Biashara haramu na njia zake katika uislamu

Biashara haramu na njia zake katika uislamu

Njia za Biashara Haramu Katika Uislamu

Miongoni mwa biashara zilizoharamu hata kama zimetokana na bidhaa halali ni;

i. Muzabanah

- Ni kunufaika kibiashara kutokana na matatizo ya watu (muuzaji na mnunuzi).


ii. Mu’awamah

- Ni uuzaji au ununuzi wa matunda au mazao shambani kabla ya kukomaa kwake na kufaa kuliwa.


iii. Hablul-Habalah

- Ni kuuza au kununua kilichoko tumboni mwa mnyama kabla hakijazaliwa.



iv. Kuuza au kununua bidhaa kabla haijafika sokoni.

Ibn Abbas (r.a) ameeleza:

“Katika mauzo aliyoyaharamisha Mtume (s.a.w) ni mauzo ya chakula mpaka

yawe mikononi mwa mnunuzi…” (Bukhari na Muslim)



v. Kuuza au kununua bidhaa iliyouzwa au kununuliwa tayari na mtu mwingine kwa kuongeza bei au namna nyingineyo.


vi. Kuuza maji au majani asili yasiyogharamiwa kwa chochote.

Jaabir (r.a) amesimulia kuwa Mtume wa Allah amekataza kuuza maji ya asili.

(Muslim)


vii. Kuuza au kununua samaki walioko baharini, ndege asiyefugwa (anayeruka angani), maziwa yangali hayajakamuliwa, kiumbe kilicho tumboni mwa mnyama, n.k.

viii. Kuuza au kununua damu, uhuru wa mtu, nywele au maziwa ya binaadamu, n.k.

ix. Kuuza au kununua mbwa, nguruwe, pombe, mizoga, masanamu, picha za watu au wanyama, n.k.

x. Ulanguzi (kuhodhi bidhaa) au kuifanya bidhaa iwe adimu sokoni ili baadae uuze kwa bei yak juu unayotaka.

xi. Kuuza au kununua kwa kupunja au kuharibu vipimo.

“Maangamizo yatawathubutikia wapunjao (wenzao vipimo)……….” (83:1-3)

xii. Kuuza kwa kuficha dosari ya bidhaa, n.k.

xiii. Kuuza au kununua bidhaa kwa wizi, hongo, rushwa, riba, n.k.

Rejea Qur’an (2:276-279)

xiv. Aina zote za kamari kama ramli, kupiga bao, utabiri, n.k.

Rejea Qur’an (5:90-91)

xv. Aina zote za miziki, ngoma, n.k.



Bidhaa Haramu Katika Uislamu

Miongoni mwa bidhaa haramu hata kama biashara yake itafanywa kihalali ni;

i. Pombe za aina zote ii. Mizoga, damu, n.k
iii. Mbwa, nguruwe, paka, n.k

iv. Masanamu, picha za watu au wanyama, n.k v. Bidhaa ya wizi, n.k.





                   

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Fiqh Main: Dini File: Download PDF Views 2347

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    👉2 kitabu cha Simulizi    👉3 Dua za Mitume na Manabii    👉4 Kitabu cha Afya    👉5 Bongolite - Game zone - Play free game    👉6 web hosting   

Post zinazofanana:

Sunnah za udhu

Posti hii inakwenda kukufundisha kuhusu sunah za udhu

Soma Zaidi...
haki ya kutaliki: kuacha na kuachwa katika ndoa ya kiislamu

Haki ya KutalikiKatika jamii nyingi za kjahili haki ya kutoa talaka iko kwa mwanamume tu na mwanamke hana haki yoyote ya kumtaliki mumee.

Soma Zaidi...
Ni ipi hukumu ya kutoa talaka hali ya kuwa umelazimishwa au ukiwa umerukwa na akili

Endapo mtu atamuacha mke pasi na ridhaa yake yaani amelazimishwa ama amemuwacha wakati amerukwa na akili. Je ni ipo hukumu yake.

Soma Zaidi...
Hadhi na Haki za Mwanamke katika jamii mbalimbali hapo zamani

Utangulizi:Uislamu unamuelekeza mwanaadamu namna nzuri ya kuendesha maisha yake katika kila kipengele cha maisha akiwa binafsi, katika familia na katika jamii.

Soma Zaidi...
Ni nini maana ya twahara na kujitwaharisha?

Posti hii inakwendabkukujiulisha maana ya twahara na jinsi ya kujitwaharisha.

Soma Zaidi...
Aina au migawanyo mbalimbali ya haki katika uislamu

Haki na uadilifu katika uislamu (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...