Mirathi Katika Uislamu, nani anarithi na ni mambo gani ya kuzingatia kabla ya kirisisha

Mirathi Katika Uislamu, nani anarithi na ni mambo gani ya kuzingatia kabla ya kirisisha

Mirathi Katika Uislamu, nani anarithi na ni mambo gani ya kuzingatia kabla ya kirisisha

Maana ya Mirathi

- Ni kanuni na taratibu za kugawa mali aliyoiacha mtu aliyekufa kwa ndugu na jamaa wa karibu kinasaba waliohai kwa mujibu wa sheria za Allah (s.w).


Mambo ya Kuzingatia kabla ya Kugawa Mali ya Urithi

a) Haki zilizofungamana na Mali ya Urithi ambazo ni;

i. Madeni

ii. Zakat kama haijatolewa.

iii. Gharama za makazi ya mkewe katika kipindi cha eda au mwaka mzima kama ataamua kubakia.
iv. Usia usiozidi 1/3 ya mali iliyoachwa.



b) Sharti za Kurithi

i. Kufa mwenye kurithiwa.

ii. Kuwepo hai mwenye kurithi wakati anakufa anayerithiwa. iii. Kukosekana mambo yenye kumzuilia mtu kurithi.




c) Mambo yanayomzuilia mtu kurithi

i. Kumuua anayemrithi hata bila ya kukusudia (japo kwa bahati mbaya). ii. Kutofautiana (kuhitilifiana) katika dini kati ya mrithi na mrithiwa.
iii. Mtoto aliyezaliwa nje ya ndoa hatamrithi baba aliyemzaa wala baba hatamrithi huyo mtoto.




d) Sababu za Kurithi

i. Kuwa na nasaba na marehemu anayemrithi.

ii. Kuwa katika ndoa ya halali na marehemu anayemrithi.

iii. Kuacha huru, yaani mwenye kumuacha huru mtumwa wake, ana nafasi ya kumrithi huru wake.




Mgawanyo wa Mirathi kwa Mujibu wa Qur'an (4:11-12), (4:176) ni:

a) Wanaume Wenye kurithi wako 15 kama ifuatayo;

i. Mtoto mwanamume.

ii. Mtoto mwanamume wa mtoto mwanaume (mjukuu). iii. Baba
iv. Babu wa kwa baba.

v. Ndugu mwanaume wa kwa baba na mama. vi. Ndugu mwanaume wa kwa baba tu.
vii. Ndugu mwanaume wa kwa mama tu.

viii. Mtoto mwanaume wa kwa ndugu mwanamume wa kwa baba na mama. ix. Mtoto mwanaume wa ndugu mwanaume wa kwa baba tu.
x. Ami (baba mdogo) wa kwa baba na mama (ndugu yake baba). xi. Ami wa kwa baba tu.
xii. Mtoto mwanaume wa Ami wa kwa baba na mama. xiii. Kijana mwanaume wa Ami wa kwa baba.
xiv. Mume.

xv. Bwana mwenye kumuacha huru mtumwa wake.



b) Wanawake Wenye kurithi wako 10 kama ifuatavyo;

i. Binti (mtoto mwanamke).

ii. Binti wa mtoto mwanaume (mjukuu). iii. Mama.
iv. Dada wa kwa baba na mama. v. Dada wa kwa baba.
vi. Dada wa kwa mama. vii. Bibi mzaa baba.
viii. Bibi mzaa mama. ix. Mke.
x. Bibi mwenye kumuacha huru mtumwa wake.



c) Kuzuiliana

Jumla ya wanaorithi ni 25 (wanaume 15 na wanawake 10), wanakutana wote pamoja, hawawezi kurithi wote ila baadhi yao huwazuilia wengine wasipate fungu au wapate fungu dogo. Hii ni kama ifuatavyo;
i. Mtoto mwanamume hazuiliwi na mtu

ii. Mjukuu huzuiliwa na mtoto mwanaume, na kila mtoto wa kiume aliyekaribu na marehemu humzuilia aliye mbali.
iii. Baba hazuiliwi na mtu

iv. Babu wa upande wowote huzuiliwa na baba au babu wa karibu zaidi.

v. Ndugu wa kwa baba na mama huzuiliwa na mtoto mwanamume au mjukuu au baba.
vi. Ndugu wa kwa baba huzuiliwa na ndugu wa kwa baba na mama; na kila amzuiliye ndugu wa mama, vile vile kila amzuiliaye ndugu wa kwa baba na mama akiwa pamoja na binti au binti wa mtoto wa kiume (mjukuu) au wote wawili.
vii. Ndugu wa kwa mama huzuiliwa na mtoto au mtoto wa mtoto mwanamume au baba au babu.
viii. Mume hazuiliwi na mtu ix. Mke hazuiliwi na mtu
x. Binti hazuiliwi xi. Mama hazuiliwi
xii. Bibi huzuiliwa na mama



d) Mafungu ya Urithi yako 6 ambayo ni;

i. Nusu (1/2). ii. Robo (1/4).
iii. Thuluthi (1/3).
iv. Thuluthi mbili (2/3). v. Sudusi (1/6).
vi. Thumuni (1/8)



e) Wenye Mafungu Maalumu wako 12, kama ifuatavyo;

i. Baba ii. Babu iii. Binti
iv. Binti wa mtoto mwanamume (mjukuu)

v. Ndugu wa kwa mama

vi. Dada wa kwa baba na mama vii. Dada wa kwa baba
viii. Dada wa kwa mama ix. Mama
x. Bibi

xi. Mume xii. Mke



Asaba

- Ni warithi wasiokuwa na mafungu maalum.

