SABABU ZA MIMBA KUTOKA


image


Post hii inahusu zaidi sababu za mimba kutoka, hili ni tatizo ambalo linawakumba wanawake wengi ambapo mimba utoka kabla ya kumfikisha mda wake, kwa kawaida Ili kawaida mimba nyingi utoka zikiwa na miezi chini ya Saba au wengine wanaweza kusema kwamba mimba utoka zikiwa na wiki ishilini na nne. Kwa hiyo zifuatazo ni baadhi ya sababu zinazochangia mimba kutoka.


Sababu za mimba kutoka.

1. Sababu ya kwanza ni kuwepo kwa maambukizi hasa kwa akina Mama.

Maambukizi kama vile kaswende kisonono na mengine kama hayo usababisha mimba kutoka hasa pale yanaposhambuliwa sehemu ya kondo la nyuma na kusababisha kulegea na hatimaye mimba kutoka.

 

2.  Kuwepo kwa homa inayozidi kipimo au homa kuwa juu sana, kwa kawaida kiwango cha homa kwa mwanamke kinapaswa kuwa kawaida ila kikizidi kiasi usababisha kuwepo kwa kuharibu sehemu mbalimbali hasa kwa mtoto hatimaye kusababisha mimba kutoka, kwa hiyo akina Mama wanapaswa kufahamu kwamba homa yoyote isiyo ya kawaida wakati wa ujauzito ni hatari kwa makuzi ya mtoto tumboni.

 

3. Mishutuko mbalimbali.

Mishutuko mbalimbali inayoweza kuwa ya moja kwa Moja au isiyokuwa ya Moja kwa Moja usababisha mimba kutoka, kwa mfano mama kupigwa sehemu za tumbo usababisha mishutuko kwenye sehemu zilizoshikilia mtoto na kusababisha mimba kutoka au kwa wakati mwingine mishutuko inayosababishwa na msongo wa mawazo pamoja na mambo ya kusikitisha yanaweza kusababisha mimba kutoka. Kwa hiyo jamii inapaswa kumtunza Mama na kuhakikisha anapata mazingira mazuri Ili kuweza kuruhusu mimba kukua vizuri.

 

4. Magonjwa mbalimbali nayo usababisha mimba kutoka.

Kuna baadhi ya magonjwa ambayo usababisha mimba kutoka hasa kama ni ya mda mrefu kwa mama mjamzito hayo ni kama kisukari cha kupanda na kushuka, shinikizo la damu na ukosefu wa baadhi ya homoni au vichocheo vinavyosababisha makuzi ya mtoto mfano kichocheo cha progesterone kikipungua ni hatari kwa makuzi ya mtoto tumboni, sio kwamba walio na magonjwa haya wote mimba utoka hapana ila wakiamua kuchukua matibabu na kufuata mashariti Wana uwezo wa kujifungua salama. Kwa hiyo kama mjamzito yeyote anajua ana tatizo hilo ni vizuri kabisa kupata ushauri kwa wataalamu wa afya na kupata matibabu Ili kuokoa maisha ya Mama na mtoto.

 

5. Baadhi ya madawa na mazingira magumu usababisha mimba kutoka.

Kuna watu ambao katika maisha yao wamezoea kutumia madawa ambayo ni hatari wakiendelea kutumia hasa wakiwa na wajawazito madawa hayo ni kama madawa ya kulevya,watumiaji wa quinine wakiwa na malaria, matumizi ya vinywaji vikali kama vile konyagi matumizi ya sigara, haya yote usababisha kutoka kwa mimba kabla ya wakati, kwa hiyo ni vizuri kabisa kama mama akubeba mimba anapaswa kuachana nayo kabisa Ili aweze kupata mtoto mwenye afya.

 

6. Kukosa mlo  kamili wa kutosha na wenye virutubisho mbalimbali.

Kwa kawaida mama akibeba mimba damu upungua kwa hiyo anapaswa kula vyakula vya kuongeza damu Ili kuweza kupata mtoto mwenye afya na afya ya mama mwenyewe, ila Kuna akina Mama ambao wakibeba mimba hawali kabisa au wanakula chakula kidogo hali inayosababishwa kutoka kwa mimba au wakati mwingine wanakula aina Moja ya chakula na kusababisha kukosa kwa madini kwa mtoto hatimaye mimba kutoka, kwa hiyo akina Mama wanashauliwa kula mboga za majani, matunda na vyakula vya madini ya chuma.

 

7. Kuwepo kwa maambukizi kwenye mfuko wa kizazi.

Kuna wakati mwingine kwenye mfuko wa kizazi kunakuwepo na maambukizi, hali ambayo usababisha mimba kutoka kwa sababu ya kuwepo kwa maambukizi. Kwa hiyo akina Mama wanapaswa kutumia dawa mbalimbali Ili kuweza kuepuka mimba kutoka kwa sababu ya kuwepo kwa maambukizi.

 

8. Kutoa mimba mara kwa mara.

Hii ni tabia inayohusu zaidi akina dada wakiwa bado hawajahitaji watoto ila wanakuwa na wapenzi wao hali inayosababisha kubeba mimba na kutoka kwa hiyo kwenye mfumo wa uzazi ujitengenezea mazingira ya kutoa mimba kabla ya kukomaa hali inayosababisha mimba kutoka kwa sababu ya mazoea ya mara kwa mara. Kwa hiyo akina dada wanapaswa kuacha tabia ya kutoa mimba ila watumie uzazi wa mpango au wasubiri wakati.

