picha

Nguzo kuu za umama katika umri wa kupata watoto na kulea watoto

Posti hii inahusu zaidi nguzo kuu za umama katika umri wa kujifungua na kulea watoto, ni kipindi ambacho mama anakuwa analea watoto kwa kawaida kadri ya makadirio kipindi hiki uanza kati ya miaka kumi na mitano mpaka arobaini kwa walio wengi na kinaweza k

Nguzo za kuu za umama  katika kipindi cha kujifungua na kulea watoto.

1.Mama akiwa katika kipindi cha kujifungua na kulea watoto katika kipindi hiki anapaswa kuwa na nguzo kuu muhimu zinazopaswa kumwongoza ili aweze kupata watoto wenye afya nzuri na makuzi mema pasipokuwa na magonjwa na vizuizi vyovyote wakati wa makuzi ya mtoto mpaka mtoto anafikia umri wa miaka mitano na kuzidi kwa hiyo zifuatazo ni nguzo kuu za umama.

 

2.Uzazi wa mpango.

Wazazi wote wawili wanapaswa kutumia uzazi wa mpango ambao wanaona unafaa kwao baada ya kupata ushauri kutoka kwa wataalamu wa afya, kwa kutumia uzazi wa mpango wazazi wanaweza kupata idadi ya watoto ambao wanawahitaji na watoto wanaweza kupata malezi muhimu na mapenzi kutoka kwa wazazi wao, kwa kutumia uzazi wa mpango uepusha kubwa na watoto wanaofuatana sana na kusababisha ukuaji wa watoto kubwa wa shida na kusababisha umaskini ambapo mama baada ya kufanya shughuli mbalimbali za kuongeza uchumi anatumia mda mwingi kulea watoto.

 

3.Kuhudhulia kliniki wakati wote wa ujauzito na baada ya kujifungua pale anampeleka mtoto.

Mama akibeba mimba tu anapaswa kwenda kliniki ili kuweza kuona maendeleo ya mimba na kupata elimu mbalimbali hasa kuhusu Dalili za hatari wakati wa ujauzito pia mama anapaswa kupima maambukizi ili aweze kumkinga mtoto na Maambukizi yoyote yale, kwa hiyo hata mama akijifungua anapaswa kupeleka  mtoto wake kliniki ili apate chanjo mbalimbali za kumkinga na magonjwa kama vile kifua kikuu, kupooza na magonjwa mbalimbali, kwa hiyo akina Mama mnapaswa kuhudhuria kliniki kwa sababu kuna faida nyingi kwa Mama na mtoto pia.

 

4. Kuzuia maambukizi kutoka kwa Mama kwenda kwa mtoto wakati wa ujauzito.

Mama akiwa na mimba anapaswa kupima maambukizi yote kwa awamu mbili ya kwanza ni pale anapobeba mimba tu na wakati akiwa na miezi minane ya ujauzito hii ni kwa sababu ya kuepuka kumwambukiza mtoto akiwa kwenye tumbo la Mama, na wakati wa kujifungua kwa kumpatia mama dawa za kupunguza makali ya virus vya ukimwi na mtoto akizaliwa na Mama mwenye Maambukizi anapaswa kupewa dawa pindi anapozaliwa hata kama yeye hana Maambukizi kwa hiyo huwa kwenye uangalizi kwa kipindi cha miezi sita.

 

5.Uangalizi wa Mama na mtoto ndani ya masaa ishirini na manne.

Mama anapojifungua salamu huwa kwenye uangalizi ndani ya masaa ishirini na manne ili kuangalia kama kuna mabadiliko yoyote yanayoweza kujitokeza kwa mtoto na Mama pia kwa hiyo kama hakuna mabadiliko yoyote mama anaruhusiwa kutoka hospitalini na kama kuna mabadiliko yoyote Mama na mtoto watapaswa kutibiwa kufuatana na hali zao.

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Uzazi Main: Afya File: Download PDF Views 1408

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Simulizi za Hadithi Audio    👉2 kitabu cha Simulizi    👉3 Dua za Mitume na Manabii    👉4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉5 Kitabu cha Afya    👉6 web hosting   

Post zinazofanana:

MAUMIVU WAKATI WA TENDO LA NDOA

Maumivu wakati wa tendo la ndoa kitaalamu huitwa dyspareunia.

Soma Zaidi...
je mwana mke ana weza kubeba mimba kama hayupo kwenye siku zake za hatali ama

Mimba haipatikani kila siku, na pia mimba huingia kwa siku moja na katika muda mmoja. Baada ya mimba kutungwa hakuna tena nafasi ya kutungwa mimba nyingine.

Soma Zaidi...
Mambo yanayopunguza nguvu za kiume

Posti hii inaelezea kuhusiana na nguvu za kiume zinavyopungua na Ni Mambo gani yanayofanya zipungue

Soma Zaidi...
Huduma kwa wasioona hedhi

Posti hii inahusu zaidi msaada au namna ya kuwahudumia wale wasioona hedhi na wamefikiwa kwenye umri wa kuweza kuona hedhi.

Soma Zaidi...
mpenzi wangu nimeshiriki nae tendo la ndoa akiwa siku zake za hatar kwa siku 3 lakin hajashika mimba tatizo linaweza kuwa ni nini?

Kupata ujauzito hufungamana na mambo mengi ikiwepo afya vya wawili yaani me na mume na mengineyo. Unaweza kushiriki sikuvhatari na usiupate mimba. Postivhii ibakwendavkukufahamisha undani wa jambo hili.

Soma Zaidi...
Faida na hasara za kutumia uzazi wa mpango

Tunaposema uzazi wa mpango, tunamaanisha ile hali ya kuachanisha muda kutoka mtoto hadi mwingine. Inatakiwa angalau mtoto na mtoto wapishane miaka miwili. Uzazi wa mpango ni maamuzi kati ya mama na baba.

Soma Zaidi...
Aina mbalimbali za mimba kutoka.

Post hii inahusu zaidi aina mbalimbali za mimba kutoka, hizi ni jinsi mimba inavyoonyesha dalili za kutoka na nyingine zinaweza kuonyesha dalili Ila kwa sababu ya huduma mbalimbali za kwanza hizo mimba zinaweza kudhibiiwa na mtoto akazaliwa.

Soma Zaidi...
Je bado unasumbuliwa na nguvu za kiume?

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu njia za kuondoa tatizo la nguvu za kiume

Soma Zaidi...
Namna ya kuangalia maendeleo ya mtoto akiwa tumboni mwa Mama

Posti hii inahusu zaidi namna ya kuangalia maendeleo ya mtoto akiwa tumboni mwa mama, zoezi hili ufanyika kila mwezi pale mama anapokuja kwenye mahudhurio kwa kufanya hivyo tunaweza kuja maendeleo ya mtoto kwa kila mwezi.

Soma Zaidi...