picha

Namna ya kuchoma chanjo

Posti hii inahusu zaidi namna ya kuchoma chanjo, ni njia ambazo utumika kutoa chanjo kwa watoto na watu wazima kwa utaratibu uliowekwa.

Namna ya kuchoma chanjo.

1.Kwanza kabisa unapaswa kumsalimia mteja na kujitambulisha kwake na yeye kujitambulisha kwake na pia unapaswa kutoa elimu kuhusu chanjo unavyoenda kutoa chanjo.

 

2.Baada ya hapo unapaswa kuandaa vifaa vya kumchoma mteja chanjo kama vile chanjo yenyewe na hakikisha kama imepita mda wake, andaa bomba la kuchoma chanjo, tray ya kuwekea vifaa na mahitaji yote yanayohitajika.

 

 

3.Kuandaa sehemu kwa ajili ya mgonjwa, na  pima dawa kwa kadiri ya hitaji na kama kuna chanjo mbili yaani ya matone na sindano unapaswa kuanza na matone na baadae unamalizia na sindano kwa kufanya hivyo  inaepuka usumbufu kutoka kwa mtoto.

 

 

4.Baada ya kumchoma mtoto chanjo unatupa bomba kwenye box maalum na pia unamshukuru Mteja kwa ushirikiano aliouonyesha na ujamwambia tarehe ya kurudi kama hajamaliza chanjo.

 

5.Unampatia mteja nafasi ya kuuliza maswali , hakikisha unatoa majibu sahihi kama hauna majibu sahihi usijibu swali unaweza kuuliza kwa wahudumu wengine na kuhakikisha kubwa mteja ameondoka na jibu sahihi.

 

 

6.Unarudisha vifaa kwenye sehemu yake.

Na wakati wa kurudisha vifaa hakikisha kuwa temperature ya kwenye box la kutunzia chanjo iko sahihi yaani kuanzia 2 mpaka nane kama zinakuwa kati ya hizo hiyo ni sahihi kama ni juu yake au pungufu hali hiyo si sahihi kwa hiyo tunapaswa kufanya utaratibu unaofaa.

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Huduma Main: Post File: Download PDF Views 1922

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 ai web app     👉2 kitabu cha Simulizi     👉3 Kitau cha Fiqh     👉4 Madrasa kiganjani     👉5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉6 web hosting    

Post zinazofanana:

Mfuno wa damu na makundi manne ya damu na asili yake nani anayepasa kutoa damu?

Posti hii inakwenda kukujuza kuhusu makundi manne ya damu, asili yake, maana ya antijeni na antibody, pia utajifunza kuhusu mfumo wa Rh. Mwisho utajifunza watu wanaopasa kutoa damu.

Soma Zaidi...
Fahamu kuhusu madhara ya uzito mkubwa

Posti hii inahusu zaidi madhara ambayo yanaweza kutokea kwa mtu mwenye uzito mkubwa,kwa kawaida ili mtu aweze kuwa na uzito wa kawaida ni vizuri na kiafya kupima urefu ukilinganisha na uzito wa mtu.

Soma Zaidi...
Namna ya kuyatunza macho

Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu namna ya kuyatunza macho

Soma Zaidi...
HUDUMA YA KWANZA KWA MTU ALIYEZIMIA (CARDIOPULMONARYRESUSCITATION) AU CPR

Kuzimia ni hali ya kupoteza fahamu ambako kunaendana na kutokuhema.

Soma Zaidi...
Fahamu kuhsu vitamini E na kazi zake mwilini

Je unazijuwa faida za kuwa na vitamini E mwilini mwako.Unahani utapata matatizo yapi ya kiafya endapo utakuwa na upungufu wa vitamini E mwilini? Makala hii ni kwa ajili yako.

Soma Zaidi...
Huduma ya Kwanza kwa mtu aliyeng'atwa na nyoka

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu huduma ya Kwanza kwa mtu aliyeng'atwa na nyoka

Soma Zaidi...