picha

Sifa za uchumi wa kiislamu na njia halali za uchumi na umiliki mali katika uislamu

Sifa za uchumi wa kiislamu na njia halali za uchumi na umiliki mali katika uislamu

Sifa za uchumi wa kiislamu na njia halali za uchumi na umiliki mali katika uislamu

Uchumi Katika Uislamu

Maana ya Uchumi

- Ni uzalishaji, usambazaji na utumiaji wa mali, rasilimali na huduma mbalimbali katika jamii ili kujenga mahusiano kati ya binaadamu na Allah (s.w).


Sifa za Uchumi wa Kiislamu

1. Dhana ya mafanikio

Huzingatia hatima yake ambayo ni kupata radhi za Allah (s.w) pekee.


2. Dhana ya umilikaji mali

Mmiliki hakika wa pekee wa mali na rasilimali zote ni Allah (s.w).


3. Dhana ya bidhaa

Ni kitu kilicho safi, kizuri, twahara, halali, n.k.



4. Dhana ya matumizi

Haifai kufuja au kutumia mali au rasilimali kwa njia za haramu.



5. Mizani ya wakati katika kutumia

Ni kujiuliza, nini matokeo ya mali au rasilimali hiyo baada ya muda fulani?


Njia na Misingi ya Uchumi Halali Katika Uislamu

i. Pasiwe na udanganyifu wowote katika uuzaji na ununuzi wa bidhaa au mali.

Rejea Qur’an (17:35), (26:181-183), (83:1-4)



ii. Pasiwe na viapo katika kuuza au kununua bidha, kwani ni miongoni mwa kuuza kwa ujanja-ujanja.
Abu Qatada ameeleza kuwa Mtume wa Allah amesema:

“Kuwa mwangalifu na viapo vingi katika uuzaji, kwa sababu japo

kunarahisisha uuzaji, kuna punguza baraka” (Muslim).



iii. Pawe na uhuru kamili kwa mnunuzi kuikataa au kuikubali bidhaa baada ya kuiangalia.
iv. Bidhaa yenyewe iwe halali na iwe imechumwa kwa misingi ya halali pia.

v. Kuwepo na maelewano kati ya muuzaji na mnunuzi bila masharti. Dosari yeyote ya bidhaa ijulikane kabla ya manunuzi kufanyika.
vi. Muuzaji awe na uhuru wa kuuza bidhaa yake kwa bei yenye maslahi kwake na isiwe ya kumnyonya mnunuzi.



                   

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Fiqh Main: Post File: Download PDF Views 3931

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉2 Madrasa kiganjani     👉3 Kitau cha Fiqh     👉4 Kitabu cha Afya     👉5 Tafasiri ya Riyadh Swalihina     👉6 Dua za Mitume na Manabii    

Post zinazofanana:

Maana ya swala

Maana ya Swala Maana ya Swala kilugha(a) Kilugha Katika lugha ya Kiarabu neno Swalaat lina maana ya ombi au dua.

Soma Zaidi...
Nguzo za swala ya maiti

Mambo ya faradh kwa maiti ya muislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Zijuwe sunnha 9 za swala

Post hii inakwenda kukufundisha sunnah 9 za swala. Sunnah hizi ni zile ambazo ukiziwacha swala yako haibatiliki.

Soma Zaidi...