Na tukiutafiti Uislamu kwa makini kama mfumo kamili wa maisha tunaona unadhihiri ukweli wa aya hii ya Qur-an.
Na tukiutafiti Uislamu kwa makini kama mfumo kamili wa maisha tunaona unadhihiri ukweli wa aya hii ya Qur-an. Uislamu unatoa mwongozo wa maisha haya na ya akhera na hakuna jambo lililo muhimu katika kumuongoza mwanaadamu
lisilokuwemo katika mwongozo aliokuja nao Muhammad (s.a.w). Hivyo hoja ya kuhitaji Mtume ili aje kukamilisha dini pia inaondoka.
Hata hivyo kuna baadhi ya watu wanaosema kwamba kupita tu kwa muda mrefu ni sababu ya kuhitaji Mtume mwingine. Hii ni kwa sababu wanasema mwongozo ulioletwa karne 14 zilizopita ni wa kale mno kiasi kwamba hauwezi kukidhi mahitaji ya watu wa leo. Mawazo haya hayana msingi kabisa, kwa sababu zifu atazo:
(i)Mafunzo ya Uislamu ni ya milele, kwa sababu ni ufunuo utokao kwa Mwenyezi Mungu mjuzi wa yote ya kale, ya sasa na yajayo, tena basi mwenye uhai wa milele. Elimu ya binaadamu ndiyo yenye ukomo, na ni jicho la binaadamu ambalo haliwezi kuona hata kesho achilia mbali miaka milioni mmoja ijayo. Elimu na hikima ya Mwenyezi Mungu imesalimika na upungufu kama huo.
(ii)Uislamu umeegemeza mafundisho yake juu ya umbile la binaadamu. Na umbile la binaadamu limesalia vile vile katika zama zote. Watu wote wamejengwa kwa majengo yale yale yaliyowajenga watu wa kale kabisa na hivyo umbile lao kimsingi ni lilelile.
(iii)Katika maisha ya binaadamu kuna mizani inayoridhisha kabisa baina ya mambo yanayodumu na mambo yanayobadilika. Misingi muhimu na maadili makuu hayabadiliki na sura ya nje ndiyo inayoweza kubadilika kutokana na kupita kwa muda.
Qur-an na sunna zinatoa kanuni au misingi ya kudumu na kwa kutumia ijitihadi misingi hiyo inaweza kutekelezwa kadri hali itakavyobadilika.
Uislamu ndio dini pekee iliyoweka utaratibu madhubuti unaoweza kuoanisha maendeleo ya binaadamu na misingi ya Kitabu cha Allah (s.w) na Sunnah ya Mtume wake Muhammad (s.a.w).
Na tukirudi katika lile sharti letu la tatu kuhitajia kuletwa Mtume mwingine, tunaona kuwa Muhammad (s.a.w) hakuletwa kwa taifa au watu maalum bali kwa walimwengu wote.
Qur-an in as em a:“Sema (Ewe Nabii Muhammad): “Enyi w atu! Hakika mimi ni Mtume wa Mwenyezi Mungu kwenu nyinyi nyote”. (7:158)“Nasi hatukukutuma ila uwe rehema kwa walimwengu wote.” (21:107).
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiw ana App yetu. Bofya liln hapo chini kuweza ku download
Download NowJe! umeipenda hii post?
Ndio Hapana Save post
Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Topic: Tawhid Main: Post File: Download PDF Share On Facebook or Whatsapp Views 1442
Sponsored links
👉1
Kitabu cha Afya
👉2
Simulizi za Hadithi Audio
👉3
kitabu cha Simulizi
👉4
Madrasa kiganjani
👉5
Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)
👉6
Kitau cha Fiqh
Ni yupi mtume wa mwisho? na je ni kwa nini Muhammad ndiye mtume wa mwisho?
Soma Zaidi...
Maana ya uislamu.
Kwenye kipengele hichi titajifunza maana ya uislamu,na maana nyingine tofauti. Soma Zaidi...
DUA YA 1 - 10
1. Soma Zaidi...
Kuongea na Allah (s.w) nyuma ya Pazia
Hii ni njia ambayo mwanaadamu huongeleshwa moja kwa moja na Allah (s. Soma Zaidi...
Muumini ni yule ambaye anazungumza ukweli
Ukweli ni katika sifa za waumini. Siku zote hakuna hasara katika kusema ukweli. Kinyume chake uongo ni katika madhambi makubwa sana. Soma Zaidi...
Kubisha hodi katika nyakati za faragha katika familia
“Enyi mlioamini! Soma Zaidi...
Mgawanyo wa elimu usiokubalika katika uislamu
Mgawanyo wa elimu usiokubalika katika uislamu Ni upi?
(EDK form 1: mgawanyo wa elimu usiokubalika katika uislamu) Soma Zaidi...
mwanadamu hawezi kuishi bila ya Dini
Soma Zaidi...
Sifa za wuamini zilizotajwa katika surat Al-ma'aarij
Kwa hakika binaadamu ameumbwa, hali ya kuwa mwenye pap atiko. Soma Zaidi...
Maswali juu ya mtazamo wa uislamu kuhusu dini
Mtazamo wa uislamu kuhusu dini (EDK form 2:dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...