Maana ya Elimu katika uislamu na nani aliye elimika?
Hili ni swali kutoka katika maarifa ya elimu ya dini ya kiislamu kidato cha kwanza (EDK FORM 1)
Swali: Nini maana ya Elimu na ni nani aliye elimika?
Jibu:
- Katika Uislamu Elimu maana yake ni:
- Ujuzi unaoambatana na utendaji au
- Mabadiliko ya tabia yanayoambatana (yanayotokana) na ujuzi au
- Ujuzi unaomuwezesha mtu kufanya (kutenda) jambo kwa ufanisi au inavyotakikana.
- Nani aliyeelimika? (Sifa za mtu aliyeelimika).
- Aliyeelimika ni yule mwenye ujuzi unaomuwezesha kutenda (kufanya) jambo kwa ufanisi na inavyotakikana.
- Mjuzi wa Qur’an na Sunnah ni yule anayeendesha kila kipengele cha maisha yake ya binafsi na kijamii kwa mujibu wa Qur’an na Sunnah.
- Watakapo fanana kimwenendo na kitabia wale wenye elimu na wasiokuwa na elimu, basi wenye elimu watakuwa hawajaelimika ila wamesoma tu.
“……………Sema, Je! Wanaweza kuwa sawa wale wanaojua na wale wasiojua? Wanaotanabahi ni wale wenye akili tu………”(39:9).
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
Share follows: 0 |
Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 kitabu cha Simulizi 👉2 Bongolite - Game zone - Play free game 👉3 ai web app 👉4 Simulizi za Hadithi Audio 👉5 Kitabu cha Afya 👉6 Kitau cha Fiqh
👉1 kitabu cha Simulizi 👉2 Bongolite - Game zone - Play free game 👉3 ai web app 👉4 Simulizi za Hadithi Audio 👉5 Kitabu cha Afya 👉6 Kitau cha Fiqh
Post zinazofanana:
Kuongea na Allah (s.w) nyuma ya Pazia
Hii ni njia ambayo mwanaadamu huongeleshwa moja kwa moja na Allah (s.
Soma Zaidi...Maana ya kuamini malaika katika maisha ya kila siku
Nguzo za imani (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)
Soma Zaidi...Humtegemea Mwenyezi Mungu peke yake
Hawamuogopi au kumtegemea yeyote kinyume na Mwenyezi Mungu.
Soma Zaidi...KUAMINI VITABU VYA ALLAH (S.W)
Mtu hawi Muumini wa kweli mpaka awe na yakini juu ya vitabu vya Allah (s.
Soma Zaidi...