Kwa nini ni muhimu kuswali? Post hii itakwenda kukufundisha kuhusu umuhimu wa kusimamisha swala.
Umuhimu wa Kusimamisha Swala
Kwa mujibu wa Hadith ya Ibn Umar (r.a) tuliyoirejea mwanzoni, kusimamisha swala ni nguzo ya pili ya nguzo za Uislamu. Katika kuonyesha umuhimu wa kusimamisha nguzo hii Mtume (s.a.w) a me sem a:
“Sw ala ndio nguzo kubw a ya Dini (Uislamu) mwenye kusimamisha swala amesimamisha dini (Uislamu) na mwenye kuiacha swala amevunja Dini .” (Uislamu)”
Katika Hadithi nyingine, amesimulia Jabir (r.a) kuwa Mtume wa Allah amesema:
“Tofauti yetu sisi (Waislamu) na ukafiri ni kuacha swala”. (Muslim) Pia Mtume (s.a.w) amesema:
“Tofauti iliyopo kati yetu (Waislamu) na wengine (wasiokuw a Waislamu) ni swala ”. (Ahmad, Abu Daud, An-Nasai, Tirmidh)
Kutokana na hadithi hizi, tunajifunza kuwa mtu ambaye hasimamishi swala, hatakama anajiita Muislamu si Muislamu bali ni kafiri kama makafiri wengine. Anakuwa kafiri kwa sababu amekanusha amri ya Allah iliyowazi kama inavyobainika katika aya zifuatazo:
“Waambie waja wangu walioamini, wasimamishe swala. ”(14:31)
“... Basi simamisheni swala, kwa hakika swala kwa waumini ni faradhi iliyow ekewa nyakati makhsusi.” (4:1 03)
“Na waamrishe watu wako kuswali (kusimamisha swala) na uendelee mwenyewe kwa hayo...” (20:132).
Tukumbuke kuwa hawi Muumini yule anayekuwa na hiari katika kutekeleza amri ya Allah na Mtume wake kama tunavyokumbushwa katika aya ifuatayo:
“Haiwi kwa mwanamume aliyeamini wala kwa mwanamke aliyeamini, Mwenyezi Mungu na Mtume wake wanapokata shauri, wawe na hiari katika shauri lao. Na mwenye kumuasi Mwenyezi Mungu na Mtume wake, hakika amepotea upotofu ulio wazi”. (33:36)
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.
Download NowJe umeipenda post hii ?
Haki na uadilifu katika uislamu (EDK form 3: Dhana ya elimu ya uislamu)
Soma Zaidi...Hapa utajifunza faida za ndoa katika Jamii na kwa wanadamu kiafya, kiroho, kiuchumi
Soma Zaidi...Msimamo wa Uislamu juu ya kudhibiti uzaziKama tulivyoona, msukumo wa kampeni ya kudhibiti kizazi, umetokana na mfumo mbaya wa kijamii na kiuchumi ulioundwa na wanadamu kutokana na matashi yao ya ubinafsi.
Soma Zaidi...Kwenye kipengele hichi tutajifinza vyanzo mbalimbali vya sheria ua kiislamu.
Soma Zaidi...Assalamu Alaykum Warahmatu-llah Wabarakaatuh Naomba kuuliza: Je kama maiti imekatika baadhi ya viungo je viungo vyake tunafata utaratibu gani katika kumuosha na kumkafini?
Soma Zaidi...Haki na uadilifu katika uislamu (EDK form 3: Dhana ya elimu ya uislamu)
Soma Zaidi...Nguzo za uislamu (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu)
Soma Zaidi...Post hii itakufundisha taratibu za kuajiri, kufanya kazi na malipo.
Soma Zaidi...Post hii itakufundisha namna ya kutwaharisha Najisi.
Soma Zaidi...