picha

Kiasi cha mahari kilicho bora kinachofaaa katika uislamu

Uislamu haukuwekabkiwango maalumu cha mahari. Mwanamke anaweza tajabkiasi atakacho. Ila vyema kuzingatia haya wakayi wa kutamka mahari yako.

Kiasi gani Kinachojuzu kutolewa Mahari?

Hapana kiwango maalum cha mahari kilichowekwa na Sheria ya Kiislamu. Mahari ni haki ya mwanamke mwenye kuolewa na ndiye pekee mwenye uhuru kamili wa kutaja kiasi cha mahari anachokitaka. Akipenda anaweza kudai mrundi wa dhahabu na fedha (Qur-an: 4:20), au akitaka anaweza kupokea kiasi kidogo sana cha mali kama vile shilingi 1/- au chini zaidi kuliko hivyo au akitaka anaweza akasamehe asitake kitu chochote ila kauli nzuri tu.

 


Lakini tunashauriwa katika Qur-an kuwa mtoaji mahari na mpokeaji mahari waangaliane hali. Kama hali ya mtoaji ni nzuri, ni vyema azidishe mahari kuliko kile kiasi kilichotajwa iwapo ana uwezo huo. Na mpokeaji wa mahari, endapo ataona hali ya mtoaji si nzuri kiuchumi, basi ampunguzie mahari na apokee kiasi kidogo zaidi ya kile alichokitaja mwanzoni. Huku kuangaliana hali kunazidisha mapenzi na huruma baina ya mume na mke.

 


Pamoja na kuwa mahari hayana kiwango maalum kilichowekwa, inashauriwa yasiwe ya juu sana kiasi cha kuifanya ndoa kuwa jambo gumu na kurahisisha uzinifu katika jamii. Hebu tuusikilize ushauri wa Umar bin Khattab (r.a) (Khalifa wa Pili wa Mtume (s.a.w) ambaye amesema:

 

"Kuweni waangalfu msfanye mahari ghali. Ingelikuwa kufanya hivyo ni jambo zuri la kumpelekea mtu kwenye ucha-Mungu, Mtume (s.a.w) angelikuwa wa kwanza katikajambo hilo. Sikumbuki kumuona Mtume (s.a.w) katika lwmuoa yeyote katika wake zake au katika lwwaoza yeyote katika binti zake kwa zaidi ya Wakia 12.5 (lwmi na mbili na nusu) ambazo ni sawa na Dirham 500".

 


Pia katika hadithi iliyosimuliwa na Jabir (r.a) Mtume (s.a.w) amesema: Atakayetoa viganja viwili vya tende au shairi kama mahari ya mkewe (naye akaridhia) atakuwa ameufanya uchi wa mkewe uwe halali kwake. (Abu Daud).

 

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Fiqh Main: Dini File: Download PDF Views 1903

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Kitau cha Fiqh    👉2 Simulizi za Hadithi Audio    👉3 web hosting    👉4 Kitabu cha Afya    👉5 Bongolite - Game zone - Play free game    👉6 kitabu cha Simulizi   

Post zinazofanana:

Sunnah za udhu

Posti hii inakwenda kukufundisha kuhusu sunah za udhu

Soma Zaidi...
Mambo yanayoharibu Udhu (yanayobatilisha udhu)

Post hii inakwenda kukufundisha mambo ambayo hubatilisha udhu yaani mam,boa mbayo yanaharibu udhu.

Soma Zaidi...
Namna ya kuswali hatuwa kwa hatuwq

Post hii itakufundisha jinsi ya kuswali hatuwa kwa hatuwa.

Soma Zaidi...
Mda wa mwisho wa kula daku mwezi wa ramadhani

Post hii fupi itakwenda kukujulisha utaratibu wa kula daku.

Soma Zaidi...
Taratibu za mirathi katika zama za ujahilia

Kabla ya kuhubiriwa uislamu watu wa Maka walikuwa na tarayibu zenye dhuluma ndani yake katika ugawaji wa mirathi.

Soma Zaidi...
Jinsi ya kufanya suluhu kati ya mume na mke.

Post hii inakwenda kukufundisha kuhusu jinsi ya kufanya suluhu katika ndoa.

Soma Zaidi...
Nini maana ya kusimamisha swala?

Je kusimamisha swala kuna maana gani kwenye uislamu?

Soma Zaidi...