- Warithi hawa wanaweza kupata mali yote kama hakuna wa kurithi au kupata kilichobaki baada ya wenye mafungu kupata haki zao.
- Nao wako aina tatu;



a) Asaba kwa nafsi yake

Ni wale wanaume tu ambao uhusiano wao na marehemu haukuingiliwa na mwanamke. Nao ni;
i. Mtoto mwanamume ii. Baba
iii. Babu (baba yake baba)

iv. Ndugu wa kwa baba na mama v. Ndugu wa kwa baba
vi. Mtoto mwanaume wa ndugu wa kwa baba na mama vii. Mtoto mwanaume wa ndugu wa kwa baba
viii. Ami (baba mdogo) wa kwa baba na mama ix. Ami wa kwa baba

x. Mtoto mwanaume wa Ami wa kwa baba na mama xi. Mtoto mwanaume wa Ami wa kwa baba
xii. Bwana na bibi mwenye kumuacha mtumwa wake huru xiii. Asaba wa mwenye kumuacha mtumwa huru.




b) Asaba wa pamoja na mtu mwingine. Nao ni;

i. Binti akiwa pamoja na kijana mwanamume

ii. Binti wa mtoto wa kiume (mjukuu) akiwa pamoja na mtoto mwanaume wa mtoto mwanaume (mjukuu wa kiume).
iii. Dada wa kwa baba na mama akiwa pamoja na ndugu wa kwa baba na mama.
iv. Dada wa kwa baba akiwa pamoja na ndugu wa kwa baba.

v. Dada wa kwa baba na mama au wa kwa baba akiwa pamoja na babu.



c) Asaba kwa sababu ya mtu mwingine nao ni;

i. Dada wa kwa baba na mama au wa kwa baba tu akiwa pamoja na binti au binti wa mtoto wa kiume au wote wawili.


? Musharakah ' kushirikiana fungu katika kurithi

- Ni pale ambapo asaba wana daraja sawa na wenye fungu, hivyo asaba na wenye fungu watashirikiana kugawana fungu hilo.




Kuongeza Mafungu ya kurithi (Awl)

- Iwapo idadi ya mafungu yatakayogawiwa warithi wenye mafungu maalum ni kubwa kuliko mafungu yaliyopatikana kwa njia ya K.D.S, idadi ya mafungu iongezeke ili kila mmoja apate haki yake.



                   



Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Kama unahitaji kuuliza maswali Bofya hapa

Mwandhishi Tarehe 2018-08-01     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 997


Download our Apps
👉1 Madrasa kiganjani     👉2 Kitau cha Fiqh     👉3 kitabu cha Simulizi     👉4 Kitabu cha Afya    

Post zifazofanana:-

Watu wanaowajibikiwa kuhiji
Soma Zaidi...

Swala ya Idi al-fitir na namna ya kuiendea
Soma Zaidi...

UKITAKA KUOMBA BASI MUOMBE ALLAH, UKIMKUMBUKA WAKATI WA RAHA ATAKUKUMBUKA WAKATI WA DHIKI, SHIDA NA TAABU
' ' ' ' ' ' ' ' ': "' ' ' ' ' ' ' ' ' ' ': '... Soma Zaidi...

Hadithi Ya 33: Jukumu La Ushahidi Liko Kwa Yule Anayedai Na Kula Kiapo Kunamuwajibikia Yule Anayekana
Soma Zaidi...

Ni yapi mambo yanayoharibu Swaumu na Mambo yanayobatilisha funga
Soma Zaidi...

JARIBIO LA TATU LA A LADINI
Soma Zaidi...

DARSA ZA TAWHID
Jifunze tawhid yaani kumpwekesha Allah subhaanah wata'aala Soma Zaidi...

IBADA YA HIJA NA NAMNA YA KUITEKELEZA
Soma Zaidi...

'Allah (s.w) humwingiza katika rahma zake amtakaye na kumwacha kupotea amtakaye'
Soma Zaidi...

yaliyomo: HUKUMU YA MIM SAKINA, NUN SAKINA, MADA, WAQFU, QALAQALA, TAFKHIM NA TARQIQ, USOMAJI WA QURAN
DARSA ZA TAJWID YALIYOMOSURA YA 01 . Soma Zaidi...

Hadhi na Haki za Mwanamke katika jamii mbalimbali hapo zamani
Utangulizi:Uislamu unamuelekeza mwanaadamu namna nzuri ya kuendesha maisha yake katika kila kipengele cha maisha akiwa binafsi, katika familia na katika jamii. Soma Zaidi...

HISTORIA YA NABII IBRAHIIM(A.S) NA KUANDALIWA KWAKE:
Nabii Ibrahiim(a. Soma Zaidi...