Post hii inakwenda kukufundisha kuhusu nadharia ya kupata mtoto wa kiume.
Habari,
Nashukuru kwa kuelewa jinsi ya kukokotoa siku na kupata siku za kutungwa mimba. Mimi siku zangu hubadilika mara kwa mara, lakini mara nyingi huwa siku 31 au 32. Shida yangu ni kupata mtoto wa kiume, nifanyeje katika hilo?
Jibu
Kwanza kabisa, ni vizuri kujua kuwa kupata mtoto wa kiume au wa kike hakuna njia yenye uhakika wa kitaalamu. Kuna nadharia nyingi ambazo watu huzitumia na wengine hudai zimewasaidia, lakini hakuna uthibitisho wa asilimia 100. Hata hivyo, wacha nikuchagulie baadhi ya nadharia maarufu:
1. Lishe yenye kalori nyingi
Baadhi ya tafiti zimeonyesha kuwa mwanamke anayekula chakula chenye kalori nyingi ana nafasi kubwa ya kupata mtoto wa kiume.
Kalori ni kipimo cha nishati kinachopatikana kwenye chakula. Vyakula vyenye kalori nyingi ni pamoja na vyakula vya wanga (wali, viazi, mikate), vyenye mafuta (karanga, mbegu, parachichi, samli, siagi) na nyama.
Pia inashauriwa kula vyakula vyenye madini ya potasiamu kama ndizi, na kutumia chumvi ya kawaida kwa kiasi.
Sababu: Chumvi na vyakula vya potasiamu husaidia kufanya mazingira ya uke na mji wa mimba yawe na asili ya alkali. Hali hii husaidia mbegu za kiume kuishi muda mrefu zaidi.
2. Kufika kileleni mapema
Tafiti fulani zinasema kuwa mwanamke akiwahi kufika kileleni kabla ya mume, huongeza uwezekano wa kupata mtoto wa kiume. Hii ni kwa sababu mbegu za kiume husafiri kwa kasi zaidi kuliko mbegu za kike.
3. Mkao baada ya tendo
Wengine huamini kuwa baada ya tendo la ndoa, mwanamke akilala ubavu wa kulia husaidia mbegu za kiume kufika kwa haraka zaidi kwenye yai.
4. Mbinu za mikao ya tendo la ndoa
Kuna wanaoamini kuwa mikao fulani, kama ule wa “kifo cha mende” (doggy style), husaidia kwa sababu uume unakaribia zaidi kwenye mlango wa kizazi, na hivyo mbegu za kiume kufika haraka.
Hitimisho
Hizi zote ni nadharia tu, si njia za kitaalamu zenye uhakika. Watu wengine hudai zimewasaidia, lakini mara nyingi inaweza kuwa ni kwa bahati tu.
Kwa ushauri wa kibinafsi, unaweza kujaribu ile ya kwanza (lishe yenye kalori nyingi na vyakula vyenye potasiamu), ila usitumie chumvi nyingi kupita kiasi kwani inaweza kuathiri afya.
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu
Umeionaje Makala hii.. ?
Posti hii inahusu zaidi madhara ya kutumia madawa ya kupunguza maumivu,ni madhara ambayo utokea kwa mtu anayetumia madawa ya kupunguza maumivu.
Soma Zaidi...Inatakiwa angalau nafasivkati ya mtoto na mtoto wapishane miaka miwili.
Soma Zaidi...Tezi dume hii ni tezi inayopatikana katika katika mfumo wa uzazi wa mwanaume Ila hujulikana kama PROSTATE GLAND. pia hukua karibu na kibofu Cha mkojo na mirija ya mkojo hutumika kuzalisha majimaji (simen) yanayobeba mbegu hivyo bas mk
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi mapendekezo muhimu kwa wajawazito, haya ni mapendekezo yaliyotolewa na wataalamu wa afya ili wajawazito waweze kule mimba zao vizuri na kuweza kujifungua vizuri na kupata watoto wenye afya njema na makuzi mazuri pasipokuwepo na ule
Soma Zaidi...Post hii inazungumzia mama wajawazito Mara tu mama anapohisi kuwa yeye ni mjamzito anashauriwa kuanza clinic.na clinic hizi zinasaidia kuwapatia wakina mama elimu,namna ya kumkinga Mtoto asipatwe na maradhi Kama UKIMWI. Pia mama anapoanza clinic
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi mambo mbalimbali ambayo yanapelekea Mjamzito kutokwa na damu, hizi ni baadhi ya sababu ambazo usababisha Mjamzito kutokwa na damu.
Soma Zaidi...Swali langu ni hili doktaJe siku sahihi yakufanya tendo la ndoa niipi ukipata siku zake za hatari?
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi maumivu wakati wa hedhi, haya ni maumivu ambayo utokea wakati wa hedhi kwa wanawake walio wengi, wengine huwa hawayapati kabisa na wengine hutapata na kwa kiwango kikubwa kutegemea na matatizo mbalimbali kama tutakavyoona.
Soma Zaidi...Posti hii inazungumzia Faida za Uzazi wa mpango kwa watoto, mama, wanandoa, na jamii au JUMUIYA.
Soma Zaidi...Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu sababu za kujaa tmgesi tumbon
Soma Zaidi...