Jinsi ya kutekeleza funga za sunnah

Jinsi ya kutekeleza funga za sunnah

Hapa utajifunza muda wa kutia jia katika funga za sunnah. Pia utajifunza kuhusu uhuru ulio nao

Jiunge nasi WhatsApp
Upate Update zetu

Nia katika Funga za Sunnah

Katika funga ya Ramadhani, kutokana na hadith iliyosimuliwa na Hafsah (r.a), funga haisihi endapo mtu hatatia nia ya kufunga usiku kabla ya Alfajir kuingia. Lakini katika funga za Sunnah mtu anaweza kunuia swaum mchana kabla ya kuingia adhuhuri, endapo atakuwa hajala chochote tangu alfajir, kama inavyobainika katika Hadithi ifuatayo:
Aysha (r.a) ameeleza kuwa siku moja Mtume wa Allah (s.a.w) aliniuliza:
“Aysha, una chochote (cha kula)?” Nikasema: “Mjumbe wa Allah, hatuna
chochote ”. Ndipo akas em a: “Nim efunga ”. (Muslim).

 

Uhuru wa kuvunja Funga ya Sunnah

 


Mtu aliyefunga sunnah ana uhuru kamili wa kufungua katikati endapo ataona ni vyema kwake kufanya hivyo. Tunajifunza hili katika Hadith zifuatazo:
Aysha (r.a) ameeleza: Mtume wa Allah alikuja kwangu akasema: “Una chochote cha kula?” Nikajibu: “Hapana.” Kisha akasema: “Basi, nitafunga ”. Kisha siku nyingine alitujia tukamwambia: Mtume wa Allah, tumeletewa zawadi ya Hais (aina ya chakula). Ndipo akasema: “Nionyeshe, nilikuwa nimefunga tangu alfajir, kisha alikula. ” (Muslim).

 


Ummi Hani (r.a) ameeleza kuwa katika siku ya kutekwa Makka Fatma (r.a) alikaa kushotoni mw a Mtume na Ummi Hani alikuwa kuliani kw ake. Kisha Walidah (r.a) alileta kikombe cha maji, alichukua akanywa, kisha Ummi Hani naye alichukua na kunywa. Akasema: Ee Mtume wa Allah, nilifunga na sasa nimefungua. akamuuliza: Ulikuwa unalipa? Akajibu: ‘Hapana ’ Akasema Mtume (s.w.): “Haidhuru iwapo ilikuwa ni funga ya sunnah. Mtu anayefunga funga ya sunnah ana uhuru kamili. Akipenda atafunga na akipenda ataacha.” (Abu Daud, Tirmidh, Ahmad). Aliyefunga Sunnah akikaribishwa aseme: “Nimefunga”
Mtu aliyefunga akikaribishwa chakula aseme ‘nimefunga’ kama tunavyofahamishw a katika Hadith ifuatayo:

 


Abu Hurairah (r.a) ameeleza kuwa Mtume wa Allah (s.a.w) amesema:“Kama mmoja wenu atakaribishwa chakula akiwa amefunga s em a: “Nim efunga ”:. (Muslim).
Si vibaya mtu asiyefunga kula mbele ya yule aliyefunga, bali mfungaji hupata ujira kwa kule kuamua kwake kuendelea kufunga pamoja na kuwaona wengine wakila mbele yake. Tunajifunza katika Hadith zifuatazo:

 


Ummi Umrah bin Ka ’ab (r.a) amesimulia: Mtume (s.a.w) alimtembelea na akamuandalia chakula, Mtume akamwambia kula. Akasema: “Nimefunga. ” Ndipo Mtume (s.a.w) akasema: “Wakati kitu kinapoliw a mbele ya mtu aliyefunga, malaika wanamrehemu mpaka wamalize kula” (Ahm ad).

