Post hii inakwenda kukufundisha kuhusu nadharia ya kupata mtoto wa kiume.
Habari,
Nashukuru kwa kuelewa jinsi ya kukokotoa siku na kupata siku za kutungwa mimba. Mimi siku zangu hubadilika mara kwa mara, lakini mara nyingi huwa siku 31 au 32. Shida yangu ni kupata mtoto wa kiume, nifanyeje katika hilo?
Jibu
Kwanza kabisa, ni vizuri kujua kuwa kupata mtoto wa kiume au wa kike hakuna njia yenye uhakika wa kitaalamu. Kuna nadharia nyingi ambazo watu huzitumia na wengine hudai zimewasaidia, lakini hakuna uthibitisho wa asilimia 100. Hata hivyo, wacha nikuchagulie baadhi ya nadharia maarufu:
1. Lishe yenye kalori nyingi
Baadhi ya tafiti zimeonyesha kuwa mwanamke anayekula chakula chenye kalori nyingi ana nafasi kubwa ya kupata mtoto wa kiume.
Kalori ni kipimo cha nishati kinachopatikana kwenye chakula. Vyakula vyenye kalori nyingi ni pamoja na vyakula vya wanga (wali, viazi, mikate), vyenye mafuta (karanga, mbegu, parachichi, samli, siagi) na nyama.
Pia inashauriwa kula vyakula vyenye madini ya potasiamu kama ndizi, na kutumia chumvi ya kawaida kwa kiasi.
Sababu: Chumvi na vyakula vya potasiamu husaidia kufanya mazingira ya uke na mji wa mimba yawe na asili ya alkali. Hali hii husaidia mbegu za kiume kuishi muda mrefu zaidi.
2. Kufika kileleni mapema
Tafiti fulani zinasema kuwa mwanamke akiwahi kufika kileleni kabla ya mume, huongeza uwezekano wa kupata mtoto wa kiume. Hii ni kwa sababu mbegu za kiume husafiri kwa kasi zaidi kuliko mbegu za kike.
3. Mkao baada ya tendo
Wengine huamini kuwa baada ya tendo la ndoa, mwanamke akilala ubavu wa kulia husaidia mbegu za kiume kufika kwa haraka zaidi kwenye yai.
4. Mbinu za mikao ya tendo la ndoa
Kuna wanaoamini kuwa mikao fulani, kama ule wa “kifo cha mende” (doggy style), husaidia kwa sababu uume unakaribia zaidi kwenye mlango wa kizazi, na hivyo mbegu za kiume kufika haraka.
Hitimisho
Hizi zote ni nadharia tu, si njia za kitaalamu zenye uhakika. Watu wengine hudai zimewasaidia, lakini mara nyingi inaweza kuwa ni kwa bahati tu.
Kwa ushauri wa kibinafsi, unaweza kujaribu ile ya kwanza (lishe yenye kalori nyingi na vyakula vyenye potasiamu), ila usitumie chumvi nyingi kupita kiasi kwani inaweza kuathiri afya.
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu
Umeionaje Makala hii.. ?
Posti hii inahusu zaidi mabadiliko kwenye Matiti kwa Mama mjamzito, hali hii utokea pale ambapo mama akibeba mimba Kuna mabadiliko kwenye Matiti kama ifuayavyo.
Soma Zaidi...Ni ngumu ila nitakujuza namna ya kuitambuwa mimba ya siku moja hadi 3, mimba ya wiki moja na mimba ya miezi mitatu kwa dalili.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi dalili za hatari kwa Mama mjamzito, ni Dalili ambazo ujitokeza kwa Mama mjamzito, hizi Dalili zisipofanyiwa kazi mapema zinaweza kuleta shida kwa Mama kwa hiyo jamii nzima inapaswa kujua Dalili hizi na kuchukua hatua endapo zitajio
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi mabadiliko kwenye tumbo la uzazi la Mama pindi anapobeba mimba, ni mabadiliko yanayotokea kwa mwanamke anapobeba mimba kama ifuatavyo.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi kazi ya mdalasini katika matibabu ya homoni kwa wanawake.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi sababu mbalimbali ambazo zinamfanya mama au dada kutobeba mimba. Kwa hiyo tutaziona hapo chini kama ifuatavyo.
Soma Zaidi...Posti hii inaelezea namna mwanamke anavyoweza kupata Ugonjwa wa Maambukizi ya mfumo wa Uzazi.
Soma Zaidi...Maumivu ya hedhi (dysmenorrhea) ni maumivu makali au ya kubana sehemu ya chini ya tumbo. Wanawake wengi hupatwa na Maumivu ya hedhi kabla tu na wakati wa hedhi zao. Kwa wanawake wengine, usumbufu huo ni wa kuudhi tu. Kwa wengine, 
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi sababu za kukosa hedhi wakati mda wa kuona hedhi umefika ni tatizo linalowasumbua baadhi ya wasichana wachache katika jamii na hii ni kwa sababu zifuatazo.
Soma Zaidi...