Biashara haramu na njia zake katika uislamu

Biashara haramu na njia zake katika uislamu

Biashara haramu na njia zake katika uislamu

Njia za Biashara Haramu Katika Uislamu

Miongoni mwa biashara zilizoharamu hata kama zimetokana na bidhaa halali ni;

i. Muzabanah

- Ni kunufaika kibiashara kutokana na matatizo ya watu (muuzaji na mnunuzi).


ii. Mu’awamah

- Ni uuzaji au ununuzi wa matunda au mazao shambani kabla ya kukomaa kwake na kufaa kuliwa.


iii. Hablul-Habalah

- Ni kuuza au kununua kilichoko tumboni mwa mnyama kabla hakijazaliwa.



iv. Kuuza au kununua bidhaa kabla haijafika sokoni.

Ibn Abbas (r.a) ameeleza:

“Katika mauzo aliyoyaharamisha Mtume (s.a.w) ni mauzo ya chakula mpaka

yawe mikononi mwa mnunuzi…” (Bukhari na Muslim)



v. Kuuza au kununua bidhaa iliyouzwa au kununuliwa tayari na mtu mwingine kwa kuongeza bei au namna nyingineyo.


vi. Kuuza maji au majani asili yasiyogharamiwa kwa chochote.

Jaabir (r.a) amesimulia kuwa Mtume wa Allah amekataza kuuza maji ya asili.

(Muslim)


vii. Kuuza au kununua samaki walioko baharini, ndege asiyefugwa (anayeruka angani), maziwa yangali hayajakamuliwa, kiumbe kilicho tumboni mwa mnyama, n.k.

viii. Kuuza au kununua damu, uhuru wa mtu, nywele au maziwa ya binaadamu, n.k.

ix. Kuuza au kununua mbwa, nguruwe, pombe, mizoga, masanamu, picha za watu au wanyama, n.k.

x. Ulanguzi (kuhodhi bidhaa) au kuifanya bidhaa iwe adimu sokoni ili baadae uuze kwa bei yak juu unayotaka.

xi. Kuuza au kununua kwa kupunja au kuharibu vipimo.

“Maangamizo yatawathubutikia wapunjao (wenzao vipimo)……….” (83:1-3)

xii. Kuuza kwa kuficha dosari ya bidhaa, n.k.

xiii. Kuuza au kununua bidhaa kwa wizi, hongo, rushwa, riba, n.k.

Rejea Qur’an (2:276-279)

xiv. Aina zote za kamari kama ramli, kupiga bao, utabiri, n.k.

Rejea Qur’an (5:90-91)

xv. Aina zote za miziki, ngoma, n.k.



Bidhaa Haramu Katika Uislamu

Miongoni mwa bidhaa haramu hata kama biashara yake itafanywa kihalali ni;

i. Pombe za aina zote ii. Mizoga, damu, n.k
iii. Mbwa, nguruwe, paka, n.k

iv. Masanamu, picha za watu au wanyama, n.k v. Bidhaa ya wizi, n.k.





                   

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu Rajabu
Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Fiqh Main: Post File: Download PDF
Views: 3479

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 kitabu cha Simulizi     👉2 Kitabu cha Afya     👉3 Simulizi za Hadithi Audio     👉4 Dua za Mitume na Manabii     👉5 Bongolite - Game zone - Play free game     👉6 ai web app    

Post zinazofanana:

Sera ya uchumi katika uislamu

Hapa utajifunza sera za kiuchumi katika uchumi wa kiislamu. Hapa utajifunza sera kuu tatu za uchumi wa kiislamu.

Soma Zaidi...
Tofauti kati ya hijjah na umrah

Nguzo za uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Utaratibu wa kuzika maiti ya kiislamu, hatua kwa hatua

Kuzika Kuzika ni kitendo cha nne cha faradh tunacho lazimika kumfanyia ndugu yetu aliyetutangulia kufa.

Soma Zaidi...
NI ZIPI SWALA ZA SUNNAH: (qabliya (kabliya) na baadiya, tahajudi, tarawehe, qiyamu layl, shukr, istikhara)

Sunnah za SwalaSunnah za Swala Vipengele vya sunnah katika swala ni vile ambavyo mwenye kuswali akivitenda husaidia sana kukuza daraja ya swala yake na kuipa nguvu na msukumo mkubwa wa kuiwezesha kufikia lengo lililokusudiwa kwa urahisi zaidi.

Soma Zaidi...