Ni upibutaratibu wa kuingia eda na kutoka eda

Ni upibutaratibu wa kuingia eda na kutoka eda

Katika uislamu hakuna sheria ya mwanamke kuingizwa eda na kutolewa eda kama ilivyozoeleka. Endelea na post hii ujifunze zaidi

Jiunge nasi WhatsApp
Upate Update zetu

Kuingizwa au Kutolewa Eda

Katika sheria ya Kiislamu hapana suala Ia kuingizwa au kutolewa eda na Sheikh. Kizuka huanza eda baada tu ya kufariki mumewe na eda yake huisha mara tu baada ya muda wa miezi mine na siku kumi kuisha. Wala hapana vazi maalum Ia kukalia eda. Si nguo nyeupe, wala nyeusi, wala kuvaa matambara kama baadhi ya watu wanavyoitakidi. Mwanamke mfiwa atabakia nyumbani kwa mumewe au kwa warithi wa mumewe katika sitara kama kawaida anavyotakiwa awe mwanamke yeyote wa Kiislamu na ataendelea kufanya shughuli zake za nyumbani na nje ya nyumbani zilizo katika mipaka ya sheria ya Kiislamu. Wala hapana sheria yoyote ya kukaa nyumbani kivivu-vivu kama wanavyoitakidi watu wengine.
 
 
 
 
Hekima kubwa ya kuamrishwa kizuka kukaa eda, pamoja na haja ya kuangaliwa uwezekano wa kuachwa na mimba, kunampa kizuka nafasi ya kutulizana na kuliwazika baada ya kupatwa na msiba mkubwa kiasi hicho. Pamoja na kuwa mwanamke baada ya kipindi cha eda huwa huru kutoka nyumbani kwa mumewe marehemu na kuolewa na mume mwingine, akitaka kubakia katika nyumba ya mumewe pamoja na watoto wake, ana haki kisheria kama tunavyojifunza katika aya ifuatayo:
 
 
 
Na wale waliofishwa miongoni mwenu na wakawacha wake, wawausie (warithi wao) kwa ajili ya wake zao kupata matumizi ya mwaka mmoja bila ya kutolewa (katika nyumba za waume zao). Na kama wanawake wenyewe wakiondoka, basi si kosa juu yenu kwa yale waliyoyafanya kwa nafsi zao
 
 
 
 
wenyewe yanayofuata sharia. Na Mwenyezi Mungu ni mwenye nguvu, mwenye hi/dma. (2:240).
Katika baadhi ya jamii za kijahili pamekuwa na mtindo wa kuwarithi wanawake waliofiwa na waume zao kama mali inavyorithiwa na jamaa wa marehemu. labia hii ya kumdhalilisha mwanamke na kumnyima uhuru wake wa kuolewa na mwanamume ampendaye imepigwa marufuku katika sheria ya Kiislamu kama tunavyojifunza katika aya ifuatayo:
 
 
 
Enyi mlioamini! Si halali kwenu kurithi wanawake kwa jeuri. Wala msiwazulie (kuolewa na waume wengine) iii mpate kuwanyang 'anya baadhi ya vile mlivyowapa (katika urithi wa waume zao...) (4:19)
 
 
 
 
Ama mwanamke mjane mwenyewe akiridhika kuolewa na ndugu au jamaa wa marehemu mumewe, ili aweze kubakia pale na watoto wake hapana ubaya ili mradi tu wafunge ndoa kama ilivyo katika sheria.
 
 

Download Post hii hapa

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Fiqh Main: Dini File: Download PDF Views 8786

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 kitabu cha Simulizi    👉2 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉3 Kitau cha Fiqh    👉4 Kitabu cha Afya    👉5 Bongolite - Game zone - Play free game    👉6 Simulizi za Hadithi Audio   

Post zinazofanana:

Jinsi ya kuswali swala ya kuoatwa kwa juwa ama swala ya kuoatwa kwa mwezi.
Jinsi ya kuswali swala ya kuoatwa kwa juwa ama swala ya kuoatwa kwa mwezi.

Post hii itakufundisha kuhusu swala ya kupatwa yaani kupatwa kwa juwa na kupatwa kwa mwezi swalat kusuf na swalat khusuf

Soma Zaidi...
Aina mbili za talaka zisizo na rejea katika uislamu
Aina mbili za talaka zisizo na rejea katika uislamu

Huwezi kuruhusiwa kumrejea mke endapo utamuacha kwa talaka hizi mbili.

Soma Zaidi...
Watu wanaolazimika kufunga mwezi wa Ramadhani
Watu wanaolazimika kufunga mwezi wa Ramadhani

Hapa utajifunza watu ambao wanalazimika kufunga mwezi wa Ramadhani.

Soma Zaidi...
MAANA YA ZAKA NA SADAKA KULUNGA NA KISHERIA PAMOJA NA TOFAUTI ZAO
MAANA YA ZAKA NA SADAKA KULUNGA NA KISHERIA PAMOJA NA TOFAUTI ZAO

MAANA YA ZAKA NA SADAKA KULUNGA NA KISHERIA PAMOJA NA TOFAUTI ZAO.

Soma Zaidi...
Hutuba ya Ndoa - Khutbat nikah
Hutuba ya Ndoa - Khutbat nikah

Hii ni hutuba ya ndoa kwa ufupi, Imekusanya mambo ya msingi yanayohitajika katika hutuba ya ndoa

Soma Zaidi...
Sunnah za funga ya ramadhan
Sunnah za funga ya ramadhan

Nguzo za uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Sanda ya mtoto
Sanda ya mtoto

Mambo ya faradh kwa maiti ya muislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...