Posti hii inahusu zaidi sababu za kondo la nyuma kuwa mbele ya mlango wa kizazi, kwa kawaida kondo la nyuma huwa nyuma ya mlango wa kizazi ila Kuna wakati kondo la nyuma ujishikisha mbele ya mlango wa kizazi.
1. Kwanza kabisa tunapaswa kujua kuwa mtoto akija kuzaliwa utanguliza kichwa na kutoka kwenye tumbo la Mama ila Kuna wakati mwingine kondo la nyuma ndilo utangulia na kufuatia mtoto hii ni hatari kwa mtoto kwa Sababu hii kesi kama haijakutana na myaalamu wa kuzalisha mtoto anaweza kufia tumboni kwa hiyo ni vizuri kumtambua dalili na kumsaidia mama akaweza kujifungua salama.
2. Sababu ya kutanguliza kondo la nyuma badala ya mtoto pengine nikwa sababu ya kuwepo kwa maambukizi in kwenye mfuko wa kizazi kwa hiyo kondo la nyuma uweza kujishikisha sehemu ambayo Haina maambukizi na kusababisha kondo la nyuma kutangulia mapema wakati mtoto anapozaliwa.
3. Kuwepo kwa makovu kwenye mfuko wa uzazi.
Pengine kwenye mfuko wa kizazi panakuwepo na jeraha na jeraha hilo kwa wakati mwingine uwa kwenye sehemu ambayo kondo la nyuma linapasaw kujishikiza kwa hiyo ujishikiza sehemu yoyote ambayo ni tofauti na sehemu ya kawaida.
4. Kuwepo kwa upasuaji ambao umefanyika kabla ya mimba haijatungwa na yenyewe usababisha kuwepo kwa kitendo cha kondo la nyuma kujishikiza chini ya mlango wa kizazi na kusababisha madhara makubwa wakati wa kujifungua.
5. Mwonekano wa tumbo la uzazi kutokuwa la kawa, Kuna wakati mwingine tunaweza kumwona mtu yupo anatembea na ameumbika kawaida kwa nje ila ukija kuangalia kwa ndani mfuko wa uzazi ni tofauti na wengine kwa kitaalamu huitwa abnormally of uterus, kwa hiyo kama hauko kawaida usababisha kondo la nyuma kujishikiza sehemu yoyote isiyokuwa ya kawaida na kusababisha kondo la nyuma kutangulia mtoto.
6. Kwa kawaida kuja kumtambua kuwa Mama ana tatizo hili ni kufuatana na ujuzi wa muuguzi kwa sababu Mama anakuwa na uchungu kawaida na sifa zote za kujifungua ila shida kilichotangulia ndicho hakieleweki, kwa hiyo hali hii ikigundulika ni vizuri kumpeleka mama hospital Ili kuweza kumsaidia zaidi maana kama hakuna huduma mtoto anaweza kufia tumboni
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetuUmeionaje Makala hii.. ?
Share On:
Maumivu ya hedhi (dysmenorrhea) ni maumivu makali au ya kubana sehemu ya chini ya tumbo. Wanawake wengi hupatwa na Maumivu ya hedhi kabla tu na wakati wa hedhi zao. Kwa wanawake wengine, usumbufu huo ni wa kuudhi tu. Kwa wengine, 
Soma Zaidi...Utajifunza sababu za kuweo kwa maumivu ya uume wbaada ya tendo la ndoa na wakati wa tendo la ndoa.
Soma Zaidi...Post hii inahusu zaidi dawa ya tetracycline katika kupambana na bakteria,ni mojawapo ya antibiotics au anti bacteria ambayo upambana na bakteria kama tutakavyoona hapo mbeleni.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi hatua ambazo unaweza kuzitumia ili kuweza kutibu uvimbe au kwa kitaalamu huitwa fibroids. Hizi hatua zikitumika uweza kusaidia kupunguza kiwango cha kupata au kuwepo kwa uvimbe kwenye kizazi.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi kazi ya homoni ya testosterone, hii homoni kwa kiwango kikubwa ukutwa kwa wanaume ndiyo homoni ambayo umfanya mwanaume aonekane jinsi alivyokuwa na sifa zake zote.
Soma Zaidi...Post hii inahusu zaidi njia mbalimbali ambazo mtoa huduma anaweza kuzitumia kuangalia kama mtoto amevunjika baada ya kuzaliwa.
Soma Zaidi...