- Riba ni kipato chochote kile cha ziada kutokana na mkopo au mtaji bila kushiriki katika faida au hasara.
- Riba ni kipato chochote kile cha ziada kutokana na mkopo au mtaji bila kushiriki katika faida au hasara.
Rejea Qurβan (2:275-276)
Uharamu wa Riba
i. Uislamu umeharamisha riba kwa sababu ni dhulma (unyonyaji) kwa mnyonge mwenye dhiki aliyekopa ili kukidhi haja ya msingi kimaisha.
ii. Riba inahamisha mali na rasilimali kutoka kwa maskini au wanyonge kwenda kwa matajiri.
iii. Riba huondoa usawa na uadilifu katika kugawa na kutumia mali na rasilimali baina ya maskini au wanyonge na matajiri.
iv. Riba imeharamishwa kwa sababu huleta maisha ya kivivu na kutowajibika kwa matajiri, kuchuma bila jasho lolote.
v. Riba ina sababisha watu maskini na wanyonge wabakie kuishi kidhalili kwa kuwatumikia matajiri tu.
vi. Riba husababisha uchumi kuzorota kwa kumikiwa na watu wachache au vyombo kama mabenki, bima, kwa mfumo wa riba.
Madhara ya Riba Katika Jamii
i. Riba inachafua nafsi ya tajiri, kwa kuwa bahili, mchoyo asiyetayari kuwasaidia maskini, wanyonge na wenye shida mpaka bila malipo yeyote ya ziada.
ii. Riba huchafua mali ya tajiri kutokana na njia haramu za kuchuma na kumiliki bila kuzingatia mipaka.
iii. Riba inakandamiza wanyonge, maskini na wenye dhiki na matatizo, wenye kuhitajia misaada ili waweze kuishi.
iv. Riba inaharibu uchumi na maendeleo ya jamii kwa kudhulumu kundi la maskini na kufaidisha kundi la matajiri.
v. Riba inahamisha uchumi, mali na rasilimali kutoka kwa maskini na wanyonge kwenda kwa matajiri.
Je! umeipenda hii post?
Ndio Hapana Save post
Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Topic: Fiqh Main: Post File: Download PDF Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 970
Sponsored links
π1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)
π2 Kitau cha Fiqh
π3 Kitabu cha Afya
π4 kitabu cha Simulizi
π5 Madrasa kiganjani
π6 Simulizi za Hadithi Audio
Sanda ya mtoto
Mambo ya faradh kwa maiti ya muislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...
Nguzo za kufunga ramadhani
Nguzo za uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...
NAMNA ZA ZAKA (AINA NA MGAWANYIKO WA ZAKA) ZAKA IPO MAKUNDI MANGAPI?
Soma Zaidi...
hizi ndio nguzo za swala, swala za faradhi na suna
Soma Zaidi...
Maana na taratibu za kiuchumi katika uislamu
Soma Zaidi...
Zifahamu njia za kutwaharisha, aina za maji, udongo na Namna ya kujitwaharisha
Soma Zaidi...
Swala ya jamaa na taratibu zake
Post hii inakwenda kukufundisha kuhusu swala ya jamaa na taratibu zake. Soma Zaidi...
Matendo ya hijjah na umrah
Nguzo za uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...
ZIJUE HUKUMU NA FADHILA ZA KUTOA ZAKA KATIKA UISLAMU
Zaka ni nini? Soma Zaidi...
Dhana ya haki na uadilifu katika uislamu
HAKI NA UADILIFU KATIKA UISLAMU. Soma Zaidi...
Sera ya uchumi katika Uislamu
4. Soma Zaidi...
Dua ya kuzuru makaburi, na utaratibu wa kuzuru makaburi
Kuzuru makaburi ni katika matendo ya sunah yaani unapata thawabu kwa kwenda klizuru kaburi. Soma Zaidi...