Aina mbili za talaka zisizo na rejea katika uislamu


image


Huwezi kuruhusiwa kumrejea mke endapo utamuacha kwa talaka hizi mbili.


2.Talaka Isiyorejewa
Talaka isiyorejewa ni ile ambayo mtu hawezi tena kumrejea mkewe hata kama watasuluhishana kabla ya eda au baada ya eda. Kuna ama kuu mbili za talaka zisizorejewa:
(a)Talaka Tatu.
(b)Talaka ya Li'aan.

 


(a)Talaka tatu
Talaka tatu zinapatikana kwa kutamka dhamira ya kumuacha mke mara tatu katika kila twahara ndani ya twahara tatu za eda. Vile vile zitahesabika talaka tatu kama mume katika muda wa ndoa yao amewahi kutoa talaka rejea mbili kwa kipindi kimoja cha eda au vipindi tofauti ambapo walipatana na kurejeana. Pia kama mtu na mkewe waliwahi kuvunja ndoa mara moja kwa talaka mbili kisha mara zote hizo mbili walipatana kufunga ndoa tena watakapopeana talaka katika ndoa yao hii ya mwisho, talaka hiyo itahesabika kuwa ni talaka ya tatu.

 

Ni kinyume kabisa na sheria ya Kiislamu kutoa talaka tatu mfululizo katika kikao kimoja au katika twahara moja kwa matamshi. Wanachuoni wengi wamekubaliana kuwa talaka ya namna hiyo itahesabiwa kuwa ni talaka moja. Waislamu wanaofanya hivyo, wajue kuwa huko ni kuzifanyia mzaha aya za Mwenyezi Mungu na kuvuka mipaka ya Mwenyezi Mungu. "Na anayeruka mipaka ya Mwenyezi Mungu basi amejidhulumu nafsi yake " (65:1).

 


Uislamu umekataza vikali mchezo wa kutoa talaka tatu kwa mpigo kama tunavyojifunza katika hadithi: Mahmuud bin Labiid (r.a) ameeleza kuwa Mtume wa Mwenyezi Mungu alieelezwa juu ya mtu aliyetoa talaka tatu mfululizo kwa mkewe. Kisha Mtume alisimama akiwa amechukizwa sana na akasema: "Unacheza na Kitabu cha Mwenyezi Mungu (s.w) nikiwa bado tupo pamoja (nikiwa bado s/afa)?" (Mtume alikasirika) kwa kiasi ambacho mtu mmoja alisimama akauliza: Je, siwezi kumuua? (Nisai)

 


Hukumu ya talaka tatu ni kwamba baada ya mume kutamka talaka ya tatu hawezi tena kumrejea mkewe katika kipindi cha eda hata kama watapatana vipi. Baada ya kipindi cha eda kwisha, mkewe atakuwa ameachika kwa talaka tatu na atakuwa huru kuolewa na mume mwingine yeyote aliyehalalishwa kwake katika sheria ya Kiislamu. Lakini ni haramu mwanamke huyo kuolewa na mumewe wa kwanza mpaka aolewe na mume mwingine. Kisha akiachika kwa mume wa pili kwa sababu za msingi au akiachwa mjane, ndipo itakuwa halali kwake kuolewa na mume wake wa kwanza. Ndoa ya namna hii inajulikana kwa jina Ia "Tahliil". Qur-an inabainisha hukumu hii katika aya ifuatayo:

 


Na kama amempa talaka (ya tatu) basi (mwanamume huyo) si halali kwake baada ya hapo mpaka aolewe na mume mwingine. Na (mwanamume huyo mwingine) akimwacha, basi hapana dhambi kwao kurejeana (kwa kuoana tena) wakiona kuwa watasimamisha mipaka ya Mwenyezi Mungu. Na hii ni mipaka ya Mwenyezi Mungu anayoibainisha kwa watu wajuao. (2:230)

 


Hukumu hii kali imetolewa iii Waislamu wasifanye mas-khara na talaka. Kuna baadhi ya Waislamu, wakikwaruzana tu kidogo na wake zao hutishia talaka au anatoa talaka kabisa. Mtu akiendelea na mchezo huu atajistukia ameshamuacha mkewe kwa talaka tatu na hana namna tena ya kumrejea. Ni katika mchezo huu wa kutoa talaka tatu bila kufikiri na kumuogopa Mwenyezi Mungu, baadhi ya Waislamu wameishia katika majuto. Baadhi ya Waislamu wanadiriki kumdanganya Mwenyezi Mungu kwa mtu kumuhonga mume mwingine amuoe mtalaka wake kwa lengo Ia kumuacha baada ya muda mfupi (na ikiwezekana asimguse) iii awe halali kuolewa na mume wake wa mwanzo. Huku ni kuzifanyia mzaha sheria za Mwenyezi Mungu na ni Haramu ya uwazi. Ndoa za namna hiyo hazisihi mbele ya Mwenyezi Mungu (s.w).

