Menu



Nini maana ya kutosheka na faida za kutosheka

32.

Nini maana ya kutosheka na faida za kutosheka

32. Kuwa Mwenye Kutosheka



Kutosheka ni kuridhika na neema uliyonayo. Kutosheka ni utajiri kuliko utajiri wote uliopo ulimwenguni.
Abu Hurairah (r.a) amesimulia kuwa Mtume wa Allah amesema, utajiri si kuwa na mali nyingi lakini utajiri ni kutosheka”. (Bukhari na Muslim)
Muislamu anatakiwa awe ni mwenye kutosheka na kile alichoruzukiwa na Mola wake. Kila mtu amekadiriwa riziki yake na Allah (s.w). Hakuna mwenye uwezo wa kumpunguzia au kumzidishia mtu riziki. Hili linabainishwa katika Qur-an katika usia wa Mzee Luqman kwa mwanawe:



Ewe mwanangu! Kwa hakika jambo lolote lijapokuwa na uzito wa chembe ya hardali, likawa ndani ya jabali au mbinguni au katika ardhi, Mwenyezi Mungu atalileta (amlipe mstahiki); bila shaka Mwenyezi Mungu ni Mjuzi wa mambo yaliyofichikana, (na) Mjuzi wa mambo yaliyo dhahiri. (31:16)
Pia Allah (s.w) anatuhakikishia:


“Na hakuna mnyama yoyote katika ardhi ila riziki yake iko juu ya Allah...” (11:6)
Juu ya moyo wa kutosheka Mtume (s.a.w) anatuwaidhi katika Hadithi ifuatayo:
Imesimuliwa katika mamlaka ya Abdullah Bin Amr bin al-’As (r.a) kuwa Mtume wa Allah amesema: “Yule aliyeingia Uislamu na akajaaliwa kupata riziki inayotosheleza mahitaji yake muhimu na Mwenyezi Mungu akamfanya kuwa mwenye kutosheka na kila alichotunukiwa, hakika amefuzu kikweli”. (Muslim)




                   


Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass

Nyuma Endelea


Je umeipenda post hii ?

Ndio            Hapana            Save post
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Jifunze Main: Dini File: Download PDF Views 981

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Kitau cha Fiqh    👉2 Madrasa kiganjani    👉3 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉4 kitabu cha Simulizi    👉5 Kitabu cha Afya    👉6 Simulizi za Hadithi Audio   

Post zinazofanana:

quran na sayansi

2:UUMBWAJI KWA MAJI YA UZAZIUumbwaji wa mwanadamu umepitia hatua mbalimbali na haya yote yamefanywa kwa sababumaalumu ili tipate mazingatio.

Soma Zaidi...
Aina za hadithi

Sunnah na hadithi (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Mawaidha Kutokwa kwa Shekhe

Karibu kwenye Darsa za mawaidha na Mafundisho ya dini.

Soma Zaidi...
HUYU NDIYE MUUMINI WA KWELI KATIKA UISLAMU

عَنْ أَبِي حَمْزَةَ أَنَسِ بْنِ مَالِكٍ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ خَادِمِ رَسُولِ اللَّهِ صلى الله عليه و سلم عَنْ النَّبِيِّ صلى الله عليه ?...

Soma Zaidi...
Kwanini Ni muhimu kusimamisha uislamu katika jamii

Dini anayostahiki kufuata mwanadamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Uchambuzi wa hadithi za mtume

Sunnah na hadithi (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
sura ya 02

Jifunze namna ya kusoma quran, pata mafunzo ya tajwid hapa

Soma Zaidi...