Sifa za uchumi wa kiislamu na njia halali za uchumi na umiliki mali katika uislamu

Sifa za uchumi wa kiislamu na njia halali za uchumi na umiliki mali katika uislamu

Sifa za uchumi wa kiislamu na njia halali za uchumi na umiliki mali katika uislamu

Uchumi Katika Uislamu

Maana ya Uchumi

- Ni uzalishaji, usambazaji na utumiaji wa mali, rasilimali na huduma mbalimbali katika jamii ili kujenga mahusiano kati ya binaadamu na Allah (s.w).


Sifa za Uchumi wa Kiislamu

1. Dhana ya mafanikio

Huzingatia hatima yake ambayo ni kupata radhi za Allah (s.w) pekee.


2. Dhana ya umilikaji mali

Mmiliki hakika wa pekee wa mali na rasilimali zote ni Allah (s.w).


3. Dhana ya bidhaa

Ni kitu kilicho safi, kizuri, twahara, halali, n.k.



4. Dhana ya matumizi

Haifai kufuja au kutumia mali au rasilimali kwa njia za haramu.



5. Mizani ya wakati katika kutumia

Ni kujiuliza, nini matokeo ya mali au rasilimali hiyo baada ya muda fulani?


Njia na Misingi ya Uchumi Halali Katika Uislamu

i. Pasiwe na udanganyifu wowote katika uuzaji na ununuzi wa bidhaa au mali.

Rejea Qur’an (17:35), (26:181-183), (83:1-4)



ii. Pasiwe na viapo katika kuuza au kununua bidha, kwani ni miongoni mwa kuuza kwa ujanja-ujanja.
Abu Qatada ameeleza kuwa Mtume wa Allah amesema:

β€œKuwa mwangalifu na viapo vingi katika uuzaji, kwa sababu japo

kunarahisisha uuzaji, kuna punguza baraka” (Muslim).



iii. Pawe na uhuru kamili kwa mnunuzi kuikataa au kuikubali bidhaa baada ya kuiangalia.
iv. Bidhaa yenyewe iwe halali na iwe imechumwa kwa misingi ya halali pia.

v. Kuwepo na maelewano kati ya muuzaji na mnunuzi bila masharti. Dosari yeyote ya bidhaa ijulikane kabla ya manunuzi kufanyika.
vi. Muuzaji awe na uhuru wa kuuza bidhaa yake kwa bei yenye maslahi kwake na isiwe ya kumnyonya mnunuzi.



                   

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Fiqh Main: Dini File: Download PDF Views 2417

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
πŸ‘‰1 Kitabu cha Afya    πŸ‘‰2 Kitau cha Fiqh    πŸ‘‰3 kitabu cha Simulizi    πŸ‘‰4 Simulizi za Hadithi Audio    πŸ‘‰5 Bongolite - Game zone - Play free game    πŸ‘‰6 Dua za Mitume na Manabii   

Post zinazofanana:

Haki za raia katika dola ya kiislamu

Haki na uadilifu katika uislamu (EDK form 3: Dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Tofauti kati ya zakat na sadaqat

Nguzo za Imani, tofauti kati ya sadaqat na zakat (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Mambo yanayotenguwa udhu

Post hiibinakwenda kukufundisha mambo ambayo yanaharibu udhu.

Soma Zaidi...
Mambo yaliyo haramu kwa mwenye hedhi na nifasi

Katika post hii utakwenda kujifunza mambo ambayo ni haramu kwa mwanamke aliye na hedhi na nifasi

Soma Zaidi...
Riba na Madhara Yake Katika Jamii

- Riba ni kipato chochote kile cha ziada kutokana na mkopo au mtaji bila kushiriki katika faida au hasara.

Soma Zaidi...
Haki za binadamu kwa ujumla (basic human rights)

Haki na uadilifu katika uislamu (EDK form 3: Dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...