 


Buraidah (r.a) amesimulia kuwa Bilal alikuja kwa Mtume (s.a.w) akamkuta anafungua kinywa. Mtume w a Allah akamkaribisha Bilal akamwambia: “Kifungua kinywa, Ee Bilal.” Bilal akasema: Nimefunga. Ee! Mtume wa Allah.’ Kisha Mtume wa Allah akasema: “Tunakula riziki yetu na riziki ya Bilal ya hali ya juu. Riziki ya hali ya juu kuliko zote ni Pepo. Unafahamu Ee Bilal kwamba mifupa ya mtu aliyefunga inamtukuza Allah na Malaika wanamuombea msamaha kwa muda wote ambao watu wanakula karibu yake?” (Baihaqi).

 


Funga za Sunnah na utekelezaji wa majukumu

 


Endapo kufunga sunnah kutamfanya mtu ashindwe kutekeleza majukumu yake kwa wengine katika jamii, ni vyema kutofunga. Katika Hadith tunafahamishwa kuwa wakeze Mtume (s.a.w) walikuwa aghlabu hawafungi mbali ya Ramadhani na Shaabani kwa kuhofia kushindwa kutekeleza wajibu wao kwa Mtume (s.a.w). Katika mwezi wa Shaaban Mtume (s.a.w) alikuwa akifunga sana kuliko miezi mingine:

 


Aysha (r.a) ameeleza: Kama mmoja wetu aliacha siku katika Ramadhani (kwa udhuru wa sheria) katika maisha ya Mtume (s.a.w) hakuweza kuzilipa alipokuwa na Mtume wa Allah mpaka Shaaban inaingia.” (Muslim).

 


Hadith hii inasisitiza kuwa kwa kuchelea kutoweza kutekeleza wajibu wao kwa Mtume wa Allah, wakeze Mtume(s.a.w) hawakuthubutu kufunga walipokuwa na Mtume. Mwanamke haruhusiwi kufunga sunnah mpaka aridhiwe na mume wake.

 

Download Post hii hapa

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Fiqh Main: Dini File: Download PDF Views 1296

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Madrasa kiganjani    👉2 kitabu cha Simulizi    👉3 Bongolite - Game zone - Play free game    👉4 Kitabu cha Afya    👉5 Simulizi za Hadithi Audio    👉6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)   

Post zinazofanana:

Taratibu za kutaliki katika uislamu.
Taratibu za kutaliki katika uislamu.

Hapa utajifunza taratibu zinazofuatwa wakati wa kukusudia kumuacha mke. Pia utajifunza sababu za kiwepo kwa eda baada ya kuachwa mwanamke.

Soma Zaidi...
Funga ya ramadhan na nyinginezo
Funga ya ramadhan na nyinginezo

Nguzo za uislamu (EDK form 2; dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Mwenendo wa mwenye kunuia hijjah na umrah
Mwenendo wa mwenye kunuia hijjah na umrah

Nguzo za uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Zijuwe funga za sunnah na jinsi ya kuzifunga
Zijuwe funga za sunnah na jinsi ya kuzifunga

Post hii inakwenda kukufundisha kuhusu funga za sunnah na jinsi ya kuzigunga.

Soma Zaidi...
Mgogoro wa kuandama kwa mwezi, Je mwezi wa Kimataifa ama kila Mji na mwezi wake?
Mgogoro wa kuandama kwa mwezi, Je mwezi wa Kimataifa ama kila Mji na mwezi wake?

Mwezi ukionekana sehemu moja, Waislamu wote ulimwenguni watalazimika kufunga?

Soma Zaidi...
Jinsi ya kiswali swala ya tahajud na swala za usiku yaani qiyamu layl
Jinsi ya kiswali swala ya tahajud na swala za usiku yaani qiyamu layl

Post hii itakujuza jinsi ya kiswali swala ya tahajudi. Pia utajifunza jinsi ya kuswali swala za usikubyaanibqiyamublayl

Soma Zaidi...
Tofauti ya uchumi wa kiislamu na usio wa kiisalmu
Tofauti ya uchumi wa kiislamu na usio wa kiisalmu

Tofauti kati ya mfumo wa uchumi wa Kiislamu na ile ya Kitwaghuti (i) Dhana ya mafanikioKatika mtazamo wa uchumi wa Kiislamu mafanikio yanatazamwa kwa kuzingatia hatima ya ama mtu kupata radhi za Mwenyezi Mungu au kubeba laana ya Mwenyezi Mungu.

Soma Zaidi...