- Riba ni kipato chochote kile cha ziada kutokana na mkopo au mtaji bila kushiriki katika faida au hasara.
- Riba ni kipato chochote kile cha ziada kutokana na mkopo au mtaji bila kushiriki katika faida au hasara.
Rejea Qurβan (2:275-276)
Uharamu wa Riba
i. Uislamu umeharamisha riba kwa sababu ni dhulma (unyonyaji) kwa mnyonge mwenye dhiki aliyekopa ili kukidhi haja ya msingi kimaisha.
ii. Riba inahamisha mali na rasilimali kutoka kwa maskini au wanyonge kwenda kwa matajiri.
iii. Riba huondoa usawa na uadilifu katika kugawa na kutumia mali na rasilimali baina ya maskini au wanyonge na matajiri.
iv. Riba imeharamishwa kwa sababu huleta maisha ya kivivu na kutowajibika kwa matajiri, kuchuma bila jasho lolote.
v. Riba ina sababisha watu maskini na wanyonge wabakie kuishi kidhalili kwa kuwatumikia matajiri tu.
vi. Riba husababisha uchumi kuzorota kwa kumikiwa na watu wachache au vyombo kama mabenki, bima, kwa mfumo wa riba.
Madhara ya Riba Katika Jamii
i. Riba inachafua nafsi ya tajiri, kwa kuwa bahili, mchoyo asiyetayari kuwasaidia maskini, wanyonge na wenye shida mpaka bila malipo yeyote ya ziada.
ii. Riba huchafua mali ya tajiri kutokana na njia haramu za kuchuma na kumiliki bila kuzingatia mipaka.
iii. Riba inakandamiza wanyonge, maskini na wenye dhiki na matatizo, wenye kuhitajia misaada ili waweze kuishi.
iv. Riba inaharibu uchumi na maendeleo ya jamii kwa kudhulumu kundi la maskini na kufaidisha kundi la matajiri.
v. Riba inahamisha uchumi, mali na rasilimali kutoka kwa maskini na wanyonge kwenda kwa matajiri.
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.
Download NowUmeionaje Makala hii.. ?
Suala la omba-ombaTukiliangalia suala la omba-omba kwa upana kidogo, ambalo hivi sasa linaongelewa katika vikao mbalimbali vya kitaifa na kimataifa, tutaona kuwa ni Uislamu pekee unaotoa namna bora ya kulishughulikia suala hili.
Soma Zaidi...Wajibu wa KufanyakaziUislamu siyo tu unawahimiza watu kufanya kazi na kutokuwa wavivu bali kufanya kazi ni Ibada.
Soma Zaidi...Nguzo za uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)
Soma Zaidi...Post hii itakufundisha mambo ambayo yatasababisha swqla yako isikubaliwe.
Soma Zaidi...Post hii inakwenda kukupa sifa za imamu wa msikitini anayepasa kuswalisha swala ya jamii.
Soma Zaidi...Nguzo za uislamu,kutoa zakat na sadaqat (EDK form 2; dhana ya elimu ya uislamu)
Soma Zaidi...