Makatazo ya kujiepusha nayo

Makatazo ya kujiepusha nayo

(2) Makatazo ya kujiepusha nayo



Yale waumini wanayowajibika kujiepusha nayo kwa mnasaba wa aya tulizozipitia (17:23-40) ni haya yafuatayo:



(a) Kujiepusha na kumshirikisha Allah (s.w)
Kumshirikisha Allah (s.w) ni kujaalia kuwa Allah (s.w) anao washirika wake wanaomsaidia katika kuendesha masuala mbali mbali katika mchakato mzima wa maisha ya dunia. Allah (s.w) hushirkishwa kinadharia na kiutendaji.



Allah (s.w) hushikirishwa kinadharia kwa kujaalia kiumbe kisicho na uwezo wowote, kama vile sanamu, jiwe kubwa, mti mkubwa, majini, malaika, n.k.; kuwa ni mungu na kukielekea kwa maombi na kukitegemea kama apasavyo kuombwa na kutegemewa Allah (s.w). Hii ni shiriki katika Dhati ya Allah (s.w). Pia Allah (s.w) hushirikishwa kinadharia, kwa kumnasibisha na kiumbe au kukipachika kiumbe sifa anazostahiki kusifiwa kwazo. Hii ni shiriki katika sifa za Allah (s.w).


Allah (s.w) hushirikishwa kiutendaji kwa kutiiwa kanuni na sharia na kufuatwa miongozo ya maisha iliyotungwa na watu kinyume na mwongozo wa maisha wa Allah (s.w) kupitia kwa Mitume wake na Vitabu vyake. Kumtii yeyote kinyume na kanuni na sharia za Allah (s.w) ni kumshirikisha Allah (s.w) katika Mamlaka yake. Na kupitisha hukumu yoyote kinyume na alivyohukumu Allah (s.w) ni kumshirikisha katika Hukumu zake. Shirk ndio kiini na chanzo kikuu cha maovu yote duniani na ndio msingi mkuu wa dhuluma (rejea Qur-an 31:13)




                   


Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Tawhid Main: Dini File: Download PDF Views 800

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
πŸ‘‰1 Kitau cha Fiqh    πŸ‘‰2 kitabu cha Simulizi    πŸ‘‰3 Kitabu cha Afya    πŸ‘‰4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    πŸ‘‰5 Madrasa kiganjani    πŸ‘‰6 Bongolite - Game zone - Play free game   

Post zinazofanana:

Kuamini vitabu vya mwenyezi Mungu (s.w)..

Nguzo za imani (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Kutowatii Wazazi katika kumuasi Allah (s.w)

"Na (wazazi wako) wakikushurutisha kunishirikisha na (yale) ambayo huna ilimu nayo, usiwatii; lakini kaa nao kwa wema hapa duniani (Maadamu ni wazee wako, ila usiwafuate tu mwenendo wao mbaya); Shika mwenendo wa wale wanaoelekea kwangu, kisha marejeo yenu

Soma Zaidi...
Athari za vita vya Uhud

Vita vya uhudi viliweza kuleta athari nyingi. Post hii itakuletea athari baadhi za vita hivyo.

Soma Zaidi...
Kuangamizwa Waovu na Kuokolewa Waumini

Baada ya kuonywa wasionyeke, Allah(s.

Soma Zaidi...
KUAMINI MALAIKA

Jifunze tawhid yaani kumpwekesha Allah subhaanah wata'aala

Soma Zaidi...
Kujiepusha na Shirk

Shirki ni kitendo chochote cha kukipa kiumbe nafasi ya Allah (s.

Soma Zaidi...