image

Jinsi ya kuswali kuswali swala ya maiti

Post hii itakufundisha kuhusu swala ya maiti, nguzo za swala ya maiti, sharti za swwla ya maiti na jinsi ya kuiswali.

Masharti ya Swala ya Maiti

Masharti ya swala ya maiti ni yale yale ya swala ya kawaida kwa wenye kumswalia maiti bali kwa maiti mwenyewe kuna masharti yafu atayo:
(i) Maiti awe Muislamu kwani Allah (s.w) amesema:“Wala usimswalie abadan mmoja wao (makafiri na wanafiki) yeyote akifa”. (9:84)
(ii)Maiti awe ameshaoshwa.
(iii)Maiti awekwe mbele ya wanaomswalia. Lakini pia inajuzu kumswalia maiti ambaye hayupo,swala ya ghaibu. Maiti zikiwa nyingi zitapangwa mbele za kiume zikiwa karibu na Imamu, kisha zitaswaliwa swala moja tu.
(iv)Maiti asiwe shahidi.Kwa mujibu wa Sunnah ya Mtume (s.a.w) watu waliokufa katika vita vya kupigania dini ya Allah (s.w) hawaoshwi wala kuswaliwa.Mtume (s.a.w) aliamuru Mashahidi katika vita vya Uhud wasioshwe wala wasiswaliwe. (Abu Daud).

 

Nguzo za Swala ya Maiti

 


Nguzo za swala ya maiti ni tofauti kidogo na zile za swala ya kawaida. Tofauti na swala ya kawaida, swala ya maiti ina kusimama tu, hakuna rukuu, sijda wala vikao. Nguzo za swala ya maiti ni hizi zifuatazo:
1. Nia.

 

2. Takbira ya kuhirimia
(Takbira ya kwanza) anavyoswaliwa katika swala ya
kawaida
3. Kusoma suratul fatiha

 

4. Kuleta takbira ya pili

 

5. Kumswalia Mtume(s.a.w) kama

 


6. Kuleta takbira ya tatu.
7. Kumuombea dua maiti
Kuleta takbira ya nne
8. Kutoa salaamu

 

Sunnah za Swala ya Maiti

 


Nguzo za swala ya maiti ni hizi zifuatazo:

 


1.Kusoma Audhubillah kabla ya Al-fatiha.
2.Kusema Amin baada ya Al-fatiha.
3.Kuyasema yote yanayosemwa katika swala hii kimya kimya, ila Imamu atatoa Takbira Nne naSalam kwa sauti. Iswaliwe jamaa na safu ziwe witri; 1, 3, 5, 7, 9, n.k 4.Kuwaombea Waislamu wote dua pamoja na maiti. Baada ya Takbira ya Nne na kabla ya Salaam kuomba dua ifu atayo:

 


“ Alahumma laatahrimn aa ajrahu, walaataftinaa ba’adahu”
“Ewe Mwenyezi Mungu, usitunyime malipo yake na usitujaribu baada yake.”
5.Kutoa Salaam ya kwanza na ya pili kwa ukamilifu wake.
6.Imamu kusimama karibu na kichwa cha maiti ya kiume na kusisima karibu na kiuno (nyonga) ya maiti ya kike.

 


Namna ya Kutekeleza Swala ya Maiti

 


Utaratibu wa kusimamisha swala ya maiti ni kama ifuatavyo:
1. Maiti iwekwe mbele.
2. Imamu asimame katikati ya mwili wa maiti kama maiti ni ya kike na asimame sawa na mabega kama maiti ni ya kiume.Iwapo maiti zinazoswaliwa ni zaidi ya mmoja zipangwe moja mbele ya nyingine .Maiti za kiume zikiwa karibu na Imamu.

 

3.Wanaomfuata Imamu wasimame kwenye mistari yenye idadi ya witri; 1, 3, 5, 7, n.k.
4.Baada ya kusimama hivyo swala itaanza na kuendelea kama ifuatavyo:
(i)Nia - nia ya kumswalia maiti iliyo mbele huwekwa moyoni (si lazima kutamka).
(ii)Kisha nia hii huambatanishwa na Takbira ya kwanza - Takbira ya kawaida ya kuanzia swala - nayo ni kusema: Allahu Akbar.
(iii)Imamu na Maamuma watasoma Suratul Fatiha kimya kimya.
(iv)Baada ya kuimaliza Suratul- Fatiha Imamu atasema tena Allahu Akbar na Maamuma watafuatisha hivyo hivyo - bila ya kuinua mikono.
(v)Imamu na Maamuma watamswalia Mtume (s.a.w) kimya kimya kama ilivyo katika tahiyyatu ya mwisho ya swala ya kawaida.
(vi)Baada ya kumswalia Mtume, Imamu atasema tena - Allahu Akbar na Maamuma watafuatisha hivyo hivyo kimya kimya bila ya kuinua mikono.
(vii)Kisha kimya kimya maiti huombewa dua yoyote ile katika zile alizotufundisha Mtume (s.a.w). Moja kati ya dua hizo ni hii iliyosimuliwa na Abu Hurairah na kupokelewa na Maimamu wa hadith - Ahmad, Abu Daud, Timidh na Ibn Majah.

