picha

Kondo la nyuma kuwa mbele ya mlango wa kizazi

Posti hii inahusu zaidi sababu za kondo la nyuma kuwa mbele ya mlango wa kizazi, kwa kawaida kondo la nyuma huwa nyuma ya mlango wa kizazi ila Kuna wakati kondo la nyuma ujishikisha mbele ya mlango wa kizazi.

Sababu za kondo la nyuma kuwa mbele ya mlango wa kizazi.

1. Kwanza kabisa tunapaswa kujua kuwa mtoto akija kuzaliwa utanguliza kichwa na kutoka kwenye tumbo la Mama ila Kuna wakati mwingine kondo la nyuma ndilo utangulia na kufuatia mtoto hii ni hatari kwa mtoto kwa Sababu hii kesi kama haijakutana na myaalamu wa kuzalisha mtoto anaweza kufia tumboni kwa hiyo ni vizuri kumtambua dalili na kumsaidia mama akaweza kujifungua salama.

 

2. Sababu ya kutanguliza kondo la nyuma badala ya mtoto pengine nikwa sababu ya kuwepo kwa maambukizi in kwenye mfuko wa kizazi kwa hiyo kondo la nyuma uweza kujishikisha sehemu ambayo Haina maambukizi na kusababisha kondo la nyuma kutangulia mapema wakati mtoto anapozaliwa.

 

3. Kuwepo kwa makovu kwenye mfuko wa uzazi.

Pengine kwenye mfuko wa kizazi panakuwepo na jeraha na jeraha hilo kwa wakati mwingine uwa kwenye sehemu ambayo kondo la nyuma linapasaw kujishikiza kwa hiyo ujishikiza sehemu yoyote ambayo ni tofauti na sehemu ya kawaida.

 

4. Kuwepo kwa upasuaji ambao umefanyika kabla ya mimba haijatungwa na yenyewe usababisha kuwepo kwa kitendo cha kondo la nyuma kujishikiza chini ya mlango wa kizazi na kusababisha madhara makubwa wakati wa kujifungua.

 

5.  Mwonekano wa tumbo la uzazi kutokuwa la kawa, Kuna wakati mwingine tunaweza kumwona mtu yupo anatembea na ameumbika kawaida kwa nje ila ukija kuangalia kwa ndani mfuko wa uzazi ni tofauti na wengine kwa kitaalamu huitwa abnormally of uterus, kwa hiyo kama hauko kawaida usababisha kondo la nyuma kujishikiza sehemu yoyote isiyokuwa ya kawaida na kusababisha kondo la nyuma kutangulia mtoto.

 

6. Kwa kawaida kuja kumtambua kuwa Mama ana tatizo hili ni kufuatana na ujuzi wa muuguzi kwa sababu Mama anakuwa na uchungu kawaida na sifa zote za kujifungua ila shida kilichotangulia ndicho hakieleweki, kwa hiyo hali hii ikigundulika ni vizuri kumpeleka mama hospital Ili kuweza kumsaidia zaidi maana kama hakuna huduma mtoto anaweza kufia tumboni

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Uzazi Main: Post File: Download PDF Views 4688

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
πŸ‘‰1 ai web app     πŸ‘‰2 Kitau cha Fiqh     πŸ‘‰3 web hosting     πŸ‘‰4 Simulizi za Hadithi Audio     πŸ‘‰5 Tafasiri ya Riyadh Swalihina     πŸ‘‰6 kitabu cha Simulizi    

Post zinazofanana:

Jinsi mimba inavyotungwa na namna ambavyo jinsia ya mtoto inavyotokea

Posti hii hasa inahusu kasoro ,utatuzi,na jinsi ya kutunga mimba kwa upande wa mwanamke na mwanaumeΒ  .itatupelekea jinsi ya kuangalia kasoro na jinsi ya kutatua hizo kasoro katika jamii zetu.

Soma Zaidi...
Umuhimu wa uzazi wa mpango

Uzazi wa mpango ni njia inayotumiwa na WA awake na wasichana Ili kupata idadi ya watoto wanaowahitaji na kuepuka mimba zisizotarajiwa.

Soma Zaidi...
Njia za kugundua kama mtoto amevunjika baada ya kuzaliwa

Post hii inahusu zaidi njia mbalimbali ambazo mtoa huduma anaweza kuzitumia kuangalia kama mtoto amevunjika baada ya kuzaliwa.

Soma Zaidi...
Tabia za Ute wa siku za hatari kupata mimba au ovulation

Posti hii inahusu zaidi tabia mbalimbali za Ute wa ovulation kwa sababu Ute huu huwa tofauti na Ute mwingine kwa sababu ya kuwepo kwa tabia zake za kipekee kama tutakavyoona.

Soma Zaidi...
Mabadiliko kwenye uke wa Mama pale anapobeba mimba.

Posti hii inahusu zaidi mabadiliko kwenye uke wa Mama pale anapobeba tu mimba, Mama anapobeba mimba Kuna mabadiliko Katika uke wa Mama kama ifuayavyo.

Soma Zaidi...
Madhara ya kiafya ya kupiga punyeto

Post hii inakwenda kukutania madhara ya kuoiga punyeto kwa afya yako.

Soma Zaidi...