Hadhi na haki za mwanamke katika jamii za Kigiriki hapo zamani

(a) UgirikiTunajifunza katika historia ya Ulimwengu kuwa jamii ya Wagiriki ilikuwa miongoni mwa jamii zilizoanza kustarabika.

Hadhi na haki za mwanamke katika jamii za Kigiriki hapo zamani

(a) Ugiriki
Tunajifunza katika historia ya Ulimwengu kuwa jamii ya Wagiriki ilikuwa miongoni mwa jamii zilizoanza kustarabika. Lakini utakuta kuwa hadhi ya mwanamke katika jamii hiyo ilikuwa chini sana. Bwana E.A. Allen katika kitabu chake "History of Civilization Vol. 3" anasema mwanamke wa Kigiriki alilazimishwa kuolewa pasina idhini yake. Mumewe huyo alihesabiwa kuwa Bwana (Lord) wake. Mwanamke alihesabiwa kuwa ni kama mtoto na kwahiyo alitakiwa kumtii mumewe bila kuhoji. Wanawake huko Ugiriki waligawanyika katika makundi matatu:



(i)Makahaba (Malaya) ambao kazi yao ilikuwa ni kuwastarehesha wanaume tu.
(ii)Watumishi ambao kazi yao ilikuwa kuangalia na kutunza siha za mabwana zao.
(iii)Wake amabo kazi yao ni kuzaa na kulea watoto.



Mke alitakiwa awe mwadilifu na achunge murua wake lakini haikuwa vibaya kwa mwanamume kujamii nje ya ndoa. Matokeo ya utaratibu huu ni kuwa wanawake makahaba wakawavutia watu wa ngazi zote - wanafalsafa, washairi, wanahistoria, wanafasihi na wasanii. Picha na sanamu za wanawake walio uchi zikazidi kuchochea zinaa na ufasiki. Ndoa ikaja kuonekana kuwa kero na zinaa ikawa jambo takatifu. Kuzama katika uzinifu kuliwapeleka Wagiriki kuchonga na kuabudu Aphrodite - mungu wa kike wa urembo na mahaba.


Kwa mujibu wa mafundisho ya Wagiriki ni kuwa huyo "Aphrodite" anasemekana kuwa alikuwa ni mungu wa kike aliyeolewa na mungu mwingine. Lakini hakutosheka na mume huyo mmoja. Akaanza kuzini na miungu wengine watatu na akawa pia anazini na binaadamu mmoja. Mungu huyo alipofanya jimai na binaadamu, wakazaa mungu wa kiume aliyeitwa Cupid yaani mungu wa mapenzi. Uzinifu wa "Aphrodite" na kuabudiwa kwake na Wagiriki ni kielelezo cha namna jamii hii iliwatukuza makahaba na kuupa uzinzi hadhi kubwa.


Kutokana na haya tunajifunza kuwa mwanzoni mwanamke katika jamii ya Ugiriki alidunishwa sana. Baadaye jamii ilipopiga hatua mbele katika maendeleo ya kiuchumi, hadhi duni ya mwanamke ilibadilishwa sura. Mwanamke aligeuzwa kuwa chombo cha kuwastarehesha wanaume jambo ambalo lililzidi kumdunisha na kumdhalilisha.




                   


Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Fiqh Main: Dini File: Download PDF Views 1085

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Simulizi za Hadithi Audio    👉2 kitabu cha Simulizi    👉3 Kitabu cha Afya    👉4 Kitau cha Fiqh    👉5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉6 Bongolite - Game zone - Play free game   

Post zinazofanana:

Sifa za imamu wa swala ya jamaa

Post hii inakwenda kukupa sifa za imamu wa msikitini anayepasa kuswalisha swala ya jamii.

Soma Zaidi...
Taratibu za mirathi katika zama za ujahilia

Kabla ya kuhubiriwa uislamu watu wa Maka walikuwa na tarayibu zenye dhuluma ndani yake katika ugawaji wa mirathi.

Soma Zaidi...
MAANA YA ZAKA NA SADAKA KULUNGA NA KISHERIA PAMOJA NA TOFAUTI ZAO

MAANA YA ZAKA NA SADAKA KULUNGA NA KISHERIA PAMOJA NA TOFAUTI ZAO.

Soma Zaidi...
Kwa nini lengo la kutoa zaka halifikiwi na watoaji zaka?

Kwa nini Lengo la Zakat na Sadaqat Halijafikiwa katika Jamii yetu?

Soma Zaidi...
NI LIPI HASA LENGO LA KUFARADHISHWA SWALA ZA FARADHI NA KUWEPO KWA SWALA ZA SUNNAH (SUNA)

Lengo la Kusimamisha SwalaBila shaka swala imepewa umuhimu mkubwa kiasi cha kufanywa nguzo kubwa ya Uislamu kutokana na lengo lake.

Soma Zaidi...
Ni kwa nini lengo la Funga na swaumu halifikiwi na wafungaji?

Kwa nini Lengo la Funga halifikiwi na Wafungaji Wengi?

Soma Zaidi...