 


(viii) Baada ya dua hii imamu atasema tela Allahu Akbar na maamuma watafanya vivyo hivyo bila ya kunyanyua mikono.

 

(ix) Waombewe dua waislamu wote dua ifuatayo inaweza kutumika:

 


"Rabbana ighfir lanaa wali-ikhwaaninal-lladhiina sabaquuna bil-iiman, walaa taj-'al fii quluubinaa ghilal-Lilladhiina aamanuu, Rabbanaa in-naka ra-ufur-rahiim"

 

“... Mola wetu! Tusamehe sisi na ndugu zetu waliotutangulia (kufa) katika Imani (ya Kiislamu). Wala usijaalie katika nyoyo zetu uadui kuw afanyia Wa is lamu wenzetu. Mola wetu! Hakika wewe ni Mpole sana, mwenye Rehma mno”. (59:10)
(x) Baada ya dua hii itatolewa Salaam ya kumaliza swala na ni bora kuirefusha kidogo kuliko ile ya swala ya kawaida kwa kusema: "As-salaamu 'alaykum warahmatulllahi wabarakaatuh.

 

Amani iwe juu yenu na Rehma za Allah na Baraka zake.

 


Swala ya maiti pia inaweza kuswaliwa kwa ghaib, yaani bila ya kuwa na jeneza mbele. Mtume (s.a.w) mara kadhaa katika maisha yake, aliongoza swala ya maiti wa mbali na karibu waliokwisha zikwa kama tunavyofahamishwa katika Hadith zifu atazo:

 


Abu Hurairah (r.a) amesimulia kuw a Mtume wa Allah (s.a.w) alitoa habari za kifo cha Najashi (Mfalme wa Uhabeshi) kwa watu katika siku aliyokufa, akaenda nao katika sehemu ya kuswalia, akafanya mistari pamoja nao kisha akapiga takbira nne (yaani akaongoza swala ya Jeneza). (Bukhari na Muslim).

 


Ibn Abbas (r.a)amesimulia kuw a Mtume wa Allah alipita karibu na kaburi alimozikwa maiti usiku uliopita. Akauliza: Ni wakati gani alizikwa? Walijibu: Usiku uliopita. Akauliza: Kwa nini hamkunifahamisha? Walijibu: Tulizika katika giza la usiku. Kwa hiyo hatukupenda kukuamsha usingizini. Kisha alisimama na tukaunda mistari nyuma yake akaiswalia maiti ile. (Bukhari na Muslim).

 


Kusindikiza Jeneza
Baada ya maiti kuswaliwa jeneza litaongozwa kuelekea kaburini. Inatakiwa Waislamu walisindikize jeneza; wasiliweke mpaka likalishwe chini. Pia Mtume (s.a.w) ametuamrisha kusimama tutakapoona jeneza likipitishwa:

 


Jabir (r.a) amesimulia: Wakati Jeneza lilipokuwa linapita, Mtume (s.a.w) alisimama nasi pia tukasimama pamoja naye. Tukauliza: Ewe Mtume wa Allah! Hakika huyo ni Myahudi. Akasema: “Hakika kifo ni tishio. Kw a hiyo w akati wote mtakapoona Jeneza likipita simameni”.(Bukhari

 

Maandamano ya mazishi yawe kimya kimya.Kumsindikiza maiti kwa muziki na vilio ni haramu.


 


‹ Nyuma      › Endelea           





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 1586


Sponsored links
👉1 Madrasa kiganjani     👉2 Kitabu cha Afya     👉3 Kitau cha Fiqh     👉4 kitabu cha Simulizi    

Post zifazofanana:-

Namna ya kuswali hatuwa kwa hatuwq
Post hii itakufundisha jinsi ya kuswali hatuwa kwa hatuwa. Soma Zaidi...

Hadhi na Haki za Mwanamke Katika Jamii
Soma Zaidi...

Je ni zipi nguzo za uislamu, na ni ngapi nguzo za uislamu?
Post hii itakujuza maana ya uislamu na nguzo zake. Soma Zaidi...

Hii ndio hutuba ya ndoa ya kiislamu
Hapa utajifunza utaratibu wa hutuba ya ndoa ya kiislamu. Sharti za jutuba ya ndoa na jinsibya kuozesha Soma Zaidi...

Funga za kafara, aina zake na sababu za funga hizi za kafara na hukumu zake
Soma Zaidi...

Haki na wajibu kwa mayatima
Soma Zaidi...

Zaka ni nini? Nini maana ya zaka katika uislamu
Zaka, kilugha ni kukua; kubariki na kuzidi kheri. Soma Zaidi...

Maana ya kusimamisha swala
Nguzo za uislamu (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Funga za Sunnah na umuhimu wake
Nguzo za uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Hukumu ya kufinga kwa kifuata kuandama kwa mwezi
Ni muda gani unatakiwa ufunge ramadhani, je kuandama kwa mwezi kwa kiona ama hata kusiki. Soma Zaidi...

kuletewa ujumbe
(c)Kuletewa Ujumbe na Malaika kutoka kwa Allah (s. Soma Zaidi...

Ni nini maana ya uchumi katika uislamu
Katikabuislamu dhana ya uchumi imetofautiana na dhana ya kidunia hivi leo ambapo kamari na riba ni moja ya vitu muhimu katika uchumi. Soma Zaidi...