Maswali juu ya Nguzo za uislamu

Nguzo za uislamu (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu)

Zoezi la 4.

(a)  Ni upi mtazamo wa Uislamu juu ya maada ya ibada?

(b)  Ni lipi malengo ya ibada maalumu?

(a)  Swala katika Uislamu ina umuhimu gani?

(b)  Kwa ushahidi wa aya ainisha lengo kuu la swala.

(c)  Bainisha jinsi lengo la swala linavofikiwa kwa mwenye kuswali.

(a)  Dhihirisha matunda ya kusimamisha ibada ya swala kikamilifu.

(b)  Tofautisha baina ya kuswali na kusiamamisha swala.

Kwa hakika swala ikiswaliwa vilivyo humuepusha mwenye kuswali na mambo machafu na maovu (29:45).

Toa sababu tano ni kwa nini waislamu pamoja na kuswali kwao mara tano kwa siku hawajapata matunda ya swala zao?

 

(a)  Eleza maana ya zakat kilugha na kisheria.

(b)  Bainisha nafasi ya Zakat katika Uislamu.

(c)  Fafanua lengo la Zakat na jinsi linavyofikiwa.

Pamoja na waislamu wachache kutoa Zakat, lakini matunda yake hayaonekani katika jamii.  

Bainisha sababu zinazopelekea kukosekana matunda ya Zakat ndani ya jamii.

(a)  Eleza maana ya swaumu kilugha na kisheria.

(b)  Ni upi umuhimu na nafasi ya funga kwa muislamu?

Kwa ushahidi wa aya, bainisha lengo la funga na onesha jinsi linavyofikiwa na mfungaji.

(a)  Onesha zinazopatikana kutokana na funga ya mwezi wa Ramadha.

(b) Mmefaradhishiwa kufunga kama walivyofaradhishiwa wale waliokuwa kabla yenu (2:183).

Toa sababu zinazoonyesha funga ya mwezi wa Ramadhan kufaradhishwa katika mwezi huo.

 

Wengi wafungao mwezi wa Ramadhan hawafikii malengo ya fungo zao. Unafikiri ni kwa nini?

 

(a)  Ni ipi maana ya Hijja kilugha na kisheria.

(b)  Hijja ni ibada ya muda maalumu. Fafanua miezi ya Hijjah na tarehe ambayo ibada za Hijja huanza rasmi huko Makkah.

 

Toa mafunzo yatokanayo na vitendo vya ibada ya Hijjah vifuatavyo:

  (i)  Tawafu   (ii)  Sai  (iii)  Kisimamo cha Arafa  (iv)  Kupiga kambi Mina 

  (v)  Kutupa mawe  (vi)  Kuchinja mnyama.

 

(a) Ni lipi lengo kuu la ibada ya Hijjah au Umrah?

(b) Bainisha sababu tano, pamoja na waislamu kukusanyika mamilioni kila mwaka katika mji wa Makkah kwa ajili ya Hijjah, bado matunda yake hayaonekani katika jamii.

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Fiqh Main: Dini File: Download PDF Views 2598

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 web hosting    👉2 Kitau cha Fiqh    👉3 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    👉4 Madrasa kiganjani    👉5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉6 Simulizi za Hadithi Audio   

Post zinazofanana:

Taratibu za mahari katika uislamu

Hapa utajifunza taratibu za kutaja mahari katika uislamu.

Soma Zaidi...
Sifa za imamu wa swala ya jamaa

Post hii inakwenda kukupa sifa za imamu wa msikitini anayepasa kuswalisha swala ya jamii.

Soma Zaidi...
Hukumu na sherei zinazohusu ajira na kazi katika uislamu

Wajibu wa KufanyakaziUislamu siyo tu unawahimiza watu kufanya kazi na kutokuwa wavivu bali kufanya kazi ni Ibada.

Soma Zaidi...
Jinsi ya kukaa itiqaf na taratibu zake

Hapa utajifunza kuhusu taratibu za ibada ya itiqaf yaani kukaa msikitini kwa ajili ya ibada.

Soma Zaidi...
Utaijuwaje kama swala yako imekubalika

Hapa tunakwenda kuona jinsi ya kuzitathmini swala zetu.

Soma Zaidi...
Lengo la hijjah na matendo ya ibada ya hijjah na mafunzo yatokanayo

Nguzo za uislamu (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Jinsi ya kushona sanda ya maiti na kumvisha yaani kumkafini

Hapa utajifunza taratibu za kumkafini maiti wa kiislamu. Yaani kushona sanda yake na kumvisha.

Soma Zaidi...