Kwa nini hakuna haja ya Mtume mwingine baada ya Muhammad

Na tukiutafiti Uislamu kwa makini kama mfumo kamili wa maisha tunaona unadhihiri ukweli wa aya hii ya Qur-an.

Kwa nini hakuna haja ya Mtume mwingine baada ya Muhammad

Kwa nini hakuna haja ya mtume Mwingine baada ya muhammad?


Na tukiutafiti Uislamu kwa makini kama mfumo kamili wa maisha tunaona unadhihiri ukweli wa aya hii ya Qur-an. Uislamu unatoa mwongozo wa maisha haya na ya akhera na hakuna jambo lililo muhimu katika kumuongoza mwanaadamu


lisilokuwemo katika mwongozo aliokuja nao Muhammad (s.a.w). Hivyo hoja ya kuhitaji Mtume ili aje kukamilisha dini pia inaondoka.
Hata hivyo kuna baadhi ya watu wanaosema kwamba kupita tu kwa muda mrefu ni sababu ya kuhitaji Mtume mwingine. Hii ni kwa sababu wanasema mwongozo ulioletwa karne 14 zilizopita ni wa kale mno kiasi kwamba hauwezi kukidhi mahitaji ya watu wa leo. Mawazo haya hayana msingi kabisa, kwa sababu zifu atazo:



(i)Mafunzo ya Uislamu ni ya milele, kwa sababu ni ufunuo utokao kwa Mwenyezi Mungu mjuzi wa yote ya kale, ya sasa na yajayo, tena basi mwenye uhai wa milele. Elimu ya binaadamu ndiyo yenye ukomo, na ni jicho la binaadamu ambalo haliwezi kuona hata kesho achilia mbali miaka milioni mmoja ijayo. Elimu na hikima ya Mwenyezi Mungu imesalimika na upungufu kama huo.



(ii)Uislamu umeegemeza mafundisho yake juu ya umbile la binaadamu. Na umbile la binaadamu limesalia vile vile katika zama zote. Watu wote wamejengwa kwa majengo yale yale yaliyowajenga watu wa kale kabisa na hivyo umbile lao kimsingi ni lilelile.



(iii)Katika maisha ya binaadamu kuna mizani inayoridhisha kabisa baina ya mambo yanayodumu na mambo yanayobadilika. Misingi muhimu na maadili makuu hayabadiliki na sura ya nje ndiyo inayoweza kubadilika kutokana na kupita kwa muda.


Qur-an na sunna zinatoa kanuni au misingi ya kudumu na kwa kutumia ijitihadi misingi hiyo inaweza kutekelezwa kadri hali itakavyobadilika.


Uislamu ndio dini pekee iliyoweka utaratibu madhubuti unaoweza kuoanisha maendeleo ya binaadamu na misingi ya Kitabu cha Allah (s.w) na Sunnah ya Mtume wake Muhammad (s.a.w).



Na tukirudi katika lile sharti letu la tatu kuhitajia kuletwa Mtume mwingine, tunaona kuwa Muhammad (s.a.w) hakuletwa kwa taifa au watu maalum bali kwa walimwengu wote.


Qur-an in as em a:โ€œSema (Ewe Nabii Muhammad): โ€œEnyi w atu! Hakika mimi ni Mtume wa Mwenyezi Mungu kwenu nyinyi nyoteโ€. (7:158)โ€œNasi hatukukutuma ila uwe rehema kwa walimwengu wote.โ€ (21:107).



                   


Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Tawhid Main: Dini File: Download PDF Views 2342

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
๐Ÿ‘‰1 Bongolite - Game zone - Play free game    ๐Ÿ‘‰2 Kitabu cha Afya    ๐Ÿ‘‰3 Kitau cha Fiqh    ๐Ÿ‘‰4 kitabu cha Simulizi    ๐Ÿ‘‰5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    ๐Ÿ‘‰6 Simulizi za Hadithi Audio   

Post zinazofanana:

ALAMA YA MUUMINI WA UKWELI KATIKA UISLAMU

ุนูŽู†ู’ ุฃูŽุจููŠ ู‡ูุฑูŽูŠู’ุฑูŽุฉูŽ ุฑูŽุถููŠูŽ ุงู„ู„ู‡ู ุนูŽู†ู’ู‡ู ุฃูŽู†ูŽู‘ ุฑูŽุณููˆู„ูŽ ุงู„ู„ูŽู‘ู‡ู ุตู„ู‰ ุงู„ู„ู‡ ุนู„ูŠู‡ ูˆ ุณู„ู… ู‚ูŽุงู„ูŽ: "ู…ูŽู†ู’ ูƒูŽุงู†ูŽ ูŠูุคู’ู…ูู†ู ุจูุงูŽู„ู„ูŽู‘ู‡ู ูˆูŽุงู„ู’ูŠูŽูˆู’ู…ู...

Soma Zaidi...
Elimu ya mwingozo na elimu ya mazingira katika uislamu

Mahusiano kati ya elimu ya mwongizo na elimu ya mazingira katika uislamu.

Soma Zaidi...
MAANA NA HUKUMU YA TAJWIDI

Jifunze namna ya kusoma quran, pata mafunzo ya tajwid hapa

Soma Zaidi...
Mtazamo wa uislamh juu ya ibada

Katika kipengele hich tutajifunza dhana ya ibada katika uislamu,maana ua ibada

Soma Zaidi...
Aina kuu za dini

Katika kipengele hichi tutajifunza aina kuu mbili za dini.

Soma Zaidi...
Kuamini mitume wa mwenyezi Mungu

Nguzo za Imani (EDK form 2:. Dhana ya elimu ya uislamu

Soma Zaidi...