Njia za kiasili zilizotumika zamani kqtika kupima ujauzito

Somo hili linakwenda kukuletea njia za asili walizotumia zamani katika kupima ujauzito

NJIA ZA KIASILI WALIZOTUMIA ZAMANI KUPIMA UJAUZITO:

1.Kukojoa kwenye nafaka (mbegu za ngano na shayiri)Tafiti zilizofnywa na wavumbuzi wa mabo ya kale (archeologist) wamegunduwa kuwa yapata miaka 1350 KK kabla ya kuzaliwa Yesu kuwa wanawake wa Misri (Egypt) walikuwa wanapotaka kujuwa kama wamebeba ujauzito walikuwa wakichukuwa viroba vya ngano na shayiri (barley) kisha wanakojolea kiroba chote. Kama ngano itaota basi mwanamke ana ujauziti tena wa mtoto wa kike. Na kama shayiri itaota atakuwa na ujauzito wa mtoto wa kiume. Na kama nafaka hizi hazitaota basi mwanamke hana ujauzito.

 

Ni kuwa katika mwanamke mjamzito kwenye mojo wake kuna homoni ambazo zinachochea ukuwaji wa mbegu. Baada ya kukojolea pishori lile mbegu hazifukiwi, hivyo ztaota mulemule kwenye kiroba kile bila ya kufukiwa kwenye udogo. Miaka ya 1960 wanasayanzi wa leo walifanya tafiti wakagunduwa kuwa njia hii ni sahihi ya asilimoa 70%.

 

2.Kitunguu.Njia hii ilifanywa na wagiriki mikaa ya zamani sana. Matabibu wa kigiriki walikuwa wanapotaka kujuwa kama mwanmke ana ujauzito walikuwa wakiinguiza kwenye uke wa mwanamke kitunguu na kukiacha humo kwa usiku mzima. Na kama ikifika asubuhi mwanamke akawa anatowa harufu ya kitunguu kwenye mdomo wake basi ana ujauzito. Wagiriki waliamini kuwa mwanamke akiwa na ujauzito uke wake unauwezo mkubwa wa kufyonza vitu. Tafiti hii haikuweza kuthibitishwa na sayansi hili leo.

 

3.Kwa kutumia funguo ama kitasa.Njia hii ilifanya kwa namna hii, endapo mwanamke anajihisi ni mjamzito alikuwa anachukuwa fnguo ama kitasa kisha anaweka kwenye bakuli kisha anakojowa kiasi cha mkojo kuzamisha funguo ama kitasa kisha anaacha hivyo kwa muda wa masaa matatu. Kama akitowa hakuna mabadiliko ya michubuko ama rangi ana chochote basi mwanamke ni mjamzito. Njia hii [ia haikuweza kuthibitishwa hivi leo.

 

4.Kwa kuangalia rangi ya macho.Moja katika matabibu wa zamani sana wa kifaransa aliyetambulika kama Jacques Guillemeau yeye aliamini kuwa macho ndio kioo cha mwili, hivyo unaweza kujuwa maradhi na hali ya mwili wa kutumia macho. Aliamini kuwa mwanamke mjamzito macho yake yameingia ndani kidogo, mboni ya macho yake imesinyaa kidogo na mishipa ya neva ilajitokeza pembezoni mwa macho. Wanasayansi wa leo pia wameshindwa kuthibitisha usahihi wa njia hii, ijapokuwa ni kweli mabadiliko yanaweza kutokea kwenye macho ila si kwa kipindi cha mwanzo.

 

5.Njia uliyojulikana kama Piss ProphetsNjia hii ilitumiaka miaka ya 1600, matabibu hawa walikuwa wakipima ujauzito kwa kutumia kuangalia mkojo. Hawa waliamini kuwa mkojo wa mjamzito unakuwa ni msafi naani hauna uchafu, una rangi ya limao bivu lililopauka lakini unakuwa na ukungu kwa mbali juu yake. Pia matabibu hawa hawakuishia hapa walikuwa wakiangalia uwepo wa maradhi engine kwa kuangalia mkojo. Wanasayansi wa leo pia wameshindwa kuthibitisha usahihi wa njia hii.

 

6.Kwa kutumia riboni:Njia hii ilikuwa na mzunguruko kidogo, nikuwa mwanamke anapojihisi ni mjamzito anakwenda kwa tabibu. Tabibu atamwambia akojoe kwenye beseni, kisha tabibu atachukuwa riboni na kuitia kwenye beseni lenye mkojo. Baada ya muda ataitoa na kuikausha, kisha ataichoma mbele karibu na mwanamke. Kama harufu ya riboni itamfanya mwanamke ahisi kichefuchefu basi atakuwa ana ujauzito. Wanasayansi waleo pia hawakuweza kuthibitisha njia hii.

