image

Mtazamo na Msimamo wa Uislamu Juu ya Kudhibiti Uzaz (uzazi wa mpango) na hukumu yake

Mtazamo na Msimamo wa Uislamu Juu ya Kudhibiti Uzaz (uzazi wa mpango) na hukumu yake

4. Mtazamo na Msimamo wa Uislamu Juu ya Kudhibiti Uzazi

Kupanga Uzazi Katika Uislamu

- Uislamu unawataka watu kuoana na kuzaana kwa utaratibu na mfumo mzuri ili kutunza na kulea maadili ya familia.


- Uislamu umeweka utaratibu wa umri wa kuzaa kati ya mtoto na mtoto kwa muda wa miaka miwili.
Rejea Qur’an (2:233)

- Uislamu umekataza watu kuzaa nje ya ndoa ambao ni wa kiholela na usiokuwa na malezi bora ya kifamilia.


- Uislamu umeruhusu kuzuia mimba tu kama mwanamke ananyonyesha mtoto mchanga au atadhurika kiafya au kuhatarisha maisha yake.

- Uislamu umeweka utaratibu wa kuzaa na kulea kama njia pekee ya kuendeleza na kujenga kizazi cha mwanaadamu katika maadili na uchumi pia.



Sababu za Uislamu Kupinga Dhana ya Kudhibiti Uzazi

i. Sera ya kudhibiti uzazi inachochea zinaa ambayo ni njia chafu, mbaya na ina madhara makubwa katika jamii ya binaadamu.
Rejea Qur’an (17:32), (24:2)



ii. Sera ya kudhibiti uzazi ni kupinga na kuingilia mpango wa Allah (s.w) katika kupanga uzazi kwa njia ya ndoa.
Rejea Qur’an (2:187), (2:233), (30:21)



iii. Dhana kuwa kuongezeka watu hupunguza riziki ni potofu na ni shirki, kwani ni kukana uwezo wa Allah (s.w) wa Kuruzuku na Kumiliki kila kitu.
Rejea Qur’an (29:60)

iv. Kudhibiti uzazi ni kupoteza stara, hifadhi, huruma na mapenzi ya kweli baina ya mwanamke na mwanamume ambapo ni kinyume na utaratibu wa Allah (s.w).

v. Kudhibiti uzazi kwa hofu ya umaskini ni haramu, kwani kila kiumbe Allah

(s.w) amekikadiria riziki yake.

Rejea Qur’an (17:31)

vi. Sera juu ya kudhibiti uzazi inalengo la kuepuka jukumu la kuzaa, kulea na kuendeleza kizazi kwa utaratibu unaofaa.


vii. Sera ya kudhibiti uzazi ni kuchochea ngono huru, ukahaba, kuzaliwa watoto kiholela wasiokuwa na baba na kuondoa nafasi ya ndoa katika jamii.

viii. Kudhibiti uzazi ni dhana ya uchoyo, ubadhirifu na ulafi wa kutaka kumiliki na kutumia rasilimali, uchumi, siasa, n.k kwa watu wachache




Sababu Zinazokulika Kudhibiti Uzazi Katika Uislamu

i. Kuhifadhi au kulinda afya ya mama asishike mimba baada ya kuthibitishwa na daktari anayeaminika kuwa itahatarisha afya au uhai wake.


ii. Iwapo mama ananyonyesha mtoto mchanga kwani mtoto anaweza kuathirika kiafya.

iii. Ikiwa mwanamke hawezi kuzaa ila kwa kufanyiwa operesheni, atalazimika kuzuia mimba baada ya kuzaa kwa operesheni mimba tatu.



Baadhi ya Njia Zinazotumika Kudhibiti Uzazi

a) Njia za Kisasa (Morden Method):

i. Kondom, mipira ya kiume na kike (Contraceptives). ii. Kitanzi-loop (Intra uterine device).
iii. Vidonge vya majira (Ant baby pill).

iv. Kufunga kitanzi kwa mwanamke (Tube Legation). v. Kufunga uzazi kwa wanaume (Vasectomy).
vi. Kutoa mimba (abortion).

vii. Uzazi wa maabara (test tube babies).

viii. Kukodisha matumbo ya wanawake wengine, kupandikiza mbegu (surrogate mothers)




b) Njia za Asilia, Maumbile (Natural Method):

i. Kufuata kalenda ya uzazi ya mwanamke (Menstrual Period or Circle).

ii. Kumwaga mbegu za uzazi nje kwa mwanamume (Coitus Interrunts or withdrawal)



                   





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 651


Sponsored links
👉1 Kitabu cha Afya     👉2 Kitau cha Fiqh     👉3 kitabu cha Simulizi     👉4 Madrasa kiganjani    

Post zifazofanana:-

Jinsi ya kuswali swala vitani
Post hii itakufundisha taratibu zinazofanyika ilibkuswalibukiwa vitani. Soma Zaidi...

NINI MAANA YA KUSIMAMISHA SWALA, KATIKA UISLAMU (NI YUPI TARQU SWALA) yaani mwenye kuacha swala)
Kusimamisha Swala. Soma Zaidi...

Mambo yanayoharibu Udhu (yanayobatilisha udhu)
Post hii inakwenda kukufundisha mambo ambayo hubatilisha udhu yaani mam,boa mbayo yanaharibu udhu. Soma Zaidi...

Njia za kudhibiti riba
Ufumbuzi wa tatizo la ribaRiba imeenea na kuzoeleka duniani kwa kiasi ambacho watu wengi wanadhani kuwa bila riba hakuna shughuli yoyote ya uchumi inayowezekana. Soma Zaidi...

Kumuandaa maiti punde baada ya kufariki dunia
Soma Zaidi...

Aina za talaka zinazo rejewa
Soma Zaidi...

Jinsi ya kutwaharisha aina mbalimbali za najisi
Kila najisi ina namna yake ya kutwaharisha, hata hivyo namna hizo hufanana. Katika post hii utakwenda kujifunza jinsi ya kutwaharisha najisi mbalimbali. Soma Zaidi...

Maana ya sadaqat
Nguzo za imani, maana ya sadaqat (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Maana ya talaka na kuacha ama kuachwa
Maana ya TalakaTalaka ni utaratibu wa kuvunja mkataba wa ndoa waliofunga mume na mke wakati wa kufunga ndoa mbele ya mashahidi wawili. Soma Zaidi...

NI ZIPI SWALA ZA SUNNAH: (qabliya (kabliya) na baadiya, tahajudi, tarawehe, qiyamu layl, shukr, istikhara)
Sunnah za SwalaSunnah za Swala Vipengele vya sunnah katika swala ni vile ambavyo mwenye kuswali akivitenda husaidia sana kukuza daraja ya swala yake na kuipa nguvu na msukumo mkubwa wa kuiwezesha kufikia lengo lililokusudiwa kwa urahisi zaidi. Soma Zaidi...

Maandalizi kwa ajili ya kifo
Mwanadamu anatakiwa aishi huku akikumbuka kuwa ipo siki atakufa. Hivyo basi inatupata lujiandaa mapema kwa ajili ya kifo. Soma Zaidi...

Waislamu wanaolazimika kufunga
Nguzo za uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...