Jinsi ya kutekeleza funga za sunnah

Jinsi ya kutekeleza funga za sunnah

Hapa utajifunza muda wa kutia jia katika funga za sunnah. Pia utajifunza kuhusu uhuru ulio nao

Download Post hii hapa

Nia katika Funga za Sunnah

Katika funga ya Ramadhani, kutokana na hadith iliyosimuliwa na Hafsah (r.a), funga haisihi endapo mtu hatatia nia ya kufunga usiku kabla ya Alfajir kuingia. Lakini katika funga za Sunnah mtu anaweza kunuia swaum mchana kabla ya kuingia adhuhuri, endapo atakuwa hajala chochote tangu alfajir, kama inavyobainika katika Hadithi ifuatayo:
Aysha (r.a) ameeleza kuwa siku moja Mtume wa Allah (s.a.w) aliniuliza:
“Aysha, una chochote (cha kula)?” Nikasema: “Mjumbe wa Allah, hatuna
chochote ”. Ndipo akas em a: “Nim efunga ”. (Muslim).

 

Uhuru wa kuvunja Funga ya Sunnah

 


Mtu aliyefunga sunnah ana uhuru kamili wa kufungua katikati endapo ataona ni vyema kwake kufanya hivyo. Tunajifunza hili katika Hadith zifuatazo:
Aysha (r.a) ameeleza: Mtume wa Allah alikuja kwangu akasema: “Una chochote cha kula?” Nikajibu: “Hapana.” Kisha akasema: “Basi, nitafunga ”. Kisha siku nyingine alitujia tukamwambia: Mtume wa Allah, tumeletewa zawadi ya Hais (aina ya chakula). Ndipo akasema: “Nionyeshe, nilikuwa nimefunga tangu alfajir, kisha alikula. ” (Muslim).

 


Ummi Hani (r.a) ameeleza kuwa katika siku ya kutekwa Makka Fatma (r.a) alikaa kushotoni mw a Mtume na Ummi Hani alikuwa kuliani kw ake. Kisha Walidah (r.a) alileta kikombe cha maji, alichukua akanywa, kisha Ummi Hani naye alichukua na kunywa. Akasema: Ee Mtume wa Allah, nilifunga na sasa nimefungua. akamuuliza: Ulikuwa unalipa? Akajibu: ‘Hapana ’ Akasema Mtume (s.w.): “Haidhuru iwapo ilikuwa ni funga ya sunnah. Mtu anayefunga funga ya sunnah ana uhuru kamili. Akipenda atafunga na akipenda ataacha.” (Abu Daud, Tirmidh, Ahmad). Aliyefunga Sunnah akikaribishwa aseme: “Nimefunga”
Mtu aliyefunga akikaribishwa chakula aseme ‘nimefunga’ kama tunavyofahamishw a katika Hadith ifuatayo:

 


Abu Hurairah (r.a) ameeleza kuwa Mtume wa Allah (s.a.w) amesema:“Kama mmoja wenu atakaribishwa chakula akiwa amefunga s em a: “Nim efunga ”:. (Muslim).
Si vibaya mtu asiyefunga kula mbele ya yule aliyefunga, bali mfungaji hupata ujira kwa kule kuamua kwake kuendelea kufunga pamoja na kuwaona wengine wakila mbele yake. Tunajifunza katika Hadith zifuatazo:

 


Ummi Umrah bin Ka ’ab (r.a) amesimulia: Mtume (s.a.w) alimtembelea na akamuandalia chakula, Mtume akamwambia kula. Akasema: “Nimefunga. ” Ndipo Mtume (s.a.w) akasema: “Wakati kitu kinapoliw a mbele ya mtu aliyefunga, malaika wanamrehemu mpaka wamalize kula” (Ahm ad).

