picha

Msimamo wa uislamu juu ya utumwa

Haki na uadilifu katika uislamu (EDK form 3: Dhana ya elimu ya uislamu)

     5.2. Msimamo wa Uislamu juu ya Utumwa.
Hali ya Utumwa kabla ya Mtume Muhammad (s.a.w).
-  Biashara ya utumwa ilidumu na kuenea sana enzi za ujahili takribani nchi na 
mabara mbali mbali hasa nchi za Magharibi, Uarabuni, Bara la Asia na      kwingineko Duniani. 

-  Watumwa walikuwa wakikamatwa na kutezwa nguvu bila kujali utu na  
    ubinaadamu wao.

-  Watumwa walimilikiwa kwa kuuzwa na kununuliwa kama bidhaa za biashara
    au kwa matumizi mengineyo pia.

-  Watumwa walikuwa wakitumika kama sehemu ya starehe na kiburudisho kwa
   wakubwa zao.

-  Mateso, unyama na ukatili ilikuwa desturi ya kufanyiwa watumwa na mabwana
    zao katika kutimiza matashi yao.

-  Watumwa walikuwa hawana uhuru wa kufanya na kufuata mila, desturi au dini 
    waitakayo na waipendayo wao wenyewe bila ruhusa ya wakubwa wao.

- Watumwa walikuwa wakitumikishwa kama wanyama au hata zaidi ya wanyama 
    kwa kufanyishwa kazi ngumu zilizozidi uwezo wao.

-  Kila jaribio la ubaya lilifanywa kupitia watumwa, mfano makali ya kisu, mkuki, 
    mshale, n.k yalijaribiwa kwa watumwa.

-  Watumwa ndio ilikuwa nyenzo pekee ya kufanyia kazi, kubebea na kusafirishia
    mizigo mikubwa kwa masafa ya mbali.

-  Hadhi na nafasi kati ya mabwa na watumwa ilikuwa na utofauti mkubwa mno, 
   kiasi kwamba bwana anaweza kumdhalilisha mtumwa kwa namna apendavyo. 

-  Huduma na misaada ya kiutu kwa watumwa ilikuwa hafifu mno, kiasi kwamba
   mtumwa akiugua au kukosa uwezo wa kuzalisha mali alikuwa hana faida tena
   kwa bwana.

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu
Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Fiqh Main: Post File: Download PDF Views 2693

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Simulizi za Hadithi Audio     👉2 Bongolite - Game zone - Play free game     👉3 Dua za Mitume na Manabii     👉4 Kitau cha Fiqh     👉5 ai web app     👉6 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    

Post zinazofanana:

Tofauti ya uchumi wa kiislamu na usio wa kiisalmu

Tofauti kati ya mfumo wa uchumi wa Kiislamu na ile ya Kitwaghuti (i) Dhana ya mafanikioKatika mtazamo wa uchumi wa Kiislamu mafanikio yanatazamwa kwa kuzingatia hatima ya ama mtu kupata radhi za Mwenyezi Mungu au kubeba laana ya Mwenyezi Mungu.

Soma Zaidi...
Masharti ya swala

Sharti za SwalaSharti za Swala Sharti za swala ni yale mambo ya lazima anayotakiwa Muislamu ayachunge na kuyatekeleza kabla hajaanza kuswali.

Soma Zaidi...