 

7.Kwa kutimia Sungura ama wanyama wadogo wadogo kama panya.Njia hii iligunduliwa miaka ya 1900 na matabibu waliojulikana kwa majina ya Bernhard Zondek na Selmar Aschheim. Hawa miaka ya 1940 waliamini kuwa mkojo wa mjamzito ukiingizwa kwenye mwili wa vijinyama vidogo basi ovari zao huwa kubwa. Baadaye jaribio hili lilijikita sana kwa kutumia sungura. Wanasayansi wa leo walionyesha kuwa njia hii ilikuwa na ukweli kiasi japo sio njia nzuri maana ilihitajika kumuuwa sungura ili kuchunguza kama ovari zimekuwa kubwa.

 

8.Kwa kutumia chura.Njia hii ilianza kutumika Afrika ya Kusini. Wao walikuwa wakutumia chura wa kike. Waliamini kuwa endapo chura wa kieke akichomwa sindano yenye mkojo wa mwanamke mjamzito, basi chura huyo atataga mayai ndani ya masaa 12.

 

Njia nyingine:9.Kuangalia mwendo, yaani jinsi anavyotembea mjamzito ni tofauti na mwanamke asiye mjamzito.10.Kwa kuaangalia ongezeko la mapigo ya moyo. Kama mapigo ya moyo yameongezeka basi mwanamke ana ujauzito.

 

Njia zilizotajwa hapo juu zilikuwa zukitumika katika nyakati zake na zilionekana kusaidia kwa wakati ule. Ni kweli njia hizo zina madhaifu makubwa lakini si kila wakati zilikuwa zikikosea. Wakati mwingine zilikuwa zikipatia, ni kwa sababu mwanamke alikuwa ni mjamzito kweli. Hata hivyo ilibidi pia kuangalia dalili nyingine za ujauziti ndipo tabubu alikuwa akitoa jibu.

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Uzazi Main: Afya File: Download PDF Views 2554

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Bongolite - Game zone - Play free game    👉2 kitabu cha Simulizi    👉3 Simulizi za Hadithi Audio    👉4 Kitabu cha Afya    👉5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉6 Kitau cha Fiqh   

Post zinazofanana:

Mbinu za kuwakinga watoto na saratani.

Posti hii inahusu zaidi mbinu ambazo tunaweza kuzitumia ili kuwakinga watoto dhidi ya saratani, kama tulivyotangulia kusema kwamba saratani ya watoto mara nyingi Usababishwa na akina Mama hasa kwa sababu ya mtindo wa maisha wakati wa ujauzito kwa hiyo tun

Soma Zaidi...
Ongezeko la homoni ya estrogen

Posti hii inahusu zaidi ongezeko la homoni ya estrogen, kwa kawaida homoni hii ya estrogen inapaswa kulingana ikitokea ikaongezeka uleta madhara mbalimbali kwenye mwili na Kuna dalili ambazo zzz inaweza kujionesha wazi mpaka tukafahamu kuwa ni tatizo la o

Soma Zaidi...
Changamoto za kwenye ndoa kwa waliotoa mimba mara Kwa mara

Posti hii inahusu zaidi changamoto za kwenye ndoa kwa wale waliotoa mimba mara Kwa mara,hizi ni changamoto za wakati wa kufanya tendo na mme wake au mtu mwingine kwa ajili ya kupata mtoto.

Soma Zaidi...
Hatua za Kuzuia Maambukizi ya Uvimbe kwenye ovari na mirija ya uzazi

Posti hii inazungumzia kuhusiana na hatua za kujikinga na Maambukizi ya Uvimbe kwenye ovari na kwenye mirija ya uzazi

Soma Zaidi...
Dalili za kujifunguwa, na dalili za uchungu wa kujifunguwa

Nitajuwaje kama mjamzito amekaribia kujifunguwa, ni dalili gani anaonyesha, dalili za uchungu wa kujifunguwa

Soma Zaidi...
Fahamu dalili za hatari kwa wajawazito.

Posti hii inahusu zaidi dalili za hatari kwa mama mjamzito, kwa sababu kuna baadhi ya Dalili zikitokea kwa mama mjamzito ni vizuri kabisa kuwahi hospitali mara moja.

Soma Zaidi...
Maumivu ya uume baada ya tendo la ndoa

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu maumivu ya uume baada ya tendo la ndoa

Soma Zaidi...
Dalili za Utasa wa wanaume

Posti hii inazungumzia kuhusiana na Utasa wa Mwanaume hutokana na uzalishaji mdogo wa mbegu za kiume, utendakazi usio wa kawaida wa manii au kuziba kwa manii ambayo huzuia utoaji wa mbegu za kiume. Magonjwa, majeraha, matatizo ya kiafya sugu, u

Soma Zaidi...
CHANGAMOTO ZA UJAUZITO, NA DALILI ZAKE NA NAMNA YA KUKABILIANA NAZO

Utawezaje kukabiliana na changamoto za ujauzito, je ni zipi changamoto hizo. Hapa nitakujuza.

Soma Zaidi...
Fahamu Ute unaotoka wakati wa ujauzito

Posti hii inahusu zaidi Ute unaotoka wakati wa ujauzito, kwa kawaida wakati wa ujauzito Kuna Ute ambao utoka na ni tofauti na kawaida pale mwanamke akiwa Hana mimba.

Soma Zaidi...