Kwa nini ni muhimu kuswali? Post hii itakwenda kukufundisha kuhusu umuhimu wa kusimamisha swala.
Umuhimu wa Kusimamisha Swala
Kwa mujibu wa Hadith ya Ibn Umar (r.a) tuliyoirejea mwanzoni, kusimamisha swala ni nguzo ya pili ya nguzo za Uislamu. Katika kuonyesha umuhimu wa kusimamisha nguzo hii Mtume (s.a.w) a me sem a:
“Sw ala ndio nguzo kubw a ya Dini (Uislamu) mwenye kusimamisha swala amesimamisha dini (Uislamu) na mwenye kuiacha swala amevunja Dini .” (Uislamu)”
Katika Hadithi nyingine, amesimulia Jabir (r.a) kuwa Mtume wa Allah amesema:
“Tofauti yetu sisi (Waislamu) na ukafiri ni kuacha swala”. (Muslim) Pia Mtume (s.a.w) amesema:
“Tofauti iliyopo kati yetu (Waislamu) na wengine (wasiokuw a Waislamu) ni swala ”. (Ahmad, Abu Daud, An-Nasai, Tirmidh)
Kutokana na hadithi hizi, tunajifunza kuwa mtu ambaye hasimamishi swala, hatakama anajiita Muislamu si Muislamu bali ni kafiri kama makafiri wengine. Anakuwa kafiri kwa sababu amekanusha amri ya Allah iliyowazi kama inavyobainika katika aya zifuatazo:
“Waambie waja wangu walioamini, wasimamishe swala. ”(14:31)
“... Basi simamisheni swala, kwa hakika swala kwa waumini ni faradhi iliyow ekewa nyakati makhsusi.” (4:1 03)
“Na waamrishe watu wako kuswali (kusimamisha swala) na uendelee mwenyewe kwa hayo...” (20:132).
Tukumbuke kuwa hawi Muumini yule anayekuwa na hiari katika kutekeleza amri ya Allah na Mtume wake kama tunavyokumbushwa katika aya ifuatayo:
“Haiwi kwa mwanamume aliyeamini wala kwa mwanamke aliyeamini, Mwenyezi Mungu na Mtume wake wanapokata shauri, wawe na hiari katika shauri lao. Na mwenye kumuasi Mwenyezi Mungu na Mtume wake, hakika amepotea upotofu ulio wazi”. (33:36)
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu
Umeionaje Makala hii.. ?
Katika kipengele hiki tutajifunza nguzo za uislamu.aina tano za nguzo za uislamu,dhana ya nguzo za uislamu,lengo na umuhimu wa nguzo za uislamu
Soma Zaidi...Post hii inakwenda kukufundisha kuhusu swala ya Istikhara
Soma Zaidi...Hapa utajifunza aina za biashara ambazo ni haramu.
Soma Zaidi...Katika uislamu imekatazwa kutamani kufa hata kama utakuwa ni mtu muovu sana ama mchamungu sana.
Soma Zaidi...Benki za KiislamuBenki za Kiislamu ambazo hutoa huduma kama benki nyingine zinaendeshwa katika msingi wa biashara na sio ule wa riba.
Soma Zaidi...Kila najisi ina namna yake ya kutwaharisha, hata hivyo namna hizo hufanana. Katika post hii utakwenda kujifunza jinsi ya kutwaharisha najisi mbalimbali.
Soma Zaidi...