Kujielimisha kwa Ajili ya Allah (s.w).

Elimu ndiyo zana aliyotunukiwa mwanadamu ili aitumie kutekeleza majukumu yake kama Khalifa wa Allah (s.

Kujielimisha kwa Ajili ya Allah (s.w).

  1. Kujielimisha kwa Ajili ya Allah (s.w).

Elimu ndiyo zana aliyotunukiwa mwanadamu ili aitumie kutekeleza majukumu yake kama Khalifa wa Allah (s.w) hapa ulimwenguni. Mara tu baada ya Nabii Adam (a.s) kuumbwa na kabla hajaruzukiwa chochote na hata kabla ya kukaribishwa kwenye neema za bustanini (Peponi) alifunzwa mambo yote ya msingi yatakayomuwezesha kuwa Khalifa hapa Ulimwenguni:



“Na (Allah (s.w)) akamfundisha Adam m ajina ya vitu vyote...” (2:31).



Naye Mtume Muhammad (s.a.w) Wahyi na amri ya kwanza aliyoipokea kutoka kwa Mola wake ni kusoma kwa ajili ya Allah (s.w). Hivyo kila Muislamu analazimika kuitekeleza kwa hima amri hii ya kwanza ili aweze kumuabudu Mola wake inavyostahiki na aweze kuwa Khalifa wake hapa ulimwenguni.Aidha kila Muislamu analazimika kujielimisha mambo ya msingi yatakayomuwezesha kuwa Muumini wa kweli na kumuwezesha kuendesha maisha yake yote ya kibinafsi na kijamii kwa mujibu wa Qur-an na Sunnah.



Ni wazi kuwa Muislamu mwenye kujipamba na tabia ya kujielimisha katika mambo muhimu ya maisha kwa lengo la kupata ufanisi katika kumuabudu Allah (s.w) na kusimamisha Ukhalifa katika jamii; atakuwa tofauti kiutendaji na kiuchaji na yule aliye mvivu wa kujielimisha kama tunavyojifunza katika Qur-an:



“Je, wanaweza kuwa sawa wale wanaojua na wale wasiojua?” Wanaotanabahi ni wale wenye akili tu.” (39:9).



“Allah atawainua daraja wale walioamini miongoni mwenu;na waliopewa elimu watapata daraja zaidi...” (58:11)



Ukizingatia kuwa kutafuta elimu ni faradh kwa kila Muislamu mwanamume na mwanamke, mkubwa na mdogo, aya hizi zatosha kuwa



kichocheo kwa kila Muumini kujibidiisha kwa kujielimisha kwa ajili ya Allah(s.w) kwa kadri ya uwezo wake na kila wakati awe anaomba dua ifu atayo:



“... Mola wangu! Nizidishie elimu.” (20:114)





                   



Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Tawhid Main: Dini File: Download PDF Views 927

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Kitabu cha Afya    👉2 Madrasa kiganjani    👉3 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉4 Bongolite - Game zone - Play free game    👉5 Kitau cha Fiqh    👉6 kitabu cha Simulizi   

Post zinazofanana:

Sifa za Wanafiki zilizotajwa katika surat Hashir

Huwaoni wale wanafiki wanawaambia ndugu zao walio makafiri miongoni mwa watu waliopewa Kitabu (kabla yenu) Mayahudi (Wanawaambia): "Kama mkitolewa, (mkifukuzwa hapa) tutaondoka pamoja nanyi, wala hat utamtii yoyote kabisa juu yenu.

Soma Zaidi...
Sifa za waumini zilizotajwa katika surat As-Sajida

Nao husema (kwa maskhara): "Je, tutakapopotea katika ardhi, (tukageuka mchanga) ndio tutarudishwa katika umbo jipya?

Soma Zaidi...
Mambo anayofanyiwa maiti baada ya kufa

Dhana ya faradh kwa muislamu (EDK form 2:dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Kuwa wenye shukurani mbele ya Allah (s.w)

Mwanaadamu ametunukiwa neema mbali mbali na Mola wake kuliko viumbe wengine wote kama tuanvyojifunza katika aya mbali mbali za Qur'an.

Soma Zaidi...
Umbile la mbingu na ardhi linavyothibitisha uwepo wa Allah

Allah anatutaka kuchunguza umbile na mbingu na ardhi ili kupata mazingatio.

Soma Zaidi...
Kwa nini mwanadamu hawezi kuishi bila dini?

Mwanadamu hawezi kuishi bila dini, kwani dini imekusanya mfumo mzima wa maisha yake.

Soma Zaidi...