Posti huu inahusu zaidi malengo ya huduma za uzazi kwa akina Mama, ni huduma muhimu ambazo zimetolewa kwa akina Mama ili kuweza kuepuka hatari mbalimbali zinazowakumba akina Mama wakati wa ujauzito, kujifu na malezi ya watoto chini ya miaka mitano.
Malengo ya huduma za uzazi kwa akina Mama.
1.Kuangali Magonjwa yanayoweza kutokea kwa wajawazito na kuwapatia dawa mapema ili wasiweze kuwaambukiza watoto.hili ni lengo mojawapo kuhakikisha kubwa kama kuna dalili yoyote ya ugonjwa ambao unaweza kujitokeza na kuwa tayari kuwapatia dawa ili kutibu na kuepuka kuwaambukiza watoto wakati wa ujauzito, mfano wa magonjwa ni kaswende na HIV kutoka kwa Mama kwenda kwa mtoto na kwa asilimia tisini hili limeweza kufanikiwa katika jamii zilizo nyingi.
2.Kuhakikisha kwamba maendeleo ya mtoto na Mama yako vizuri. Kwa kuhakikisha kuwa Mama anakuwa na damu ya kutosha mwilini kwa kupima wingi wa damu, kumpatia Mama dawa za minyoo na kupima kama kuna Malaria na kumpatia Mama vidonge vya sp kwa kila udhulio na kumpatia Mama neti mara tu anapoanza kliniki kwa kufanya hivyo Mama anaweza kuwa na afya nzuri pamoja na mtoto wake.
3. Kuhakikisha kuwa Mama anajua Maana ya uzazi wa mpango ili aweze kupata watoto anaowahitaji na kuwa na distansi fulani kama ni kuzidiana miaka minne au mitano kuu kadri ya maamuzi ya wazazi wenyewe kwa kufanya hivyo watoto wanaozaliwa wanapata upendo kutoka kwa wazazi wao na pia Mama anapata nafasi ya kushiriki kwenye shughuli za kiuchumi kwa kupata mda wa kutosha badala ya kubaki katika kulea watoto wanaofuatana bila mpangilio.
4.Lengo lingine ni kuhakikisha kuwa Dalili za hatari wakati wa ujauzito zinapungua kwa kuwapatia akina mama elimu kabla ya kuanza mahudhurio ili mama akiona dalili mojawapo ambayo ni ya hatari aweze kuja hospitali mara moja ili kuepuka madhara kwa mtoto, Dalili hizo ni pamoja na mtoto kushindwa kucheza, kugongwa na kichwa, kizungu Zungu, kutoka damu ukeni, kuhisi maumivu makali ya tumbo, homa kali na mabadiliko mengine ambayo siyo ya kawaida kwa Mwanamke mjamzito.
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetuUmeionaje Makala hii.. ?
Posti hii inahusu zaidi ugonjwa wa ugumu wa choo na tiba yake kwa wajawazito, ni ugonjwa unaowapata sana akina mama wajawazito na uisha tu pale Mama anapojifungua kwa hiyo tunapaswa kujua wazi sababu za ugumu wa choo na tiba yake kwa wajawazito.
Soma Zaidi...Posti hii inaelezea namna mwanamke anavyoweza kupata Ugonjwa wa Maambukizi ya mfumo wa Uzazi.
Soma Zaidi...Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu dalili za mimba kuanzia siku ya 7 Hadi ya 14
Soma Zaidi...Posti hii inazungumzia kuhusiana na maambukizi na uvimbe katika mirija ya uzazi. Mara nyingi hutumiwa sawa na ugonjwa wa uvimbe kwenye fupa nyonga (PID), ingawa PID haina ufafanuzi sahihi na inaweza kurejelea magonjwa kadhaa ya njia ya juu ya uzazi
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi madhara ya fangasi ukeni, madhara mbalimbali yanayoweza kutokea iwapo mtu hakutibiwa fangasi mapema.
Soma Zaidi...Miongoni mwa changamoto za ujauzito ni maumivu ya tumbo. Maumivu haya yanawezakuwaya kawaida ama makali zaidi. Vyema kufika Kituo cha Afya endapoyatakuwa makali.
Soma Zaidi...Nini humaanisha kama chuchu zinauma na hupati period mwanaidi mrefu.
Soma Zaidi...Postii inafundisha maandalizi ya mama kwa ajili ya kujifungulia hii Ni muhimu Sana kwa wale ambao hawajawahi kujingua Ni mara yao ya kwanza wanatakiwa kujua na kuelewa vifaa na mahitaji kujifungulia na kwa wale wanaohudhuria clinic huwa wanafundisha.
Soma Zaidi...Kuna uwezekano una ujauzito ila hujajijuwa, huwenda hujapata dalili zozote. Unataka kujuwa kama una ujauzito baada ya tendo la ndoa.
Soma Zaidi...