picha

namna ya kutekeleza Funga za Sunnah pamoja na majukumu mengine

namna ya kutekeleza Funga za Sunnah pamoja na majukumu mengine

Nia katika Funga za Sunnah



Katika funga ya Ramadhani, kutokana na hadith iliyosimuliwa na Hafsah (r.a), funga haisihi endapo mtu hatatia nia ya kufunga usiku kabla ya Alfajir kuingia. Lakini katika funga za Sunnah mtu anaweza kunuia swaum mchana kabla ya kuingia adhuhuri, endapo atakuwa hajala chochote tangu alfajir, kama inavyobainika katika Hadithi ifuatayo:
Aysha (r.a) ameeleza kuwa siku moja Mtume wa Allah (s.a.w) aliniuliza:
“Aysha, una chochote (cha kula)?” Nikasema: “Mjumbe wa Allah, hatuna
chochote ”. Ndipo akas em a: “Nim efunga ”. (Muslim).


Uhuru wa kuvunja Funga ya Sunnah



Mtu aliyefunga sunnah ana uhuru kamili wa kufungua katikati endapo ataona ni vyema kwake kufanya hivyo. Tunajifunza hili katika Hadith zifuatazo:
Aysha (r.a) ameeleza: Mtume wa Allah alikuja kwangu akasema: “Una chochote cha kula?” Nikajibu: “Hapana.” Kisha akasema: “Basi, nitafunga ”. Kisha siku nyingine alitujia tukamwambia: Mtume wa Allah, tumeletewa zawadi ya Hais (aina ya chakula). Ndipo akasema: “Nionyeshe, nilikuwa nimefunga tangu alfajir, kisha alikula. ” (Muslim).



Ummi Hani (r.a) ameeleza kuwa katika siku ya kutekwa Makka Fatma (r.a) alikaa kushotoni mw a Mtume na Ummi Hani alikuwa kuliani kw ake. Kisha Walidah (r.a) alileta kikombe cha maji, alichukua akanywa, kisha Ummi Hani naye alichukua na kunywa. Akasema: Ee Mtume wa Allah, nilifunga na sasa nimefungua. akamuuliza: Ulikuwa unalipa? Akajibu: ‘Hapana ’ Akasema Mtume (s.w.): “Haidhuru iwapo ilikuwa ni funga ya sunnah. Mtu anayefunga funga ya sunnah ana uhuru kamili. Akipenda atafunga na akipenda ataacha.” (Abu Daud, Tirmidh, Ahmad). Aliyefunga Sunnah akikaribishwa aseme: “Nimefunga”
Mtu aliyefunga akikaribishwa chakula aseme ‘nimefunga’ kama tunavyofahamishw a katika Hadith ifuatayo:



Abu Hurairah (r.a) ameeleza kuwa Mtume wa Allah (s.a.w) amesema:“Kama mmoja wenu atakaribishwa chakula akiwa amefunga s em a: “Nim efunga ”:. (Muslim).
Si vibaya mtu asiyefunga kula mbele ya yule aliyefunga, bali mfungaji hupata ujira kwa kule kuamua kwake kuendelea kufunga pamoja na kuwaona wengine wakila mbele yake. Tunajifunza katika Hadith zifuatazo:



Ummi Umrah bin Ka ’ab (r.a) amesimulia: Mtume (s.a.w) alimtembelea na akamuandalia chakula, Mtume akamwambia kula. Akasema: “Nimefunga. ” Ndipo Mtume (s.a.w) akasema: “Wakati kitu kinapoliw a mbele ya mtu aliyefunga, malaika wanamrehemu mpaka wamalize kula” (Ahm ad).



