picha

Maswali juu ya Nguzo za uislamu

Nguzo za uislamu (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu)

Zoezi la 4.

(a)  Ni upi mtazamo wa Uislamu juu ya maada ya ibada?

(b)  Ni lipi malengo ya ibada maalumu?

(a)  Swala katika Uislamu ina umuhimu gani?

(b)  Kwa ushahidi wa aya ainisha lengo kuu la swala.

(c)  Bainisha jinsi lengo la swala linavofikiwa kwa mwenye kuswali.

(a)  Dhihirisha matunda ya kusimamisha ibada ya swala kikamilifu.

(b)  Tofautisha baina ya kuswali na kusiamamisha swala.

Kwa hakika swala ikiswaliwa vilivyo humuepusha mwenye kuswali na mambo machafu na maovu (29:45).

Toa sababu tano ni kwa nini waislamu pamoja na kuswali kwao mara tano kwa siku hawajapata matunda ya swala zao?

 

(a)  Eleza maana ya zakat kilugha na kisheria.

(b)  Bainisha nafasi ya Zakat katika Uislamu.

(c)  Fafanua lengo la Zakat na jinsi linavyofikiwa.

Pamoja na waislamu wachache kutoa Zakat, lakini matunda yake hayaonekani katika jamii.  

Bainisha sababu zinazopelekea kukosekana matunda ya Zakat ndani ya jamii.

(a)  Eleza maana ya swaumu kilugha na kisheria.

(b)  Ni upi umuhimu na nafasi ya funga kwa muislamu?

Kwa ushahidi wa aya, bainisha lengo la funga na onesha jinsi linavyofikiwa na mfungaji.

(a)  Onesha zinazopatikana kutokana na funga ya mwezi wa Ramadha.

(b) Mmefaradhishiwa kufunga kama walivyofaradhishiwa wale waliokuwa kabla yenu (2:183).

Toa sababu zinazoonyesha funga ya mwezi wa Ramadhan kufaradhishwa katika mwezi huo.

 

Wengi wafungao mwezi wa Ramadhan hawafikii malengo ya fungo zao. Unafikiri ni kwa nini?

 

(a)  Ni ipi maana ya Hijja kilugha na kisheria.

(b)  Hijja ni ibada ya muda maalumu. Fafanua miezi ya Hijjah na tarehe ambayo ibada za Hijja huanza rasmi huko Makkah.

 

Toa mafunzo yatokanayo na vitendo vya ibada ya Hijjah vifuatavyo:

  (i)  Tawafu   (ii)  Sai  (iii)  Kisimamo cha Arafa  (iv)  Kupiga kambi Mina 

  (v)  Kutupa mawe  (vi)  Kuchinja mnyama.

 

(a) Ni lipi lengo kuu la ibada ya Hijjah au Umrah?

(b) Bainisha sababu tano, pamoja na waislamu kukusanyika mamilioni kila mwaka katika mji wa Makkah kwa ajili ya Hijjah, bado matunda yake hayaonekani katika jamii.

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 2022/01/18/Tuesday - 07:28:30 pm Topic: Fiqh Main: Dini File: Download PDF Views 2951

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉2 Kitabu cha Afya    👉3 ai web app    👉4 Bongolite - Game zone - Play free game    👉5 kitabu cha Simulizi    👉6 Dua za Mitume na Manabii   

Post zinazofanana:

Njia za kujitwaharisha, na vitu vinavyotumika kujitwaharisha

Post hii inakwenda kukufundisha njia zinazotumika kujitwaharisha.

Soma Zaidi...
NI ZIPI SWALA ZA SUNNAH: (qabliya (kabliya) na baadiya, tahajudi, tarawehe, qiyamu layl, shukr, istikhara)

Sunnah za SwalaSunnah za Swala Vipengele vya sunnah katika swala ni vile ambavyo mwenye kuswali akivitenda husaidia sana kukuza daraja ya swala yake na kuipa nguvu na msukumo mkubwa wa kuiwezesha kufikia lengo lililokusudiwa kwa urahisi zaidi.

Soma Zaidi...
Vipi utapata uchamungu kupitia funga

Vipi lengo la funga litafikiwa na kumfanya mfungaji awe mchamungu.

Soma Zaidi...
Yaliyo haramu kwa mtu asiyekuwa na udhu

Post hii inakwenda kukufundisha kuhusu mambo ambauo ni haramu kwa mtu asiye na udhu.

Soma Zaidi...
Ni ipi hukumu ya kutoa talaka hali ya kuwa umelazimishwa au ukiwa umerukwa na akili

Endapo mtu atamuacha mke pasi na ridhaa yake yaani amelazimishwa ama amemuwacha wakati amerukwa na akili. Je ni ipo hukumu yake.

Soma Zaidi...