Njia za Biashara Haramu Katika Uislamu
Miongoni mwa biashara zilizoharamu hata kama zimetokana na bidhaa halali ni;
i. Muzabanah
- Ni kunufaika kibiashara kutokana na matatizo ya watu (muuzaji na mnunuzi).
ii. Mu’awamah
- Ni uuzaji au ununuzi wa matunda au mazao shambani kabla ya kukomaa kwake na kufaa kuliwa.
iii. Hablul-Habalah
- Ni kuuza au kununua kilichoko tumboni mwa mnyama kabla hakijazaliwa.
iv. Kuuza au kununua bidhaa kabla haijafika sokoni.
Ibn Abbas (r.a) ameeleza:
“Katika mauzo aliyoyaharamisha Mtume (s.a.w) ni mauzo ya chakula mpaka
yawe mikononi mwa mnunuzi…” (Bukhari na Muslim)
v. Kuuza au kununua bidhaa iliyouzwa au kununuliwa tayari na mtu mwingine kwa kuongeza bei au namna nyingineyo.
vi. Kuuza maji au majani asili yasiyogharamiwa kwa chochote.
Jaabir (r.a) amesimulia kuwa Mtume wa Allah amekataza kuuza maji ya asili.
(Muslim)
vii. Kuuza au kununua samaki walioko baharini, ndege asiyefugwa (anayeruka angani), maziwa yangali hayajakamuliwa, kiumbe kilicho tumboni mwa mnyama, n.k.
viii. Kuuza au kununua damu, uhuru wa mtu, nywele au maziwa ya binaadamu, n.k.
ix. Kuuza au kununua mbwa, nguruwe, pombe, mizoga, masanamu, picha za watu au wanyama, n.k.
x. Ulanguzi (kuhodhi bidhaa) au kuifanya bidhaa iwe adimu sokoni ili baadae uuze kwa bei yak juu unayotaka.
xi. Kuuza au kununua kwa kupunja au kuharibu vipimo.
“Maangamizo yatawathubutikia wapunjao (wenzao vipimo)……….” (83:1-3)
xii. Kuuza kwa kuficha dosari ya bidhaa, n.k.
xiii. Kuuza au kununua bidhaa kwa wizi, hongo, rushwa, riba, n.k.
Rejea Qur’an (2:276-279)
xiv. Aina zote za kamari kama ramli, kupiga bao, utabiri, n.k.
Rejea Qur’an (5:90-91)
xv. Aina zote za miziki, ngoma, n.k.
Bidhaa Haramu Katika Uislamu
Miongoni mwa bidhaa haramu hata kama biashara yake itafanywa kihalali ni;
i. Pombe za aina zote ii. Mizoga, damu, n.k
iii. Mbwa, nguruwe, paka, n.k
iv. Masanamu, picha za watu au wanyama, n.k v. Bidhaa ya wizi, n.k.
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.
Download NowUmeionaje Makala hii.. ?
(ii) Hatua za Kuzuia Uzinzi JamiiUislamu pamoja na kutoa mafunzo ya maadii yanayomuwezesha mtu binafsi ajiepushe kwa hiari yake na kitendo kibaya cha zinaa, umechukua hatua mbali mbali ambazo huifanya zinaa isiwe kitendo chepesi katika jamii.
Soma Zaidi...Hapa utajifunza jinsi ya kuozesha hatuwa kwa hatuwa. Pia utajifunza masharti ya kuoa na masharti ya kuolewa.
Soma Zaidi...Je unaijuwa mipaka yako katika kumiliki mali. Ama unajuwa haki zako katika mali inayomiliki. Endelea na somo
Soma Zaidi...Amesema mtume (s.a.w) kuwa Allah (s.w) amesema: kila amali ya mwanaadamu ni kwa ajili yake isipokuwa funga.
Soma Zaidi...Post hii itakwenda kukufundisha kuhusi swala ya tarawehe, faida zake na jinsi ya kuiswali.
Soma Zaidi...Serikali ina nafasi katika kufanya mgawanyiko katika uchumi.
Soma Zaidi...