Biashara haramu na njia zake katika uislamu
Njia za Biashara Haramu Katika Uislamu
Miongoni mwa biashara zilizoharamu hata kama zimetokana na bidhaa halali ni;
i. Muzabanah
- Ni kunufaika kibiashara kutokana na matatizo ya watu (muuzaji na mnunuzi).
ii. Mu’awamah
- Ni uuzaji au ununuzi wa matunda au mazao shambani kabla ya kukomaa kwake na kufaa kuliwa.
iii. Hablul-Habalah
- Ni kuuza au kununua kilichoko tumboni mwa mnyama kabla hakijazaliwa.
iv. Kuuza au kununua bidhaa kabla haijafika sokoni.
Ibn Abbas (r.a) ameeleza:
“Katika mauzo aliyoyaharamisha Mtume (s.a.w) ni mauzo ya chakula mpaka
yawe mikononi mwa mnunuzi…” (Bukhari na Muslim)
v. Kuuza au kununua bidhaa iliyouzwa au kununuliwa tayari na mtu mwingine kwa kuongeza bei au namna nyingineyo.
vi. Kuuza maji au majani asili yasiyogharamiwa kwa chochote.
Jaabir (r.a) amesimulia kuwa Mtume wa Allah amekataza kuuza maji ya asili.
(Muslim)
vii. Kuuza au kununua samaki walioko baharini, ndege asiyefugwa (anayeruka angani), maziwa yangali hayajakamuliwa, kiumbe kilicho tumboni mwa mnyama, n.k.
viii. Kuuza au kununua damu, uhuru wa mtu, nywele au maziwa ya binaadamu, n.k.
ix. Kuuza au kununua mbwa, nguruwe, pombe, mizoga, masanamu, picha za watu au wanyama, n.k.
x. Ulanguzi (kuhodhi bidhaa) au kuifanya bidhaa iwe adimu sokoni ili baadae uuze kwa bei yak juu unayotaka.
xi. Kuuza au kununua kwa kupunja au kuharibu vipimo.
“Maangamizo yatawathubutikia wapunjao (wenzao vipimo)……….” (83:1-3)
xii. Kuuza kwa kuficha dosari ya bidhaa, n.k.
xiii. Kuuza au kununua bidhaa kwa wizi, hongo, rushwa, riba, n.k.
Rejea Qur’an (2:276-279)
xiv. Aina zote za kamari kama ramli, kupiga bao, utabiri, n.k.
Rejea Qur’an (5:90-91)
xv. Aina zote za miziki, ngoma, n.k.
Bidhaa Haramu Katika Uislamu
Miongoni mwa bidhaa haramu hata kama biashara yake itafanywa kihalali ni;
i. Pombe za aina zote ii. Mizoga, damu, n.k
iii. Mbwa, nguruwe, paka, n.k
iv. Masanamu, picha za watu au wanyama, n.k v. Bidhaa ya wizi, n.k.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉2 Dua za Mitume na Manabii 👉3 kitabu cha Simulizi 👉4 Bongolite - Game zone - Play free game 👉5 Kitabu cha Afya 👉6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)
Post zinazofanana:
Sura zinazosomwa katika Swala ya Dhuha
Swala ya Dhuha ni swala ya sunna inayosaliwa wakati wa asubuhi baada ya jua kuchomoza na kupanda angalau kiasi cha mkuki (takribani dakika 15 baada ya jua kuchomoza) mpaka kabla ya adhuhuri. Ingawa hakuna sura maalum zilizowekwa kisheria, Mtume ﷺ alisoma baadhi ya sura zenye maana ya kuhimiza kheri na shukrani.
Soma Zaidi...Utaijuwaje kama swala yako imekubalika
Hapa tunakwenda kuona jinsi ya kuzitathmini swala zetu.
Soma Zaidi...Jinsi ambavyo mtu anazuiliwa kurithi mali ya marehemu
Endapo mtu yupp katika orodha ya wanaotakiwa kutithi, anaweza kuzuiliwa kurithi kwa kuzingatia haya.
Soma Zaidi...