Buraidah (r.a) amesimulia kuwa Bilal alikuja kwa Mtume (s.a.w) akamkuta anafungua kinywa. Mtume w a Allah akamkaribisha Bilal akamwambia: “Kifungua kinywa, Ee Bilal.” Bilal akasema: Nimefunga. Ee! Mtume wa Allah.’ Kisha Mtume wa Allah akasema: “Tunakula riziki yetu na riziki ya Bilal ya hali ya juu. Riziki ya hali ya juu kuliko zote ni Pepo. Unafahamu Ee Bilal kwamba mifupa ya mtu aliyefunga inamtukuza Allah na Malaika wanamuombea msamaha kwa muda wote ambao watu wanakula karibu yake?” (Baihaqi).



Funga za Sunnah na utekelezaji wa majukumu



Endapo kufunga sunnah kutamfanya mtu ashindwe kutekeleza majukumu yake kwa wengine katika jamii, ni vyema kutofunga. Katika Hadith tunafahamishwa kuwa wakeze Mtume (s.a.w) walikuwa aghlabu hawafungi mbali ya Ramadhani na Shaabani kwa kuhofia kushindwa kutekeleza wajibu wao kwa Mtume (s.a.w). Katika mwezi wa Shaaban Mtume (s.a.w) alikuwa akifunga sana kuliko miezi mingine:



Aysha (r.a) ameeleza: Kama mmoja wetu aliacha siku katika Ramadhani (kwa udhuru wa sheria) katika maisha ya Mtume (s.a.w) hakuweza kuzilipa alipokuwa na Mtume wa Allah mpaka Shaaban inaingia.” (Muslim).



Hadith hii inasisitiza kuwa kwa kuchelea kutoweza kutekeleza wajibu wao kwa Mtume wa Allah, wakeze Mtume(s.a.w) hawakuthubutu kufunga walipokuwa na Mtume. Mwanamke haruhusiwi kufunga sunnah mpaka aridhiwe na mume wake.




                   


Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 2018-08-01 Topic: Fiqh Main: Dini File: Download PDF Views 1349

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Kitabu cha Afya    👉2 Simulizi za Hadithi Audio    👉3 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    👉4 Kitau cha Fiqh    👉5 Bongolite - Game zone - Play free game    👉6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)   

Post zinazofanana:

Fiqh.

Kipengele hichi tutajifunza chimbuko la fiqh na maana ya figh.

Soma Zaidi...
Swala ya witiri na faida zake, na jinsi ya kuiswali

Hapa utajifunza jinsi ya kuswali swala ya witiri na faida zake kwa mwenye kuiswali.

Soma Zaidi...
Usitamani kifo hata ukiwa mchamungu mno ama muovu mno

Katika uislamu imekatazwa kutamani kufa hata kama utakuwa ni mtu muovu sana ama mchamungu sana.

Soma Zaidi...
Namna ya kutawadha hatuwa kwa hatuwa.

Post hii inakwenda kukugundisha jinsi ya kutawadha hatuwa kwa hatuwa.

Soma Zaidi...
Yajuwe masharti ya udhu yaani yanayofanya udhu kukubalika

Posti hii itakufundisha masharti yanayohitajika kwa mwenye kutaka kutia udhu.

Soma Zaidi...
Kwanini lengo la zakat na sadaqat halifikiwi katika jamii yetu

Nguzo za uislamu (EDK form 3:dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
MARADHI MENGINE 10 YANAYOTOKANA NA MBU ( matende, ngirimaji, homa ya manjano, n.k

Tofauti na maradhi yaliyotajwa hapo juu pia tafiti za kisayansi zimethibitisha kuwepo kwa maradhi mengine hatari yanayosambazwa na mbu, kama vile ngirimaji pamoja na matende.

Soma Zaidi...
NI ZIPI SWALA ZA SUNNAH: (qabliya (kabliya) na baadiya, tahajudi, tarawehe, qiyamu layl, shukr, istikhara)

Sunnah za SwalaSunnah za Swala Vipengele vya sunnah katika swala ni vile ambavyo mwenye kuswali akivitenda husaidia sana kukuza daraja ya swala yake na kuipa nguvu na msukumo mkubwa wa kuiwezesha kufikia lengo lililokusudiwa kwa urahisi zaidi.

Soma Zaidi...