Msimamo wa uislamu juu ya utumwa
Haki na uadilifu katika uislamu (EDK form 3: Dhana ya elimu ya uislamu)
5.2. Msimamo wa Uislamu juu ya Utumwa.
Hali ya Utumwa kabla ya Mtume Muhammad (s.a.w).
- Biashara ya utumwa ilidumu na kuenea sana enzi za ujahili takribani nchi na
mabara mbali mbali hasa nchi za Magharibi, Uarabuni, Bara la Asia na kwingineko Duniani.
- Watumwa walikuwa wakikamatwa na kutezwa nguvu bila kujali utu na
ubinaadamu wao.
- Watumwa walimilikiwa kwa kuuzwa na kununuliwa kama bidhaa za biashara
au kwa matumizi mengineyo pia.
- Watumwa walikuwa wakitumika kama sehemu ya starehe na kiburudisho kwa
wakubwa zao.
- Mateso, unyama na ukatili ilikuwa desturi ya kufanyiwa watumwa na mabwana
zao katika kutimiza matashi yao.
- Watumwa walikuwa hawana uhuru wa kufanya na kufuata mila, desturi au dini
waitakayo na waipendayo wao wenyewe bila ruhusa ya wakubwa wao.
- Watumwa walikuwa wakitumikishwa kama wanyama au hata zaidi ya wanyama
kwa kufanyishwa kazi ngumu zilizozidi uwezo wao.
- Kila jaribio la ubaya lilifanywa kupitia watumwa, mfano makali ya kisu, mkuki,
mshale, n.k yalijaribiwa kwa watumwa.
- Watumwa ndio ilikuwa nyenzo pekee ya kufanyia kazi, kubebea na kusafirishia
mizigo mikubwa kwa masafa ya mbali.
- Hadhi na nafasi kati ya mabwa na watumwa ilikuwa na utofauti mkubwa mno,
kiasi kwamba bwana anaweza kumdhalilisha mtumwa kwa namna apendavyo.
- Huduma na misaada ya kiutu kwa watumwa ilikuwa hafifu mno, kiasi kwamba
mtumwa akiugua au kukosa uwezo wa kuzalisha mali alikuwa hana faida tena
kwa bwana.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉2 kitabu cha Simulizi 👉3 ai web app 👉4 Simulizi za Hadithi Audio 👉5 Bongolite - Game zone - Play free game 👉6 Dua za Mitume na Manabii
Post zinazofanana:
Jinsi ambavyo mtu anazuiliwa kurithi mali ya marehemu
Endapo mtu yupp katika orodha ya wanaotakiwa kutithi, anaweza kuzuiliwa kurithi kwa kuzingatia haya.
Soma Zaidi...Namna ya kutayamamu hatuwa kwa hatuwa
Post hii inakwenda kukufundisha kuhusu jinsi yavkutayamamu.
Soma Zaidi...