picha

chimbuko la sheria katika uislamu, hukumu za sheria na kuyatambua yaliyo halali na haramu

chimbuko la sheria katika uislamu, hukumu za sheria na kuyatambua yaliyo halali na haramu

chimbuko la sheria katika uislamu, hukumu za sheria na kuyatambua yaliyo halali na haramu

Chimbuko la Sheria za Kiislamu

i. Allah (s.w) kupitia Kitabu chake - Qur’an (na Vitabu vingine vilivyotangulia)

- Ndiyo chimbuko kuu la sheria za Kiislamu.

Rejea Qur’an (5:45-47), (59:23), (17:105)



ii. Sunnah (Hadith za Mtume (s.a.w))

- Ni msingi wa pili unaotokana na mwenendo wa Mtume (s.a.w) katika kutekeleza maamrisho ya Mwenyezi Mungu (s.w).
Rejea Qur’an (53:2-4), (3:31-32), (33:21) na (59:7).

- Ndiyo chem chem kuu inayofasiri Qur’an kinadharia na kivitendo na ni

katika wahyi (ufunuo) pia.

Rejea Qur’an (53:3-4)



iii. Ijma’a.

- Maana yake ni Maafikiano ya wanachuoni (wanataaluma) wa Kiislamu katika kutoa hukumu juu ya jambo fulani lisilo na hukumu ndani ya Qur’an au Hadith kwa kupitia misingi ya Qur’an au Sunnah (Hadith).


- Ijmaa inakubalika tu isipopingana au kwenda kinyume na aya ya Qur’an

au Hadith za Mtume (s.a.w)

Rejea Qur’an (3:159), (4:59), (42:38)



iv. Qiyaas.

- Maana yake ni kuyapatia hukumu mambo yasiyo na hukumu ya moja kwa moja katika Qur’an na Sunnah kupitia misingi sahihi ya sheria, hukumu na kanuni zilizopo katika Qur’an na Sunnah.




? Halali na haramu katika Sheria ya Kiislamu

Viwango vya halali na haramu ya mambo mbali mbali katika Uislamu viko vitano;

i. Faradh

- Ni mambo yote halali yaliyolazima na wajibu kutekelezwa na watu.

Mfano; swala, zakat, funga, n.k ii. Mustahabu
- Ni mambo ambayo ni halali yaliyohimizwa kutekelezwa katika jamii.

Mfano; siasa, uchumi, utamaduni, n.k iii. Mubaha (permissible)
- Ni jambo ambalo ni halali na ni ruhusa kulifanya ila si wajibu (si lazima).

Mfano; kujenga nyumba nzuri, kuwa na kipando, n.k iv. Makruhu (Detestable)

- Ni jambo ambalo haliharamishwa moja kwa moja lakini lina madhara. v. Haramu
- Ni mambo yote yanayokiuka maamrisho ya Allah (s.w) na Mtume wake

(s.a.w).



Aina za Makosa na Adhabu Zake Katika Sheria ya Kiislamu

a) Makosa ya Hudud

- Ni yale makosa ambayo hukumu na adhabu zake zimetajwa katika Qur’an

au Hadith za Mtume (s.a.w).



- Mfano wa makosa na adhabu (hukumu) hizo ni;

Kuritadi (ridda) - ,hukumu yake ni kuuliwa. Qur’an (9:5).

Uasi (baghi) – ni kupigana kama wamekataa suluhu. Qur’an (49:9)

Wizi – ni kukatwa mkono wa kulia baada ya kutimizwa sharti kadhaa.

Qur’an (5:38)

Zinaa – hukumu yake ni kupigwa fimbo 100 hadharani. Qur’an (24:2) Ulevi – ni kupigwa viboko 80 kwa mujibu wa Hadith za Mtume (s.a.w). Qur’an (5:90)


b) Makosa ya Qisas

- Ni makosa yanayotokana na kudhulumu haki ya mtu.

- Hukumu yake ni kulipiza kisasi kwa kumfanyia kama alivyokufanyia.

