Elimu ndiyo zana aliyotunukiwa mwanadamu ili aitumie kutekeleza majukumu yake kama Khalifa wa Allah (s.
Elimu ndiyo zana aliyotunukiwa mwanadamu ili aitumie kutekeleza majukumu yake kama Khalifa wa Allah (s.w) hapa ulimwenguni. Mara tu baada ya Nabii Adam (a.s) kuumbwa na kabla hajaruzukiwa chochote na hata kabla ya kukaribishwa kwenye neema za bustanini (Peponi) alifunzwa mambo yote ya msingi yatakayomuwezesha kuwa Khalifa hapa Ulimwenguni:
“Na (Allah (s.w)) akamfundisha Adam m ajina ya vitu vyote...” (2:31).
Naye Mtume Muhammad (s.a.w) Wahyi na amri ya kwanza aliyoipokea kutoka kwa Mola wake ni kusoma kwa ajili ya Allah (s.w). Hivyo kila Muislamu analazimika kuitekeleza kwa hima amri hii ya kwanza ili aweze kumuabudu Mola wake inavyostahiki na aweze kuwa Khalifa wake hapa ulimwenguni.Aidha kila Muislamu analazimika kujielimisha mambo ya msingi yatakayomuwezesha kuwa Muumini wa kweli na kumuwezesha kuendesha maisha yake yote ya kibinafsi na kijamii kwa mujibu wa Qur-an na Sunnah.
Ni wazi kuwa Muislamu mwenye kujipamba na tabia ya kujielimisha katika mambo muhimu ya maisha kwa lengo la kupata ufanisi katika kumuabudu Allah (s.w) na kusimamisha Ukhalifa katika jamii; atakuwa tofauti kiutendaji na kiuchaji na yule aliye mvivu wa kujielimisha kama tunavyojifunza katika Qur-an:
“Je, wanaweza kuwa sawa wale wanaojua na wale wasiojua?” Wanaotanabahi ni wale wenye akili tu.” (39:9).
“Allah atawainua daraja wale walioamini miongoni mwenu;na waliopewa elimu watapata daraja zaidi...” (58:11)
Ukizingatia kuwa kutafuta elimu ni faradh kwa kila Muislamu mwanamume na mwanamke, mkubwa na mdogo, aya hizi zatosha kuwa
kichocheo kwa kila Muumini kujibidiisha kwa kujielimisha kwa ajili ya Allah(s.w) kwa kadri ya uwezo wake na kila wakati awe anaomba dua ifu atayo:
“... Mola wangu! Nizidishie elimu.” (20:114)
Umeionaje Makala hii.. ?
Mwanaadamu ametunukiwa neema mbali mbali na Mola wake kuliko viumbe wengine wote kama tuanvyojifunza katika aya mbali mbali za Qur'an.
Soma Zaidi...Nguzo za imani (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)
Soma Zaidi...Kwa kutumia akili yako unaweza kumtambua Allah bila ya shaka yeyote ile. Postbhii itakufundisha nafasi ya akilonkatika kutambuwa uwepo na Uwezo wa Allah.
Soma Zaidi...Bila shaka wanaume wenye kufuata vizuri nguzo za Uislamu, na wanawake wanaozifuata vizuri nguzo za Uislamu, na wanaume wanaoamini vizuri nguzo za Imani, na wanawake wanaoamini vizuri nguzo za Imani, na wanaume wanaotii, na wanawake wanaotii, na wanaume wa
Soma Zaidi...Maana ya dini kwa mujibu wa makafiri ina utofauti mkubwa na vile ambavyo uislamu unaamini kuhusu dini.
Soma Zaidi...Kumzulia mtu mtwahirifu kuwa amefanya tendo la zinaa pasina kuleta ushahidi stahiki ni tendo ovu mno mbele ya Allah (s.
Soma Zaidi...Lengo tarajiwa la Muhtasari huu ni kutuwezesha kuzibaini fika sifa za Waumini zilizoainishwa katika Qur'an, kisha kujipamba nazo ili tuwe waja wema watakaorehemewa na kuridhiwa na Allah (s.
Soma Zaidi...