Somo hili linakwenda kukuletea njia za asili walizotumia zamani katika kupima ujauzito
NJIA ZA KIASILI WALIZOTUMIA ZAMANI KUPIMA UJAUZITO:
1.Kukojoa kwenye nafaka (mbegu za ngano na shayiri)Tafiti zilizofnywa na wavumbuzi wa mabo ya kale (archeologist) wamegunduwa kuwa yapata miaka 1350 KK kabla ya kuzaliwa Yesu kuwa wanawake wa Misri (Egypt) walikuwa wanapotaka kujuwa kama wamebeba ujauzito walikuwa wakichukuwa viroba vya ngano na shayiri (barley) kisha wanakojolea kiroba chote. Kama ngano itaota basi mwanamke ana ujauziti tena wa mtoto wa kike. Na kama shayiri itaota atakuwa na ujauzito wa mtoto wa kiume. Na kama nafaka hizi hazitaota basi mwanamke hana ujauzito.
Ni kuwa katika mwanamke mjamzito kwenye mojo wake kuna homoni ambazo zinachochea ukuwaji wa mbegu. Baada ya kukojolea pishori lile mbegu hazifukiwi, hivyo ztaota mulemule kwenye kiroba kile bila ya kufukiwa kwenye udogo. Miaka ya 1960 wanasayanzi wa leo walifanya tafiti wakagunduwa kuwa njia hii ni sahihi ya asilimoa 70%.
2.Kitunguu.Njia hii ilifanywa na wagiriki mikaa ya zamani sana. Matabibu wa kigiriki walikuwa wanapotaka kujuwa kama mwanmke ana ujauzito walikuwa wakiinguiza kwenye uke wa mwanamke kitunguu na kukiacha humo kwa usiku mzima. Na kama ikifika asubuhi mwanamke akawa anatowa harufu ya kitunguu kwenye mdomo wake basi ana ujauzito. Wagiriki waliamini kuwa mwanamke akiwa na ujauzito uke wake unauwezo mkubwa wa kufyonza vitu. Tafiti hii haikuweza kuthibitishwa na sayansi hili leo.
3.Kwa kutumia funguo ama kitasa.Njia hii ilifanya kwa namna hii, endapo mwanamke anajihisi ni mjamzito alikuwa anachukuwa fnguo ama kitasa kisha anaweka kwenye bakuli kisha anakojowa kiasi cha mkojo kuzamisha funguo ama kitasa kisha anaacha hivyo kwa muda wa masaa matatu. Kama akitowa hakuna mabadiliko ya michubuko ama rangi ana chochote basi mwanamke ni mjamzito. Njia hii [ia haikuweza kuthibitishwa hivi leo.
4.Kwa kuangalia rangi ya macho.Moja katika matabibu wa zamani sana wa kifaransa aliyetambulika kama Jacques Guillemeau yeye aliamini kuwa macho ndio kioo cha mwili, hivyo unaweza kujuwa maradhi na hali ya mwili wa kutumia macho. Aliamini kuwa mwanamke mjamzito macho yake yameingia ndani kidogo, mboni ya macho yake imesinyaa kidogo na mishipa ya neva ilajitokeza pembezoni mwa macho. Wanasayansi wa leo pia wameshindwa kuthibitisha usahihi wa njia hii, ijapokuwa ni kweli mabadiliko yanaweza kutokea kwenye macho ila si kwa kipindi cha mwanzo.
5.Njia uliyojulikana kama Piss ProphetsNjia hii ilitumiaka miaka ya 1600, matabibu hawa walikuwa wakipima ujauzito kwa kutumia kuangalia mkojo. Hawa waliamini kuwa mkojo wa mjamzito unakuwa ni msafi naani hauna uchafu, una rangi ya limao bivu lililopauka lakini unakuwa na ukungu kwa mbali juu yake. Pia matabibu hawa hawakuishia hapa walikuwa wakiangalia uwepo wa maradhi engine kwa kuangalia mkojo. Wanasayansi wa leo pia wameshindwa kuthibitisha usahihi wa njia hii.
