Navigation Menu



image

Zijuwe sunnha 9 za swala

Post hii inakwenda kukufundisha sunnah 9 za swala. Sunnah hizi ni zile ambazo ukiziwacha swala yako haibatiliki.

Sunnah za Swala

Vipengele vya sunnah katika swala ni vile ambavyo mwenye kuswali akivitenda husaidia sana kukuza daraja ya swala yake na kuipa nguvu na msukumo mkubwa wa kuiwezesha kufikia lengo lililokusudiwa kwa urahisi zaidi. Ama mwenye kuswali akiacha kipengele chochote katika vipengele vya sunnah, swala yake itakamilika iwapo atatekeleza vipengele vyote vya nguzo. Katika Hadith tumeona kuwa Mtume (s.a.w) katika swala yake pana vipengele vya ziada ya nguzo kama ifuatavyo:


1.Kuinua viganja vya mikono mkabala na mabega, usawa wa vigingi vya masikio wakati wa kuhirimia swala, kwenda kwenye rukuu, baada ya rukuu na baada ya kutoka kwenye Tahiyyatu ya kwanza.
2.Kusoma dua baada ya takbira ya kuhirimia.
3.Kuanza na a ’udhubillaah (kumlaani Shetani) kabla ya kuanza kusoma suratul-Fatiha.
4.Kuitikia “Aamin”baada ya kumaliza Suratul Fatiha.
5.Kusoma aya za Qur-an baada ya Suratul-Fatiha katika rakaa mbili za mwanzo.
6.Kuleta Tasbih, Tahmid na dua katika rukuu, itidali na s ijda.
7.Kutoa takbira katika kubadilisha kitendo kimoja kuendea kingine isipokuwa tu kutoka kwenye rukuu kwenda kwenye itidali ndipo tunaposema: “Sami’Allahu liman hamidah - Rabbanaa lakal-hamdu”.
8.Kukaa na kusoma Tahiyyatu kila baada ya rakaa mbili, kwa swala zenye rakaa zaidi ya mbili.
9.Kusoma dua baada ya kumswalia Mtume na kabla ya kutoa S a la am.






           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu image Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Topic: Fiqh Main: Post File: Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 926


Sponsored links
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉2 Madrasa kiganjani     👉3 Simulizi za Hadithi Audio     👉4 kitabu cha Simulizi     👉5 Kitabu cha Afya     👉6 Kitau cha Fiqh    

Post zifazofanana:-

Nguzo za swala.
Kipengele hiki kinaelezea nguzo mbalimbali za kuswali. Soma Zaidi...

Aina au migawanyo mbalimbali ya haki katika uislamu
Haki na uadilifu katika uislamu (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

kanunu na sheria za biashara katika islamu
Soma Zaidi...

Hoja juu ya hitajio la kuzibiti uzazi na uzazi wa mpango
Soma Zaidi...

Namna ya kuoga josho, kujitwaharisha damu ya Hedhi, damu ya kuzaa Nifasi na Janaba
Soma Zaidi...

Funga za Sunnah na umuhimu wake
Nguzo za uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

sadaka
Soma Zaidi...

Sifa za stara na mavasi katika uislamu
2. Soma Zaidi...

Biashara haramu na njia zake katika uislamu
Soma Zaidi...

lengo la kuswali za faradhi na suna
Soma Zaidi...

Ni nini maana ya twahara na kujitwaharisha?
Posti hii inakwendabkukujiulisha maana ya twahara na jinsi ya kujitwaharisha. Soma Zaidi...

Fadhila za kufunga mwezi wa ramadhani
Soma Zaidi...