Haki za muislamu kwa muislamu mwenziwe

Hizi ndio haki kuu tano unazopasa kumpatia Muislamu mwenzio.

HAKI 5 ZA MUISLAMU ANAZOPASA KUPEWA: 

 
وعن أبي هريرة رضي الله عنه أن رسول الله صلى الله عليه وسلم قال‏:‏ ‏"‏حق المسلم علي المسلم خمس‏:‏ رد السلام، وعيادة المريض، واتباع الجنائز، وإجابة الدعوة، وتشميت العاطس” ‏(‏‏(‏متفق عليه‏)‏‏)
 
 
 
Imesimuliwa kutoka kwa Abu Hurairah kuwa Mtume s.a.w amesema : "Haki za muislamu kwa muislamu mwenziwe ni tano: kurudisha salamu, kumuangalia anapoumwa, kuifuata jeneza lake, kuitikia wito anapokuita, na kumuombea dua anapopiga chafya". 
 
 
Maelezo
Kwa mujibu wa hadithi haki hizo ni; -
1. Kujibu salamu ya Muislamu anapokusalimia. Hii inamaana kujibu salamu ni jambo la lazima. Endapo hutajibu salamu baada ya kusalimiana utakuwa umevunja haki hivyo utaingia kwenye makosa. 
 
 
2. Kwenda kumangalia anapoumwa. Nibsunnah kumuombea dua mgonjwa. Unapomuangalia mgonjwa unafaidika wewe na yeye kiroho na kiafya pia. 
 
 
3. Endapo atafariki ni haki yake kumsindikiza kwa kilifuata jeneza lake hadi kwenda kumzika. Hii inaambatana na kumswalia. Hata hivyo sio lazima kwako endapo wapo walioshiriki kumswalia. Hata hivyo kama huna uhuru ni haki yake umshindikize mpaka atakapozikwa. 
 
4. Endapo muislamu mwenzio atakuita ni haki yake kuitikie wito huo. Nenda kwanza kasikilize anakuitia nini,  kisha kukubali na kukataa hupatikana baada ya kujuwa wito ulikuwa na sababu gani. 
 
Hata hivyo haki hii inatakiwa ifanyike kwenye misingi ya sheria. Sio sawa kumuita mwanamke katika mazingiravtatnishi.  Ama hata mwanaume kumuita mwanaume kwenye mazingira hatari. Hivyo kwa kuangalia usalama wako pia haki hii inapaswa kutekelezwa katika misingi salama. 
 
 
5. Kumuombea dua anapopiga chafya. Endapo atapiga chafya na akasema alhamdu lillah wewe unatakiwa umwambie yarhamuka llahu. Kisha yeye anatakiwa ajibu yahdikumullahu wayuswlih baalakum. 
 
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Fiqh Main: Dini File: Download PDF Views 1406

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉2 Kitau cha Fiqh    👉3 Simulizi za Hadithi Audio    👉4 kitabu cha Simulizi    👉5 Kitabu cha Afya    👉6 Madrasa kiganjani   

Post zinazofanana:

Miiko au Mambo yanayoharibu/kubatilisha funga

Nguzo za uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Jinsi ya kusherehekea siku ya idi katika uislamu

Uislamu umeweka taratibu maalumu za kuzifata katika kusherehekea siku ya idi.

Soma Zaidi...
Swala ya idil fitir na idil haji nanjinsi ya kuziswali

Hapa utajifunza jinsi ya kuswali swala ya idil haji na swala ya idil fitir

Soma Zaidi...
Mambo ya kuzingatia kabla ya kugawa mirathi

Haya ni mamno muhimu yanayozingatiwa kabla ya kuanza zoezi la kugawa mirathi ya marehemu.

Soma Zaidi...
Mambo yaliyo haramu kwa mwenye hedhi na nifasi

Katika post hii utakwenda kujifunza mambo ambayo ni haramu kwa mwanamke aliye na hedhi na nifasi

Soma Zaidi...
Namna ya kuosha maiti hatua kwa hatua

Mambo ya faradh kwa maiti ya muislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Nini maana ya funga na ni lipi lengo lake

Post hii inakwenda kukufundisha kuhusu lengo la funga na maana yake katika uislamu.

Soma Zaidi...
Wenye ruhusa za kutofunga ramadhan

Nguzo za uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...