6.Kwa kutumia riboni:Njia hii ilikuwa na mzunguruko kidogo, nikuwa mwanamke anapojihisi ni mjamzito anakwenda kwa tabibu. Tabibu atamwambia akojoe kwenye beseni, kisha tabibu atachukuwa riboni na kuitia kwenye beseni lenye mkojo. Baada ya muda ataitoa na kuikausha, kisha ataichoma mbele karibu na mwanamke. Kama harufu ya riboni itamfanya mwanamke ahisi kichefuchefu basi atakuwa ana ujauzito. Wanasayansi waleo pia hawakuweza kuthibitisha njia hii.
7.Kwa kutimia Sungura ama wanyama wadogo wadogo kama panya.Njia hii iligunduliwa miaka ya 1900 na matabibu waliojulikana kwa majina ya Bernhard Zondek na Selmar Aschheim. Hawa miaka ya 1940 waliamini kuwa mkojo wa mjamzito ukiingizwa kwenye mwili wa vijinyama vidogo basi ovari zao huwa kubwa. Baadaye jaribio hili lilijikita sana kwa kutumia sungura. Wanasayansi wa leo walionyesha kuwa njia hii ilikuwa na ukweli kiasi japo sio njia nzuri maana ilihitajika kumuuwa sungura ili kuchunguza kama ovari zimekuwa kubwa.
8.Kwa kutumia chura.Njia hii ilianza kutumika Afrika ya Kusini. Wao walikuwa wakutumia chura wa kike. Waliamini kuwa endapo chura wa kieke akichomwa sindano yenye mkojo wa mwanamke mjamzito, basi chura huyo atataga mayai ndani ya masaa 12.
Njia nyingine:9.Kuangalia mwendo, yaani jinsi anavyotembea mjamzito ni tofauti na mwanamke asiye mjamzito.10.Kwa kuaangalia ongezeko la mapigo ya moyo. Kama mapigo ya moyo yameongezeka basi mwanamke ana ujauzito.
Njia zilizotajwa hapo juu zilikuwa zukitumika katika nyakati zake na zilionekana kusaidia kwa wakati ule. Ni kweli njia hizo zina madhaifu makubwa lakini si kila wakati zilikuwa zikikosea. Wakati mwingine zilikuwa zikipatia, ni kwa sababu mwanamke alikuwa ni mjamzito kweli. Hata hivyo ilibidi pia kuangalia dalili nyingine za ujauziti ndipo tabubu alikuwa akitoa jibu.
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetuUmeionaje Makala hii.. ?
Posti hii inahusu zaidi namna ya kuepuka fangasi za ukeni, ni njia ambazo usaidia kuepuka madhara ya fangasi za ukeni.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi mabaka yanayowasha chini ya matiti, ni ugonjwa ambao uwapata wanawake walio wengi na wengine hawajapata jibu Sababu zake ni zipi na pengine uchukua hatua za kutumia miti shamba wakidai juwa hospitalini nugonjwa huu hautibiwa, ila n
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi homoni ya androgen, ni homoni ambayo imo kwa wanaume na ikizidi kwa kiwango chake inaweza kuleta shida kwenye mwili wa binadamu kwa hiyo homoni hii inaweza kuleta shida iwapo ikiongezeka kwa kiasi kikubwa.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi sababu za mbegu za kiume kuwa dhaifu, hali hii uwatokea wanaume wengi kwa sababu mbalimbali za kimaisha ambazo ufanya mbegu za kiume kuwa dhaifu na kusababisha madhara makubwa zaidi kwa sababu wanaume wengi ushindwa kujiamini kwa h
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi fangasi za ukeni, hili ni tatizo kubwa ambalo linawakumba watoto, akina dada na wanawake kwa hiyo na vizuri kujua Dalili zake na kuweza kuchukua hatua mapema.
Soma Zaidi...Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu sababu za maumivu ya tumbo chini upande wa kulia
Soma Zaidi...Post hii itakujulidha mambo ambayo hupunguza nguvu za kiume
Soma Zaidi...Post hii inahusu zaidi mambo ya kuzingatia iwapo mimba imetoka mambo haya yanaweza yakawahusu akina Mama wenyewe, familia na jamii kwa ujumla.
Soma Zaidi...Nina swali langu:-je maumivu ya nyonga na tumbo la chini ni dalili ya mimba?
Soma Zaidi...Post hii inahusu zaidi sababu za kuvunjika kwa mtoto wakati wa kuzaliwa, kuna wakati mtoto anapozaliwa anaweza kuvunjika kwenye sehemu mbalimbali kwa sababu zifuatazo.
Soma Zaidi...