picha

Biashara haramu na njia zake katika uislamu

Biashara haramu na njia zake katika uislamu

Njia za Biashara Haramu Katika Uislamu

Miongoni mwa biashara zilizoharamu hata kama zimetokana na bidhaa halali ni;

i. Muzabanah

- Ni kunufaika kibiashara kutokana na matatizo ya watu (muuzaji na mnunuzi).


ii. Mu’awamah

- Ni uuzaji au ununuzi wa matunda au mazao shambani kabla ya kukomaa kwake na kufaa kuliwa.


iii. Hablul-Habalah

- Ni kuuza au kununua kilichoko tumboni mwa mnyama kabla hakijazaliwa.



iv. Kuuza au kununua bidhaa kabla haijafika sokoni.

Ibn Abbas (r.a) ameeleza:

“Katika mauzo aliyoyaharamisha Mtume (s.a.w) ni mauzo ya chakula mpaka

yawe mikononi mwa mnunuzi…” (Bukhari na Muslim)



v. Kuuza au kununua bidhaa iliyouzwa au kununuliwa tayari na mtu mwingine kwa kuongeza bei au namna nyingineyo.


vi. Kuuza maji au majani asili yasiyogharamiwa kwa chochote.

Jaabir (r.a) amesimulia kuwa Mtume wa Allah amekataza kuuza maji ya asili.

(Muslim)


vii. Kuuza au kununua samaki walioko baharini, ndege asiyefugwa (anayeruka angani), maziwa yangali hayajakamuliwa, kiumbe kilicho tumboni mwa mnyama, n.k.

viii. Kuuza au kununua damu, uhuru wa mtu, nywele au maziwa ya binaadamu, n.k.

ix. Kuuza au kununua mbwa, nguruwe, pombe, mizoga, masanamu, picha za watu au wanyama, n.k.

x. Ulanguzi (kuhodhi bidhaa) au kuifanya bidhaa iwe adimu sokoni ili baadae uuze kwa bei yak juu unayotaka.

xi. Kuuza au kununua kwa kupunja au kuharibu vipimo.

“Maangamizo yatawathubutikia wapunjao (wenzao vipimo)……….” (83:1-3)

xii. Kuuza kwa kuficha dosari ya bidhaa, n.k.

xiii. Kuuza au kununua bidhaa kwa wizi, hongo, rushwa, riba, n.k.

Rejea Qur’an (2:276-279)

xiv. Aina zote za kamari kama ramli, kupiga bao, utabiri, n.k.

Rejea Qur’an (5:90-91)

xv. Aina zote za miziki, ngoma, n.k.



Bidhaa Haramu Katika Uislamu

Miongoni mwa bidhaa haramu hata kama biashara yake itafanywa kihalali ni;

i. Pombe za aina zote ii. Mizoga, damu, n.k
iii. Mbwa, nguruwe, paka, n.k

iv. Masanamu, picha za watu au wanyama, n.k v. Bidhaa ya wizi, n.k.





                   

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 2018-08-01 Topic: Fiqh Main: Dini File: Download PDF Views 2667

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 web hosting    👉2 Simulizi za Hadithi Audio    👉3 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉4 Madrasa kiganjani    👉5 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    👉6 kitabu cha Simulizi   

Post zinazofanana:

Waislamu wanaolazimika kufunga

Nguzo za uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Maana ya hadathi na aina zake

Post hii inakwenda kukugundisha maana ya hadathi pamoja na kutaja aina za hadathi

Soma Zaidi...
Jinsi ya kuoga josho la kiislamu ( janaba, hedhi na nifasi)

Post hii inakwenda kukufundisha jinsi ya kuoga josho kisheria.

Soma Zaidi...
Njia za kujitwaharisha, na vitu vinavyotumika kujitwaharisha

Post hii inakwenda kukufundisha njia zinazotumika kujitwaharisha.

Soma Zaidi...
Haki za maadui katika vita (mateka wa kivita)

Haki na uadilifu katika uislamu (EDK form 3: Dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
haki ya kutaliki: kuacha na kuachwa katika ndoa ya kiislamu

Haki ya KutalikiKatika jamii nyingi za kjahili haki ya kutoa talaka iko kwa mwanamume tu na mwanamke hana haki yoyote ya kumtaliki mumee.

Soma Zaidi...
Jinsi ya kutawadha kama aalivyotawadha Mtume Muhammad (s.a.w)

Katika post hii utakwenda kujifunza jinsi ya kutawadha kama vile ambavyo alitawadha Mtume

Soma Zaidi...
Aina mbili za talaka zisizo na rejea katika uislamu

Huwezi kuruhusiwa kumrejea mke endapo utamuacha kwa talaka hizi mbili.

Soma Zaidi...