapa Sadaqa na zakati kabla hawajaomba.

 

(ii)Njia ya pili, ya kukomesha kuomba omba ni kujitegemea kwa kufanya kazi kwa kutumia juhudi na maarifa.

 



Sponsored Posts


  ðŸ‘‰    1 Mafunzo ya php       ðŸ‘‰    2 Magonjwa na afya       ðŸ‘‰    3 Hadiythi za alif lela u lela       ðŸ‘‰    4 Jifunze fiqh       ðŸ‘‰    5 Mafunzo ya html kwa kiswahili       ðŸ‘‰    6 Madrasa kiganjani    


Je! una maswali, mapendekezo ama maoni? tuma ujumbe wa meseji SMS hapo chini ili kuunganishwa na muhusika au bofya hapa

SMS SMS



Post Nyingine


image Kwa nini imefaradhishwa kufunga mwezi wa Ramadhani
Unaweza kijiuliza ni kwa nini hasa kimepelekea kufaradhishwa kufunga mwezi wa Ramadhani. Soma Zaidi...

image Namna ya kutawadha yaani kuchukuwa udhu
Kuchukuwavudhu ni ibada, lakini pia ni matendo ya kuufanya mwilivuwe safi. Katika post nitakwenda kukifundisha namna ya kutia udhu katika uislamu. Soma Zaidi...

image Uislamu unavyokemea tabia ya ombaomba
Uislamu umekataza tabia ya kuombaomba kama ndio njia ya kuendesha maisha. Pia ukaweka suluhisho la kukomesha tabia hiyo Soma Zaidi...

image Umuhimu wa uchumi katika uislamu
Post hii itakufundisha faida na umuhimu wa kijenga uchumi katika jamii ya kiislamu. Soma Zaidi...

image Uzuri wa Benki za kiislamu
Kwa nini benki za kiislamu ni bora kuliko benki nyingine? Soma Zaidi...

image Taratibi za malezi ya watoto wadogo baada ya talaka katika uislamu
Endapo mke na mume wameachana na hali ya kuwa mke ana watoto wachanga. Je uislamu unasemaje kuhusu taratibu za malezi? Soma Zaidi...

image Mambo yanayobatilisha funga au yanayoharibu swaumu.
Hapa utajifunza mambo ambayo akiyafanya mtu aliyefunga, basi funga yake itaharibika. Soma Zaidi...

image Swala ya jamaa na taratibu zake
Post hii inakwenda kukufundisha kuhusu swala ya jamaa na taratibu zake. Soma Zaidi...

image Je mahari inashusha hadhi ya mwanamke katika jamii
Unadhani mwanamke kupewa mahari kitendo hiki kinaweza kushusha hadhi yake? Soma Zaidi...

image Taratibu za kuchaguwa mchumba katika uislamu
Hapa utajifunza hatuwa kwa hatuwa za kuchaguwa mchumba kulingana na sheria za kiislamu. Soma Zaidi...