picha

Zifahamu sifa za mtoto mchanga.

Posti hii inahusu zaidi sifa ambazo mtoto mchanga anapaswa kuwa Nazo,ni sifa ambazo lazima zionekane kwa mtoto mchanga pale anapozaliwa na zikikosa ni lazima kuja kuwa mtoto ana matatizo mbalimbali kwa hiyo zifuatazo ni sifa za mtoto mchanga kama ifuatavy

Sifa za mtoto mchanga.

1. Mwonekano mzima wa mtoto.

Kwanza kabisa mtoto anapaswa kuwa na uzito kuanzia mbili na nukta tano mpaka tatu na nukta tano na kwa kawaida urefu wa mtoto ni kuanzia hamsini sentimita, na rangi  ya mtoto anapozaliwa ni rangi ya pinkie, kwa hiyo mtoto akiwa na uzito chini ya mbili na nukta tano anakuwa kwenye uangalizi kwa mda na pia akiwa na  uzito kuanzia tatu na nukta tano na kuendelea tunasema kwamba ni mtoto aliyezidi kwa uzito kwa hiyo naye huwa kwenye uangalizi maalumu kwa mda na baadae anaweza kuruhusiwa na kuwa kwenye uangalizi wa wazazi.

 

2.Watoto waliochini ya uzito au juu ya uzito uwa kwenye uangalizi kwa sababu, zifuatazo.

Mwenye uzito mkubwa anaweza kuwa amezoea vyakula vya kutosha kutoka kwa Mama yake akiwa tumboni akizaliwa tu anapaswa kuhudumiwa mapema na kupewa glucose Ili kulinganisha na chakula alichokuwa anakipata akiwa tumboni kwa hiyo akicheleweshwa anaweza kushuka kwa sukari. Na pia mtoto akizaliwa na uzito mdogo anapaswa kuangaliwa kwa sababu ya kupata uzito unaotakiwa kwa kihakikisha kuwa Mama yake anapewa elimu ya kumtunza mtoto mpaka akafikia kuwa na uzito unaotakiwa.

 

3. Pia mtoto akizaliwa anapaswa kuwa na kitovu kilicho kwenye tumbo na kinatakiwa kukatwa kwa uangalizi unaofaa Ili kuweza kuzuia maambukizi kutoka kwa Mama kwenda kwa mtoto, pia na Mama anapaswa kupewa elimu kuhusu namna ya kumtunza kitovu cha mtoto wafundishwe kuwa kitovu cha mtoto kinakauka baada ya siku kumi, pia akina Mama wanapaswa kukumbushwa kuwa waachane na tabia ya kuweka vitu visivyofaa kwenye kitovu kwa kufuata mila na desturi zao hali inayosababisha kuwepo kwa tetunus kwenye kitovu kikitunzwa visivyo.

 

4. Pia kitu kingine ambacho ni sifa ya mtoto ni kulia tu baada ya kuzaliwa hii ikiwa ni ishara ya uhai kwa mtoto,kwa hiyo mtoto asipolia wauguzi na wasaidizi wote wanapaswa kihakikisha mtoto analia kwa kutoa huduma ya kwanza kwa mtoto na walio wengi wanafanyiwa na wanapona na kuendelea kwenye hali ya kawaida

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu
Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Uzazi Main: Post File: Download PDF Views 3891

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Kitabu cha Afya     👉2 Bongolite - Game zone - Play free game     👉3 ai web app     👉4 Simulizi za Hadithi Audio     👉5 Madrasa kiganjani     👉6 web hosting    

Post zinazofanana:

Dalili za saratani kwa watoto.

Posti hii inahusu zaidi Dalili za saratani kwa watoto, ni Dalili ambazo ujitokeza kwa watoto na ikiwa mlezi au mzazi akiziona tu anaweza kutambua mara moja kwamba hii ni saratani au la na kama bado ana wasiwasi anaweza kupata msaada zaidi kutoka kwa wataa

Soma Zaidi...
Madhara ya fangasi ukeni

Maambukizi ya fangasi katika sehemu za Siri za mwanamke husababishwa na fangasi wanaoitwa CANDIDA ALBICANS pia maambukizi haya hujulikana kama YEAST INFECTION. Pia hupatikana katika midomo, mpira wa kupitisha chakula,kibofu Cha mkojo ,uume na uke.

Soma Zaidi...
VYAKULA VYA KUONGEZA HAMU YA TENDO LA NDOA NA NGUVU ZA KIUME

Matatizo yahusianayo na nguvu za kume na kukosa hamu ya tendo la ndoa kwahuweza kuchangiwa sana na mpangilio mbovu wa vyakula pamoja na saikolojia ya mtu.

Soma Zaidi...