chimbuko la sheria katika uislamu, hukumu za sheria na kuyatambua yaliyo halali na haramu

chimbuko la sheria katika uislamu, hukumu za sheria na kuyatambua yaliyo halali na haramu

chimbuko la sheria katika uislamu, hukumu za sheria na kuyatambua yaliyo halali na haramu

Chimbuko la Sheria za Kiislamu

i. Allah (s.w) kupitia Kitabu chake - Qur’an (na Vitabu vingine vilivyotangulia)

- Ndiyo chimbuko kuu la sheria za Kiislamu.

Rejea Qur’an (5:45-47), (59:23), (17:105)



ii. Sunnah (Hadith za Mtume (s.a.w))

- Ni msingi wa pili unaotokana na mwenendo wa Mtume (s.a.w) katika kutekeleza maamrisho ya Mwenyezi Mungu (s.w).
Rejea Qur’an (53:2-4), (3:31-32), (33:21) na (59:7).

- Ndiyo chem chem kuu inayofasiri Qur’an kinadharia na kivitendo na ni

katika wahyi (ufunuo) pia.

Rejea Qur’an (53:3-4)



iii. Ijma’a.

- Maana yake ni Maafikiano ya wanachuoni (wanataaluma) wa Kiislamu katika kutoa hukumu juu ya jambo fulani lisilo na hukumu ndani ya Qur’an au Hadith kwa kupitia misingi ya Qur’an au Sunnah (Hadith).


- Ijmaa inakubalika tu isipopingana au kwenda kinyume na aya ya Qur’an

au Hadith za Mtume (s.a.w)

Rejea Qur’an (3:159), (4:59), (42:38)



iv. Qiyaas.

- Maana yake ni kuyapatia hukumu mambo yasiyo na hukumu ya moja kwa moja katika Qur’an na Sunnah kupitia misingi sahihi ya sheria, hukumu na kanuni zilizopo katika Qur’an na Sunnah.




? Halali na haramu katika Sheria ya Kiislamu

Viwango vya halali na haramu ya mambo mbali mbali katika Uislamu viko vitano;

i. Faradh

- Ni mambo yote halali yaliyolazima na wajibu kutekelezwa na watu.

Mfano; swala, zakat, funga, n.k ii. Mustahabu
- Ni mambo ambayo ni halali yaliyohimizwa kutekelezwa katika jamii.

Mfano; siasa, uchumi, utamaduni, n.k iii. Mubaha (permissible)
- Ni jambo ambalo ni halali na ni ruhusa kulifanya ila si wajibu (si lazima).

Mfano; kujenga nyumba nzuri, kuwa na kipando, n.k iv. Makruhu (Detestable)

- Ni jambo ambalo haliharamishwa moja kwa moja lakini lina madhara. v. Haramu
- Ni mambo yote yanayokiuka maamrisho ya Allah (s.w) na Mtume wake

(s.a.w).



Aina za Makosa na Adhabu Zake Katika Sheria ya Kiislamu

a) Makosa ya Hudud

- Ni yale makosa ambayo hukumu na adhabu zake zimetajwa katika Qur’an

au Hadith za Mtume (s.a.w).



- Mfano wa makosa na adhabu (hukumu) hizo ni;

Kuritadi (ridda) - ,hukumu yake ni kuuliwa. Qur’an (9:5).

Uasi (baghi) – ni kupigana kama wamekataa suluhu. Qur’an (49:9)

Wizi – ni kukatwa mkono wa kulia baada ya kutimizwa sharti kadhaa.

Qur’an (5:38)

Zinaa – hukumu yake ni kupigwa fimbo 100 hadharani. Qur’an (24:2) Ulevi – ni kupigwa viboko 80 kwa mujibu wa Hadith za Mtume (s.a.w). Qur’an (5:90)


b) Makosa ya Qisas

- Ni makosa yanayotokana na kudhulumu haki ya mtu.

- Hukumu yake ni kulipiza kisasi kwa kumfanyia kama alivyokufanyia.

Rejea Qur’an (2:178), (5:45)



c) Makosa ya Ta’azir

- Ni makosa ambayo hukumu au adhabu yake haija tajwa moja kwa moja katika Qur’an au Hadith za Mtume (s.a.w).
- Hukumu na adhabu yake hutolewa na Jaji au hakimu kwa idhini ya kiongozi wa Kiislamu kulingana na kosa na mazingira.



Haki za Wasiokuwa Waislamu Katika Dola ya Kiislamu

Sheria ya Kiislamu inawapa haki wasiokuwa waislamu kama ifuatavyo;

i. Haki ya ulinzi wa mali na maisha yao.

- Ni haramu kumwaga damu ya asiyekuwa muislamu bila sababu ya msingi.



ii. Haki katika sheria ya jinai

- Makosa yote ya jinai (penal laws) adhabu zake ni sawa kwa waislamu na wasiokuwa waislamu pia.


iii. Haki katika sheria ya madai (civil laws)

- Hukumu na adhabu za madai ni sawa sawa kwa waislamu na wasiokuwa waislamu.


iv. Haki ya heshima

- Ni kosa na haifai kumvunjia heshima, kumdhulumu, n.k asiyekuwa muislamu kama ilivyo kwa muislamu.


v. Haki katika sheria ya mtu binafsi

- Sheria ya Kiislamu inahukumu mambo yote ya mtu binafsi kulingana na imani ya dini yake.





                   

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Fiqh Main: Dini File: Download PDF Views 2101

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Simulizi za Hadithi Audio    👉2 kitabu cha Simulizi    👉3 Madrasa kiganjani    👉4 Kitau cha Fiqh    👉5 Bongolite - Game zone - Play free game    👉6 Kitabu cha Afya   

Post zinazofanana:

Kuzika-namna ya kuzika hatua kwa hatua

Mambo ya faradh kwa maiti ya muislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Haki za muislamu kwa muislamu mwenziwe

Hizi ndio haki kuu tano unazopasa kumpatia Muislamu mwenzio.

Soma Zaidi...
NI KWA NINI TUNASWALI?, NI UPI UMUHIMU WA KUSWALI NA NI ZIPI FADHILA ZA KUSWALI

Umuhimu wa KusimamishaSwala Kwa mujibu wa Hadith ya Ibn Umar (r.

Soma Zaidi...
Zijuwe sunnha 9 za swala

Post hii inakwenda kukufundisha sunnah 9 za swala. Sunnah hizi ni zile ambazo ukiziwacha swala yako haibatiliki.

Soma Zaidi...
Hadhi na Haki za mwanamke katika jamii za Kirumi hapo zamani

(b) WarumiJamii ya Warumi nayo ni miongoni mwa jamii zinazohesabika kuwa zilianza kustaarabika mapema katika historia ya ulimwengu.

Soma Zaidi...
Hatua za kinga za ugumba na Utasa.

Ugumba ni “ugonjwa wa mfumo wa uzazi unaofafanuliwa kwa kushindwa kupata ujauzito baada ya miezi 12 au zaidi ya kujamiiana bila kinga mara kwa mara. Utasa  kutoweza kwa kiumbe hai kufanya uzazi wa ngono au kutoweza kupata mimba au kuchangia mimba.

Soma Zaidi...
Mtazamo wa uislamu juu ya ndoa ya mke zaidi ya mmoja

Je jamii inachukuliaje swala la kuoa mke zaidi ya mmoja.

Soma Zaidi...
Sharti za kutoa zaka

Masharti ya Utoaji wa Zakat na Swadaqat Utoaji katika njia ya Allah (s.

Soma Zaidi...