image

Nini maana ya Uchoyo, na madhara yake kwenye jamii

31.

Nini maana ya Uchoyo, na madhara yake kwenye jamii

31. Kuepuka Uchoyo na Ubahili



Uchoyo na ubahili ni kinyume cha ukarimu. Mtu mchoyo ana kasoro katika imani yake. Anaona kuwa chochote alichonacho amekipata kwa jitihada na akili yake tu. Pia anahofu kuwa akitoa kumpa mwingine atapungukiwa au atafilisika. Mtume (s.a.w) anatutanabahisha katika Hadithi zifuatazo:



Abu Hurairah (r.a) amesimulia kuwa Mtume wa Allah amesema: Mtu anasema: “Hiki changu! Hiki changu! Lakini ukweli ulivyo ni kwamba, vilivyo vyake katika mali yake ni vitu vitatu: “Kile alichokula au nguo aliyoivaa ikachakaa au kile alichokitoa sadaqa (hakika) amekiweka akiba, na kingine chochote zaidi ya hivi, hakika si vyake (si vyenye kumfaa) na ataondoka awaachie watu ”. (Muslim)



Abu Hurairah (r.a) amesimulia kuwa Mtume wa Allah amesema: “Chakula cha watu wawili kina watosha watu watatu, na chakula cha watu watatu kinawatosha watu wanne”.(Bukhari na Muslim)



Jabir bin Abdullah (r.a) ameeleza: Mtume w a Allah amesema: “Chakula cha mtu mmoja kinawatosha watu wawili na chakula cha watu wawili


kinawatosha watu wanne na chakula cha watu wanne kinawashibisha watu wanane”. (Muslim).
Hivyo ukizingatia Hadithi hizi, utaona kuwa hapana sababu ya Muislamu kuwa mchoyo au bahili. Uchoyo na ubahili ni tabia mbaya na malipo yake ni kwenda Motoni kama inavyobainishwa katika Qur-an:


Yule anayetoa (zaka na sadaka) na kumcha Mwenyezi Mungu. Na kusadiki jam bo jem a (akalifuata). Tutamsahilishia njia ya kw enda Peponi. Na afanyae ubakhili, asiwe na haja ya viumbe wenzake, na akakadhibisha mambo mema (asiyafanye). Tutamsahilishia njia ya kwendea Motoni. Na mali yake haitamfaa atakapokuwa anadidimia (Motoni humo). (92:5-11).




                   






           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 859


Sponsored links
👉1 Madrasa kiganjani     👉2 kitabu cha Simulizi     👉3 Kitabu cha Afya     👉4 Kitau cha Fiqh    

Post zifazofanana:-

Nini maana ya Uchoyo, na madhara yake kwenye jamii
31. Soma Zaidi...

Zijuwe Faida za Kuwa na Istiqama (Msimamo Thabiti)
38. Soma Zaidi...

VITABU VYA DINI
Soma Zaidi...

Hadhi na haki za mwanamke katika uislamu
4. Soma Zaidi...

Aina za hadithi
Sunnah na hadithi (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

jamii somo la 34
Soma Zaidi...

Nini maana ya Husda, na ni yapi madhara yake
34. Soma Zaidi...

jamii somo la 26
(vii)Hufanya bias hara na Allah (s. Soma Zaidi...

Ukarimu na Sifa za kuwa Mkarimu na faida zake
30. Soma Zaidi...

Mawaidha Kutokwa kwa Shekhe
Karibu kwenye Darsa za mawaidha na Mafundisho ya dini. Soma Zaidi...

Je wajuwa kuwa jua hujizungurusha kwenye mhimili wake?
Tulipokuwa shule tulisoma kuwa jua halizunguruki, ila dunia ndio huzunguka jua. Soma Zaidi...

Iv shekh haifai kufunga kwa nia utimize jambo labda kuna kitu unakitaka kwhy unaamua kugunga ili kama kuzidisha maombi kwa mungu jambo lifanikiwe
Ibada yavfubga ni katika ibadavanbazo hufanya nakaribia dini zote kubwa. Ibada hii imekuwaikikabiliw na naswlo mengi. Soma Zaidi...