Twahara na umuhimu wake katika uislamu

Twahara na umuhimu wake katika uislamu

Katika post hii utajifunza maana ya twahara kiligha na kishria. Pia utajifunza umuhimu wake

Jiunge nasi WhatsApp
Upate Update zetu

TWAHARA NA UMUHIMU WAKE

 

Maana Ya Twahara Katika Lugha Ya Kawaida:

 

Ni usafi na kuondosha uchafu au takataka za kihisia (kugusika) kama najsi ya mkojo au kinginecho, na za kidhahania kama kasoro (mapungufu) na maasi.

 

Kutwaharisha ni kusafisha, nako ni kupaweka mahala maalumu katika hali ya usafi. [Al-Libaab Sharhul Kitaab (1/10) na Ad-Durru Al-Mukhtaar (1/79)].

 

Ama kisharia (kitaaluma):

 

Ni kuondosha kinachozuia kuswali kama hadathi au najsi kwa kutumia maji (au kinginecho), au kuondosha hukmu yake kwa mchanga. [Al-Mughniy cha Ibn Qudaamah (1/12)].

 

 

Hukmu ya twahara:

 

Kutwaharisha najsi na kuiondosha ni jambo la wajibu ikiwa mtu atakumbuka na ataweza. Allaah (Subhaanahu wa Ta'aala) Anasema:

((وَثِيَابَكَ فَطَهِّر))

((Na nguo zako zitwaharishe)) [Al-Muddath-thir (74:4)]

 

Na Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'aala):

((أَن طَهِّرَا بَيْتِيَ لِلطَّائِفِينَ وَالْعَاكِفِينَ وَالرُّكَّعِ السُّجُودِ))

((Ya kwamba itakaseni Nyumba Yangu kwa ajili ya wanaoizunguka kwa kutufu na wanaojitenga humo kwa ‘ibaadah, na wanaoinama na kusujudu)). [Al Baqarah (2:125)]

 

Ama kujitwaharisha na hadathi, hilo ni lazima ili ruhusa ya kuswali ipatikane kwa neno lake Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam):

(( لَا تُقْبَلُ صَلَاةُ بغير طهور))

 

((Swalaah haikubaliwi bila ya wudhuu). [Swahiyh Muslim 224]

 

 

Umuhimu Wake:

 

 

1- Twahara ni sharti ya kusihi kwa sala ya mja. Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema:

((لَا تُقْبَلُ صَلَاةُ مَنْ أَحْدَثَ حَتَّى يَتَوَضَّأَ ))

((Haikubaliwi Swalaah ya mtu mwenye hadathi mpaka atawadhe)). [Imepasishwa na Al Bukhaariy (135), Muslim (225].

 

Kuswali na twahara ni kumtukuza Allaah. Na hadathi na janaba – ingawa si najsi zenye kuonekana – lakini hata hivyo ni najsi za kidhahania zenye kukifanya kilichoingiwa navyo kuonekana kichafu. Hivyo basi, kuwepo kwake huteteresha utukuzo kwa Allaah, na huenda kinyume na msingi wa usafi.

 

 

2- Allaah (Subhaanahu wa Ta'aala) Amewasifu wenye kujitwaharisha. Anasema:

 

((إِنَّ اللّهَ يُحِبُّ التَّوَّابِينَ وَيُحِبُّ الْمُتَطَهِّرِينَ))

((Hakika Allaah Anawapenda wenye kutubia mara kwa mara na Anawapenda wenye kujitwaharisha)). [Al Baqarah 2:222]

 

Akawasifu watu wa Masjid Qubaa kwa Neno Lake:

 

((فِيهِ رِجَالٌ يُحِبُّونَ أَن يَتَطَهَّرُواْ وَاللّهُ يُحِبُّ الْمُطَّهِّرِينَ))

((Ndani yake kuna watu wanaopenda kujitwaharisha, na Allaah Anawapenda wenye kujitwaharisha)). [At Tawbah 9:108]

 

 

3- Kutojali au kutotilia maanani kujitakasa na najsi, ni moja kati ya sababu za kuadhibiwa watu makaburini. Imepokelewa na Ibn 'Abbaas akisema: Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alipita kwenye makaburi mawili akasema:

 

(( إِنَّهُمَا لَيُعَذَّبَانِ وَمَا يُعَذَّبَانِ فِي كَبِيرٍ، أَمَّا هذا فَكَانَ لَا يَسْتَنزه مِنْ بَوْلِهِ، ))

((Kwa hakika wawili (hawa) wanaadhibiwa, na hawaadhibiwi kwa jambo kubwa. (la kuwashinda kutekeleza au kujiepusha nalo). Ama huyu, alikuwa hajitakasi na mkojo wake)). [Abu Daawuud (20), An Nasaaiy (31-69), na Ibn Maajah (347) kwa Sanad Swahiyh].

 

Download Post hii hapa

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Fiqh Main: Dini File: Download PDF Views 1673

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Madrasa kiganjani    👉2 Bongolite - Game zone - Play free game    👉3 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉4 kitabu cha Simulizi    👉5 Simulizi za Hadithi Audio    👉6 Kitabu cha Afya   

Post zinazofanana:

Miiko au Mambo yanayoharibu/kubatilisha funga
Miiko au Mambo yanayoharibu/kubatilisha funga

Nguzo za uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Mtazamo wa uislamu juu ya ndoa ya mke zaidi ya mmoja
Mtazamo wa uislamu juu ya ndoa ya mke zaidi ya mmoja

Je jamii inachukuliaje swala la kuoa mke zaidi ya mmoja.

Soma Zaidi...
Je ni kwa nini lengo la finga halifikiwi kwa wafungaji
Je ni kwa nini lengo la finga halifikiwi kwa wafungaji

Lengo la funga ni kuwa mchamungu sasa ni kwa nini wafungaji hawalifikii lengo hili na kuwa wachamungu.

Soma Zaidi...
 Je kama maiti imekatika baadhi ya viungo je viungo vyake tunafata utaratibu gani katika kumuosha na kumkafini?
Je kama maiti imekatika baadhi ya viungo je viungo vyake tunafata utaratibu gani katika kumuosha na kumkafini?

Assalamu Alaykum Warahmatu-llah Wabarakaatuh Naomba kuuliza: Je kama maiti imekatika baadhi ya viungo je viungo vyake tunafata utaratibu gani katika kumuosha na kumkafini?

Soma Zaidi...
Haki za viumbe na mazingira
Haki za viumbe na mazingira

Haki na uadilifu katika uislamu (EDK form 3: Dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Hijja na umrah
Hijja na umrah

Nguzo za uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Kwanini wengi wanaohijji hawafikii lengo la hijjah zao
Kwanini wengi wanaohijji hawafikii lengo la hijjah zao

Nguzo za uislamu (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...