Rejea Qur’an (2:178), (5:45)



c) Makosa ya Ta’azir

- Ni makosa ambayo hukumu au adhabu yake haija tajwa moja kwa moja katika Qur’an au Hadith za Mtume (s.a.w).
- Hukumu na adhabu yake hutolewa na Jaji au hakimu kwa idhini ya kiongozi wa Kiislamu kulingana na kosa na mazingira.



Haki za Wasiokuwa Waislamu Katika Dola ya Kiislamu

Sheria ya Kiislamu inawapa haki wasiokuwa waislamu kama ifuatavyo;

i. Haki ya ulinzi wa mali na maisha yao.

- Ni haramu kumwaga damu ya asiyekuwa muislamu bila sababu ya msingi.



ii. Haki katika sheria ya jinai

- Makosa yote ya jinai (penal laws) adhabu zake ni sawa kwa waislamu na wasiokuwa waislamu pia.


iii. Haki katika sheria ya madai (civil laws)

- Hukumu na adhabu za madai ni sawa sawa kwa waislamu na wasiokuwa waislamu.


iv. Haki ya heshima

- Ni kosa na haifai kumvunjia heshima, kumdhulumu, n.k asiyekuwa muislamu kama ilivyo kwa muislamu.


v. Haki katika sheria ya mtu binafsi

- Sheria ya Kiislamu inahukumu mambo yote ya mtu binafsi kulingana na imani ya dini yake.





                   

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 2018-08-01 Topic: Fiqh Main: Dini File: Download PDF Views 3185

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Kitabu cha Afya    👉2 Simulizi za Hadithi Audio    👉3 web hosting    👉4 Bongolite - Game zone - Play free game    👉5 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    👉6 Madrasa kiganjani   

Post zinazofanana:

kuletewa ujumbe

(c)Kuletewa Ujumbe na Malaika kutoka kwa Allah (s.

Soma Zaidi...
Sunnah za siku ya idi na utaratibu wa kusherehekea

Hapa utajifunza utaratibu wa kusherekea ifil fitir. Pia utajifunza sunnah zinazoambatsns na idil fitir

Soma Zaidi...
Sanda ya mtoto

Mambo ya faradh kwa maiti ya muislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Maana ya talaka na kuacha ama kuachwa

Maana ya TalakaTalaka ni utaratibu wa kuvunja mkataba wa ndoa waliofunga mume na mke wakati wa kufunga ndoa mbele ya mashahidi wawili.

Soma Zaidi...
Masharti ya swala

Sharti za SwalaSharti za Swala Sharti za swala ni yale mambo ya lazima anayotakiwa Muislamu ayachunge na kuyatekeleza kabla hajaanza kuswali.

Soma Zaidi...
Je ni kwa nini lengo la finga halifikiwi kwa wafungaji

Lengo la funga ni kuwa mchamungu sasa ni kwa nini wafungaji hawalifikii lengo hili na kuwa wachamungu.

Soma Zaidi...
Uislamu unavyokemea tabia ya ombaomba

Uislamu umekataza tabia ya kuombaomba kama ndio njia ya kuendesha maisha. Pia ukaweka suluhisho la kukomesha tabia hiyo

Soma Zaidi...
Swala ya kuomba mvua swalat istiqaa na jinsi ya kuiswali.

Hapa nitakujulisha kuhusu swala ya kuomba mvia, na taratibu za kuiswali.

Soma Zaidi...
Sura zinazosomwa katika Swala ya Dhuha

Swala ya Dhuha ni swala ya sunna inayosaliwa wakati wa asubuhi baada ya jua kuchomoza na kupanda angalau kiasi cha mkuki (takribani dakika 15 baada ya jua kuchomoza) mpaka kabla ya adhuhuri. Ingawa hakuna sura maalum zilizowekwa kisheria, Mtume ﷺ alisoma baadhi ya sura zenye maana ya kuhimiza kheri na shukrani.

Soma Zaidi...