image

Nini maana ya kutosheka na faida za kutosheka

32.

Nini maana ya kutosheka na faida za kutosheka

32. Kuwa Mwenye Kutosheka



Kutosheka ni kuridhika na neema uliyonayo. Kutosheka ni utajiri kuliko utajiri wote uliopo ulimwenguni.
Abu Hurairah (r.a) amesimulia kuwa Mtume wa Allah amesema, utajiri si kuwa na mali nyingi lakini utajiri ni kutosheka”. (Bukhari na Muslim)
Muislamu anatakiwa awe ni mwenye kutosheka na kile alichoruzukiwa na Mola wake. Kila mtu amekadiriwa riziki yake na Allah (s.w). Hakuna mwenye uwezo wa kumpunguzia au kumzidishia mtu riziki. Hili linabainishwa katika Qur-an katika usia wa Mzee Luqman kwa mwanawe:



Ewe mwanangu! Kwa hakika jambo lolote lijapokuwa na uzito wa chembe ya hardali, likawa ndani ya jabali au mbinguni au katika ardhi, Mwenyezi Mungu atalileta (amlipe mstahiki); bila shaka Mwenyezi Mungu ni Mjuzi wa mambo yaliyofichikana, (na) Mjuzi wa mambo yaliyo dhahiri. (31:16)
Pia Allah (s.w) anatuhakikishia:


“Na hakuna mnyama yoyote katika ardhi ila riziki yake iko juu ya Allah...” (11:6)
Juu ya moyo wa kutosheka Mtume (s.a.w) anatuwaidhi katika Hadithi ifuatayo:
Imesimuliwa katika mamlaka ya Abdullah Bin Amr bin al-’As (r.a) kuwa Mtume wa Allah amesema: “Yule aliyeingia Uislamu na akajaaliwa kupata riziki inayotosheleza mahitaji yake muhimu na Mwenyezi Mungu akamfanya kuwa mwenye kutosheka na kila alichotunukiwa, hakika amefuzu kikweli”. (Muslim)




                   






           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 643


Sponsored links
👉1 Kitau cha Fiqh     👉2 kitabu cha Simulizi     👉3 Madrasa kiganjani     👉4 Kitabu cha Afya    

Post zifazofanana:-

quran na sayansi
Soma Zaidi...

jamii somo la 34
Soma Zaidi...

tawhid
Soma Zaidi...

kuwa mwenye kusamehe, na faida zake
27. Soma Zaidi...

madhara ya kusengenya, na namna ya kuepuna usengenyaji
13. Soma Zaidi...

DARSA ZA DINI YA KIISLAMU KAMA QURAN, FIQH, SIRA, AFYA, TAJWID NA TAFSIR ZA QURAN
Soma Zaidi...

Zijuwe Faida za Kuwa na Istiqama (Msimamo Thabiti)
38. Soma Zaidi...

Zoezi 2:2
Soma Zaidi...

Zoezi - 2
1. Soma Zaidi...

Hadhi na haki za mwanamke katika uislamu
4. Soma Zaidi...

Mtazamo wa Uislamu juu ya usawa kati ya mwanaume na mwanamke
Soma Zaidi...

VITABU VYA DINI
Soma Zaidi...