Sababu za mimba kutoka


image


Post hii inahusu zaidi sababu za mimba kutoka, hili ni tatizo ambalo linawakumba wanawake wengi ambapo mimba utoka kabla ya kumfikisha mda wake, kwa kawaida Ili kawaida mimba nyingi utoka zikiwa na miezi chini ya Saba au wengine wanaweza kusema kwamba mimba utoka zikiwa na wiki ishilini na nne. Kwa hiyo zifuatazo ni baadhi ya sababu zinazochangia mimba kutoka.


Sababu za mimba kutoka.

1. Sababu ya kwanza ni kuwepo kwa maambukizi hasa kwa akina Mama.

Maambukizi kama vile kaswende kisonono na mengine kama hayo usababisha mimba kutoka hasa pale yanaposhambuliwa sehemu ya kondo la nyuma na kusababisha kulegea na hatimaye mimba kutoka.

 

2.  Kuwepo kwa homa inayozidi kipimo au homa kuwa juu sana, kwa kawaida kiwango cha homa kwa mwanamke kinapaswa kuwa kawaida ila kikizidi kiasi usababisha kuwepo kwa kuharibu sehemu mbalimbali hasa kwa mtoto hatimaye kusababisha mimba kutoka, kwa hiyo akina Mama wanapaswa kufahamu kwamba homa yoyote isiyo ya kawaida wakati wa ujauzito ni hatari kwa makuzi ya mtoto tumboni.

 

3. Mishutuko mbalimbali.

Mishutuko mbalimbali inayoweza kuwa ya moja kwa Moja au isiyokuwa ya Moja kwa Moja usababisha mimba kutoka, kwa mfano mama kupigwa sehemu za tumbo usababisha mishutuko kwenye sehemu zilizoshikilia mtoto na kusababisha mimba kutoka au kwa wakati mwingine mishutuko inayosababishwa na msongo wa mawazo pamoja na mambo ya kusikitisha yanaweza kusababisha mimba kutoka. Kwa hiyo jamii inapaswa kumtunza Mama na kuhakikisha anapata mazingira mazuri Ili kuweza kuruhusu mimba kukua vizuri.

 

4. Magonjwa mbalimbali nayo usababisha mimba kutoka.

Kuna baadhi ya magonjwa ambayo usababisha mimba kutoka hasa kama ni ya mda mrefu kwa mama mjamzito hayo ni kama kisukari cha kupanda na kushuka, shinikizo la damu na ukosefu wa baadhi ya homoni au vichocheo vinavyosababisha makuzi ya mtoto mfano kichocheo cha progesterone kikipungua ni hatari kwa makuzi ya mtoto tumboni, sio kwamba walio na magonjwa haya wote mimba utoka hapana ila wakiamua kuchukua matibabu na kufuata mashariti Wana uwezo wa kujifungua salama. Kwa hiyo kama mjamzito yeyote anajua ana tatizo hilo ni vizuri kabisa kupata ushauri kwa wataalamu wa afya na kupata matibabu Ili kuokoa maisha ya Mama na mtoto.

 

5. Baadhi ya madawa na mazingira magumu usababisha mimba kutoka.

Kuna watu ambao katika maisha yao wamezoea kutumia madawa ambayo ni hatari wakiendelea kutumia hasa wakiwa na wajawazito madawa hayo ni kama madawa ya kulevya,watumiaji wa quinine wakiwa na malaria, matumizi ya vinywaji vikali kama vile konyagi matumizi ya sigara, haya yote usababisha kutoka kwa mimba kabla ya wakati, kwa hiyo ni vizuri kabisa kama mama akubeba mimba anapaswa kuachana nayo kabisa Ili aweze kupata mtoto mwenye afya.

 

6. Kukosa mlo  kamili wa kutosha na wenye virutubisho mbalimbali.

Kwa kawaida mama akibeba mimba damu upungua kwa hiyo anapaswa kula vyakula vya kuongeza damu Ili kuweza kupata mtoto mwenye afya na afya ya mama mwenyewe, ila Kuna akina Mama ambao wakibeba mimba hawali kabisa au wanakula chakula kidogo hali inayosababishwa kutoka kwa mimba au wakati mwingine wanakula aina Moja ya chakula na kusababisha kukosa kwa madini kwa mtoto hatimaye mimba kutoka, kwa hiyo akina Mama wanashauliwa kula mboga za majani, matunda na vyakula vya madini ya chuma.

 

7. Kuwepo kwa maambukizi kwenye mfuko wa kizazi.

Kuna wakati mwingine kwenye mfuko wa kizazi kunakuwepo na maambukizi, hali ambayo usababisha mimba kutoka kwa sababu ya kuwepo kwa maambukizi. Kwa hiyo akina Mama wanapaswa kutumia dawa mbalimbali Ili kuweza kuepuka mimba kutoka kwa sababu ya kuwepo kwa maambukizi.

