- Riba ni kipato chochote kile cha ziada kutokana na mkopo au mtaji bila kushiriki katika faida au hasara.
- Riba ni kipato chochote kile cha ziada kutokana na mkopo au mtaji bila kushiriki katika faida au hasara.
Rejea Qurβan (2:275-276)
Uharamu wa Riba
i. Uislamu umeharamisha riba kwa sababu ni dhulma (unyonyaji) kwa mnyonge mwenye dhiki aliyekopa ili kukidhi haja ya msingi kimaisha.
ii. Riba inahamisha mali na rasilimali kutoka kwa maskini au wanyonge kwenda kwa matajiri.
iii. Riba huondoa usawa na uadilifu katika kugawa na kutumia mali na rasilimali baina ya maskini au wanyonge na matajiri.
iv. Riba imeharamishwa kwa sababu huleta maisha ya kivivu na kutowajibika kwa matajiri, kuchuma bila jasho lolote.
v. Riba ina sababisha watu maskini na wanyonge wabakie kuishi kidhalili kwa kuwatumikia matajiri tu.
vi. Riba husababisha uchumi kuzorota kwa kumikiwa na watu wachache au vyombo kama mabenki, bima, kwa mfumo wa riba.
Madhara ya Riba Katika Jamii
i. Riba inachafua nafsi ya tajiri, kwa kuwa bahili, mchoyo asiyetayari kuwasaidia maskini, wanyonge na wenye shida mpaka bila malipo yeyote ya ziada.
ii. Riba huchafua mali ya tajiri kutokana na njia haramu za kuchuma na kumiliki bila kuzingatia mipaka.
iii. Riba inakandamiza wanyonge, maskini na wenye dhiki na matatizo, wenye kuhitajia misaada ili waweze kuishi.
iv. Riba inaharibu uchumi na maendeleo ya jamii kwa kudhulumu kundi la maskini na kufaidisha kundi la matajiri.
v. Riba inahamisha uchumi, mali na rasilimali kutoka kwa maskini na wanyonge kwenda kwa matajiri.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
Post hii inakwenda kukugundisha kuhusu maana halisi ya ibada ya swala.
Soma Zaidi...Post hii inakwenda kukupa orodha ya vitu vilivyo najisi.
Soma Zaidi...(c) Hifadhi ya Mwanamke na Maadili ya JamiiKimaumbile wanaadam kama walivyo wanyama, wamejaaliwa kuwa na mvuto wa kimapenzi kati ya mume na mke ili kuwawezesha kutekeleza wajibu mkubwa wa kuzaana na kuendeleza kizazi.
Soma Zaidi...Hapa utajifunza utaratibu wa hutuba ya ndoa ya kiislamu. Sharti za jutuba ya ndoa na jinsibya kuozesha
Soma Zaidi...Kustawi kwa Kampeni ya Kudhibiti UzaziMiongoni mwa sababu zilizosaidia kustawi kwa kampeni hii ni matokeo ya mapinduzi ya viwanda (Industrial revolution) ya huko Ulaya.
Soma Zaidi...Ili swala itimie utahitajika kutimiza nguzo zake na masharti yake. Hapa utajifunza nguzo 17 za swala.
Soma Zaidi...Posti hii itakufundisha masharti yanayohitajika kwa mwenye kutaka kutia udhu.
Soma Zaidi...