Nguzo kuu za umama katika umri wa kupata watoto na kulea watoto
Posti hii inahusu zaidi nguzo kuu za umama katika umri wa kujifungua na kulea watoto, ni kipindi ambacho mama anakuwa analea watoto kwa kawaida kadri ya makadirio kipindi hiki uanza kati ya miaka kumi na mitano mpaka arobaini kwa walio wengi na kinaweza k
Nguzo za kuu za umama katika kipindi cha kujifungua na kulea watoto.
1.Mama akiwa katika kipindi cha kujifungua na kulea watoto katika kipindi hiki anapaswa kuwa na nguzo kuu muhimu zinazopaswa kumwongoza ili aweze kupata watoto wenye afya nzuri na makuzi mema pasipokuwa na magonjwa na vizuizi vyovyote wakati wa makuzi ya mtoto mpaka mtoto anafikia umri wa miaka mitano na kuzidi kwa hiyo zifuatazo ni nguzo kuu za umama.
2.Uzazi wa mpango.
Wazazi wote wawili wanapaswa kutumia uzazi wa mpango ambao wanaona unafaa kwao baada ya kupata ushauri kutoka kwa wataalamu wa afya, kwa kutumia uzazi wa mpango wazazi wanaweza kupata idadi ya watoto ambao wanawahitaji na watoto wanaweza kupata malezi muhimu na mapenzi kutoka kwa wazazi wao, kwa kutumia uzazi wa mpango uepusha kubwa na watoto wanaofuatana sana na kusababisha ukuaji wa watoto kubwa wa shida na kusababisha umaskini ambapo mama baada ya kufanya shughuli mbalimbali za kuongeza uchumi anatumia mda mwingi kulea watoto.
3.Kuhudhulia kliniki wakati wote wa ujauzito na baada ya kujifungua pale anampeleka mtoto.
Mama akibeba mimba tu anapaswa kwenda kliniki ili kuweza kuona maendeleo ya mimba na kupata elimu mbalimbali hasa kuhusu Dalili za hatari wakati wa ujauzito pia mama anapaswa kupima maambukizi ili aweze kumkinga mtoto na Maambukizi yoyote yale, kwa hiyo hata mama akijifungua anapaswa kupeleka mtoto wake kliniki ili apate chanjo mbalimbali za kumkinga na magonjwa kama vile kifua kikuu, kupooza na magonjwa mbalimbali, kwa hiyo akina Mama mnapaswa kuhudhuria kliniki kwa sababu kuna faida nyingi kwa Mama na mtoto pia.
4. Kuzuia maambukizi kutoka kwa Mama kwenda kwa mtoto wakati wa ujauzito.
Mama akiwa na mimba anapaswa kupima maambukizi yote kwa awamu mbili ya kwanza ni pale anapobeba mimba tu na wakati akiwa na miezi minane ya ujauzito hii ni kwa sababu ya kuepuka kumwambukiza mtoto akiwa kwenye tumbo la Mama, na wakati wa kujifungua kwa kumpatia mama dawa za kupunguza makali ya virus vya ukimwi na mtoto akizaliwa na Mama mwenye Maambukizi anapaswa kupewa dawa pindi anapozaliwa hata kama yeye hana Maambukizi kwa hiyo huwa kwenye uangalizi kwa kipindi cha miezi sita.
5.Uangalizi wa Mama na mtoto ndani ya masaa ishirini na manne.
Mama anapojifungua salamu huwa kwenye uangalizi ndani ya masaa ishirini na manne ili kuangalia kama kuna mabadiliko yoyote yanayoweza kujitokeza kwa mtoto na Mama pia kwa hiyo kama hakuna mabadiliko yoyote mama anaruhusiwa kutoka hospitalini na kama kuna mabadiliko yoyote Mama na mtoto watapaswa kutibiwa kufuatana na hali zao.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 kitabu cha Simulizi 👉2 Kitabu cha Afya 👉3 Madrasa kiganjani 👉4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉5 Kitau cha Fiqh 👉6 Bongolite - Game zone - Play free game
Post zinazofanana:
Je siku sahihi yakufanya tendo la ndoa niipi ukipata siku zake za hatari?
Swali langu ni hili doktaJe siku sahihi yakufanya tendo la ndoa niipi ukipata siku zake za hatari?
Soma Zaidi...Dalili za kujifunguwa, na dalili za uchungu wa kujifunguwa
Nitajuwaje kama mjamzito amekaribia kujifunguwa, ni dalili gani anaonyesha, dalili za uchungu wa kujifunguwa
Soma Zaidi...Sabau za maumivu ya uume baada ya tendo la ndoa
Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu sababu za maumivu ya uume baada ya tendo la ndoa
Soma Zaidi...Mambo muhimu kwa wanawake kabla ya kubeba mimba
Posti hii inahusu zaidi mambo muhimu kwa wanawake kabla ya kubeba mimba,Ni mambo ya kuzingatia ili mama akija kubeba mimba awe mzima kimwili, ki afya na kisaikolojia na hivyo hivyo Mtoto atakayezaliwa atakuwa salama.
Soma Zaidi...Dalili za Mimba ya Siku 7 kwa Mwanamke
Kipindi cha siku saba baada ya kurutubishwa kwa yai (karibu wiki moja tangu kutunga kwa mimba) ni hatua ya mwanzo kabisa ambapo kijusi kinaanza kujipandikiza kwenye mji wa mimba. Ingawa mara nyingi ni mapema mno kwa vipimo vya mkojo kuonyesha matokeo chanya, mwili wa mwanamke unaweza kuanza kuonyesha dalili fiche za kibaolojia. Makala hii inaelezea kile kinachotokea mwilini mwako katika kipindi hiki cha siku saba.
Soma Zaidi...Yajue madhara ya kutoa mimba mara Kwa mara
Posti hii inahusu zaidi madhara ambayo yanaweza kutokea kwa wale wenye tabia ya kutoa mimba mara Kwa mara .
Soma Zaidi...