Haki za muislamu kwa muislamu mwenziwe
Hizi ndio haki kuu tano unazopasa kumpatia Muislamu mwenzio.
HAKI 5 ZA MUISLAMU ANAZOPASA KUPEWA:
وعن أبي هريرة رضي الله عنه أن رسول الله صلى الله عليه وسلم قال: "حق المسلم علي المسلم خمس: رد السلام، وعيادة المريض، واتباع الجنائز، وإجابة الدعوة، وتشميت العاطس” ((متفق عليه))
Imesimuliwa kutoka kwa Abu Hurairah kuwa Mtume s.a.w amesema : "Haki za muislamu kwa muislamu mwenziwe ni tano: kurudisha salamu, kumuangalia anapoumwa, kuifuata jeneza lake, kuitikia wito anapokuita, na kumuombea dua anapopiga chafya".
Maelezo
Kwa mujibu wa hadithi haki hizo ni; -
1. Kujibu salamu ya Muislamu anapokusalimia. Hii inamaana kujibu salamu ni jambo la lazima. Endapo hutajibu salamu baada ya kusalimiana utakuwa umevunja haki hivyo utaingia kwenye makosa.
2. Kwenda kumangalia anapoumwa. Nibsunnah kumuombea dua mgonjwa. Unapomuangalia mgonjwa unafaidika wewe na yeye kiroho na kiafya pia.
3. Endapo atafariki ni haki yake kumsindikiza kwa kilifuata jeneza lake hadi kwenda kumzika. Hii inaambatana na kumswalia. Hata hivyo sio lazima kwako endapo wapo walioshiriki kumswalia. Hata hivyo kama huna uhuru ni haki yake umshindikize mpaka atakapozikwa.
4. Endapo muislamu mwenzio atakuita ni haki yake kuitikie wito huo. Nenda kwanza kasikilize anakuitia nini, kisha kukubali na kukataa hupatikana baada ya kujuwa wito ulikuwa na sababu gani.
Hata hivyo haki hii inatakiwa ifanyike kwenye misingi ya sheria. Sio sawa kumuita mwanamke katika mazingiravtatnishi. Ama hata mwanaume kumuita mwanaume kwenye mazingira hatari. Hivyo kwa kuangalia usalama wako pia haki hii inapaswa kutekelezwa katika misingi salama.
5. Kumuombea dua anapopiga chafya. Endapo atapiga chafya na akasema alhamdu lillah wewe unatakiwa umwambie yarhamuka llahu. Kisha yeye anatakiwa ajibu yahdikumullahu wayuswlih baalakum.
Download App Yetu
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.
Download Now
Nyuma
Endelea
Umeionaje Makala hii.. ?
Nzuri Mbaya Save
Author:
Rajabu 
Tarehe:
1970-01-01 03:33:44
Topic:
Fiqh
Main:
Dini
File:
Download PDF
Views
1218
Post zinazofanana:
Nguzo za uislamu, masharti ya utoaji wa zakat na sadaqat
(EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)
Soma Zaidi...
Endapo mke na mume wameachana na hali ya kuwa mke ana watoto wachanga. Je uislamu unasemaje kuhusu taratibu za malezi?
Soma Zaidi...
Nguzo za uislamu (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu)
Soma Zaidi...
Hapabutajifunza endapp mwanamke anahitaji kuachwa ni nini anatakiwa afanye.
Soma Zaidi...
Hspa utajifunza sasa jinsi ya kugawa mirathi kutokana na viwango maalumu.
Soma Zaidi...
Ni ipi raslimali ya halali kuimiliki katika uislamu.
Soma Zaidi...
Post hii inakwenda kukufundisha kuhusu swala ya Istikhara
Soma Zaidi...