image

Sababu za mimba kutoka

Post hii inahusu zaidi sababu za mimba kutoka, hili ni tatizo ambalo linawakumba wanawake wengi ambapo mimba utoka kabla ya kumfikisha mda wake, kwa kawaida Ili kawaida mimba nyingi utoka zikiwa na miezi chini ya Saba au wengine wanaweza kusema kwamba mim

Sababu za mimba kutoka.

1. Sababu ya kwanza ni kuwepo kwa maambukizi hasa kwa akina Mama.

Maambukizi kama vile kaswende kisonono na mengine kama hayo usababisha mimba kutoka hasa pale yanaposhambuliwa sehemu ya kondo la nyuma na kusababisha kulegea na hatimaye mimba kutoka.

 

2.  Kuwepo kwa homa inayozidi kipimo au homa kuwa juu sana, kwa kawaida kiwango cha homa kwa mwanamke kinapaswa kuwa kawaida ila kikizidi kiasi usababisha kuwepo kwa kuharibu sehemu mbalimbali hasa kwa mtoto hatimaye kusababisha mimba kutoka, kwa hiyo akina Mama wanapaswa kufahamu kwamba homa yoyote isiyo ya kawaida wakati wa ujauzito ni hatari kwa makuzi ya mtoto tumboni.

 

3. Mishutuko mbalimbali.

Mishutuko mbalimbali inayoweza kuwa ya moja kwa Moja au isiyokuwa ya Moja kwa Moja usababisha mimba kutoka, kwa mfano mama kupigwa sehemu za tumbo usababisha mishutuko kwenye sehemu zilizoshikilia mtoto na kusababisha mimba kutoka au kwa wakati mwingine mishutuko inayosababishwa na msongo wa mawazo pamoja na mambo ya kusikitisha yanaweza kusababisha mimba kutoka. Kwa hiyo jamii inapaswa kumtunza Mama na kuhakikisha anapata mazingira mazuri Ili kuweza kuruhusu mimba kukua vizuri.

 

4. Magonjwa mbalimbali nayo usababisha mimba kutoka.

Kuna baadhi ya magonjwa ambayo usababisha mimba kutoka hasa kama ni ya mda mrefu kwa mama mjamzito hayo ni kama kisukari cha kupanda na kushuka, shinikizo la damu na ukosefu wa baadhi ya homoni au vichocheo vinavyosababisha makuzi ya mtoto mfano kichocheo cha progesterone kikipungua ni hatari kwa makuzi ya mtoto tumboni, sio kwamba walio na magonjwa haya wote mimba utoka hapana ila wakiamua kuchukua matibabu na kufuata mashariti Wana uwezo wa kujifungua salama. Kwa hiyo kama mjamzito yeyote anajua ana tatizo hilo ni vizuri kabisa kupata ushauri kwa wataalamu wa afya na kupata matibabu Ili kuokoa maisha ya Mama na mtoto.

 

5. Baadhi ya madawa na mazingira magumu usababisha mimba kutoka.

Kuna watu ambao katika maisha yao wamezoea kutumia madawa ambayo ni hatari wakiendelea kutumia hasa wakiwa na wajawazito madawa hayo ni kama madawa ya kulevya,watumiaji wa quinine wakiwa na malaria, matumizi ya vinywaji vikali kama vile konyagi matumizi ya sigara, haya yote usababisha kutoka kwa mimba kabla ya wakati, kwa hiyo ni vizuri kabisa kama mama akubeba mimba anapaswa kuachana nayo kabisa Ili aweze kupata mtoto mwenye afya.

 

6. Kukosa mlo  kamili wa kutosha na wenye virutubisho mbalimbali.

Kwa kawaida mama akibeba mimba damu upungua kwa hiyo anapaswa kula vyakula vya kuongeza damu Ili kuweza kupata mtoto mwenye afya na afya ya mama mwenyewe, ila Kuna akina Mama ambao wakibeba mimba hawali kabisa au wanakula chakula kidogo hali inayosababishwa kutoka kwa mimba au wakati mwingine wanakula aina Moja ya chakula na kusababisha kukosa kwa madini kwa mtoto hatimaye mimba kutoka, kwa hiyo akina Mama wanashauliwa kula mboga za majani, matunda na vyakula vya madini ya chuma.

 

7. Kuwepo kwa maambukizi kwenye mfuko wa kizazi.

Kuna wakati mwingine kwenye mfuko wa kizazi kunakuwepo na maambukizi, hali ambayo usababisha mimba kutoka kwa sababu ya kuwepo kwa maambukizi. Kwa hiyo akina Mama wanapaswa kutumia dawa mbalimbali Ili kuweza kuepuka mimba kutoka kwa sababu ya kuwepo kwa maambukizi.

