picha

Sifa za uchumi wa kiislamu na njia halali za uchumi na umiliki mali katika uislamu

Sifa za uchumi wa kiislamu na njia halali za uchumi na umiliki mali katika uislamu

Sifa za uchumi wa kiislamu na njia halali za uchumi na umiliki mali katika uislamu

Uchumi Katika Uislamu

Maana ya Uchumi

- Ni uzalishaji, usambazaji na utumiaji wa mali, rasilimali na huduma mbalimbali katika jamii ili kujenga mahusiano kati ya binaadamu na Allah (s.w).


Sifa za Uchumi wa Kiislamu

1. Dhana ya mafanikio

Huzingatia hatima yake ambayo ni kupata radhi za Allah (s.w) pekee.


2. Dhana ya umilikaji mali

Mmiliki hakika wa pekee wa mali na rasilimali zote ni Allah (s.w).


3. Dhana ya bidhaa

Ni kitu kilicho safi, kizuri, twahara, halali, n.k.



4. Dhana ya matumizi

Haifai kufuja au kutumia mali au rasilimali kwa njia za haramu.



5. Mizani ya wakati katika kutumia

Ni kujiuliza, nini matokeo ya mali au rasilimali hiyo baada ya muda fulani?


Njia na Misingi ya Uchumi Halali Katika Uislamu

i. Pasiwe na udanganyifu wowote katika uuzaji na ununuzi wa bidhaa au mali.

Rejea Qur’an (17:35), (26:181-183), (83:1-4)



ii. Pasiwe na viapo katika kuuza au kununua bidha, kwani ni miongoni mwa kuuza kwa ujanja-ujanja.
Abu Qatada ameeleza kuwa Mtume wa Allah amesema:

“Kuwa mwangalifu na viapo vingi katika uuzaji, kwa sababu japo

kunarahisisha uuzaji, kuna punguza baraka” (Muslim).



iii. Pawe na uhuru kamili kwa mnunuzi kuikataa au kuikubali bidhaa baada ya kuiangalia.
iv. Bidhaa yenyewe iwe halali na iwe imechumwa kwa misingi ya halali pia.

v. Kuwepo na maelewano kati ya muuzaji na mnunuzi bila masharti. Dosari yeyote ya bidhaa ijulikane kabla ya manunuzi kufanyika.
vi. Muuzaji awe na uhuru wa kuuza bidhaa yake kwa bei yenye maslahi kwake na isiwe ya kumnyonya mnunuzi.



                   

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Fiqh Main: Post File: Download PDF Views 4177

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Simulizi za Hadithi Audio     👉2 Kitau cha Fiqh     👉3 Kitabu cha Afya     👉4 Madrasa kiganjani     👉5 ai web app     👉6 Bongolite - Game zone - Play free game    

Post zinazofanana:

Haki za maadui katika vita (mateka wa kivita)

Haki na uadilifu katika uislamu (EDK form 3: Dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Aina ya biashara zilizo haramu kwenye uislamu

Hapa utajifunza aina za biashara ambazo ni haramu.

Soma Zaidi...
Dhana ya kumiliki raslimali katika uislamu

Ni ipi raslimali ya halali kuimiliki katika uislamu.

Soma Zaidi...
Swala ya Istikhara na jinsi ya kuiswali

Post hii inakwenda kukufundisha kuhusu swala ya Istikhara

Soma Zaidi...
Jinsi ya kiswali swala ya tahajud na swala za usiku yaani qiyamu layl

Post hii itakujuza jinsi ya kiswali swala ya tahajudi. Pia utajifunza jinsi ya kuswali swala za usikubyaanibqiyamublayl

Soma Zaidi...
Faida za kuswali swala za sunnah

Hapa utajifunza faida za kuswali swala za sunnah.

Soma Zaidi...