 



Sponsored Posts


  ðŸ‘‰    1 Magonjwa na afya       ðŸ‘‰    2 Jifunze fiqh       ðŸ‘‰    3 Hadiythi za alif lela u lela       ðŸ‘‰    4 Madrasa kiganjani       ðŸ‘‰    5 Maktaba ya vitabu       ðŸ‘‰    6 Mafunzo ya php    


Je! una maswali, mapendekezo ama maoni? tuma ujumbe wa meseji SMS hapo chini ili kuunganishwa na muhusika au bofya hapa

SMS SMS



Post Nyingine


image Changamoto za kwenye ndoa kwa waliotoa mimba mara Kwa mara
Posti hii inahusu zaidi changamoto za kwenye ndoa kwa wale waliotoa mimba mara Kwa mara,hizi ni changamoto za wakati wa kufanya tendo na mme wake au mtu mwingine kwa ajili ya kupata mtoto. Soma Zaidi...

image Madhara ya mwili kushindwa kutengeneza projestron ya kutosha
Posti hii inahusu zaidi madhara ambayo mtu anaweza kupata ikiwa mwili utaeweza kutengeneza progesterone ya kutosha. Soma Zaidi...

image Dalili za kuziba kwa mirija ya uzazi
Posti hii inahusu zaidi dalili ambazo zinaweza kutokea kwa sababu ya kuziba kwa mishipa ya uzazi, ni baadhi ya dalili ambazo ujitokeza kwa sababu ya kuwepo kwa tatizo la kuziba kwa mishipa ya uzazi. Soma Zaidi...

image Sababu za mimba ya miezi 4-6 kutoka.
Posti hii inahusu zaidi sababu za mimba ya miezi kuanzia minne mpaka sita kutoka , Kuna kipindi mimba kuanzia miezi mimne mpaka sita utoka kwa sababu mbalimbali. Soma Zaidi...

image Fahamu mtoto aliyetanguliza matako wakati wa kuzaliwa
Posti hii inahusu zaidi mtoto aliyetanguliza matako wakati wa kuzaliwa, kwa kawaida tunajua kwamba mtoto wakati wa kuzaliwa ni lazima atangulize kichwa ila Kuna kipindi mtoto anatanguliza matako, kuna aina nne za mtoto kutanguliza matako. Soma Zaidi...

image je mtu kam anaona dalili za mimb ila akapima nakipim hakijamuonyesha kam ana mimb am hana je kuna uwezekan wakuw anayo
Dalili za mimba pekee haziwezi kuthibitisha uwepo wa mimba. Bila vipimo kwa. Muda sahihi huwezi kuwa. Na uhakika. Je na wewe unasumbuliwa na dalili za mimba na ukapona hakuna mimba? Makala hii ni kwa ajili yako. Swali Soma Zaidi...

image Dawa inaitwa koflame ukitumia inashida kwa mama mjamzito? Maumivu ya mgongo na nyonga zinasumbua
Maumivu ya mgongo hutokea sana kwa wajawazito. Ijapokuwa ni hali ya usumbufu sana ila hakikisha hautumii madawa kiholela kutoka maduka ya dawa ama miti shamba. Kwani ukikisea kidogobinawezabhatarisha afya ya mtoto Soma Zaidi...

image Njia za kuongeza uwezo wa kuzaa au kuzalisha.
Posti hii inahusu zaidi njia mbalimbali za kuongeza uwezo wa kuzaa au kuzalisha kwa sababu kuna familia nyingi zinakosa watoto sio kwa sababu ni tasa ila kuna njia mbalimbali za kuongeza uwezo wa kuzaa kama ifuatavyo. Soma Zaidi...

image Fahamu dalili za mapacha walio unganishwa
Mapacha walioungana ni watoto wawili wanaozaliwa wakiwa wameunganishwa kimwili. Mapacha walioungana hukua wakati kiinitete cha mapema kinapojitenga na kuunda watu wawili. Ingawa fetusi mbili zitakua kutoka kwa kiinitete hiki, zitabaki zimeunganishwa mara nyingi kwenye kifua, pelvis au matako. Mapacha walioungana wanaweza pia kushiriki kiungo kimoja au zaidi cha ndani. Mapacha wengi walioungana huzaliwa wakiwa wamekufa au hufariki muda mfupi baada ya kuzaliwa. Baadhi ya mapacha waliosalia walioungana wanaweza kutenganishwa kwa upasuaji. Mafanikio ya upasuaji wa kutenganisha mapacha walioungana inategemea mahali ambapo mapacha wameunganishwa na wangapi na viungo gani vinashirikiwa, na pia juu ya uzoefu na ujuzi wa timu ya upasuaji. Soma Zaidi...

image Dalili ninazoziona kwangu chuchu zinauma na sjapata period mwezi huu na nlishiriki tarehe 19 mwezi wa tisa
Nini humaanisha kama chuchu zinauma na hupati period mwanaidi mrefu. Soma Zaidi...