Jinsi ya kupata mtoto wa kiume

Post hii inakwenda kukufundisha kuhusu nadharia ya kupata mtoto wa kiume.

 

Habari,

Nashukuru kwa kuelewa jinsi ya kukokotoa siku na kupata siku za kutungwa mimba. Mimi siku zangu hubadilika mara kwa mara, lakini mara nyingi huwa siku 31 au 32. Shida yangu ni kupata mtoto wa kiume, nifanyeje katika hilo?

 

Jibu

Kwanza kabisa, ni vizuri kujua kuwa kupata mtoto wa kiume au wa kike hakuna njia yenye uhakika wa kitaalamu. Kuna nadharia nyingi ambazo watu huzitumia na wengine hudai zimewasaidia, lakini hakuna uthibitisho wa asilimia 100. Hata hivyo, wacha nikuchagulie baadhi ya nadharia maarufu:

 

 

1. Lishe yenye kalori nyingi

Baadhi ya tafiti zimeonyesha kuwa mwanamke anayekula chakula chenye kalori nyingi ana nafasi kubwa ya kupata mtoto wa kiume.

 

Kalori ni kipimo cha nishati kinachopatikana kwenye chakula. Vyakula vyenye kalori nyingi ni pamoja na vyakula vya wanga (wali, viazi, mikate), vyenye mafuta (karanga, mbegu, parachichi, samli, siagi) na nyama.

 

Pia inashauriwa kula vyakula vyenye madini ya potasiamu kama ndizi, na kutumia chumvi ya kawaida kwa kiasi.

 

Sababu: Chumvi na vyakula vya potasiamu husaidia kufanya mazingira ya uke na mji wa mimba yawe na asili ya alkali. Hali hii husaidia mbegu za kiume kuishi muda mrefu zaidi.

 

 

2. Kufika kileleni mapema

Tafiti fulani zinasema kuwa mwanamke akiwahi kufika kileleni kabla ya mume, huongeza uwezekano wa kupata mtoto wa kiume. Hii ni kwa sababu mbegu za kiume husafiri kwa kasi zaidi kuliko mbegu za kike.

 

 

 

3. Mkao baada ya tendo

Wengine huamini kuwa baada ya tendo la ndoa, mwanamke akilala ubavu wa kulia husaidia mbegu za kiume kufika kwa haraka zaidi kwenye yai.

 

 

4. Mbinu za mikao ya tendo la ndoa

Kuna wanaoamini kuwa mikao fulani, kama ule wa “kifo cha mende” (doggy style), husaidia kwa sababu uume unakaribia zaidi kwenye mlango wa kizazi, na hivyo mbegu za kiume kufika haraka.

 

 

Hitimisho

Hizi zote ni nadharia tu, si njia za kitaalamu zenye uhakika. Watu wengine hudai zimewasaidia, lakini mara nyingi inaweza kuwa ni kwa bahati tu.

 

Kwa ushauri wa kibinafsi, unaweza kujaribu ile ya kwanza (lishe yenye kalori nyingi na vyakula vyenye potasiamu), ila usitumie chumvi nyingi kupita kiasi kwani inaweza kuathiri afya.

 

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Uzazi Main: Afya File: Download PDF Views 3626

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉2 kitabu cha Simulizi    👉3 Kitabu cha Afya    👉4 Dua za Mitume na Manabii    👉5 Bongolite - Game zone - Play free game    👉6 Madrasa kiganjani   

Post zinazofanana:

Madhara ya kutumia madawa ya kupunguza maumivu

Posti hii inahusu zaidi madhara ya kutumia madawa ya kupunguza maumivu,ni madhara ambayo utokea kwa mtu anayetumia madawa ya kupunguza maumivu.

Soma Zaidi...
DALILI ZA TEZI DUME

Tezi dume hii ni tezi inayopatikana katika katika mfumo wa uzazi wa mwanaume Ila hujulikana kama PROSTATE GLAND. pia hukua karibu na kibofu Cha mkojo na mirija ya mkojo hutumika kuzalisha majimaji (simen) yanayobeba mbegu hivyo bas mk

Soma Zaidi...
Mapendekezo muhimu kwa wajawazito

Posti hii inahusu zaidi mapendekezo muhimu kwa wajawazito, haya ni mapendekezo yaliyotolewa na wataalamu wa afya ili wajawazito waweze kule mimba zao vizuri na kuweza kujifungua vizuri na kupata watoto wenye afya njema na makuzi mazuri pasipokuwepo na ule

Soma Zaidi...
Dalili za mama mjamzito akikaribia kujifungua

Post hii inazungumzia mama wajawazito Mara tu mama anapohisi kuwa yeye ni mjamzito anashauriwa kuanza clinic.na clinic hizi zinasaidia kuwapatia wakina mama elimu,namna ya kumkinga Mtoto asipatwe na maradhi Kama UKIMWI. Pia mama anapoanza clinic

Soma Zaidi...
Mambo yanayopelekea Mjamzito kutokwa na damu

Posti hii inahusu zaidi mambo mbalimbali ambayo yanapelekea Mjamzito kutokwa na damu, hizi ni baadhi ya sababu ambazo usababisha Mjamzito kutokwa na damu.

Soma Zaidi...
Je siku sahihi yakufanya tendo la ndoa niipi ukipata siku zake za hatari?

Swali langu ni hili doktaJe siku sahihi yakufanya tendo la ndoa niipi ukipata siku zake za hatari?

Soma Zaidi...
Maumivu wakati wa hedhi.

Posti hii inahusu zaidi maumivu wakati wa hedhi, haya ni maumivu ambayo utokea wakati wa hedhi kwa wanawake walio wengi, wengine huwa hawayapati kabisa na wengine hutapata na kwa kiwango kikubwa kutegemea na matatizo mbalimbali kama tutakavyoona.

Soma Zaidi...
Faida za Uzazi wa mpango

Posti hii inazungumzia Faida za Uzazi wa mpango kwa watoto, mama, wanandoa, na jamii au JUMUIYA.

Soma Zaidi...
Kujaa gesi tumboni

Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu sababu za kujaa tmgesi tumbon

Soma Zaidi...