Namna ya kuchoma chanjo
Posti hii inahusu zaidi namna ya kuchoma chanjo, ni njia ambazo utumika kutoa chanjo kwa watoto na watu wazima kwa utaratibu uliowekwa.
Namna ya kuchoma chanjo.
1.Kwanza kabisa unapaswa kumsalimia mteja na kujitambulisha kwake na yeye kujitambulisha kwake na pia unapaswa kutoa elimu kuhusu chanjo unavyoenda kutoa chanjo.
2.Baada ya hapo unapaswa kuandaa vifaa vya kumchoma mteja chanjo kama vile chanjo yenyewe na hakikisha kama imepita mda wake, andaa bomba la kuchoma chanjo, tray ya kuwekea vifaa na mahitaji yote yanayohitajika.
3.Kuandaa sehemu kwa ajili ya mgonjwa, na pima dawa kwa kadiri ya hitaji na kama kuna chanjo mbili yaani ya matone na sindano unapaswa kuanza na matone na baadae unamalizia na sindano kwa kufanya hivyo inaepuka usumbufu kutoka kwa mtoto.
4.Baada ya kumchoma mtoto chanjo unatupa bomba kwenye box maalum na pia unamshukuru Mteja kwa ushirikiano aliouonyesha na ujamwambia tarehe ya kurudi kama hajamaliza chanjo.
5.Unampatia mteja nafasi ya kuuliza maswali , hakikisha unatoa majibu sahihi kama hauna majibu sahihi usijibu swali unaweza kuuliza kwa wahudumu wengine na kuhakikisha kubwa mteja ameondoka na jibu sahihi.
6.Unarudisha vifaa kwenye sehemu yake.
Na wakati wa kurudisha vifaa hakikisha kuwa temperature ya kwenye box la kutunzia chanjo iko sahihi yaani kuanzia 2 mpaka nane kama zinakuwa kati ya hizo hiyo ni sahihi kama ni juu yake au pungufu hali hiyo si sahihi kwa hiyo tunapaswa kufanya utaratibu unaofaa.
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetuUmeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Kitabu cha Afya 👉2 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉3 ai web app 👉4 Simulizi za Hadithi Audio 👉5 Madrasa kiganjani 👉6 web hosting
Post zinazofanana:
Huduma ya Kwanza kwa mtu aliyepaliwa
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu huduma ya Kwanza kwa mtu aliyepaliwa
Soma Zaidi...Faida za tumbo katika mwili wa binadamu
Posti hii inahusu zaidi faida za tumbo,tumbo ni sehemu ya mwili ambayo ushughilika na kutunza chakula,
Soma Zaidi...Namna ya kumhudumia mtu aliyeingongwa na nyoka
Posti hii inahusu njia na namna ya kumhudumia aliyeingiwa na nyoka. Nyoka ni kiumbe ambacho Kina sumu kali na mtu akifinywa na nyoka asipohudumiwa anaweza kupata ulemavu au kupoteza maisha
Soma Zaidi...Njia za kukabiliana na presha ya kushuka
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu njia za kukabiliana na presha ya kushuka
Soma Zaidi...Njia za kuingiza chanjo mwilini
Posti hii inahusu njia mbalimbali ambazo utumika kupitisha chanjo, njia hizo utegemea na kazi ya chanjo kama ifuatavyo.
Soma Zaidi...