picha

kuwa na ikhlas

Ikhlas ni kufanya kila jambo jema kwa ajili ya Allah (s.

kuwa na ikhlas

  1. KUWA NA IKHLAS

Ikhlas ni kufanya kila jambo jema kwa ajili ya Allah (s.w) tu. Yaani kutoa huduma na mali kwa watu wanaohitajia msaada bila ya kutaraji malipo yoyote kutoka kwao ila kutoka kwa Allah (s.w) tu. Kwa mfano kumlisha na kumvisha fukara, maskini au yatima bila ya kutarajia hata kupata shukurani (ahsante) kutoka kwake ila tu kwa kutegemea malipo kutoka kwa Allah (s.w) ni kitendo cha Ikhlas. Wale wanaotoa misaada



kwa wanaohitajia kwa Ikhlas, wamesifiwa na Allah (s.w) katika Qur-an:



“Na huwalisha chakula maskini na yatima na wafungwa na hali yakuwa wenyewe wanakipenda (chakula hicho. Husema nyoyoni mwao wanapowapa chakula hicho): Tunakulisheni kwa ajili ya kutaka radhi ya Mw enyezi Mungu (tu). Hatutaki kw enu m alipo w ala shukurani. Hakika sisi tunamuogopa Mola wetu hiyo siku yenye shida na taabu.”

(76:8-1 0).



“Na amchaye (Mwenyezi Mungu) ataepushwa nao (huo moto uwakao kwa nguvu). Ambaye hutoa mali yake kwa ajili ya kujitakasa na hali ya kuwa hakuna yeyote anayemfanyia ihsani ili awe anamlipa. Isipokuwa (anafanya haya) kwa kutaka radhi ya Mola wake Mtukufu. Basi atapata la kumridhisha.” (92:1 7-21).

Si katika kutoa tu mali, bali lolote lile analolifanya Muislamu wa kweli hana budi kulifanya kwa nia ya kupata radhi ya Allah (s.w). Utendaji wa Mwanaadamu uliofanywa kwa Ikhlas ndio tu utakaomuwezesha kuwajibika vilivyo kwa wanaadamu wenzake na kwa Mola wake Mtukufu.

Ili kujikumbusha mara kwa mara kufanya mambo yetu kwa Ikhlas, ni Sunnah kila tunapoanza swala kabla ya kusoma Suratul-Fatiha tu seme:

“Ninauelekeza uso wangu kwa yule aliyeziumba mbingu na ardhi, hali ya kuwa nimewacha dini za upotofu mimi (nimejisalimisha ni Muislamu na ) si miongoni mwa washirikina. (6:79)



Hakika swala yangu, na ibada zangu (zote nyingine) na uzima wangu na kufa kwangu ni kwa ajili ya Mwenyezi Mungu, Bwana wa walimwengu wote. Hana mshirika wake na kwa haya ndiyo niliyoamrishwa,na mimi ni wa kwanza wa waliojisalimisha. (6:162-163)



                   

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 2018-08-01 Topic: Sunnah Main: Dini File: Download PDF Views 2877

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Madrasa kiganjani    👉2 ai web app    👉3 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    👉4 Kitau cha Fiqh    👉5 Kitabu cha Afya    👉6 kitabu cha Simulizi   

Post zinazofanana:

Dua za kuomba wakati unapokuwa na hasira ama ukiwa umekasirika

Post hii itakueleza ni dua gani unatakiwa uzisome wakati unapokiwa na hasira ama pale unapokasirika.

Soma Zaidi...
Hadithi inayotaja nguzo tano za uislamu

عَنْ أَبِي عَبْدِ الرَّحْمَنِ عَبْدِ اللَّهِ بْنِ عُمَرَ بْنِ الْخَطَّابِ رَضِيَ اللَّهُ عَنْهُمَا قَالَ: سَمِعْت رَسُولَ اللَّهِ صل?...

Soma Zaidi...
Hali ambazo akiwa nazo mwenye kuomba dua dua yake hujibiwa

Post hii inakwenda kukifundisha nibhali zipi ukiwa nazo, basi dua yako kuhubaliwa kwa urahisi.

Soma Zaidi...
Mzazi na msafiri na mwenye kudhulumiwa dua zao hujibiwa kwa haraka

Wapo watu kadhaa ambao waliomba dua hazirudi. Hapa nitakueleza wawili ambao ni mzazi na msafiri.

Soma Zaidi...
DUA ZENYE MANENO HAYA HUJIBIWA

SIFA ZA (MANENO NA MATAMSHI YA) DUA YENYE KUJIBIWA.

Soma Zaidi...
BAADHI YA DUA ZA KILA SIKU

BAADHI YA DUA ZA KILA SIKU.

Soma Zaidi...
dua ya kuomba jambo ufanikiwe

hii ni damna ya kuomba dua ukubaliwe, dua ya kuomba jambo ufanikiwe

Soma Zaidi...
HUU NDIO USIA WA MTUME KWA WAISLAMU

عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ أَنَّ رَجُلًا قَالَ لِلنَّبِيِّ صلى الله عليه و سلم أَوْصِنِي.

Soma Zaidi...