Mtazamo na Msimamo wa Uislamu Juu ya Kudhibiti Uzaz (uzazi wa mpango) na hukumu yake

Mtazamo na Msimamo wa Uislamu Juu ya Kudhibiti Uzaz (uzazi wa mpango) na hukumu yake

4. Mtazamo na Msimamo wa Uislamu Juu ya Kudhibiti Uzazi

Kupanga Uzazi Katika Uislamu

- Uislamu unawataka watu kuoana na kuzaana kwa utaratibu na mfumo mzuri ili kutunza na kulea maadili ya familia.


- Uislamu umeweka utaratibu wa umri wa kuzaa kati ya mtoto na mtoto kwa muda wa miaka miwili.
Rejea Qurโ€™an (2:233)

- Uislamu umekataza watu kuzaa nje ya ndoa ambao ni wa kiholela na usiokuwa na malezi bora ya kifamilia.


- Uislamu umeruhusu kuzuia mimba tu kama mwanamke ananyonyesha mtoto mchanga au atadhurika kiafya au kuhatarisha maisha yake.

- Uislamu umeweka utaratibu wa kuzaa na kulea kama njia pekee ya kuendeleza na kujenga kizazi cha mwanaadamu katika maadili na uchumi pia.



Sababu za Uislamu Kupinga Dhana ya Kudhibiti Uzazi

i. Sera ya kudhibiti uzazi inachochea zinaa ambayo ni njia chafu, mbaya na ina madhara makubwa katika jamii ya binaadamu.
Rejea Qurโ€™an (17:32), (24:2)



ii. Sera ya kudhibiti uzazi ni kupinga na kuingilia mpango wa Allah (s.w) katika kupanga uzazi kwa njia ya ndoa.
Rejea Qurโ€™an (2:187), (2:233), (30:21)



iii. Dhana kuwa kuongezeka watu hupunguza riziki ni potofu na ni shirki, kwani ni kukana uwezo wa Allah (s.w) wa Kuruzuku na Kumiliki kila kitu.
Rejea Qurโ€™an (29:60)

iv. Kudhibiti uzazi ni kupoteza stara, hifadhi, huruma na mapenzi ya kweli baina ya mwanamke na mwanamume ambapo ni kinyume na utaratibu wa Allah (s.w).

v. Kudhibiti uzazi kwa hofu ya umaskini ni haramu, kwani kila kiumbe Allah

(s.w) amekikadiria riziki yake.

Rejea Qurโ€™an (17:31)

vi. Sera juu ya kudhibiti uzazi inalengo la kuepuka jukumu la kuzaa, kulea na kuendeleza kizazi kwa utaratibu unaofaa.


vii. Sera ya kudhibiti uzazi ni kuchochea ngono huru, ukahaba, kuzaliwa watoto kiholela wasiokuwa na baba na kuondoa nafasi ya ndoa katika jamii.

viii. Kudhibiti uzazi ni dhana ya uchoyo, ubadhirifu na ulafi wa kutaka kumiliki na kutumia rasilimali, uchumi, siasa, n.k kwa watu wachache




Sababu Zinazokulika Kudhibiti Uzazi Katika Uislamu

i. Kuhifadhi au kulinda afya ya mama asishike mimba baada ya kuthibitishwa na daktari anayeaminika kuwa itahatarisha afya au uhai wake.


ii. Iwapo mama ananyonyesha mtoto mchanga kwani mtoto anaweza kuathirika kiafya.

iii. Ikiwa mwanamke hawezi kuzaa ila kwa kufanyiwa operesheni, atalazimika kuzuia mimba baada ya kuzaa kwa operesheni mimba tatu.



Baadhi ya Njia Zinazotumika Kudhibiti Uzazi

a) Njia za Kisasa (Morden Method):

i. Kondom, mipira ya kiume na kike (Contraceptives). ii. Kitanzi-loop (Intra uterine device).
iii. Vidonge vya majira (Ant baby pill).

iv. Kufunga kitanzi kwa mwanamke (Tube Legation). v. Kufunga uzazi kwa wanaume (Vasectomy).
vi. Kutoa mimba (abortion).

vii. Uzazi wa maabara (test tube babies).

viii. Kukodisha matumbo ya wanawake wengine, kupandikiza mbegu (surrogate mothers)




b) Njia za Asilia, Maumbile (Natural Method):

i. Kufuata kalenda ya uzazi ya mwanamke (Menstrual Period or Circle).

ii. Kumwaga mbegu za uzazi nje kwa mwanamume (Coitus Interrunts or withdrawal)



                   

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Fiqh Main: Dini File: Download PDF Views 1858

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
๐Ÿ‘‰1 Kitau cha Fiqh    ๐Ÿ‘‰2 Simulizi za Hadithi Audio    ๐Ÿ‘‰3 Bongolite - Game zone - Play free game    ๐Ÿ‘‰4 kitabu cha Simulizi    ๐Ÿ‘‰5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    ๐Ÿ‘‰6 Kitabu cha Afya   

Post zinazofanana:

NI LIPI HASA LENGO LA KUFARADHISHWA SWALA ZA FARADHI NA KUWEPO KWA SWALA ZA SUNNAH (SUNA)

Lengo la Kusimamisha SwalaBila shaka swala imepewa umuhimu mkubwa kiasi cha kufanywa nguzo kubwa ya Uislamu kutokana na lengo lake.

Soma Zaidi...
taratibu na namna ya kutaliki, na mambo ya kuzingatia

Taratibu za Kutaliki KiislamuKama palivyo na taratibu za kuoa Kiislamu ndivyo hivyo pia ilivyo katika kuvunja ndoa.

Soma Zaidi...
MAANA YA ZAKA NA SADAKA KULUNGA NA KISHERIA PAMOJA NA TOFAUTI ZAO

MAANA YA ZAKA NA SADAKA KULUNGA NA KISHERIA PAMOJA NA TOFAUTI ZAO.

Soma Zaidi...
Jukumu la serikali katika kuzuia dhuluma

Serikali ina nafasi kubwa katika kuzuia dhulma na kufanya uchumibuwe huru kuyokana na dhulma.

Soma Zaidi...
Dhana ya kumiliki raslimali katika uislamu

Ni ipi raslimali ya halali kuimiliki katika uislamu.

Soma Zaidi...
Taratibu za kufanya kazi na kuajiri katika uislamu

Post hii itakufundisha taratibu za kuajiri, kufanya kazi na malipo.

Soma Zaidi...
Jinsi ambavyo msafiri anatakiwa aswali akiwa safarini

Postvhiibinakwenda kukufundisha kuhusu swala ya msafiri na jinsi ya kuiswali.

Soma Zaidi...
Fiqh.

Kipengele hichi tutajifunza chimbuko la fiqh na maana ya figh.

Soma Zaidi...