Biashara haramu na njia zake katika uislamu

Biashara haramu na njia zake katika uislamu

Njia za Biashara Haramu Katika Uislamu

Miongoni mwa biashara zilizoharamu hata kama zimetokana na bidhaa halali ni;

i. Muzabanah

- Ni kunufaika kibiashara kutokana na matatizo ya watu (muuzaji na mnunuzi).


ii. Mu’awamah

- Ni uuzaji au ununuzi wa matunda au mazao shambani kabla ya kukomaa kwake na kufaa kuliwa.


iii. Hablul-Habalah

- Ni kuuza au kununua kilichoko tumboni mwa mnyama kabla hakijazaliwa.



iv. Kuuza au kununua bidhaa kabla haijafika sokoni.

Ibn Abbas (r.a) ameeleza:

“Katika mauzo aliyoyaharamisha Mtume (s.a.w) ni mauzo ya chakula mpaka

yawe mikononi mwa mnunuzi…” (Bukhari na Muslim)



v. Kuuza au kununua bidhaa iliyouzwa au kununuliwa tayari na mtu mwingine kwa kuongeza bei au namna nyingineyo.


vi. Kuuza maji au majani asili yasiyogharamiwa kwa chochote.

Jaabir (r.a) amesimulia kuwa Mtume wa Allah amekataza kuuza maji ya asili.

(Muslim)


vii. Kuuza au kununua samaki walioko baharini, ndege asiyefugwa (anayeruka angani), maziwa yangali hayajakamuliwa, kiumbe kilicho tumboni mwa mnyama, n.k.

viii. Kuuza au kununua damu, uhuru wa mtu, nywele au maziwa ya binaadamu, n.k.

ix. Kuuza au kununua mbwa, nguruwe, pombe, mizoga, masanamu, picha za watu au wanyama, n.k.

x. Ulanguzi (kuhodhi bidhaa) au kuifanya bidhaa iwe adimu sokoni ili baadae uuze kwa bei yak juu unayotaka.

xi. Kuuza au kununua kwa kupunja au kuharibu vipimo.

“Maangamizo yatawathubutikia wapunjao (wenzao vipimo)……….” (83:1-3)

xii. Kuuza kwa kuficha dosari ya bidhaa, n.k.

xiii. Kuuza au kununua bidhaa kwa wizi, hongo, rushwa, riba, n.k.

Rejea Qur’an (2:276-279)

xiv. Aina zote za kamari kama ramli, kupiga bao, utabiri, n.k.

Rejea Qur’an (5:90-91)

xv. Aina zote za miziki, ngoma, n.k.



Bidhaa Haramu Katika Uislamu

Miongoni mwa bidhaa haramu hata kama biashara yake itafanywa kihalali ni;

i. Pombe za aina zote ii. Mizoga, damu, n.k
iii. Mbwa, nguruwe, paka, n.k

iv. Masanamu, picha za watu au wanyama, n.k v. Bidhaa ya wizi, n.k.





                   

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Fiqh Main: Dini File: Download PDF Views 1886

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉2 Madrasa kiganjani    👉3 Kitabu cha Afya    👉4 Bongolite - Game zone - Play free game    👉5 Simulizi za Hadithi Audio    👉6 Kitau cha Fiqh   

Post zinazofanana:

Kwanini wengi wanaohijji hawafikii lengo la hijjah zao

Nguzo za uislamu (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Taratibu za kumuona mchumba katika uislamu

Hspa utajifunza taratibu za kuonana na mchumba katika uislamu.

Soma Zaidi...
NI KWA NINI TUNASWALI?, NI UPI UMUHIMU WA KUSWALI NA NI ZIPI FADHILA ZA KUSWALI

Umuhimu wa KusimamishaSwala Kwa mujibu wa Hadith ya Ibn Umar (r.

Soma Zaidi...
Namna ya kutekeleza swala ya maiti hatua kwa hatua

Mambo ya faradh kwa maiti ya muislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Nini maana ya kusimamisha swala?

Je kusimamisha swala kuna maana gani kwenye uislamu?

Soma Zaidi...
Hadathi ya kati na kati

Posti hiibinakwenda kukufundisha kuhusu hadathi ya kati na kati.

Soma Zaidi...
Kutoa kati kwa kati

Nguzo za uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...