Menu



Haki za muislamu kwa muislamu mwenziwe

Hizi ndio haki kuu tano unazopasa kumpatia Muislamu mwenzio.

HAKI 5 ZA MUISLAMU ANAZOPASA KUPEWA: 

 
وعن أبي هريرة رضي الله عنه أن رسول الله صلى الله عليه وسلم قال‏:‏ ‏"‏حق المسلم علي المسلم خمس‏:‏ رد السلام، وعيادة المريض، واتباع الجنائز، وإجابة الدعوة، وتشميت العاطس” ‏(‏‏(‏متفق عليه‏)‏‏)
 
 
 
Imesimuliwa kutoka kwa Abu Hurairah kuwa Mtume s.a.w amesema : "Haki za muislamu kwa muislamu mwenziwe ni tano: kurudisha salamu, kumuangalia anapoumwa, kuifuata jeneza lake, kuitikia wito anapokuita, na kumuombea dua anapopiga chafya". 
 
 
Maelezo
Kwa mujibu wa hadithi haki hizo ni; -
1. Kujibu salamu ya Muislamu anapokusalimia. Hii inamaana kujibu salamu ni jambo la lazima. Endapo hutajibu salamu baada ya kusalimiana utakuwa umevunja haki hivyo utaingia kwenye makosa. 
 
 
2. Kwenda kumangalia anapoumwa. Nibsunnah kumuombea dua mgonjwa. Unapomuangalia mgonjwa unafaidika wewe na yeye kiroho na kiafya pia. 
 
 
3. Endapo atafariki ni haki yake kumsindikiza kwa kilifuata jeneza lake hadi kwenda kumzika. Hii inaambatana na kumswalia. Hata hivyo sio lazima kwako endapo wapo walioshiriki kumswalia. Hata hivyo kama huna uhuru ni haki yake umshindikize mpaka atakapozikwa. 
 
4. Endapo muislamu mwenzio atakuita ni haki yake kuitikie wito huo. Nenda kwanza kasikilize anakuitia nini,  kisha kukubali na kukataa hupatikana baada ya kujuwa wito ulikuwa na sababu gani. 
 
Hata hivyo haki hii inatakiwa ifanyike kwenye misingi ya sheria. Sio sawa kumuita mwanamke katika mazingiravtatnishi.  Ama hata mwanaume kumuita mwanaume kwenye mazingira hatari. Hivyo kwa kuangalia usalama wako pia haki hii inapaswa kutekelezwa katika misingi salama. 
 
 
5. Kumuombea dua anapopiga chafya. Endapo atapiga chafya na akasema alhamdu lillah wewe unatakiwa umwambie yarhamuka llahu. Kisha yeye anatakiwa ajibu yahdikumullahu wayuswlih baalakum. 
 

Download app yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiw ana App yetu. Bofya liln hapo chini kuweza ku download

Download Now Bongoclass

           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu image Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Topic: Fiqh Main: Post File: Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Views 1105


Sponsored links
👉1 Simulizi za Hadithi Audio     👉2 Kitabu cha Afya     👉3 kitabu cha Simulizi     👉4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉5 Madrasa kiganjani     👉6 Kitau cha Fiqh    

Post zifazofanana:-

Ni ipi hukumu ya muislamu anayekula mwezi wa Ramadhani bila ya sababu ya kisheria
Endapo muislamu hatafunga mwezi wa Ramadhani bila ya ruhusa je atatakiwa afanye nini. Je ataweza kuilipa funga hiyo? Soma Zaidi...

Misingi na Maadili Katika Uislamu
5. Soma Zaidi...

haki na wajibu katika jamii
Soma Zaidi...

Mtazamo wa uislamu juu ya ndoa ya mke zaidi ya mmoja
Je jamii inachukuliaje swala la kuoa mke zaidi ya mmoja. Soma Zaidi...

Lengo la funga linavyofikiwa
Nguzo za uislamu (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

hukumu na taratibu za biashara ya ushirika na hisa katika uislamu
Soma Zaidi...

darasa la funga
Soma Zaidi...

Utaratibu wa kuzika maiti ya kiislamu, hatua kwa hatua
Kuzika Kuzika ni kitendo cha nne cha faradh tunacho lazimika kumfanyia ndugu yetu aliyetutangulia kufa. Soma Zaidi...

Hadathi ya kati na kati
Posti hiibinakwenda kukufundisha kuhusu hadathi ya kati na kati. Soma Zaidi...

Nafasi ya serikali katika ugawaji
Serikali ina nafasi katika kufanya mgawanyiko katika uchumi. Soma Zaidi...