Hadhi na Haki za Mwanamke katika jamii mbalimbali hapo zamani

Utangulizi:Uislamu unamuelekeza mwanaadamu namna nzuri ya kuendesha maisha yake katika kila kipengele cha maisha akiwa binafsi, katika familia na katika jamii.

Hadhi na Haki za Mwanamke katika jamii mbalimbali hapo zamani

Utangulizi:
Uislamu unamuelekeza mwanaadamu namna nzuri ya kuendesha maisha yake katika kila kipengele cha maisha akiwa binafsi, katika familia na katika jamii. Mfumo huu wa Uislamu, kwa kuwa umeasisiwa na Allah (s.w), Aliye Mjuzi Mwenye Hekima, ndio pekee uanomuelekeza mwanadamu kujenga familia imara iliyosimamishwa juu ya msingi wa haki na uadilifu. Hivyo utaona katika jamii zote za Ulmwengu, ni jamii ya Kiislamu pekee inayompa mwanamke hadhi na haki zake zote anazostahiki. Kinyume chake jamii nyingine zote zilizobakia, za kale na za sasa, zimemyanyasa na kumdumisha mwanamke kwa kiasi kikubwa.



Sura hii, ili kuonesha kwa uwazi ubora wa mfumo wa Kiislamu katika kumpa mwanamke hadhi na haki zake zote anazostahiki, ukilinganisha na mifumo ya maisha ya kijahili, tumeigawanya katika sehemu mbili:



Hadhi na Haki za mwanamke katika jamii za kijahili, Hadhi na Haki za mwanamke katika jamii ya Kiislamu.



Hadhi na Haki za mwanamke katika jamii za Kijahili
Hivi leo duniani kote, suala Ia hadhi na haki za mwanamke katika jamii linaongelewa katika kumbi mbali mbali za kitaifa na kimataifa. Pametokea makundi ya harakati ya kitaifa na kimataifa ya kutetea hadhi na haki za wanawake ziliziporwa na wanaume. Swali Ia kujiuliza ni; Je, jitihada hizi zimefanikiwa au zinaonyesha kuleta mafanikio yoyote hapo baadaye? Jibu Ia swali hili tutalipata baada ya kupitia mifano michache ya kihistoria inayoonesha jinsi mwanamke alivyo nyanyaswa na kudunishwa na jamii mbali mbali za kijahili na hatua zilizochukuliwa na jamii hizo ili kumkomboa. Katika sehemu hii tutazipitia jamii zifuatazo:


1.Jamii za Magharibi.
2.Jamii za Mashariki.
3.Jamii za Kiafrika.




                   


Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Fiqh Main: Dini File: Download PDF Views 916

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Bongolite - Game zone - Play free game    👉2 Simulizi za Hadithi Audio    👉3 web hosting    👉4 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    👉5 kitabu cha Simulizi    👉6 Kitabu cha Afya   

Post zinazofanana:

NI KWA NINI TUNASWALI?, NI UPI UMUHIMU WA KUSWALI NA NI ZIPI FADHILA ZA KUSWALI

Umuhimu wa KusimamishaSwala Kwa mujibu wa Hadith ya Ibn Umar (r.

Soma Zaidi...
Yaliyoharamishwa kwa mwenye kuwa katika ihram

Nguzo za uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Faida za funga

Nguzo za uislamu (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
msimamo wa uislamu juu ya kupanga uzazi na uzazi wa mpango

Msimamo wa Uislamu juu ya kudhibiti uzaziKama tulivyoona, msukumo wa kampeni ya kudhibiti kizazi, umetokana na mfumo mbaya wa kijamii na kiuchumi ulioundwa na wanadamu kutokana na matashi yao ya ubinafsi.

Soma Zaidi...
Umuhimu wa swala yaani kuswali kwa mwanadamu

Kwa nini ni muhimu kuswali? Post hii itakwenda kukufundisha kuhusu umuhimu wa kusimamisha swala.

Soma Zaidi...
Nini maana ya funga na ni lipi lengo lake

Post hii inakwenda kukufundisha kuhusu lengo la funga na maana yake katika uislamu.

Soma Zaidi...