 


Buraidah (r.a) amesimulia kuwa Bilal alikuja kwa Mtume (s.a.w) akamkuta anafungua kinywa. Mtume w a Allah akamkaribisha Bilal akamwambia: “Kifungua kinywa, Ee Bilal.” Bilal akasema: Nimefunga. Ee! Mtume wa Allah.’ Kisha Mtume wa Allah akasema: “Tunakula riziki yetu na riziki ya Bilal ya hali ya juu. Riziki ya hali ya juu kuliko zote ni Pepo. Unafahamu Ee Bilal kwamba mifupa ya mtu aliyefunga inamtukuza Allah na Malaika wanamuombea msamaha kwa muda wote ambao watu wanakula karibu yake?” (Baihaqi).

 


Funga za Sunnah na utekelezaji wa majukumu

 


Endapo kufunga sunnah kutamfanya mtu ashindwe kutekeleza majukumu yake kwa wengine katika jamii, ni vyema kutofunga. Katika Hadith tunafahamishwa kuwa wakeze Mtume (s.a.w) walikuwa aghlabu hawafungi mbali ya Ramadhani na Shaabani kwa kuhofia kushindwa kutekeleza wajibu wao kwa Mtume (s.a.w). Katika mwezi wa Shaaban Mtume (s.a.w) alikuwa akifunga sana kuliko miezi mingine:

 


Aysha (r.a) ameeleza: Kama mmoja wetu aliacha siku katika Ramadhani (kwa udhuru wa sheria) katika maisha ya Mtume (s.a.w) hakuweza kuzilipa alipokuwa na Mtume wa Allah mpaka Shaaban inaingia.” (Muslim).

 


Hadith hii inasisitiza kuwa kwa kuchelea kutoweza kutekeleza wajibu wao kwa Mtume wa Allah, wakeze Mtume(s.a.w) hawakuthubutu kufunga walipokuwa na Mtume. Mwanamke haruhusiwi kufunga sunnah mpaka aridhiwe na mume wake.

 

Download Post hii hapa

Jiunge nasi WhatsApp
Upate Update zetu

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Fiqh Main: Dini File: Download PDF Views 1256

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Simulizi za Hadithi Audio    👉2 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉3 Madrasa kiganjani    👉4 Kitabu cha Afya    👉5 Kitau cha Fiqh    👉6 kitabu cha Simulizi   

Post zinazofanana:

 Ubainifu kati ya halali na Haramu na kujiepusha na mambo yanayo tatiza
Ubainifu kati ya halali na Haramu na kujiepusha na mambo yanayo tatiza

عَنْ أَبِي عَبْدِ اللَّهِ النُّعْمَانِ بْنِ بَشِيرٍ رَضِيَ اللَّهُ عَنْهُمَا، قَالَ: سَمِعْت رَسُولَ اللَّهِ صلى الله عليه و سلم يَقُ?...

Soma Zaidi...
Jinsi ya kumuandaa maiti baada ya kufa
Jinsi ya kumuandaa maiti baada ya kufa

Haya ni maandalizi ya kumuandaa maiti baada ya kufariki.

Soma Zaidi...
Mafunzo ya swala
Mafunzo ya swala

Jifunze namna ya kuswali, zijuwe aina za swala na ujifunze masharti ya swala, kwa nini swala hazijibiwi? nini kifanyike?

Soma Zaidi...
Fiqh.
Fiqh.

Kipengele hichi tutajifunza chimbuko la fiqh na maana ya figh.

Soma Zaidi...
Ijuwe swala ya Tawbah na jinsi ya kuiswali
Ijuwe swala ya Tawbah na jinsi ya kuiswali

Post hii itakufundisha kuhusu swala ya sinnah ya tawba.

Soma Zaidi...
 Riba na Madhara Yake Katika Jamii
Riba na Madhara Yake Katika Jamii

- Riba ni kipato chochote kile cha ziada kutokana na mkopo au mtaji bila kushiriki katika faida au hasara.

Soma Zaidi...
Haki za muislamu kwa muislamu mwenziwe
Haki za muislamu kwa muislamu mwenziwe

Hizi ndio haki kuu tano unazopasa kumpatia Muislamu mwenzio.

Soma Zaidi...