Maswali juu ya Nguzo za uislamu


image


Nguzo za uislamu (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu)


Zoezi la 4.

(a)  Ni upi mtazamo wa Uislamu juu ya maada ya ibada?

(b)  Ni lipi malengo ya ibada maalumu?

(a)  Swala katika Uislamu ina umuhimu gani?

(b)  Kwa ushahidi wa aya ainisha lengo kuu la swala.

(c)  Bainisha jinsi lengo la swala linavofikiwa kwa mwenye kuswali.

(a)  Dhihirisha matunda ya kusimamisha ibada ya swala kikamilifu.

(b)  Tofautisha baina ya kuswali na kusiamamisha swala.

Kwa hakika swala ikiswaliwa vilivyo humuepusha mwenye kuswali na mambo machafu na maovu (29:45).

Toa sababu tano ni kwa nini waislamu pamoja na kuswali kwao mara tano kwa siku hawajapata matunda ya swala zao?

 

(a)  Eleza maana ya zakat kilugha na kisheria.

(b)  Bainisha nafasi ya Zakat katika Uislamu.

(c)  Fafanua lengo la Zakat na jinsi linavyofikiwa.

Pamoja na waislamu wachache kutoa Zakat, lakini matunda yake hayaonekani katika jamii.  

Bainisha sababu zinazopelekea kukosekana matunda ya Zakat ndani ya jamii.

(a)  Eleza maana ya swaumu kilugha na kisheria.

(b)  Ni upi umuhimu na nafasi ya funga kwa muislamu?

Kwa ushahidi wa aya, bainisha lengo la funga na onesha jinsi linavyofikiwa na mfungaji.

(a)  Onesha zinazopatikana kutokana na funga ya mwezi wa Ramadha.

(b) Mmefaradhishiwa kufunga kama walivyofaradhishiwa wale waliokuwa kabla yenu (2:183).

Toa sababu zinazoonyesha funga ya mwezi wa Ramadhan kufaradhishwa katika mwezi huo.

 

Wengi wafungao mwezi wa Ramadhan hawafikii malengo ya fungo zao. Unafikiri ni kwa nini?

 

(a)  Ni ipi maana ya Hijja kilugha na kisheria.

(b)  Hijja ni ibada ya muda maalumu. Fafanua miezi ya Hijjah na tarehe ambayo ibada za Hijja huanza rasmi huko Makkah.

 

Toa mafunzo yatokanayo na vitendo vya ibada ya Hijjah vifuatavyo:

  (i)  Tawafu   (ii)  Sai  (iii)  Kisimamo cha Arafa  (iv)  Kupiga kambi Mina 

  (v)  Kutupa mawe  (vi)  Kuchinja mnyama.

 

(a) Ni lipi lengo kuu la ibada ya Hijjah au Umrah?

(b) Bainisha sababu tano, pamoja na waislamu kukusanyika mamilioni kila mwaka katika mji wa Makkah kwa ajili ya Hijjah, bado matunda yake hayaonekani katika jamii.



Sponsored Posts


  ðŸ‘‰    1 Tunakukaribisha kwenye Maktaba yetu       ðŸ‘‰    2 Download App zetu hapa ujifunze zaidi       ðŸ‘‰    3 Madrasa kiganjani offline       ðŸ‘‰    4 Jifunze Fiqh    


Je una maswali, maoni ama ushauri, tutumie sms ✉ bofya hapa hapa, ama wasiliana nasi kwa WhatsApp bofya hapa



Post Nyingine


image Mambo muhimu anayofanyiwa muislamu kabla ya kufa
Dhana ya faradh kwa muislamu (EDK form 2:dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

image Elimu yenye manufaa
Elimu yenye manufaa Ni ipi? (EDK form 1:elimu yenye manufaa) Soma Zaidi...

image Kutoa vilivyo halali
Nguzo za uislamu (EDK form 2:dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

image Madhumuni ya dola ya uislamu
Dola ya uislamu madinah (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

image Kwanini wengi wanaoswali hawafikii lengo la swala zao
Nguzo za uislamu (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

image Athari za kumuamini mwenyezi Mungu katika maisha ya kila siku
Nguzo za imani (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

image Maswali juu ya dini anayostahiki kufuata mwanadamu
Dini anayostahiki kufuata mwanadamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

image Kwanini funga imefaradhishwa mwezi wa ramadhani
Nguzo za uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

image Makundi ya dini za wanaadamu
Kwenye kipengele hichi tutajifunza makundi ya dini za watu. Na makundi hayo ni matatu. Soma Zaidi...

image Kuanzishwa kwa dola ya kiislamu madinah
Dola ya kiislamu madinah (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...