picha

Kwanini Ni muhimu kusimamisha uislamu katika jamii

Dini anayostahiki kufuata mwanadamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Kwa nini ni muhimu Kusimamisha Uislamu katika jamii?        

Ni muhimu Uislamu kusimama katika jamii ili matunda yafuatayo yapatikane;

  1. Waumini wataweza kumuabudu Mwenyezi Mungu (s.w) ipasavyo kwa mujibu wa Qur’an na Sunnah kwa kila kipengele cha maisha ya kila siku binafsi na jamii katika siasa, uchumi, elimu, utamaduni kama wanavyotekeleza swala, funga, hija, n.k.

Rejea Qur’an (51:56), (2:21-22), (7:54), (9:31), (2:85), (2:208), (2:193), (4:75-76), (9:38), (8:39), (22:40) na (47:7).

      2. Kupatikanaamani ya kweli na kuondoka hofu na mashaka katika jamii. Hii ni baada ya waumini kuchukua hatamu ya uongozi katika jamii kwa mujibu wa muongozo na sheria za Mwenyezi Mungu (s.w).

Rejea Qur’an (57:25), (2:257) na (5:90-91).

3. Wauminiataweza kuamrisha mema na kukataza maovu kikamilifu katika jamii pasina kikwazo chochote pindi watakapochukua nafasi ya kuiongoza jamii.

Rejea Qur’an (22:41) na (3:110).

 

  1. Kuikinga jamii na majanga mbali mbali. Waumini watakapochukua nafasi za kuiongoza jamii ndio itakuwa sababu ya kutoweka maovu ndani jamii ambayo ndio sababu ya kupatikana majanga katika jamii.

Rejea Qur’an (8:25).

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Jifunze Main: Post File: Download PDF Views 3017

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
๐Ÿ‘‰1 ai web app     ๐Ÿ‘‰2 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     ๐Ÿ‘‰3 Bongolite - Game zone - Play free game     ๐Ÿ‘‰4 Madrasa kiganjani     ๐Ÿ‘‰5 Simulizi za Hadithi Audio     ๐Ÿ‘‰6 Dua za Mitume na Manabii    

Post zinazofanana:

Kushika mwenendo wa kati "Na ushike mwenendo wa katiโ€ฆ." (31:19)

Mwenendo wa kati ni mwenendo ulioepukana na kibri na majivuno kwa upande mmoja na ulioepukkana na udhalili na unyonge kwa upande mwingine.

Soma Zaidi...
Zingatio:

Swala husimama kwa kuhifadhiwa na kuswaliwa kwa khushui na kudumu na swala katika maisha yote.

Soma Zaidi...
Uandishi wa hadithi wakati wa maswahaba wa mtume (s.a.w)

Sunnah na hadithi (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
KULA HALALI NA ZILICHO KIZURI NI AMRI KATIKA UISLAMU

ุนูŽู†ู’ ุฃูŽุจููŠ ู‡ูุฑูŽูŠู’ุฑูŽุฉูŽ ุฑูŽุถููŠูŽ ุงู„ู„ู‡ู ุนูŽู†ู’ู‡ู ู‚ูŽุงู„ูŽ: ู‚ูŽุงู„ูŽ ุฑูŽุณููˆู„ู ุงู„ู„ูŽู‘ู‡ู ุตู„ู‰ ุงู„ู„ู‡ ุนู„ูŠู‡ ูˆ ุณู„ู… "ุฅู†ูŽู‘ ุงู„ู„ูŽู‘ู‡ูŽ ุทูŽูŠูู‘ุจูŒ ู„ูŽุง ูŠูŽู‚ู’ุจูŽู„ู ุฅู„ูŽู‘ุง ุทูŽูŠ...

Soma Zaidi...
sura ya 02

Jifunze namna ya kusoma quran, pata mafunzo ya tajwid hapa

Soma Zaidi...