Maana ya Elimu katika uislamu na nani aliye elimika?
Hili ni swali kutoka katika maarifa ya elimu ya dini ya kiislamu kidato cha kwanza (EDK FORM 1)
Swali: Nini maana ya Elimu na ni nani aliye elimika?
Jibu:
- Katika Uislamu Elimu maana yake ni:
- Ujuzi unaoambatana na utendaji au
- Mabadiliko ya tabia yanayoambatana (yanayotokana) na ujuzi au
- Ujuzi unaomuwezesha mtu kufanya (kutenda) jambo kwa ufanisi au inavyotakikana.
- Nani aliyeelimika? (Sifa za mtu aliyeelimika).
- Aliyeelimika ni yule mwenye ujuzi unaomuwezesha kutenda (kufanya) jambo kwa ufanisi na inavyotakikana.
- Mjuzi wa Qur’an na Sunnah ni yule anayeendesha kila kipengele cha maisha yake ya binafsi na kijamii kwa mujibu wa Qur’an na Sunnah.
- Watakapo fanana kimwenendo na kitabia wale wenye elimu na wasiokuwa na elimu, basi wenye elimu watakuwa hawajaelimika ila wamesoma tu.
“……………Sema, Je! Wanaweza kuwa sawa wale wanaojua na wale wasiojua? Wanaotanabahi ni wale wenye akili tu………”(39:9).
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 ai web app 👉2 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉3 Kitau cha Fiqh 👉4 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉5 web hosting 👉6 Simulizi za Hadithi Audio
Post zinazofanana:
Maamrisho ya kushikamana nayo
Yale tunayoamrishwa kushikamana nayo ni haya yafuatayo: (i)Kumuabudu Allah (s.
Soma Zaidi...Mambo ya lazima kufanyiwa maiti ya muislamu
Mambo ya faradhi kuhusu maiti ya muislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)
Soma Zaidi...Maana ya kuamini malaika katika maisha ya kila siku
Nguzo za imani (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)
Soma Zaidi...Ni Ipi Elimu yenye manufaa
Elimu inaweza kugawanyika katika makundibmrngine mawili ambayo ni elimu yenye manufaa na elimubisiyi na manufaa
Soma Zaidi...Njia anazotumia Mwenyezi Mungu (s.w) kuwafundisha na kuwasiliana na wanaadamu
Njia ambazo Allah hutumia kuwasiliana na wanadamu nakuwafundisha elimu mbalimbali. (Edk form 1 dhana ya Elimu)
Soma Zaidi...