Kiasi cha mahari kilicho bora kinachofaaa katika uislamu


image


Uislamu haukuwekabkiwango maalumu cha mahari. Mwanamke anaweza tajabkiasi atakacho. Ila vyema kuzingatia haya wakayi wa kutamka mahari yako.


Kiasi gani Kinachojuzu kutolewa Mahari?

Hapana kiwango maalum cha mahari kilichowekwa na Sheria ya Kiislamu. Mahari ni haki ya mwanamke mwenye kuolewa na ndiye pekee mwenye uhuru kamili wa kutaja kiasi cha mahari anachokitaka. Akipenda anaweza kudai mrundi wa dhahabu na fedha (Qur-an: 4:20), au akitaka anaweza kupokea kiasi kidogo sana cha mali kama vile shilingi 1/- au chini zaidi kuliko hivyo au akitaka anaweza akasamehe asitake kitu chochote ila kauli nzuri tu.

 


Lakini tunashauriwa katika Qur-an kuwa mtoaji mahari na mpokeaji mahari waangaliane hali. Kama hali ya mtoaji ni nzuri, ni vyema azidishe mahari kuliko kile kiasi kilichotajwa iwapo ana uwezo huo. Na mpokeaji wa mahari, endapo ataona hali ya mtoaji si nzuri kiuchumi, basi ampunguzie mahari na apokee kiasi kidogo zaidi ya kile alichokitaja mwanzoni. Huku kuangaliana hali kunazidisha mapenzi na huruma baina ya mume na mke.

 


Pamoja na kuwa mahari hayana kiwango maalum kilichowekwa, inashauriwa yasiwe ya juu sana kiasi cha kuifanya ndoa kuwa jambo gumu na kurahisisha uzinifu katika jamii. Hebu tuusikilize ushauri wa Umar bin Khattab (r.a) (Khalifa wa Pili wa Mtume (s.a.w) ambaye amesema:

 

"Kuweni waangalfu msfanye mahari ghali. Ingelikuwa kufanya hivyo ni jambo zuri la kumpelekea mtu kwenye ucha-Mungu, Mtume (s.a.w) angelikuwa wa kwanza katikajambo hilo. Sikumbuki kumuona Mtume (s.a.w) katika lwmuoa yeyote katika wake zake au katika lwwaoza yeyote katika binti zake kwa zaidi ya Wakia 12.5 (lwmi na mbili na nusu) ambazo ni sawa na Dirham 500".

 


Pia katika hadithi iliyosimuliwa na Jabir (r.a) Mtume (s.a.w) amesema: Atakayetoa viganja viwili vya tende au shairi kama mahari ya mkewe (naye akaridhia) atakuwa ameufanya uchi wa mkewe uwe halali kwake. (Abu Daud).

 



Sponsored Posts


  ðŸ‘‰    1 Jifunze Fiqh       ðŸ‘‰    2 Tunakukaribisha kwenye Maktaba yetu       ðŸ‘‰    3 Madrasa kiganjani offline       ðŸ‘‰    4 Download App zetu hapa ujifunze zaidi    


Je una maswali, maoni ama ushauri, tutumie sms ✉ bofya hapa hapa, ama wasiliana nasi kwa WhatsApp bofya hapa



Post Nyingine


image Sifa za kuwa maamuma kwenye swala na namna ya kumfuata imamu
Post hii inakwenda kukuelezea sifa za kuwa maamuma na taratibu za kumfuata imamu. Soma Zaidi...

image Maana ya hadathi na aina zake
Post hii inakwenda kukugundisha maana ya hadathi pamoja na kutaja aina za hadathi Soma Zaidi...

image Mambo ya kuzingatia kabla ya kugawa mirathi
Haya ni mamno muhimu yanayozingatiwa kabla ya kuanza zoezi la kugawa mirathi ya marehemu. Soma Zaidi...

image Mgawanyo wa mirathi kutoka kwenye Quran
Quran imegawanya mirathi katika haki. Mgawanyo huu ndio unaotakiwa utumike na si vinhinevyo. Soma Zaidi...

image Warithi wasio na mafungu maalumu katika uislamu
Hapa utajifunza watu wanaorithi bila ya kuwekewa mafungu maalumu au viwango maalumi vya kurithi. Soma Zaidi...

image Jinsi ya kufanya suluhu kati ya mume na mke.
Post hii inakwenda kukufundisha kuhusu jinsi ya kufanya suluhu katika ndoa. Soma Zaidi...

image Yaliyo haramu kwa mtu asiyekuwa na udhu
Post hii inakwenda kukufundisha kuhusu mambo ambauo ni haramu kwa mtu asiye na udhu. Soma Zaidi...

image Historia ya adhana na Iqama na jinsi ya kuadhini.
Hadithi hii inakwenda kukufundisha historia fupi ya adhana pia utakwenda kujifunza jinsi ya kuadhini na kuqimu. Soma Zaidi...

image Jinsi ya kiswali swala ya haja
Post hii itakufundisha kuhusu swala ya haja na jisi ya kuiswali. Soma Zaidi...

image Taratibu za kutaliki katika uislamu.
Hapa utajifunza taratibu zinazofuatwa wakati wa kukusudia kumuacha mke. Pia utajifunza sababu za kiwepo kwa eda baada ya kuachwa mwanamke. Soma Zaidi...