 

8. Kutoa mimba mara kwa mara.

Hii ni tabia inayohusu zaidi akina dada wakiwa bado hawajahitaji watoto ila wanakuwa na wapenzi wao hali inayosababisha kubeba mimba na kutoka kwa hiyo kwenye mfumo wa uzazi ujitengenezea mazingira ya kutoa mimba kabla ya kukomaa hali inayosababisha mimba kutoka kwa sababu ya mazoea ya mara kwa mara. Kwa hiyo akina dada wanapaswa kuacha tabia ya kutoa mimba ila watumie uzazi wa mpango au wasubiri wakati.

 





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Topic: Uzazi Main: Post File: Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 1629


Sponsored links
👉1 Simulizi za Hadithi Audio     👉2 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉3 kitabu cha Simulizi     👉4 Kitabu cha Afya     👉5 Madrasa kiganjani     👉6 Kitau cha Fiqh    

Post zifazofanana:-

faida za tendo ka ndoa wakati wa ujauzito
Kufanya tendo la ndoa wakati wa ujauzito kina faida nyingi kwa mama na mtoto. Miongni mwa faida hizo ni kuimarisha mfumo wa kinga wa mama, kumuondolea stress na ukuajinmzuri wa mimba Soma Zaidi...

Sababu za kutokea uvimbe kwenye kizazi.
Posti hii inahusu zaidi sababu za kuwepo kwa uvimbe kwenye kizazi,kwa kawaida tumesikia akina mama wengi wanalalamika kuhusu kuwepo kwa uvimbe kwenye kizazi na wengine hawajui sababu zake kwa hiyo sababu zifuatazo ni za kuwepo kwa uvimbe kwenye kizazi. Soma Zaidi...

Njia za kuzuia Malaria kwa wajawazito
Posti hii inahusu zaidi njia mbalimbali za kuzuia Malaria kwa wajawazito na watoto wao wakiwa bado tumboni, tunajuwa wazi kuwa wajawazito wakipata Malaria inaweza kupelekea mimba kutoka kwa hiyo ili kuzuia tatizo hili zifuatazo ni njia zilizowekwa ili kuz Soma Zaidi...

Mabaka yanayowasha chini ya matiti.
Posti hii inahusu zaidi mabaka yanayowasha chini ya matiti, ni ugonjwa ambao uwapata wanawake walio wengi na wengine hawajapata jibu Sababu zake ni zipi na pengine uchukua hatua za kutumia miti shamba wakidai juwa hospitalini nugonjwa huu hautibiwa, ila n Soma Zaidi...

Tatizo la kutokwa na majimaji kwenye uume.
Posti hii inahusu zaidi tatizo la kutokwa na majimaji kwenye uume, ni tatizo ambalo uwakumba baadhi ya wanaume kwa sababu mbalimbali na pia Ugonjwa huu unatibika hasa kwa wale wanaowahi kupata matibabu. Soma Zaidi...

Huduma kwa mama mwenye kifafa cha mimba.
Posti hii inahusu zaidi huduma ambazo wajawazito wanaweza kuzipata wakiwa na Dalli au tayari wana kifafa cha mimba. Soma Zaidi...

Faida na hasara za kutumia kondomu kama njia ya uzazi wa mpango
Kondomu ni mpira ambao uwekwa kwenye uke au uume kwa ajili ya kuzuia mimba wakati wa kujamiiana Soma Zaidi...

Uchungu usio wa kawaida kwa akina Mama.
Posti hii inahusu zaidi uchungu usio wa kawaida kwa akina Mama, kwa kawaida uchungu unapaswa kuwa ndani ya masaa Kumi na mawili ila Kuna wakati mwingine uchungu unaweza kuwa zaidi ya masaa Kumi na mawili na kusababisha madhara yasiyo ya kawaida kwa Mama n Soma Zaidi...

Dalili za mimba changa
Zijuwe dalili 17 za mimba na mimba changa, kuanzia siku ya kwanza mpaka mwezi mmoja Soma Zaidi...

dalili za uchungu kwa mama mjamzito
Makala hii itakwenda kukufundisha baadhi ya dalili za uchungu kwa mama mjamzito. Soma Zaidi...

Tabia za Ute wa siku za hatari kupata mimba au ovulation
Posti hii inahusu zaidi tabia mbalimbali za Ute wa ovulation kwa sababu Ute huu huwa tofauti na Ute mwingine kwa sababu ya kuwepo kwa tabia zake za kipekee kama tutakavyoona. Soma Zaidi...

Madhara ya mwili kushindwa kutengeneza projestron ya kutosha
Posti hii inahusu zaidi madhara ambayo mtu anaweza kupata ikiwa mwili utaeweza kutengeneza progesterone ya kutosha. Soma Zaidi...