Msimamo wa uislamu juu ya utumwa

Haki na uadilifu katika uislamu (EDK form 3: Dhana ya elimu ya uislamu)

     5.2. Msimamo wa Uislamu juu ya Utumwa.
Hali ya Utumwa kabla ya Mtume Muhammad (s.a.w).
-  Biashara ya utumwa ilidumu na kuenea sana enzi za ujahili takribani nchi na 
mabara mbali mbali hasa nchi za Magharibi, Uarabuni, Bara la Asia na      kwingineko Duniani. 

-  Watumwa walikuwa wakikamatwa na kutezwa nguvu bila kujali utu na  
    ubinaadamu wao.

-  Watumwa walimilikiwa kwa kuuzwa na kununuliwa kama bidhaa za biashara
    au kwa matumizi mengineyo pia.

-  Watumwa walikuwa wakitumika kama sehemu ya starehe na kiburudisho kwa
   wakubwa zao.

-  Mateso, unyama na ukatili ilikuwa desturi ya kufanyiwa watumwa na mabwana
    zao katika kutimiza matashi yao.

-  Watumwa walikuwa hawana uhuru wa kufanya na kufuata mila, desturi au dini 
    waitakayo na waipendayo wao wenyewe bila ruhusa ya wakubwa wao.

- Watumwa walikuwa wakitumikishwa kama wanyama au hata zaidi ya wanyama 
    kwa kufanyishwa kazi ngumu zilizozidi uwezo wao.

-  Kila jaribio la ubaya lilifanywa kupitia watumwa, mfano makali ya kisu, mkuki, 
    mshale, n.k yalijaribiwa kwa watumwa.

-  Watumwa ndio ilikuwa nyenzo pekee ya kufanyia kazi, kubebea na kusafirishia
    mizigo mikubwa kwa masafa ya mbali.

-  Hadhi na nafasi kati ya mabwa na watumwa ilikuwa na utofauti mkubwa mno, 
   kiasi kwamba bwana anaweza kumdhalilisha mtumwa kwa namna apendavyo. 

-  Huduma na misaada ya kiutu kwa watumwa ilikuwa hafifu mno, kiasi kwamba
   mtumwa akiugua au kukosa uwezo wa kuzalisha mali alikuwa hana faida tena
   kwa bwana.

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Fiqh Main: Dini File: Download PDF Views 2111

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Bongolite - Game zone - Play free game    👉2 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    👉3 Madrasa kiganjani    👉4 Simulizi za Hadithi Audio    👉5 Kitau cha Fiqh    👉6 kitabu cha Simulizi   

Post zinazofanana:

Namna lengo la zakat linavyofikiwa

Nguzo za uislamu (EDK form 3:dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Dhana ya haki na uadilifu katika uislamu

Haki na uadilifu katika uislamu (EDK form 3:dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Hutuba ya Ndoa - Khutbat nikah

Hii ni hutuba ya ndoa kwa ufupi, Imekusanya mambo ya msingi yanayohitajika katika hutuba ya ndoa

Soma Zaidi...
Jinsi ya kuswali kuswali swala ya maiti

Post hii itakufundisha kuhusu swala ya maiti, nguzo za swala ya maiti, sharti za swwla ya maiti na jinsi ya kuiswali.

Soma Zaidi...
Maana ya Twahara na umuhimu wake katika uislamu

Katika somo hili utakwenda kujifunza maana ya Twahara Kwa mujibu wa mafundisho ya Uislamu

Soma Zaidi...