Haki na uadilifu katika uislamu (EDK form 3: Dhana ya elimu ya uislamu)
5.2. Msimamo wa Uislamu juu ya Utumwa.
Hali ya Utumwa kabla ya Mtume Muhammad (s.a.w).
- Biashara ya utumwa ilidumu na kuenea sana enzi za ujahili takribani nchi na
mabara mbali mbali hasa nchi za Magharibi, Uarabuni, Bara la Asia na kwingineko Duniani.
- Watumwa walikuwa wakikamatwa na kutezwa nguvu bila kujali utu na
ubinaadamu wao.
- Watumwa walimilikiwa kwa kuuzwa na kununuliwa kama bidhaa za biashara
au kwa matumizi mengineyo pia.
- Watumwa walikuwa wakitumika kama sehemu ya starehe na kiburudisho kwa
wakubwa zao.
- Mateso, unyama na ukatili ilikuwa desturi ya kufanyiwa watumwa na mabwana
zao katika kutimiza matashi yao.
- Watumwa walikuwa hawana uhuru wa kufanya na kufuata mila, desturi au dini
waitakayo na waipendayo wao wenyewe bila ruhusa ya wakubwa wao.
- Watumwa walikuwa wakitumikishwa kama wanyama au hata zaidi ya wanyama
kwa kufanyishwa kazi ngumu zilizozidi uwezo wao.
- Kila jaribio la ubaya lilifanywa kupitia watumwa, mfano makali ya kisu, mkuki,
mshale, n.k yalijaribiwa kwa watumwa.
- Watumwa ndio ilikuwa nyenzo pekee ya kufanyia kazi, kubebea na kusafirishia
mizigo mikubwa kwa masafa ya mbali.
- Hadhi na nafasi kati ya mabwa na watumwa ilikuwa na utofauti mkubwa mno,
kiasi kwamba bwana anaweza kumdhalilisha mtumwa kwa namna apendavyo.
- Huduma na misaada ya kiutu kwa watumwa ilikuwa hafifu mno, kiasi kwamba
mtumwa akiugua au kukosa uwezo wa kuzalisha mali alikuwa hana faida tena
kwa bwana.
Umeionaje Makala hii.. ?
Ni muda gani unatakiwa ufunge ramadhani, je kuandama kwa mwezi kwa kiona ama hata kusiki.
Soma Zaidi...Maana ya Swala Maana ya Swala kilugha(a) Kilugha Katika lugha ya Kiarabu neno ยSwalaatย lina maana ya ยombi au ยdua.
Soma Zaidi...Haya ni mamno muhimu yanayozingatiwa kabla ya kuanza zoezi la kugawa mirathi ya marehemu.
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwedna kujifunza jinsi ya kutwaharisha aina mbalimbali za najisi kwa mujibu wa mafundiso ya Mtume Muhammad (s.a.w)
Soma Zaidi...Masharti ya Utoaji wa Zakat na Swadaqat Utoaji katika njia ya Allah (s.
Soma Zaidi...Mambo ya faradh kwa maiti ya muislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)
Soma Zaidi...Endapo mke na mume wameachana na hali ya kuwa mke ana watoto wachanga. Je uislamu unasemaje kuhusu taratibu za malezi?
Soma Zaidi...