Hadhi na Haki za mwanamke katika jamii za Kirumi hapo zamani

Hadhi na Haki za mwanamke katika jamii za Kirumi hapo zamani

(b) WarumiJamii ya Warumi nayo ni miongoni mwa jamii zinazohesabika kuwa zilianza kustaarabika mapema katika historia ya ulimwengu.

Jiunge nasi WhatsApp
Upate Update zetu

Hadhi na Haki za mwanamke katika jamii za Kirumi hapo zamani

(b) Warumi
Jamii ya Warumi nayo ni miongoni mwa jamii zinazohesabika kuwa zilianza kustaarabika mapema katika historia ya ulimwengu. Je jamii hii ilimpa mwanamke heshima na hadhi anayostahiki? Katika historia ya Urumi tunajifunza kuwa Warumi walimwona mwanamke kama mtoto anayetakiwa kuangaliwa na kukemewa. Akiolewa yeye na mali yake ni mali ya mume. Akikosea, mume alikuwa na mamlaka ya kupitisha hukumu yoyote.aliyoweza hata ya kutoa adhabu ya kifo.



Mwanamke alikatazwa kushiriki katika jambo lolote. Hakuruhusiwa kutoa ushahidi wala kumuwekea mtu dhamana. Mumewe akifariki, Shemeji zake walikuwa na haki ya kumrithi.



Hapo awali katika historia ya Urumi, wanawake walibakia nyumbani na ukahaba (umalaya) haukujulikana. Mtu kufanya kitendo cha mapenzi na mkewe kama vile kumbusu mkewe hadharani ilionekana ni kitendo kiovu na utovu wa adabu na heshima. Kiongozi mmoja wa Kirumi alishutumiwa vibaya na raia wake kwa kitendo cha kumbusu mkewe mbele ya binti yake.



Warumi waliposongambele katika maendeleo ya kijamii, waliona wamkomboe mwanamke kwa kulegeza sharia ya ndoa kiasi cha kuifanya kama mkataba wa wawili wanaopendana. Wanawake walipewa haki ya kurithi na walikuwa huru na mamlaka ya baba au mume. Katika wakati huu sio tu kuwa wanawake wa Kirumi walijitegemea kiuchumi bali walikuwa wakiwakopesha waume zao kwa nba kubwa kwa kiasi kwamba Wanaume ambao wake zao walikuwa matajiri walijikuta wamekuwa watumwa wao.
Kutaliki kulikuwa jambo jepesi na ndoa zilikatika bila ya sababu za msingi.


Kwa mfano Seneca (4B.C - 65 A.D), Mwanfalsafa Mashuhuri wa Kirumi alitoa shutuma kwa watu wake kutokana na kiwango cha talaka kilicho kithini katika jamii yake kwa kusema: "Now divorce is not regarded as something shameful in Rome. Woman calculate their age by the number of husbands they have taken."



Tafsiri:
"Talaka sasa hainonekani kuwa nijambo la aibu hapa Urumi. Wanawake wanahesabu umri wao kwa idadi ya Wanaume waliofunga nao ndoa."



Yaani, wanawake wa Kirumi katika wakati huo wa historia, kwa uhuru waliopewa na jamii waliweza kuolewa na wanaume wengi kwa muda mfupi. Kwa mfano Martial (43 A.D - 104 A.D) ameeleza juu ya mwanamke aliyeolewa na wanaume kumi. Juvenal (60 A.D - 130 A.D) ameandika juu ya mwanamke aliyeolewa na wanaume wanane, mmoja baada ya mwingine, katika kipindi cha miaka 8. St. Jerome (340 A.D - 420 A.D) ameeleza juu ya mwanamke wa ajabu ambaye mume wake wa mwisho alikuwa wa 23, mmoja baada ya mwingine. Yeye mwenyewe kwa mumewe huyo wa mwisho alikuwa ni mke wake wa 21. ni katika wakati huu uzinifu ulianza kustawi na wazinifu hawakuhesabiwa kuwa ni wakosaji wanaostahiki kuadhibiwa.



Katika historia hii fupi, tunajifunza jisni mwanamke alivyokandamizwa na jamii hapo awali na tumeona hali ya mwanamke ilivyokuwa baada ya kukombolewa. Je, ukombozi huu ulimpa mwanamke hadhi yake anayostahiki?




                   


Download Post hii hapa

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Fiqh Main: Dini File: Download PDF Views 1020

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
๐Ÿ‘‰1 Madrasa kiganjani    ๐Ÿ‘‰2 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    ๐Ÿ‘‰3 Bongolite - Game zone - Play free game    ๐Ÿ‘‰4 Simulizi za Hadithi Audio    ๐Ÿ‘‰5 Kitau cha Fiqh    ๐Ÿ‘‰6 kitabu cha Simulizi   

Post zinazofanana:

Swala ya jamaa.
Swala ya jamaa.

Kipengele hiki tutajifunza kusimamisha swala ya jamaa,swala za ijumaa.

Soma Zaidi...
Madhara ya riba kwenye jamii
Madhara ya riba kwenye jamii

Haya ni madhara ya riba katika jamii. Ni kwa namna gani jamii inadhurika kutokana na riba?

Soma Zaidi...
Jinsi ya kuswali swala vitani
Jinsi ya kuswali swala vitani

Post hii itakufundisha taratibu zinazofanyika ilibkuswalibukiwa vitani.

Soma Zaidi...
Hukumu ya kufinga kwa kifuata kuandama kwa mwezi
Hukumu ya kufinga kwa kifuata kuandama kwa mwezi

Ni muda gani unatakiwa ufunge ramadhani, je kuandama kwa mwezi kwa kiona ama hata kusiki.

Soma Zaidi...
Mwenendo wa Mtu aliyetoa Shahada
Mwenendo wa Mtu aliyetoa Shahada

Muislamu aliyetoa shahada ya kweli hanabudiย kumfanya Mtume (s.

Soma Zaidi...
Kiasi cha mahari kilicho bora kinachofaaa katika uislamu
Kiasi cha mahari kilicho bora kinachofaaa katika uislamu

Uislamu haukuwekabkiwango maalumu cha mahari. Mwanamke anaweza tajabkiasi atakacho. Ila vyema kuzingatia haya wakayi wa kutamka mahari yako.

Soma Zaidi...
Miiko au Mambo yanayoharibu/kubatilisha funga
Miiko au Mambo yanayoharibu/kubatilisha funga

Nguzo za uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Zijuwe sunnha 9 za swala
Zijuwe sunnha 9 za swala

Post hii inakwenda kukufundisha sunnah 9 za swala. Sunnah hizi ni zile ambazo ukiziwacha swala yako haibatiliki.

Soma Zaidi...
Mambo anayofanyiwa mtu anayekaribia kufa
Mambo anayofanyiwa mtu anayekaribia kufa

Haya ni maandalizi anayofanyiwa mtu aliye katika kilevi cha kifo yaani sakaratul maut

Soma Zaidi...