Mtazamo na Msimamo wa Uislamu Juu ya Kudhibiti Uzaz (uzazi wa mpango) na hukumu yake

Mtazamo na Msimamo wa Uislamu Juu ya Kudhibiti Uzaz (uzazi wa mpango) na hukumu yake

4. Mtazamo na Msimamo wa Uislamu Juu ya Kudhibiti Uzazi

Kupanga Uzazi Katika Uislamu

- Uislamu unawataka watu kuoana na kuzaana kwa utaratibu na mfumo mzuri ili kutunza na kulea maadili ya familia.


- Uislamu umeweka utaratibu wa umri wa kuzaa kati ya mtoto na mtoto kwa muda wa miaka miwili.
Rejea Qurโ€™an (2:233)

- Uislamu umekataza watu kuzaa nje ya ndoa ambao ni wa kiholela na usiokuwa na malezi bora ya kifamilia.


- Uislamu umeruhusu kuzuia mimba tu kama mwanamke ananyonyesha mtoto mchanga au atadhurika kiafya au kuhatarisha maisha yake.

- Uislamu umeweka utaratibu wa kuzaa na kulea kama njia pekee ya kuendeleza na kujenga kizazi cha mwanaadamu katika maadili na uchumi pia.



Sababu za Uislamu Kupinga Dhana ya Kudhibiti Uzazi

i. Sera ya kudhibiti uzazi inachochea zinaa ambayo ni njia chafu, mbaya na ina madhara makubwa katika jamii ya binaadamu.
Rejea Qurโ€™an (17:32), (24:2)



ii. Sera ya kudhibiti uzazi ni kupinga na kuingilia mpango wa Allah (s.w) katika kupanga uzazi kwa njia ya ndoa.
Rejea Qurโ€™an (2:187), (2:233), (30:21)



iii. Dhana kuwa kuongezeka watu hupunguza riziki ni potofu na ni shirki, kwani ni kukana uwezo wa Allah (s.w) wa Kuruzuku na Kumiliki kila kitu.
Rejea Qurโ€™an (29:60)

iv. Kudhibiti uzazi ni kupoteza stara, hifadhi, huruma na mapenzi ya kweli baina ya mwanamke na mwanamume ambapo ni kinyume na utaratibu wa Allah (s.w).

v. Kudhibiti uzazi kwa hofu ya umaskini ni haramu, kwani kila kiumbe Allah

(s.w) amekikadiria riziki yake.

Rejea Qurโ€™an (17:31)

vi. Sera juu ya kudhibiti uzazi inalengo la kuepuka jukumu la kuzaa, kulea na kuendeleza kizazi kwa utaratibu unaofaa.


vii. Sera ya kudhibiti uzazi ni kuchochea ngono huru, ukahaba, kuzaliwa watoto kiholela wasiokuwa na baba na kuondoa nafasi ya ndoa katika jamii.

viii. Kudhibiti uzazi ni dhana ya uchoyo, ubadhirifu na ulafi wa kutaka kumiliki na kutumia rasilimali, uchumi, siasa, n.k kwa watu wachache




Sababu Zinazokulika Kudhibiti Uzazi Katika Uislamu

i. Kuhifadhi au kulinda afya ya mama asishike mimba baada ya kuthibitishwa na daktari anayeaminika kuwa itahatarisha afya au uhai wake.


ii. Iwapo mama ananyonyesha mtoto mchanga kwani mtoto anaweza kuathirika kiafya.

iii. Ikiwa mwanamke hawezi kuzaa ila kwa kufanyiwa operesheni, atalazimika kuzuia mimba baada ya kuzaa kwa operesheni mimba tatu.



Baadhi ya Njia Zinazotumika Kudhibiti Uzazi

a) Njia za Kisasa (Morden Method):

i. Kondom, mipira ya kiume na kike (Contraceptives). ii. Kitanzi-loop (Intra uterine device).
iii. Vidonge vya majira (Ant baby pill).

iv. Kufunga kitanzi kwa mwanamke (Tube Legation). v. Kufunga uzazi kwa wanaume (Vasectomy).
vi. Kutoa mimba (abortion).

vii. Uzazi wa maabara (test tube babies).

viii. Kukodisha matumbo ya wanawake wengine, kupandikiza mbegu (surrogate mothers)




b) Njia za Asilia, Maumbile (Natural Method):

i. Kufuata kalenda ya uzazi ya mwanamke (Menstrual Period or Circle).

ii. Kumwaga mbegu za uzazi nje kwa mwanamume (Coitus Interrunts or withdrawal)



                   

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Fiqh Main: Dini File: Download PDF Views 2226

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
๐Ÿ‘‰1 Kitabu cha Afya    ๐Ÿ‘‰2 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    ๐Ÿ‘‰3 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    ๐Ÿ‘‰4 Bongolite - Game zone - Play free game    ๐Ÿ‘‰5 Dua za Mitume na Manabii    ๐Ÿ‘‰6 Kitau cha Fiqh   

Post zinazofanana:

MALI ZISIZORUHUSIWA KUTOLEWA ZAKA

*Suala la kumilikiwa binaadam (utumwa), japokuwa linaendelea kutajwa kwenye Sharia (katika vitabu), ni suala ambalo haliko.

Soma Zaidi...
Kwa nini waislamu wanaoa mke zaidi ya mmoja

Post hiibitakugundisha hekima ya kuruhusiwa kuoa mke zaidi ya mmoja katika sheria za kiislamu.

Soma Zaidi...
Hukumu ya kufinga kwa kifuata kuandama kwa mwezi

Ni muda gani unatakiwa ufunge ramadhani, je kuandama kwa mwezi kwa kiona ama hata kusiki.

Soma Zaidi...
Ni nini maana ya Talaka katika uislamu

Post hii inakwenda kukufundisha maana ya neno talaka katika uislamu kisheria na kilugha.

Soma Zaidi...
Nguzo za swaumu (kufinga)

Hapa utajifunza nguzo kuu za swaumu. Kama hazitatimia nguzo hizi basi swaumu itakuwa ni batili.

Soma Zaidi...
Mgawanyo wa mirathi kutoka kwenye Quran

Quran imegawanya mirathi katika haki. Mgawanyo huu ndio unaotakiwa utumike na si vinhinevyo.

Soma Zaidi...
Usitamani kifo hata ukiwa mchamungu mno ama muovu mno

Katika uislamu imekatazwa kutamani kufa hata kama utakuwa ni mtu muovu sana ama mchamungu sana.

Soma Zaidi...
Mtazamo wa uislamu juu ya ndoa ya mke zaidi ya mmoja

Je jamii inachukuliaje swala la kuoa mke zaidi ya mmoja.

Soma Zaidi...