picha

Kwa namna gani nabii Musa na Bi Mariam waliweza kuzungumza na Allah nyuma ya pazia

Nabii Musa na Mama yake nabii Isa bi Mariam waliweza kuwasiliana na Allah nyuma ya pazia.

(b)Kuongea na Allah (s.w) nyuma ya Pazia

 

Hii ni njia ambayo mwanaadamu huongeleshwa moja kwa moja na Allah (s.w) kwa sauti ya kawaida pasina kumuona. Kutokana na ushahidi wa Qur-an njia hii imetumika kwa Mitume na wateule wengine wa Allah (s.w).

 

Nabii Mussa (a.s) ni miongoni mwa Mitume waliosemeshwa na Allah (s.w).kama tunavyofahamishwa kisa chake katika Qur-an: Basi Musa alipotimiza muda, akasafiri pamoja na ahali zake (watu wake kurejea kwao Misri). Aliona moto upande wa mlimani akawaambia ahali zake; ‘Ngojeni, hakika nimeona moto, labda nitakuleteeni habari za huko au kijinga cha moto ili muote! (28:29) 8 Basi alipoufikia aliitwa kutoka upande wa kuliani wa bonde hilo katika kiwanja kilichobarikiwa, kutoka mtini: “Ewe Mussa! Bila shaka mimi ndiye Mwenyezi Mungu, Mola wa walimwengu.” (28:30) Kwa njia ya nyuma ya pazia, Nabii Mussa (a.s) aliongea na Allah mara nyingi na mara zote hizo hakuweza kumuona. Alipoomba amuone alijibiwa kama inavyooneshwa katika aya zifuatazo:

 

Na alipofika Mussa katika miadi yetu na Mola wake akazungumza naye, (Mussa) akasema: “Mola wangu! Nionyeshe (nafsi yako) ili nikuone” Akasema (Mwenyezi Mungu): “Hutaniona, lakini tazama jabali (lililoko mbele yako) kama litakaa mahali pake utaweza kuniona”. Basi Mola wake alipojionyesha katika jabali, alilifanya liwe lenye kuvunjika vunjika na Mussa akaanguka hali ya kuzimia. Alipozindukana akasema “Utukufu ni wako. Natubu kwako, na mimi ni wa kwanza wa wanaoamini (haya)” (7:143).

 

Pia tunafahamishwa katika Qur-an kuwa Bibi Maryam, mama wa Nabii Issa (a.s) naye aliongeleshwa nyuma ya pazia wakati wa kumzaa Issa Bin Maryamu kama ilivyo katika aya zifuatazo: 9 “Kisha uchungu ukampeleka katika shina la mtende, (akawa anazaa na huku) anasema:“Laiti ningelikufa kabla ya haya, na ningekuwa niliyesahaulika kabisa.(19:23) Mara ikamfikia sauti kutoka chini yake ikamwambia usihuzunike. Hakika Mola wako amejaalia kijito cha maji chini yako.(19:24) na litikise kwako shina la mtende, litakuangushia tende nzuri, zilizo mbivu. (19:25) Basi ule na unywe na litulie jicho (lako). Na kama ukimuona mtu yeyote (akauliza habari juu ya mtoto huyu), sema:“Hakika mimi nimeweka nadhiri kwa Mwingi wa Rehma ya kufunga, kwa hiyo leo sitasema na mtu” (19:26).

 

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Tawhid Main: Post File: Download PDF Views 1888

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Bongolite - Game zone - Play free game     👉2 Kitau cha Fiqh     👉3 Dua za Mitume na Manabii     👉4 Kitabu cha Afya     👉5 Tafasiri ya Riyadh Swalihina     👉6 Simulizi za Hadithi Audio    

Post zinazofanana:

Mazingatio kabla ya kuosha maiti

Mambo ya faradh kwa maiti ya muislamu (EDK form 2:dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Mwanadamu hawezi kuishi bila dini kutokana na vipawa alivyooewa na Allah

Je ni kwa nini mwanadamu hawezi kuishi bila ya kuwa na dini?. Vipawa alivyopewa na Allahni jibu tosha juu ya swali jilo

Soma Zaidi...
(b)Umbile la Mwanaadamu ni la kidini

Ukizingatia maana halisi ya dini, kuwa dini ni utaratibu wa maisha, utadhihirikiwa kuwa umbile la mwanaadamu ni la kidini.

Soma Zaidi...
Maswali kuhusu njia za kumjua mwenyezi Mungu

Nguzo za imani (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu

Soma Zaidi...
Vipi Allah huwasiliana na wanadamu kwa kupitia njia ya maandishi

Allah hutumia maandishi kuwafundisha wanadamu. Mfano mzuri ni nabii Musa ambaye alipewa vibao vya maandishi.

Soma Zaidi...
Maana ya muislamu.

Kwenye kipengele hichi tutajifunza ni nani muislamu.

Soma Zaidi...