 


(b)Talaka ya Li'aan
Talaka hii hupatikana kwa viapo viwili cha mume na mke. Ikitokea kwamba mume au mke amemkamata mwenzie ugoni lakini hapana mashahidi wanne walioshuhudia kitendo hicho ila yeye mwenyewe itabidi, kama mume ndiye aliyemkamata mkewe ugoni, aape kwa kurudia mara nne kuwa anashuhudia kuwa mkewe mzinifu, kisha mara ya tano aape kwamba Iaana ya Mwenyezi Mungu iwe juu yake ikiwa yeye ni miongoni mwa waongo. Mke naye ataapa mara nne kujitetea kuwa yeye hakufanya kitendo hicho kisha mara ya tano aape kuwa Iaana ya Mwenyezi Mungu iwe juu yake kama mumewe ni miongoni mwa wasemao kweli. Viapo hivi vinabainishwa katika aya zifuatazo:

 

Na wale wanaowasingizia wake zao (kuwa wamezini) na hawana mashahidi ila nafsi zao, basi ushahidi wa mmoja wao utakuwa kushuhudilia mara nne kwa kiapo cha Mwenyezi Mungu ya kwamba: bila shaka yeye ni mmoja wa wanaosema kweli.

 


Na mara ya tano (aape) kwamba laana ya Mwenyezi Mungu iwe juu yake ikiwa ni miongoni mwa waongo. Na (mke) itamuondokea adhabu kwa kutoa shahada mara nne kwa kiapo cha Mwenyezi Mungu ya kwamba (mume) ni miongoni mwa waongo.

 


Na mara ya tano (aape) ya kwamba hasira ya Mwenyezi Mungu iwe juu yake kama (mumewe) yu miongoni mwa wanaosema kweli, (na yeye mke ndiye mwongo). (24:6-9)
Baada ya kuapizana hivi, hapo hapo ndoa itakuwa imevunjika moja kwa moja kwani wawili hawa hawategemewi tena kurejeana na kukaa kwa furaha na amani.

 



Sponsored Posts


  ðŸ‘‰    1 Jifunze Fiqh       ðŸ‘‰    2 Download App zetu hapa ujifunze zaidi       ðŸ‘‰    3 Madrasa kiganjani offline       ðŸ‘‰    4 Tunakukaribisha kwenye Maktaba yetu    


Je una maswali, maoni ama ushauri, tutumie sms ✉ bofya hapa hapa, ama wasiliana nasi kwa WhatsApp bofya hapa



Post Nyingine


image Namna ya kutayamamu hatuwa kwa hatuwa
Post hii inakwenda kukufundisha kuhusu jinsi yavkutayamamu. Soma Zaidi...

image Jinsi ya kiswali swala ya haja
Post hii itakufundisha kuhusu swala ya haja na jisi ya kuiswali. Soma Zaidi...

image Sifa za kuwa maamuma kwenye swala na namna ya kumfuata imamu
Post hii inakwenda kukuelezea sifa za kuwa maamuma na taratibu za kumfuata imamu. Soma Zaidi...

image Kujitwaharisha kutokana na najisi
Post hii itakufundisha namna ya kutwaharisha Najisi. Soma Zaidi...

image Ni upi umuhimu wa kufunga katika uislamu
Post hii inakwenda kukufundisha kuhusu umuhimu wa kufunga kiroho, kiafya na kijamii. Soma Zaidi...

image Nini maana ya kusimamisha swala
Post hii inakwenda kukufundisha maana ya kusimamisha swala kama inavyotumika kisheria. Soma Zaidi...

image Nguzo za swaumu (kufinga)
Hapa utajifunza nguzo kuu za swaumu. Kama hazitatimia nguzo hizi basi swaumu itakuwa ni batili. Soma Zaidi...

image Dhana ya kumiliki raslimali katika uislamu
Ni ipi raslimali ya halali kuimiliki katika uislamu. Soma Zaidi...

image Madhara ya riba kwenye jamii
Haya ni madhara ya riba katika jamii. Ni kwa namna gani jamii inadhurika kutokana na riba? Soma Zaidi...

image Jinsi ya kusherehekea siku ya idi katika uislamu
Uislamu umeweka taratibu maalumu za kuzifata katika kusherehekea siku ya idi. Soma Zaidi...