Namna ya kuchoma chanjo

Namna ya kuchoma chanjo

Posti hii inahusu zaidi namna ya kuchoma chanjo, ni njia ambazo utumika kutoa chanjo kwa watoto na watu wazima kwa utaratibu uliowekwa.

Namna ya kuchoma chanjo.

1.Kwanza kabisa unapaswa kumsalimia mteja na kujitambulisha kwake na yeye kujitambulisha kwake na pia unapaswa kutoa elimu kuhusu chanjo unavyoenda kutoa chanjo.

 

2.Baada ya hapo unapaswa kuandaa vifaa vya kumchoma mteja chanjo kama vile chanjo yenyewe na hakikisha kama imepita mda wake, andaa bomba la kuchoma chanjo, tray ya kuwekea vifaa na mahitaji yote yanayohitajika.

 

 

3.Kuandaa sehemu kwa ajili ya mgonjwa, na  pima dawa kwa kadiri ya hitaji na kama kuna chanjo mbili yaani ya matone na sindano unapaswa kuanza na matone na baadae unamalizia na sindano kwa kufanya hivyo  inaepuka usumbufu kutoka kwa mtoto.

 

 

4.Baada ya kumchoma mtoto chanjo unatupa bomba kwenye box maalum na pia unamshukuru Mteja kwa ushirikiano aliouonyesha na ujamwambia tarehe ya kurudi kama hajamaliza chanjo.

 

5.Unampatia mteja nafasi ya kuuliza maswali , hakikisha unatoa majibu sahihi kama hauna majibu sahihi usijibu swali unaweza kuuliza kwa wahudumu wengine na kuhakikisha kubwa mteja ameondoka na jibu sahihi.

 

 

6.Unarudisha vifaa kwenye sehemu yake.

Na wakati wa kurudisha vifaa hakikisha kuwa temperature ya kwenye box la kutunzia chanjo iko sahihi yaani kuanzia 2 mpaka nane kama zinakuwa kati ya hizo hiyo ni sahihi kama ni juu yake au pungufu hali hiyo si sahihi kwa hiyo tunapaswa kufanya utaratibu unaofaa.

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu Rajabu
Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Huduma Main: Post File: Download PDF Views: 1932

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Dua za Mitume na Manabii     👉2 Tafasiri ya Riyadh Swalihina     👉3 ai web app     👉4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉5 Madrasa kiganjani     👉6 kitabu cha Simulizi    

Post zinazofanana:

Huduma ya Kwanza kwa mtu aliyepaliwa

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu huduma ya Kwanza kwa mtu aliyepaliwa

Soma Zaidi...
Huduma ya Kwanza kwa mtu aloanguka kifafa

Somo hili linakwenda kukueleza jinsi ya kumfanyia huduma ya Kwanza kwa mtu aloanguka kifafa

Soma Zaidi...
Namna ya kuyatunza macho

Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu namna ya kuyatunza macho

Soma Zaidi...
Vipimo vya minyoo

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu vipimo vya minyoo

Soma Zaidi...
Ugonjwa wa Pumu, dalili zake na njia za kujilinda dhidi ya Pumu.

Pumu ni ugonjwa ambao huathiri sehemu ya kupitisha hewa kwenda kwenye mapafu ya binadamu kitaalamu huitwa bronchioles. Mtu mwenye pumu huwa na michubuko sugu mwilini kwenye mirija yake ya kupitisha hewa. Hali ambayo husababisha kuvimba kwa kuta za mirija

Soma Zaidi...
Huduma kwa wenye ugonjwa wa herpes simplex au vipele kwenye midomo na sehemu za siri

Post hii inahusu zaidi tiba na huduma kwa wenye ugonjwa wa herpes simplex au vipele kwenye midomo na sehemu za siri.

Soma Zaidi...