 

8. Kutoa mimba mara kwa mara.

Hii ni tabia inayohusu zaidi akina dada wakiwa bado hawajahitaji watoto ila wanakuwa na wapenzi wao hali inayosababisha kubeba mimba na kutoka kwa hiyo kwenye mfumo wa uzazi ujitengenezea mazingira ya kutoa mimba kabla ya kukomaa hali inayosababisha mimba kutoka kwa sababu ya mazoea ya mara kwa mara. Kwa hiyo akina dada wanapaswa kuacha tabia ya kutoa mimba ila watumie uzazi wa mpango au wasubiri wakati.

 



Sponsored Posts


  ðŸ‘‰    1 Download App zetu hapa ujifunze zaidi       ðŸ‘‰    2 Tunakukaribisha kwenye Maktaba yetu       ðŸ‘‰    3 Jifunze Fiqh       ðŸ‘‰    4 Madrasa kiganjani offline    


Je una maswali, maoni ama ushauri, tutumie sms ✉ bofya hapa hapa, ama wasiliana nasi kwa WhatsApp bofya hapa



Post Nyingine


image Vyanzo vya magonjwa yanayotokea kwenye sehemu za siri
Posti hii inahusu zaidi vyanzo vya magonjwa yanayotokea kwenye sehemu za siri,kwa sababu siku kwa siku kuna magonjwa mengi yanayotokea kwenye sehemu za siri ila kuna vyanzo mbalimbali ambavyo usababisha kuwepo kwa magonjwa kwenye sehemu mbalimbali za siri kama tutakavyoona. Soma Zaidi...

image Dr nahis kuchanganyikiwa nimetoka niliingia hedhi tar 18 mwezi wa9 lakini saivi Jana tena nmeingia dr hii imekaaje mimi?
Kamaumeshawahi kujiuliza kuhusu kutokwaba damu tofautivna siku za hedhi, base mwaka hii ni kwaajiki yako. Soma Zaidi...

image Tofauti za uke
Posti hii inahusu zaidi tofauti mbalimbali za uke, kwa sababu ya kuwepo kwa matatizo mbalimbali kwenye mwili wa binadamu kuna tofauti mbalimbali za ute kutegemea na hali iliyopo. Soma Zaidi...

image Habari Mimi ni mjamzito was miezi Tisa sasa nimeanza kutokwa na maji kidogo kidogo ukeni bila uchungu na no mimba yangu ya kwanza he Kuna shida?
Ujauzito husababisha mabadiliko mengi mwilini, ikiwepo ongezeko la Majimaji ukeni ifikapo tarehe za kukaribia kujifunguwa. Majimaji haya ni muhimu kwa afya ya mtoto aliye tumboni. Soma Zaidi...

image Mambo muhimu kuhusu mbegu za kiume
Post hii inahusu zaidi mambo muhimu ambayo tunapaswa kujua au kufahamu kuhusu mbegu za kiume, kwa kuwa mbegu za kiume usaidia katika utungaji wa mimba kwa hiyo ni vizuri kabisa kuzitunza Ili kuweza kuepuka matatizo mbalimbali ambayo yanaweza kutokea kwa sababu ya kutokutunza vizuri mbegu za kiume. Soma Zaidi...

image Je inaweza ukaingia period wakati unaujauzito?
Ukiwa mjamzito unaweza kushuhudia kutokwa na damu. Je damu hii ni ya hedhi? Soma Zaidi...

image Madhara ya fangasi ukeni
Maambukizi ya fangasi katika sehemu za Siri za mwanamke husababishwa na fangasi wanaoitwa CANDIDA ALBICANS pia maambukizi haya hujulikana kama YEAST INFECTION. Pia hupatikana katika midomo, mpira wa kupitisha chakula,kibofu Cha mkojo ,uume na uke. Soma Zaidi...

image Madhara ya kupungua kwa homoni ya projestron
Posti hii inahusu zaidi madhara ambayo yanaweza kutokea ikiwa homoni ya projestron ikipungua mwilini na pia kuweza kutambua dalili za kupungua kwa homoni hii ya progesterone. Soma Zaidi...

image Habari, naomba kuulizia, nimadhara gani atayapata mwanamke akitolewa bikra bila kukusudia
Je unawaza nini endapo bikra itatolewa bila wewe kukusudia, je imetolewa kwa njia ya kawaida yaani uume ama ilikuwa ni ajali? Soma Zaidi...

image Dalili za kifafa cha mimba.
Posti hii inahusu zaidi Dalili za Mama mwenye kifafa cha mimba, ili kifafa cha mimba kiweze kutokea lazima kuna dalili ambazo uweza kutokea kwa Mama kama ifuatavyo. Soma Zaidi...