image

Nadharia ya uchumi kiislamu

1.

Nadharia ya uchumi kiislamu

1.Nadharia ya uchumi wa Kiislamu
Mfumo wa uchumi katika Uislamu ni utaratibu utokanao na Qur-an na Sunnah juu ya uzalishaji, umilikaji, usambazaji, na utumiaji wa mali na huduma pamoja na miiko yake. Kwa msingi huo, uchumi huo umejengwa juu ya fikra ya ukati na kati (Iqtisaad), hivyo umetofautiana na mifumo mingine iliyobuniwa na watu.


Dhana (concept) ya ukati (Iqtisaad) katika shughuli za kiuchumi ni kule kutoa uhuru kwa mtu binafsi (sekta binafsi) kuchuma na kumiliki mali ili iwe motisha kwake ya kuchapa kazi wakati huo huo serikali ikisimamia na kutoa miongozo katika uzalishaji na ugawaji, na vile vile kuwa na sekta zake (sekta za umma) ili kila mwana jamii apate haki za kimsingi. Mifumo iliyobuniwa na watu imeathiriwa na udhaifu wa kibinaadamu wa kuelemea upande huu au ule.



Ipo mifumo ya kiuchumi kama vile ubepari ambao umeelemea mno katika ubinafsi kiasi ambacho umepuuza kabisa haki za kijamii. Katika mfumo huu (ubepari) umma hauna chake; mali, huduma na shughuli mbali mbali hubinafsishwa. Wachache chini ya mfumo huu ndio hunufaika na rasilimali za Taifa. Hujilimbikizia mali, na motisha yao ya uzalishaji ni ile faida waipatayo. Serikali kuu ya mfumo huu wa kibepari hushirikiana na wachache hao waliohodhi mali, kuwanyonya walio wengi.



Pia, kuna mfumo wa uchumi wa Kikomunist au Kijamaa ambao nadharia yake imeelemea mno katika “usawa” wa sare kiasi cha kudhoofisha mno motisha ya watu binafsi na hivyo kupelekea kukosekana kwa ufanisi katika uzalishaji. Katika mfumo huu mali na shughuli mbali mbali hutaifishwa (toka milki ya watu binafsi kuwa milki ya taifa).


Ukweli ni kwamba huwa si mali ya taifa kama inavyotangazwa bali mbiu ya “usawa”, na “mali ya umma”, chini ya mfumo huu, ni mwavuli tu uliokinga kikundi cha watu kilichojipa mamlaka ya uendeshaji wa nchi kwa sura ya chama au serikali kwa maslahi ya kikundi hicho. Kikundi hicho ndicho humiliki na kutafuna mali huku wananchi wengi wakiendelea kudhulumiwa kwa sababu mbali mbali. Hivyo hakuna usawa ulio chini ya mfumo huu bali ni ubinafsi ule ule ambao huhamishwa toka kwa mtu binafsi kwenda kwenye kikundi fulani.




                   






           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 305


Sponsored links
👉1 Kitau cha Fiqh     👉2 kitabu cha Simulizi     👉3 Kitabu cha Afya     👉4 Madrasa kiganjani    

Post zifazofanana:-

Swala ya tarawehe jinsi ya kuiswali
Post hii itakwenda kukufundisha kuhusi swala ya tarawehe, faida zake na jinsi ya kuiswali. Soma Zaidi...

Hukumu ya Talaka kabla ya kufanya jimai
Talaka Kabla ya Jimai:Mwanamume au mwanamke anaweza kughairi na kuamua kuvunja ndoa mapema kabla ya kufanya tendo Ia ndoa. Soma Zaidi...

Yaliyoharamishwa kwa mwenye kuwa katika ihram
Nguzo za uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Namna ya kutambuwa kibla na umuhimu wa kuelekea kibla wakati wa kuswali
4. Soma Zaidi...

Aina za swala..
Nguzo za uislamu,aina za swala (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Mda wa mwisho wa kula daku mwezi wa ramadhani
Post hii fupi itakwenda kukujulisha utaratibu wa kula daku. Soma Zaidi...

Kumkafini (kumvisha sanda maiti)
Mambo ya faradh kwa maiti ya muislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Ijuwe ibada ya zaka na sadaka na namna ya kuitekeleza
Soma Zaidi...

Wanaorithi katika wanaume na wanawake na kiwango wanachorithi
Soma Zaidi...

Aina za talaka, sharti zake na taratibu za kutaliki katika uislamu
Maana: ni utaratibu wa kuvunja mkataba wa ndoa baina ya mume na mke mbele ya mashahidi wawili kwa kuzingatia sheria ya Kiislamu. Soma Zaidi...

Namna ya kuosha maiti hatua kwa hatua
Mambo ya faradh kwa maiti ya muislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Kwa nini imefaradhishwa kufunga katika Mwezi wa ramadhani?
Soma Zaidi...