Post hii inakwenda kukufundisha kuhusu nadharia ya kupata mtoto wa kiume.
Habari,
Nashukuru kwa kuelewa jinsi ya kukokotoa siku na kupata siku za kutungwa mimba. Mimi siku zangu hubadilika mara kwa mara, lakini mara nyingi huwa siku 31 au 32. Shida yangu ni kupata mtoto wa kiume, nifanyeje katika hilo?
Jibu
Kwanza kabisa, ni vizuri kujua kuwa kupata mtoto wa kiume au wa kike hakuna njia yenye uhakika wa kitaalamu. Kuna nadharia nyingi ambazo watu huzitumia na wengine hudai zimewasaidia, lakini hakuna uthibitisho wa asilimia 100. Hata hivyo, wacha nikuchagulie baadhi ya nadharia maarufu:
1. Lishe yenye kalori nyingi
Baadhi ya tafiti zimeonyesha kuwa mwanamke anayekula chakula chenye kalori nyingi ana nafasi kubwa ya kupata mtoto wa kiume.
Kalori ni kipimo cha nishati kinachopatikana kwenye chakula. Vyakula vyenye kalori nyingi ni pamoja na vyakula vya wanga (wali, viazi, mikate), vyenye mafuta (karanga, mbegu, parachichi, samli, siagi) na nyama.
Pia inashauriwa kula vyakula vyenye madini ya potasiamu kama ndizi, na kutumia chumvi ya kawaida kwa kiasi.
Sababu: Chumvi na vyakula vya potasiamu husaidia kufanya mazingira ya uke na mji wa mimba yawe na asili ya alkali. Hali hii husaidia mbegu za kiume kuishi muda mrefu zaidi.
2. Kufika kileleni mapema
Tafiti fulani zinasema kuwa mwanamke akiwahi kufika kileleni kabla ya mume, huongeza uwezekano wa kupata mtoto wa kiume. Hii ni kwa sababu mbegu za kiume husafiri kwa kasi zaidi kuliko mbegu za kike.
3. Mkao baada ya tendo
Wengine huamini kuwa baada ya tendo la ndoa, mwanamke akilala ubavu wa kulia husaidia mbegu za kiume kufika kwa haraka zaidi kwenye yai.
4. Mbinu za mikao ya tendo la ndoa
Kuna wanaoamini kuwa mikao fulani, kama ule wa “kifo cha mende” (doggy style), husaidia kwa sababu uume unakaribia zaidi kwenye mlango wa kizazi, na hivyo mbegu za kiume kufika haraka.
Hitimisho
Hizi zote ni nadharia tu, si njia za kitaalamu zenye uhakika. Watu wengine hudai zimewasaidia, lakini mara nyingi inaweza kuwa ni kwa bahati tu.
Kwa ushauri wa kibinafsi, unaweza kujaribu ile ya kwanza (lishe yenye kalori nyingi na vyakula vyenye potasiamu), ila usitumie chumvi nyingi kupita kiasi kwani inaweza kuathiri afya.
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu
Umeionaje Makala hii.. ?
Posti hii inahusu zaidi upungufu wa homoni ya estrogen na dalili zake, aina hii ya homoni ikipungua mwilini uleta madhara na matatizo mbalimbali kwenye mwili.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi umuhimu wa uzazi wa mpango kwa watoto, sio akina Mama peke yao wanaofaidika na uzazi wa mpango vile vile na watoto wanafaidika na uzazi wa mpango kama ifuatavyo.
Soma Zaidi...Post hii inahusu zaidi mambo muhimu ambayo tunapaswa kujua au kufahamu kuhusu mbegu za kiume, kwa kuwa mbegu za kiume usaidia katika utungaji wa mimba kwa hiyo ni vizuri kabisa kuzitunza Ili kuweza kuepuka matatizo mbalimbali ambayo yanaweza kutokea kwa s
Soma Zaidi...Posti inahusu zaidi njia maalum za uzazi wa mpango kwa wanaonyonyesha,Ni njia za uzazi ambazo wanaonyesha wanatumia kwa sababu kuna njia nyingine zikitumiwa na wanaonyonyesha zinaweza kuleta matatizo kwa watoto au kusababisha maziwa kutokuwa na vitamini v
Soma Zaidi...Post hii inahusu zaidi viti vilivyopo kwenye maji ya Amniotic fluid, ni jumla ya vitu vyote vilivyopo kwenye maji ya Amniotic fluid.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi namna ya kutibu tatizo la ugumba kwa Mwanaume, ni njia ambazo utumiwa na wataalam mbalimbali Ili kuweza kutibu tatizo la ugumba kwa wanaume.
Soma Zaidi...Nini humaanisha kama chuchu zinauma na hupati period mwanaidi mrefu.
Soma Zaidi...Point hii inahusu zaidi mbinu za kupunguza Kichefuchefu hasa kwa wagonjwa na watumiaji wa madawa mbalimbali yanayoweza kusababisha kichefuchefu.
Soma Zaidi...Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu sababu za maumivu ya tumbo chini upande wa kulia
Soma Zaidi...Post hii inahusu zaidi sababu za kutoshika mimba kwa mwanamke, kuna kipindi ambacho mwanamke hushindwa kushika mimba kuna sababu mbalimbali mojawapo ni kama zifuatazo
Soma Zaidi...