Kujielimisha kwa Ajili ya Allah (s.w).

Elimu ndiyo zana aliyotunukiwa mwanadamu ili aitumie kutekeleza majukumu yake kama Khalifa wa Allah (s.

Kujielimisha kwa Ajili ya Allah (s.w).

  1. Kujielimisha kwa Ajili ya Allah (s.w).

Elimu ndiyo zana aliyotunukiwa mwanadamu ili aitumie kutekeleza majukumu yake kama Khalifa wa Allah (s.w) hapa ulimwenguni. Mara tu baada ya Nabii Adam (a.s) kuumbwa na kabla hajaruzukiwa chochote na hata kabla ya kukaribishwa kwenye neema za bustanini (Peponi) alifunzwa mambo yote ya msingi yatakayomuwezesha kuwa Khalifa hapa Ulimwenguni:



“Na (Allah (s.w)) akamfundisha Adam m ajina ya vitu vyote...” (2:31).



Naye Mtume Muhammad (s.a.w) Wahyi na amri ya kwanza aliyoipokea kutoka kwa Mola wake ni kusoma kwa ajili ya Allah (s.w). Hivyo kila Muislamu analazimika kuitekeleza kwa hima amri hii ya kwanza ili aweze kumuabudu Mola wake inavyostahiki na aweze kuwa Khalifa wake hapa ulimwenguni.Aidha kila Muislamu analazimika kujielimisha mambo ya msingi yatakayomuwezesha kuwa Muumini wa kweli na kumuwezesha kuendesha maisha yake yote ya kibinafsi na kijamii kwa mujibu wa Qur-an na Sunnah.



Ni wazi kuwa Muislamu mwenye kujipamba na tabia ya kujielimisha katika mambo muhimu ya maisha kwa lengo la kupata ufanisi katika kumuabudu Allah (s.w) na kusimamisha Ukhalifa katika jamii; atakuwa tofauti kiutendaji na kiuchaji na yule aliye mvivu wa kujielimisha kama tunavyojifunza katika Qur-an:



“Je, wanaweza kuwa sawa wale wanaojua na wale wasiojua?” Wanaotanabahi ni wale wenye akili tu.” (39:9).



“Allah atawainua daraja wale walioamini miongoni mwenu;na waliopewa elimu watapata daraja zaidi...” (58:11)



Ukizingatia kuwa kutafuta elimu ni faradh kwa kila Muislamu mwanamume na mwanamke, mkubwa na mdogo, aya hizi zatosha kuwa



kichocheo kwa kila Muumini kujibidiisha kwa kujielimisha kwa ajili ya Allah(s.w) kwa kadri ya uwezo wake na kila wakati awe anaomba dua ifu atayo:



“... Mola wangu! Nizidishie elimu.” (20:114)





                   



Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Tawhid Main: Dini File: Download PDF Views 884

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Bongolite - Game zone - Play free game    👉2 Kitau cha Fiqh    👉3 Dua za Mitume na Manabii    👉4 Kitabu cha Afya    👉5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉6 Tafasiri ya Riyadh Swalihina   

Post zinazofanana:

Himizo la kuwasamehe waliotukosea

“Na wasiape wale wakarimu na wenye wasaa miongoni mwenu, kujizuia kuwasaidia jamaa zao, maskini na wale waliohama kwa ajili ya Dini ya Allah; na wasamehe na waachilie mbali (wapuuze yaliyopita).

Soma Zaidi...
Sifa za wuamini zilizotajwa katika surat Al-ma'aarij

Kwa hakika binaadamu ameumbwa, hali ya kuwa mwenye pap atiko.

Soma Zaidi...
Nafsi ya mwanadamu inavyothinitisha uwepo wa Allah

Mwanadamu ukifikiria vyema. Kuhusu nafsi yako, hakika utapatabfikra yabuwepp wa Mwenyezi Mungu

Soma Zaidi...
Ushahidi juu ya kosa la Uzinifu

Ushahidi wa kuthibitisha kutendeka kwa kosa la uzinifu unapatikana kwa namna tatu zifuatzo: (i)Kushuhudia tendo hilo likifanyika kwa wakati mmoja watu wanne Mukalafu (Walio baleghe na wenye akili timamu), wakiwa ni Waislamu waadilifu.

Soma Zaidi...
Kuangamizwa Waovu na Kuokolewa Waumini

Baada ya kuonywa wasionyeke, Allah(s.

Soma Zaidi...
Kwa nini mwanadamu hawezi kuishi bila dini?

Mwanadamu hawezi kuishi bila dini, kwani dini imekusanya mfumo mzima wa maisha yake.

Soma Zaidi...