Maswali juu ya Nguzo za uislamu
Nguzo za uislamu (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu)
Zoezi la 4.
(a) Ni upi mtazamo wa Uislamu juu ya maada ya ibada?
(b) Ni lipi malengo ya ibada maalumu?
(a) Swala katika Uislamu ina umuhimu gani?
(b) Kwa ushahidi wa aya ainisha lengo kuu la swala.
(c) Bainisha jinsi lengo la swala linavofikiwa kwa mwenye kuswali.
(a) Dhihirisha matunda ya kusimamisha ibada ya swala kikamilifu.
(b) Tofautisha baina ya kuswali na kusiamamisha swala.
Kwa hakika swala ikiswaliwa vilivyo humuepusha mwenye kuswali na mambo machafu na maovu (29:45).
Toa sababu tano ni kwa nini waislamu pamoja na kuswali kwao mara tano kwa siku hawajapata matunda ya swala zao?
(a) Eleza maana ya zakat kilugha na kisheria.
(b) Bainisha nafasi ya Zakat katika Uislamu.
(c) Fafanua lengo la Zakat na jinsi linavyofikiwa.
Pamoja na waislamu wachache kutoa Zakat, lakini matunda yake hayaonekani katika jamii.
Bainisha sababu zinazopelekea kukosekana matunda ya Zakat ndani ya jamii.
(a) Eleza maana ya swaumu kilugha na kisheria.
(b) Ni upi umuhimu na nafasi ya funga kwa muislamu?
Kwa ushahidi wa aya, bainisha lengo la funga na onesha jinsi linavyofikiwa na mfungaji.
(a) Onesha zinazopatikana kutokana na funga ya mwezi wa Ramadha.
(b) Mmefaradhishiwa kufunga kama walivyofaradhishiwa wale waliokuwa kabla yenu (2:183).
Toa sababu zinazoonyesha funga ya mwezi wa Ramadhan kufaradhishwa katika mwezi huo.
Wengi wafungao mwezi wa Ramadhan hawafikii malengo ya fungo zao. Unafikiri ni kwa nini?
(a) Ni ipi maana ya Hijja kilugha na kisheria.
(b) Hijja ni ibada ya muda maalumu. Fafanua miezi ya Hijjah na tarehe ambayo ibada za Hijja huanza rasmi huko Makkah.
Toa mafunzo yatokanayo na vitendo vya ibada ya Hijjah vifuatavyo:
(i) Tawafu (ii) Sai (iii) Kisimamo cha Arafa (iv) Kupiga kambi Mina
(v) Kutupa mawe (vi) Kuchinja mnyama.
(a) Ni lipi lengo kuu la ibada ya Hijjah au Umrah?
(b) Bainisha sababu tano, pamoja na waislamu kukusanyika mamilioni kila mwaka katika mji wa Makkah kwa ajili ya Hijjah, bado matunda yake hayaonekani katika jamii.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Dua za Mitume na Manabii 👉2 web hosting 👉3 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉4 Kitabu cha Afya 👉5 Madrasa kiganjani 👉6 Tafasiri ya Riyadh Swalihina
Post zinazofanana:
Je kama maiti imekatika baadhi ya viungo je viungo vyake tunafata utaratibu gani katika kumuosha na kumkafini?
Assalamu Alaykum Warahmatu-llah Wabarakaatuh Naomba kuuliza: Je kama maiti imekatika baadhi ya viungo je viungo vyake tunafata utaratibu gani katika kumuosha na kumkafini?
Soma Zaidi...Hadathi ya kati na kati
Posti hiibinakwenda kukufundisha kuhusu hadathi ya kati na kati.
Soma Zaidi...Mambo yanayobatilisha funga au yanayoharibu swaumu.
Hapa utajifunza mambo ambayo akiyafanya mtu aliyefunga, basi funga yake itaharibika.
Soma Zaidi...Kiasi cha mahari kilicho bora kinachofaaa katika uislamu
Uislamu haukuwekabkiwango maalumu cha mahari. Mwanamke anaweza tajabkiasi atakacho. Ila vyema kuzingatia haya wakayi wa kutamka mahari yako.
Soma Zaidi...Dhamana ya Kuchunga Ahadi Katika Uislamu
Kuchunga au kutekeleza ahadi ni miongoni mwa vipengele muhimu vya tabia ya muumini wa kweli.
Soma Zaidi...Mda wa mwisho wa kula daku mwezi wa ramadhani
Post hii fupi itakwenda kukujulisha utaratibu wa kula daku.
Soma Zaidi...